R.B
JF-Expert Member
- May 10, 2012
- 6,296
- 2,578
[h=2] [/h] Ijumaa, Julai 19, 2013 05:33 Na Shomari Binda, Rorya
DIWANI wa Kata ya Tai (CHADEMA), Godfrey Masirori amesifia jitihada zinazofanywa na Mbunge wa Jimbo la Rorya, Lameck Airo (CCM), kwa kushiriki shughuli mbalimbali za maendeleo jimboni humo, akisema kuwa ni wa vitendo si wa kuongea.
Kauli hiyo aliitoa katika mkutano wa hadhara ulioandaliwa na mbunge huyo katika Kijiji cha Sota, baada ya ziara ya kukagua shughuli za maendeleo za jimbo hilo na kuendesha harambee ya kuchangia ujenzi wa madarasa ya Shule ya Msingi Majengo, iliyopo katika kata hiyo baada ya kuezuliwa na upepo.
Masirori alisema mbunge huyo amekuwa ni mwepesi wa kujitoa na kushiriki mambo mbalimbali ya kimaendeleo katika jimbo na pale yanapotokea majanga amekuwa akifika kwa wakati na kushirikiana na wananchi kutafuta ufumbuzi.
Masirori alisema, harambee iliyofanywa na mbunge huyo katika mkutano wa hadhara japo ni wa kushtukiza, lakini inaonyesha ni jinsi gani anavyoguswa na matatizo ya wananchi wa Rorya na kutaka majengo yaliyoezuliwa na upepo yaweze kukamilika na wanafunzi waendelee na masomo.
Ndugu zangu hii shule ni yetu na wanafunzi wanaosoma hapa ni wetu, naungana na mbunge kwa kuchangia Sh laki moja ili shule hii iweze kukamilika kwa wakati na vijana wetu waendelee na masomo.
"Katika suala la shughuli za maendeleo, itikadi za kisiasa tunaweka pembeni na kwa pamoja tunashiriki shughuli za kimaendeleo. Jambo hili linalofanywa na mbunge ni jambo jema na kila mmoja ana kila sababu ya kusifia jambo hili, alisema Masirori.
Akizungumza katika mkutano huo, mbunge huyo alisema aliguswa na taarifa ya kuezuliwa kwa shule hiyo akiwa katika vikao vya Bunge na kuamua kuaga ili kuweza kushiriki moja kwa moja katika tatizo hilo.
Ndugu zangu niliguswa na suala hili na kuamua kuaga bungeni, lakini kabla sijafika hapa tayari niliagiza mafundi kuja kuangalia athari iliyopatikana hapa na kuanza kwa ujenzi, lakini kazi hii inahitaji ushirikiano ili vijana wetu waendelee kusoma.
"Sasa hivi suala la elimu ndilo linaloangaliwa katika kila sehemu, lazima majengo haya yakamilike na watoto wetu wasome, naomba kila mmoja aje kuchangia ili madarasa haya yaliyoezuliwa yaweze kukamilika, alisema Lameck.
Katika harambee hiyo, zaidi ya Sh milioni mbili zilipatikana zikiwemo ahadi ya mifuko 19 ya saruji.
DIWANI wa Kata ya Tai (CHADEMA), Godfrey Masirori amesifia jitihada zinazofanywa na Mbunge wa Jimbo la Rorya, Lameck Airo (CCM), kwa kushiriki shughuli mbalimbali za maendeleo jimboni humo, akisema kuwa ni wa vitendo si wa kuongea.
Kauli hiyo aliitoa katika mkutano wa hadhara ulioandaliwa na mbunge huyo katika Kijiji cha Sota, baada ya ziara ya kukagua shughuli za maendeleo za jimbo hilo na kuendesha harambee ya kuchangia ujenzi wa madarasa ya Shule ya Msingi Majengo, iliyopo katika kata hiyo baada ya kuezuliwa na upepo.
Masirori alisema mbunge huyo amekuwa ni mwepesi wa kujitoa na kushiriki mambo mbalimbali ya kimaendeleo katika jimbo na pale yanapotokea majanga amekuwa akifika kwa wakati na kushirikiana na wananchi kutafuta ufumbuzi.
Masirori alisema, harambee iliyofanywa na mbunge huyo katika mkutano wa hadhara japo ni wa kushtukiza, lakini inaonyesha ni jinsi gani anavyoguswa na matatizo ya wananchi wa Rorya na kutaka majengo yaliyoezuliwa na upepo yaweze kukamilika na wanafunzi waendelee na masomo.
Ndugu zangu hii shule ni yetu na wanafunzi wanaosoma hapa ni wetu, naungana na mbunge kwa kuchangia Sh laki moja ili shule hii iweze kukamilika kwa wakati na vijana wetu waendelee na masomo.
"Katika suala la shughuli za maendeleo, itikadi za kisiasa tunaweka pembeni na kwa pamoja tunashiriki shughuli za kimaendeleo. Jambo hili linalofanywa na mbunge ni jambo jema na kila mmoja ana kila sababu ya kusifia jambo hili, alisema Masirori.
Akizungumza katika mkutano huo, mbunge huyo alisema aliguswa na taarifa ya kuezuliwa kwa shule hiyo akiwa katika vikao vya Bunge na kuamua kuaga ili kuweza kushiriki moja kwa moja katika tatizo hilo.
Ndugu zangu niliguswa na suala hili na kuamua kuaga bungeni, lakini kabla sijafika hapa tayari niliagiza mafundi kuja kuangalia athari iliyopatikana hapa na kuanza kwa ujenzi, lakini kazi hii inahitaji ushirikiano ili vijana wetu waendelee kusoma.
"Sasa hivi suala la elimu ndilo linaloangaliwa katika kila sehemu, lazima majengo haya yakamilike na watoto wetu wasome, naomba kila mmoja aje kuchangia ili madarasa haya yaliyoezuliwa yaweze kukamilika, alisema Lameck.
Katika harambee hiyo, zaidi ya Sh milioni mbili zilipatikana zikiwemo ahadi ya mifuko 19 ya saruji.