Diwani aliyechomwa Kisu afariki dunia

Diwani aliyechomwa Kisu afariki dunia

poleni familia ya marehemu

huyu alikuwa diwani kupitia CDM alichomwa kisu na mpenzi wake alikuwa naye kiongozi wa CDM
 
Ndio huyu ni Diwani wa CDM ambapo alichomwa kisu na mpenzi wake ambae ana cheo cha Mkurugenzi wa Mafunzo CDM TAIFA VIJANA kama cjakosea na anatoka Kilimanjaro
 
Hiyo formulae ilishafutwa enzi za Zakayo! Sasa kila alietubu akirudisha mali huku kanisani sadaka atoe nani? Tutakosa hata mabenchi wangu!
Kutubu bila kurudisha kura ulizoiba haisaidii. Unatubu halafu unaendelea kukalia kiti!!!!!!!!!
 
Ina maana Chadema hawakumchukulia hatua huyo Mkurugenzi? This is the highest form of women's abuse. Kulikuwa na kesi? Jamaa alishinda?
Ndio huyu ni Diwani wa CDM ambapo alichomwa kisu na mpenzi wake ambae ana cheo cha Mkurugenzi wa Mafunzo CDM TAIFA VIJANA kama cjakosea na anatoka Kilimanjaro
 
RIP marehemu Tuse,mwanga wa milele ukuangazie.
 
Mkuu huyu ndiye yule Diwani aliyechomwa na Mkurugenzi wa Uhamasishaji? Mungu amrehemu
 
Rest In Peace Chanceller Tuse!
Other many are coming behind!
 
Poleni familia na wanachadema

Ni mchezo mchafu wa magamba huo,mtu kachomwa kisu chini ya titi tangu trh 25 kalazwa na hajapata hata sindano ya tetenus unategemea nini?RIP kamanda,hiyo kata magamba muisahau tu.
 


Diwani wa Chama cha Kata ya Mtibwa, wilayani Mvomero, mkoa wa Morogoro Chadema, Tusekile Mwakyoma(28), amefariki dunia, baada ya kuchomwa kwa kisu na mchumba wake.
Diwani huyo alifariki jana majira ya saa 6:00 mchana katika Hospitali ya misheni ya Bwagala alikokuwa amelazwa, baada ya kuchomwa na kisu na mchumba wake kwa kile kinachoelezwa kuwa wivu wa mapenzi.

Marehemu Tusikile anadaiwa kuchomwa na kisu Desemba 26, mwaka jana katika ziwa la kushoto na mchumba wake ambaye ni Mkurugenzi wa Mafunzo na Uenezi wa Chama cha Chadema katika wilaya ya Mvomero, Songa Mgweno.

Mtuhumiwa ambaye ni mkazi wa kijiji cha Kilimanjaro, inadaiwa kuwa baada ya kufanya kitendo hicho alitoweka.
Mkuu wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai (RCI) Mkoa wa Morogoro, Hamis Selemani,alithibitisha kutokea kwa kifo cha diwani huyo na kueleza kuwa Jeshi la Polisi linaendelea kumtafuta mtuhumiwa huyo ili afikishwe mahakamani.

Kwa mujibu wa ofisa huyo, kabla ya kufikwa na mauti hayo, marehemu alieleza kuwa siku ya tukio, mchumba wake Mgweno alimpigia simu saa mbili usiku aende nyumbani kwake katika kijiji cha Kilimanjaro ili akachukue fedha alizokuwa akimdai Shilingi 200,000.


Akisema kuwa marehemu likwenda huko na kuamua kulala na ilipofika alfajiri alimuamsha na kumuuliza amefanya juhudi gani kuhakikisha wazazi wake wanakubali amuoe ambapo marehemu alimwambia kuwa hana jibu.


"Tuliendelea kulala lakini baada ya muda aliendelea kunipapasa nikasikia maumivu makali chini ya ziwa la kushoto baada ya kujichunguza nikaona kisu kikininginia," alisema marehemu wakati alipokuwa amelazwa.


Marehemu alieleza kuwa Mgweno aliendelea kumkaba koo na kuchomoa kisu hicho na kutaka kumpiga kingine, lakini alijitahidi kumdhibiti huku akipiga kelele kuomba msaada ambapo ndugu wa mwanaume waliamka na kwenda chumbani kwao kutoa msaada.


Alieleza kuwa ndugu wa Mgweno waliamua kumchukua na kumpeleka marehemu katika hospitali ya misheni ya Bwagala ambapo alipatiwa matibabu, lakini hali yake iliendelea kuwa mbaya mpaka alipofariki dunia.


Akizungumza kwa simu na gazeti hili, Mwenyekiti wa Baraza la Madiwani wa Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero, Jonas Zeland, alithibitisha kifo cha diwani huyo na kueleza kuwa alipata taarifa hizo kupitia kwa wazazi wa marehemu.


Zeland alisema kuwa anawasiliana na Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero, Sara Linoma, kwa ajili ya kusafirisha mwili wa marehemu leo kuelekea mkoani Mbeya kwa ajili ya mazishi.





CHANZO: NIPASHE
 
RIP,
Huyu jamaa ana matatizo ya akili lazima. Imeniuma sana! Yaani alijiandaa kabisa kummuua mchumba wake, maana alikuwa tayari ana kisu na alikuwa katika hali ambayo huwezi kumdahania. Huyu ni wa kunyongwa kabisa!
 
Back
Top Bottom