Habari Wakuu,
Najua wengi wamekutana na jambo hili nina mpenzi wangu mwaka wa tatu sasa ila dini tofauti na nikimuuliza kuhusiana na dini anawaka anasema itakua namtafutia sababu tuachane.
Nifahaishane faida na hasara za kuishi kwa dini tofauti ndani ya ndoa.
Mimi Christian binti Islamic
Mmhhhhmm ... dear hata sijui nisemeje .. Binafsi nakushauri Fanya Funga na maombi ili Mungu akufunilie yaliyo sirini.... Hivi vitu vinasumbua sana Baadae .. I speak from my experience .. For what I went through I wouldn't want any of my children to go through this again.. Wazazi wangu hawakuwa Dini moja ..nililelewa Kiislam full na Madrasah niliisoma . Ilinichanganya nilipokuwa nikiona huku nalelelewa na kufunzwa Kiislam but kule watu wanakwenda Church kumshangilia Yesu kwa furaha nikitaka kwenda nakatazwa niliimbiwa kule hakunifai.. Kuna kipindi kulikuwa na mikutano Tanga High School , Makorora , Mkwakwani na Mabawa mtoto Mimi nimo si nilikuwa napagawa na miujiza niliyokuwa nikihadithiwa na watoto wenzangu.. Dear Siku ilifika nikasema hata na Mimi nataka nishuhudie kwa macho yangu.. Nilipoanza kushuhudia kwa macho hata Madrasah nikawa mtoro nilikuwa nashangazwa na nguvu za Huyu Yesu anayetoa mapepo , kufufua watu, na kufungua watu.. nikitoroka madrasah nikirudi home ni viboko tena vya nguvu .. pamoja nimechapwa leo kesho yake nilirudia tena .( mwili wote una makovu kwa fimbo sababu ? Ya Yesu) Hebu niambie je haya maisha unataka aje kupitia uzao wako.? Najua for now kila mtu atataka umuoe huyo mpenzio .. But what about your heart says? Beside the love you have for her..
Ndugu nakushauri kaa chini na mwenzio Fanya nae maongezi kwa utaratibu tuu na kwa Upendo .. Na usichoke kumuombea na kumuhubiria Habari Njema za Yesu .. Kwa maana sio waislamu wote wasiopenda kibadilisha Dini . Wengine ni waaoga. Wanaogopa kukataliwa na kupewa laana na wazazi ( Haya yalinikuta Mimi lakini hadi sasa bado Niko hai Nasonga na Yesu na anazidi kunipigania. Na mzazi amejirudi na wengine wanafuata mmoja mmoja ) . Dear maisha ya ndoa si kama ya Ku date or ya Uchumba. For now kila kitu unaona its okay because hamjaoana dear .. Mkishaooana maisha huwa yanabadilika ... Na katika hayo mabadiliko kunakuwa na mapito . Katika kipindi hicho chote mtamuhitaji Mungu sana na mtataka kuwa na ukaribu nae. Sasa sijui mtamuitaje huyo Mungu. Mtamuita as Jesus or as Allah.? Na maombi ya wanandoa yana Nguvu sana.. Kazi kwako .. Funga na Maombi Mungu akuongoze vyema.. Samahani nilipokukwaza. Good Luck.. Thanks..