Yaani upumbavu kweli:
Matajiri wa KUZUNGU - yaani Uzungu ni sifa nyingine zaidi ya utajiri. Katika market ya Fort Lauderdale nyumba ile ya vyumba viwili tena ya kizamani sana (1967) iliuzwa kwa $235,000 tu halafu mtu anasema ni sehemu ya matajiri wa Kizungu tu. Anaweza kuwa ana point nyingine lakini hiyo juu inamdiscredit kabisa.
Haaa jirani umeona na wewe eeh?
Huo ni zaidi ya ushamba!
Marekani ya karne ya 21 mtu bado analeta mambo kujidai kuhusu mtaa ambao eti hauna weusi.
Kwanza kajuaje hauna weusi? Kuna vibao vimebandikwa visemavyo 'For Whites Only'? Sidhani.
Yaani kwake uzungu sijui ndo nini tu. Nadhani yeye kuolewa na mzungu ni kama vile ni genetic step up.
Mara eti shule asomaye mwanaye hakuna ngozi nyeusi...I mean, so what's the big deal?
Halafu anaponda sehemu ambazo hata hazijui vizuri.
Na kununua kijumba cha bei kubwa kwenye viunga vya L.A. wala si ujanja kama unaweza kununua jumba kubwa zaidi lenye square footage ya kutosha na yard space ya kumwaga kwa bei hiyo hiyo kwenye jimbo au mji mwingine.
Huko L.A. sana sana unacholipia ni jina tu na si ubora wa kile unachokinunua.
Hao akina Warren Buffet bado wanaishi kwenye nyumba zao huko Omaha, Nebraska huku ndo matajiri wakubwa duniani.
Sijawahi kuona mtu mshamba kama huyo dada. Eti hakuna ngozi nyeusi.....hahahahahahaaaa.
Swala la rangi ya ngozi limebaki kuwa ni ishu kwa wajinga na wapumbavu wachache sana na yeye akiwa mmojawapo maana hata White House mkazi wake ni ngozi nyeusi. Justice Department nayo inaongozwa na ngozi nyeusi. State Department nayo ishaongozwa na ngozi nyeusi.
Rangi ya ngozi siyo dili. Ni ujuha tu kung'ang'ania dhana zilizokwishapitwa na wakati.