Diamond ni Balozi mzuri, asemehewe

Mshana Jr

Platinum Member
Aug 19, 2012
269,634
697,845
Natambua wazi alijiharibia pakubwa alipojiunga na KAYAFA kupitia kazi zake. Na niliwahi kuandika uzi kumhusu yeye na Konde boy kwamba kitendo hicho kina athari kisanii huko mbeleni.

Kuna ambao walinibeza sana lakini always muda ni hakimu wa haki na kamwe maandishi hayafutiki!

Hapa nisiwazungumzie haters wa kawaida wa Diamond. Huwezi kupendwa na kila mtu wala huwezi kuchukiwa na kila mtu. Wala nisiwazungumzie wale haters ambao kwa kushindwa kwao kimaisha basi hasira zao zote wanazihamishia kwa waliofanikiwa.

Hapa tujadiliane na wenye hoja kwa muktadha wa Tanzania kama taifa lililopitia madhila makubwa chini ya mkono dhalimu wa mtu mmoja tu. Huyu ndio alimponza Diamond!

Sometimes ni lazima kuambiana ukweli hata kama ukweli huo hatutaki kuusikia na hauna ladha wala mvuto! Kuna wakati ukweli huwa mchungu kama pakanga!

Ni ukweli usiopingika kwamba:-

- Diamond ndio msanii mwenye mafanikio zaidi kwa sasa Tanzania

- Diamond ndio msanii tajiri zaidi kwasasa Tanzania

- Diamond ndio msanii aliyetangaza mziki wa bongo ndani na nje ya nchi kuliko mwanamuziki mwingine yeyote wa bongo fleva

- Kupitia kazi zake ameweza kuitangaza Tanzania pakubwa sana Duniani

- Amekuwa ni balozi wetu kwenye tasnia ya sanaa ya mziki nje ya mipaka ya Tanzania!

Kwenye mashindano kuna washindi na washindwa! Diamond kashindwa. Na sababu za kushindwa zipo nyingi. Hata kama tutakataa ile kampeni ya watu wa jamhuri ya Twitter lakini ilichagiza pakubwa mno kudhoofisha ushindi wake!

Ana la kujifunza kubwa sana hapa. Hasa kama asiposhupaza shingo!

Mashindano yameisha! Na Diamond kashindwa sasa ni wakati wa marejeo.. Haters wake ni vifijo na nderemo kila kona! Sasa wanaenda mbali zaidi! Wanamdiss na kumdhihaki mavazi aliyovaa siku ya shindano.

Tukiwa na Tafakuri hatupaswi kumbeza wala kumcheka! Angevaa nini sasa ili amridhishe kila mmoja? Chochote ambacho angevaa kingekosolewa na kusifiwa kwa wakati mmoja! Watanzania hatuna vazi rasmi la taifa. Vazi la kimasai kwa sehemu kubwa ndio huchukuliwa kama utambulisho wa taifa.

Ubunifu wa Diamond kuvalia 'kimasai' ni wa kupongezwa japo umekutana na ukosolewaji mkubwa mitandaoni.. Lakini tukumbuke jambo moja muhimu sana. Diamond hakwenda kwenye shughuli ya kitamaduni bali kisanii. Hivyo nakshi na vionjo alivyoongeza kwenye lile vazi vilikuwa vya kisanii zaidi kuliko kuzingatia mila na tamaduni za kimasai. ASAMEHEWE!

Mwisho kabisa:

Pamoja na mashindano haya kuendelea kumpa Diamond mileage kimataifa na kuzidi kuitangaza Tanzania hata kama kakosa tuzo! Lakini ni muda sahihi kwake sasa kujirudi na kujitafakari upya! Pamoja na kuwa na haki ya kisiasa ya kuchagua chama cha siasa apendacho. Lakini kama msanii anatakiwa kuwa mwerevu sana linapokuja suala la kuwagawa mashabiki wake kwa mitazamo yake kisiasa.

Kazi yake ma mashabiki wake ni muhimu sana kuliko mapenzi yake kwa watawala wa kisiasa!

DIAMOND IKIKUPENDEZA OMBA RADHI
 
Kwa mara ya kwanza leo naona nitaenda tofauti na wewe.

Mengi umesema ya kweli, lakini kuhusu kumsamehe itakuwaje asamehewe wakati yeye bado kakomaza shingo hataki kukubali kuwa alitumia umaarufu wake kumuunga mkono mtu aliyekuwa anakandamiza na kuua washabiki wake na Watanzania wengine.

Shida kubwa ya Diamond ni kukosa timu ya washauri wazuri na kuendesha shughuli zake kwa kufuata mirindimo ya Kiki na wapambe mbuzi.

Hivi ndugu yangu Mshana Jr kwani mashambilizi yalipoanza kuhusu BETAwards angejitokeza na kuomba radhi kwa maneno machache;

"Nadhani kuna mahali nilikosea washabiki wangu na wasio washabiki, Nisameheni nawapenda sana" unadhani nani angeendelea kumsema?

Hivyo nami nikiona kejeli kwake nitaishia kucheka tuu kwani bado hajatambua kosa lake na anaendelea na kiburi.

20210629_044721.jpg
 
Kwa siasa nilizoziona awamu ya tano zilikuwa za hovyo sana, akina diamond na wasani wengine nadhani walifuata upepo wa siasa zilivyokuwa. Kama mwendazake angelikutaka umsaidie kupiga kampeni kupitia sanaa sidhani kama wengeliktaaa, na kama angelikataa ubabe ungelitumika kubambikiza makosa ya jinai.

Nitakupa mfano mdogo, Mimi niligombea uongozi wa CWT ngazi ya wilaya mwezi machi mwaka Jana 2020, niliitwa kwenye kamati ya ulinzi na usalama chini ya DC, Emmanuel kipole, niliombwa kadi ya CCM na bahati mbaya sikuwa nayo, nilitafutiwa zengwe nikakamatwa kuwa natoa rushwa, lakini nikakubali mapambano, siku ya uchaguzi kikakatwa tena, kwa amri ya DC na akaandika barua kwa msimamizi wa uchaguzi akigushi saini yangu kuwa nimejitoa kwenye uchaguzi.

Uchaguzi ukafanyika huku nikiwa nieshikiliwa, na jina likiwa limeondolewa kwenye ballot paper.

Kwa aina ya uongozi ulivyokuwa ki ukweli wasanii wote walienda kule bila kupenda, Bali kwa hofu tu.
 
Asamehewe kwa lipi? Kwani ameomba radhi?
Kusamehewa huja baada ya mtu kuomba radhi, unashauri vipi mtu aanze kusamehewa kabla haujawekeza kwenye kushauri aombe radhi (kwa mujibu wa thread tittle)
Sometimes msahama si lazima mtu akuombe radhi..mbona tunakosewa na kusamehe daily bila kuombwa radh?
 
Natambua wazi alijiharibia pakubwa alipojiunga na KAYAFA kupitia kazi zake.. Na niliwahi kuandika uzi kumhusu yeye na Konde boy kwamba kitendo hicho kina athari kisanii huko mbeleni
Kuna ambao walinibeza sana lakini always muda ni hakimu wa haki na kamwe maandishi hayafutiki!
Hapa nisiwazungumzie haters wa kawaida wa Diamond! Huwezi kupendwa na kila mtu wala huwezi kuchukiwa na kila mtu..!!!
Asamehewe kwa lipi? Baada ya kuona mmemshindwa kum-disqualify kwa petition mnaanza tunga asamehewe? Kawaomba msamaha? Huyu kijana aendelee kukaza nati hadi watu wanyooke kama rula...
 
Kwa mara ya kwanza leo naona nitaenda tofauti na wewe.
Mengi umesema ya kweli, lakini kuhusu kumsamehe itakuwaje asamehewe wakati yeye bado kakomaza shingo hataki kukubali kuwa alitumia umaarufu wake kumuunga mkono mtu aliyekuwa anakandamiza na kuua washabiki wake na Watanzania wengine.
Shida kubwa ya Diamond ni kukosa timu ya washauri wazuri na kuendesha shughuli zake kwa kufuata mirindimo ya Kiki na wapambe mbuzi.
Hivi ndugu yangu Mshana Jr kwani mashambilizi yalipoanza kuhusu BETAwards angejitokeza na kuomba radhi kwa maneno machache;
"Nadhani kuna mahali nilikosea washabiki wangu na wasio washabiki, Nisameheni nawapenda sana" unadhani nani angeendelea kumsema?
Hivyo nami nikiona kejeli kwake nitaishia kucheka tuu kwani bado hajatambua kosa lake na anaendelea na kiburi.
View attachment 1834181
Asante Chakaza natambua mawazo yako na kuyathamini .. Unawakilisha wengi tulioumizwa na matendo ya kayafa.. Na ndio maana nikamalizia kwa kumuasa Diamond aombe radhi...AKIPENDA NA AKIJISIKIA LAKINI! Kama hana maono kimo cha mbilikimo
 
Asamehewe kwa lipi? Baada ya kuona mmemshindwa kum-disqualify kwa petition mnaanza tunga asamehewe? Kawaomba msamaha?
Huyu kijana aendelee kukaza nati hadi watu wanyooke kama rula...
Pole naona umekurupuka usingizini ukakimbilia JF
 
Natambua wazi alijiharibia pakubwa alipojiunga na KAYAFA kupitia kazi zake.. Na niliwahi kuandika uzi kumhusu yeye na Konde boy kwamba kitendo hicho kina athari kisanii huko mbeleni
Kuna ambao walinibeza sana lakini always muda ni hakimu wa haki na kamwe maandishi hayafutiki!
Hapa nisiwazungumzie haters wa kawaida wa Diamond! Huwezi kupendwa na kila mtu wala huwezi kuchukiwa na kila mtu..!!! Wal

Mkuu siyo "tujipange kumwombea mzee baba msamaha ambaye leo hana nafasi hiyo?" - maneno haya yake Nigrastratatract si ya kubeza:

IMG_20210629_064224_125.jpg


"Sisi ni wamoja!" -- Alizoeleka kusikika mzee baba.

Hata bwana Chuck Norris alizoeleka katika kujikita kuwapigania wale ambao hawakuweza kupambana wenyewe.
 
Amefanya vzr Kwenye kuitangaza Tanzania n.a. utamaduni wetu n.a amekuwa Balozi mzur . Kwenye shuka kumekosekana visit tz home of kilmanjar and serenget.n.a. Tanzanite nying angeweka shingon.
 
Natambua wazi alijiharibia pakubwa alipojiunga na KAYAFA kupitia kazi zake.. Na niliwahi kuandika uzi kumhusu yeye na Konde boy kwamba kitendo hicho kina athari kisanii huko mbeleni
Kuna ambao walinibeza sana lakini always muda ni hakimu wa haki na kamwe maandishi hayafutiki!
Ukweli mchungu.....
Hapa ni siasa za upande mmoja na chuki za makundi...

Kwa upande wa siasa.

BAVICHA wanashangilia kufeli kwa Almasi.
Ila... Almasi ingekuwa upande wa BAVICHA , hizi kelele zingekuwa za makundi tu (Team sijui nani.....).

Nafahamu kuwa, kukemea kilicho kibaya si lazima uwe na chama bali position ulinayo kwenye jamii inatosha.

Tanzania ina mastaa wengi, na ukiacha Ney wa mitego na Roma, hakuna mwingine aliwahi kukemea uovu.

Ila angalia kilicho mkuta Roma, na raia wote waliufyata. Roma hadi leo anarukaruka tu..(rudi home Roma).

Angalia kilicho mkuta Ney, bahati yake Hayati alimtetea, ila angekaza mda huu Ney angekuwa kwenye list ya wafungwa walio samehewa na Samia.

Yote hayo na mengine mengi yalitokea ila kwa unafki wetu tulijichimbia majumbani na nyuma ya keyboard tukiandika #AACHIWE.

Maneno bila vitendo ni uoga, na ukijulikana kuwa wewe ni muoga utachezewa tu Kwa sababu utaongea yataisha.

Almasi huo ujinga ndio hataki kabisa, na sio almasi tu bali wasanii wengi wako hivyo.

Kwa ufupi tu....
Mazingira hayakumruhusu Almasi kukemea, na hayo mazingira yalitengenezwa na hao wanao hitaji kusemewa.

IKUMBUKWE.
Watanzania ni wanafki, huwa hatuchelewi kumgeuka mtu.
 
Ukweli mchungu.....
Hapa ni siasa za upande mmoja na chuki za makundi...

Kwa upande wa siasa.

BAVICHA wanashangilia kufeli kwa Almasi.
Ila... Almasi ingekuwa upande wa BAVICHA , hizi kelele zingekuwa za makundi tu (Team sijui nani.....).

Nafahamu kuwa, kukemea kilicho kibaya si lazima uwe na chama bali position ulinayo kwenye jamii inatosha.

Tanzania ina mastaa wengi, na ukiacha Ney wa mitego na Roma, hakuna mwingine aliwahi kukemea uovu.

Ila angalia kilicho mkuta Roma, na raia wote waliufyata. Roma hadi leo anarukaruka tu..(rudi home Roma).

Angalia kilicho mkuta Ney, bahati yake Hayati alimtetea, ila angekaza mda huu Ney angekuwa kwenye list ya wafungwa walio samehewa na Samia.

Yote hayo na mengine mengi yalitokea ila kwa unafki wetu tulijichimbia majumbani na nyuma ya keyboard tukiandika #AACHIWE.

Maneno bila vitendo ni uoga, na ukijulikana kuwa wewe ni muoga utachezewa tu Kwa sababu utaongea yataisha.

Almasi huo ujinga ndio hataki kabisa, na sio almasi tu bali wasanii wengi wako hivyo.

Kwa ufupi tu....
Mazingira hayakumruhusu Almasi kukemea, na hayo mazingira yalitengenezwa na hao wanao hitaji kusemewa.

IKUMBUKWE.
Watanzania ni wanafki, huwa hatuchelewi kumgeuka mtu.
Ulikuwa na hoja nzuri sana lakini ukaharibu hapa
BAVICHA wanashangilia kufeli kwa Almasi.
Ila... Almasi ingekuwa upande wa BAVICHA , hizi kelele zingekuwa za makundi tu (Team sijui nani.....).
 
Ulikuwa na hoja nzuri sana lakini ukaharibu hapa
BAVICHA wanashangilia kufeli kwa Almasi.
Ila... Almasi ingekuwa upande wa BAVICHA , hizi kelele zingekuwa za makundi tu (Team sijui nani.....).
Almasi alishapewa tuzo ya kofia na mwendazake,inamtosha Sana hio.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom