Diamond amzawadia Gari mzee Gurumo

Diamond amzawadia Gari mzee Gurumo

kokotoa

Senior Member
Joined
Aug 15, 2009
Posts
109
Reaction score
114
Mwanamuziki wa kizazi kipya diamond,kamkabidhi gari kama zawadi ya kustaafu mzee gurumo.

source:StarTV
 
safi,amefanya jambo jema,sikuwa mshabiki wa diamond lkn sasa namkubali,na nimemgundua ana akili kuliko watu niliowatarajia wanaofanya kazi.Gari sawa,lkn mzee gurumo anaonekana hali ya uchumi c nzuri sasa cjui swala la mafuta,na service ya gari itkuwaje?ni changamoto kwake.Na wasanii wengine wnye mafanikio wafanya kama diamond,warudishe kidogo walichonacho kwenye jamii
 
Sound good! especially for things done to the needy. On the other hand you may start thinking this noble course as Placement, layering ........ should I add Integration? Does someone think the same as I do? connect the dots... you may see the FIU at the end of the tunnel.
 
Safi sana, dogo Diamond.
..Hakuna safi sana hapo. Huyo mzee amefanya kazi ya muziki kwa miaka 53 kama ajira yake aliwajibika kutafuta hiyo gari kwa jasho lake. Sio kuja kulialia eti anastaafu muziki hana hata baiskeli. We mwajiri wako unamfanyia kazi anakulipa mshahara usipopanga mipango yako usitarajie ukistaafu kazi umlaumu au ulaumu umma kuwa kwa miaka uliyofanya kazi hujafanya jambo la maana. Kwanza atakuwa na uwezo wa kulihudumia hilo gari au Diamond atamuwekea na mafuta,bima, service etc etc? Haijatulia kabisa.
 
Safi sana dogo,usijali kuna watu watakuja na kukubeza lakini usife moyo mzee ngurumo amefanya muziki kwa muda mrefu lakin mapato ya bendi yameliwa na wachache kama ishu ya bib kidude tu ikiwezekana angalia na jinsi ya kumfungulia biashara
 
Inaelekea wengi wetu hatutaki kuelewa kuwa wanamuziki na wasanii kama Mzee Gurumo walifanyakazi kwa bidii wakati ambapo sanaa ilikuwa hailipi kama sasa. Akina Gurumo waliwika sana miaka iliyopita lakini walichoweza kufanya ni kuweka chakula mezani. Ilikuwa ni ndoto kwa mwanamuziki kumiliki gari au nyumba ingawa baadhi, kama Mzee Gurumo, walifanikiwa kujenga vibanda baada ya kujinyima sana. Hali ni tofauti kabisa miaka hii ambapo wasanii wakubwa kama Diamond wanalipwa hadi shilingi milioni 20 kwa shoo moja. Miaka hii ukiwa na kipaji na bahati na ukikubalika basi ni rahisi sana kuwa tajiri na tuna mifano kama Diamond na Lady Jay Dee. Vipaji sasa vinalipa. Watu kama Mbaraka Mwinshehe, Marijani Rajab na Hemed Maneti wamekufa masikini sio kwa sababu hawakujipanga, bali waliishi kipindi kibaya (they lived at the wrong time). Nimeguswa na kitendo cha Diamond kwa sababu huyu ni kijana mdogo aliyezaliwa wakati safari ya Mzee Gurumo katika muziki ikielekea ukingoni lakini ameweza kutambua mchango mkubwa wa mzee huyu katika muziki wa Tanzania na Afrika kwa ujumla. Kama hatutaki kumsaidia mzee wa watu tukae kimya badala ya kumkashifu.
 
Back
Top Bottom