Dhana na maisha kama safari ya kumbukumbu

Dhana na maisha kama safari ya kumbukumbu

Bano faith

Member
Joined
Jun 16, 2025
Posts
6
Reaction score
6
DHANA YA MAISHA KAMA SAFARI YA KUMBUKUMBU.
Ikiwa maisha ni mkusanyiko wa kumbukumbu, basi kuishi ni kukumbuka. Na kama mwanadamu amezaliwa na kumbukumbu za maisha ya nyuma, basi kuishi ni kuendeleza mfuatano wa kumbukumbu hizo. Kifo basi si mwisho wa uhai tu, bali ni mwisho wa uwezo wa kukumbuka -kama vile gari linavyosimama baada ya mafuta kuisha.

2. KIFO KAMA FORMAT YA KUMBUKUMBU.
Kwa mantiki hii, kifo kinaweza kuonekana kama mfumo wa asili wa kuanzisha upya kumbukumbu. Kama kumbukumbu zimefikia kikomo au zimejaa, basi kifo hutokea kuruhusu mwanzo mpya au nafsi kurudi tena ikiwa safi (idea ya reincarnation).

3. KUMBUKUMBU KAMA KIINI CHA UTAMBULISHO:
Ikiwa kumbukumbu ndizo zinatufanya kuwa sisi, basi kupotea kwa kumbukumbu ni sawa na kupotea kwa nafsi. Kwa hiyo, wakati kumbukumbu zinapoisha kabisa, nafsi pia hufa—na hivyo kifo ni matokeo ya mwisho wa utambulisho wa nafsi.

4. ULINGANIFU NA TEK NOLOJIA (kwa mfano, simu au kompyuta):
Kama kumbukumbu ni ‘storage’, basi kujaa kwa ‘storage’ au kufeli kwake kunaweza kusababisha mfumo mzima kufa au kusitisha kazi. Kifo cha mwanadamu basi kinakuwa ni kama ‘shutdown’ ya kifaa kutokana na kuharibika au kuisha kwa kumbukumbu.

Kwa kifupi:
Unapoweka hoja hii kifalsafa, unaweza kusema:
Kumbukumbu ni mwendelezo wa maisha, na maisha ni mwendelezo wa kumbukumbu. Kifo kinapotokea, huenda ni kwa sababu chanzo kikuu cha kumbukumbu—nafsi—imefikia kikomo chake cha uwezo wa kukumbuka, hivyo inazimika kama taa bila mafuta.

HOJA MPYA YA MWAKA 2025: DHANA MPYA YA UHAI NA KIFO – “MWISHO WA KUMBUKUMBU, MWANZO WA KIFO”
Na: BANO

“Ikiwa mwanadamu alizaliwa akiwa na kumbukumbu ya maisha ya nyuma, basi je, kifo chake si matokeo ya mwisho wa uwezo wa kukumbuka?”

Katika falsafa hii, Bano anawasilisha dhana kwamba maisha ya binadamu hayajengwi tu na pumzi au mapigo ya moyo, bali na mkusanyiko wa kumbukumbu. Kila tukio, hisia, na uzoefu hujaza hifadhi ya kipekee ndani ya nafsi ya binadamu.

Kifo, kwa mtazamo huu, siyo tu mwisho wa mwili—bali ni mwisho wa safari ya kumbukumbu. Nafsi inapofikia kiwango cha mwisho cha kukumbuka, uhai unazimika, kama taa yenye mafuta yaliyokwisha.

Hii hoja inabeba changamoto kwa sayansi, roho, na teknolojia, ikileta swali la msingi: Je, maisha ni kumbukumbu pekee?

Bano anawaita wanafalsafa wa leo kuchunguza zaidi:

Je, tunapoishi tunajaza kumbukumbu, au tunaitafuta nafsi kwa njia ya kukumbuka?

Na zaidi: Je, kifo ni mwisho au mwanzo wa kusahaulika?

"Karibu kwenye falsafa ya Bano – fikra mpya za kizazi cha kufikiri kwa kina."
 
Kwa mantiki hii, kifo kinaweza kuonekana kama mfumo wa asili wa kuanzisha upya kumbukumbu. Kama kumbukumbu zimefikia kikomo au zimejaa, basi kifo hutokea kuruhusu mwanzo mpya au nafsi kurudi tena ikiwa safi (idea ya reincarnation).
Vipi kwa watoto wanaokufa wakiwa wadogo labda miaka 3 hivyo kumbukumbu zao ndio zimefika kikomo muda huo, au tuseme kama binadamu akifanikiwa kujua kuzuia aging na kuishi milele hivyo nafsi haitajaa kumbu kumbu.

Kwenye Law of thermodynamics wanasema in a closed system you eventually die, hivyo kama tukifanikiwa ku open the box na energy ikawa ina flow toka nje theoriticaly tunaweza kuishi milele, scientifically aging ni kama error imetokea kwenye mitochondria cell kama engine ya mwili, ikifanyika genetic coding ya kuzia hiyo error theoritically tunaweza ishi milele

Hivyo kama tukifanikiwa hivyo kifo kitakuwa hakina maana, na kama kifo kisipokuwa na maana basi kumbu kumbu za kuishi zitapoteza pia maana, sababu neno kumbu kumbu linafanya kazi kama past tense baada ya mtu kupotezana na mtu wa karibu aidha kwa kusafiri au kufa ila kufa ndio nyenzo kubwa ya kuleta maana ya neno kumbu kumbu
 
DHANA YA MAISHA KAMA SAFARI YA KUMBUKUMBU.
Ikiwa maisha ni mkusanyiko wa kumbukumbu, basi kuishi ni kukumbuka. Na kama mwanadamu amezaliwa na kumbukumbu za maisha ya nyuma, basi kuishi ni kuendeleza mfuatano wa kumbukumbu hizo. Kifo basi si mwisho wa uhai tu, bali ni mwisho wa uwezo wa kukumbuka -kama vile gari linavyosimama baada ya mafuta kuisha.

2. KIFO KAMA FORMAT YA KUMBUKUMBU.
Kwa mantiki hii, kifo kinaweza kuonekana kama mfumo wa asili wa kuanzisha upya kumbukumbu. Kama kumbukumbu zimefikia kikomo au zimejaa, basi kifo hutokea kuruhusu mwanzo mpya au nafsi kurudi tena ikiwa safi (idea ya reincarnation).

3. KUMBUKUMBU KAMA KIINI CHA UTAMBULISHO:
Ikiwa kumbukumbu ndizo zinatufanya kuwa sisi, basi kupotea kwa kumbukumbu ni sawa na kupotea kwa nafsi. Kwa hiyo, wakati kumbukumbu zinapoisha kabisa, nafsi pia hufa—na hivyo kifo ni matokeo ya mwisho wa utambulisho wa nafsi.

4. ULINGANIFU NA TEK NOLOJIA (kwa mfano, simu au kompyuta):
Kama kumbukumbu ni ‘storage’, basi kujaa kwa ‘storage’ au kufeli kwake kunaweza kusababisha mfumo mzima kufa au kusitisha kazi. Kifo cha mwanadamu basi kinakuwa ni kama ‘shutdown’ ya kifaa kutokana na kuharibika au kuisha kwa kumbukumbu.

Kwa kifupi:
Unapoweka hoja hii kifalsafa, unaweza kusema:
Kumbukumbu ni mwendelezo wa maisha, na maisha ni mwendelezo wa kumbukumbu. Kifo kinapotokea, huenda ni kwa sababu chanzo kikuu cha kumbukumbu—nafsi—imefikia kikomo chake cha uwezo wa kukumbuka, hivyo inazimika kama taa bila mafuta.

HOJA MPYA YA MWAKA 2025: DHANA MPYA YA UHAI NA KIFO – “MWISHO WA KUMBUKUMBU, MWANZO WA KIFO”
Na: BANO

“Ikiwa mwanadamu alizaliwa akiwa na kumbukumbu ya maisha ya nyuma, basi je, kifo chake si matokeo ya mwisho wa uwezo wa kukumbuka?”

Katika falsafa hii, Bano anawasilisha dhana kwamba maisha ya binadamu hayajengwi tu na pumzi au mapigo ya moyo, bali na mkusanyiko wa kumbukumbu. Kila tukio, hisia, na uzoefu hujaza hifadhi ya kipekee ndani ya nafsi ya binadamu.

Kifo, kwa mtazamo huu, siyo tu mwisho wa mwili—bali ni mwisho wa safari ya kumbukumbu. Nafsi inapofikia kiwango cha mwisho cha kukumbuka, uhai unazimika, kama taa yenye mafuta yaliyokwisha.

Hii hoja inabeba changamoto kwa sayansi, roho, na teknolojia, ikileta swali la msingi: Je, maisha ni kumbukumbu pekee?

Bano anawaita wanafalsafa wa leo kuchunguza zaidi:

Je, tunapoishi tunajaza kumbukumbu, au tunaitafuta nafsi kwa njia ya kukumbuka?

Na zaidi: Je, kifo ni mwisho au mwanzo wa kusahaulika?

"Karibu kwenye falsafa ya Bano – fikra mpya za kizazi cha kufikiri kwa kina."
Kumbukumbu zikiisha na mtu anakufa hii hoja sidhani kama ni kweli kwasababu unapozaliwa huwi na chochote unachokumbuka hapa duniani na badala yake kumbukumbu hujengwa kwa kuona kuskia kusoma na hata kujifunza kwa vitendo.

Kwahiyo kadri unavyoishi ndivyo unavyojifunza mambo mapya pamoja na historia ya yale ambayo yaliwahi kuwako na ufadhi wa mambo hayo kichwani mwako ndio hutengeneza kumbukumbu.

Mtu ambae hawezi kukumbuka vitu anarudi katika hali ya utoto na muunganiko wake na dunia unapotea ila hawezi akapoteza uhai kwakua kumbukumbu zimefutika ndani yake.
 
Kumbukumbu zikiisha na mtu anakufa hii hoja sidhani kama ni kweli kwasababu unapozaliwa huwi na chochote unachokumbuka hapa duniani na badala yake kumbukumbu hujengwa kwa kuona kuskia kusoma na hata kujifunza kwa vitendo.

Kwahiyo kadri unavyoishi ndivyo unavyojifunza mambo mapya pamoja na historia ya yale ambayo yaliwahi kuwako na ufadhi wa mambo hayo kichwani mwako ndio hutengeneza kumbukumbu.

Mtu ambae hawezi kukumbuka vitu anarudi katika hali ya utoto na muunganiko wake na dunia unapotea ila hawezi akapoteza uhai kwakua kumbukumbu zimefutika ndani yake.
Binadamu hufikiri kuwa maisha huanza pale anapozaliwa, na hufa pale pumzi inapotoweka. Lakini mtazamo huu ni mwembamba. Kwa sababu, je, tungeuliza: ni kwa nini mtoto anapozaliwa hulia? Haoni, hasikii, hajui jina lake—lakini ana hofu, huzuni au hamu ya kujificha kwenye kifua cha mama. Hisia hizi hazijafundishwa; ni mizizi ya kumbukumbu ambayo haikupitia kalamu ya dunia. Hii ni kumbukumbu ya nafsi, iliyo chini ya utambuzi, sehemu ya "subconscious" iliyo ya kale kuliko lugha, na pana kuliko fahamu ya kawaida.

Kwa hiyo, kifo hakiwezi kuwa tu mwisho wa mwili, bali ni ukomo wa uwezo wa nafsi kuwasiliana kupitia mwili. Pale ambapo kumbukumbu ya fahamu (conscious memory) inapofifia kama vile kwa mzee anayeanza kupoteza kumbukumbu muunganiko wa nafsi na mwili huanza kuyeyuka. Huo ndio mwanzo wa mwisho.

Katika maana hii, maisha ni mwendelezo wa hisia zisizoandikwa; ni somo ambalo linaendelea kujifunza kupitia miili ya muda, hadi litatimiza ukamilifu wake. Kifo ni kuendelea kwa safari hiyo, si mwisho wake.

Nafsi haikumbuki kwa akili, inahisi kwa ukimya.
 
je, tungeuliza: ni kwa nini mtoto anapozaliwa hulia? Haoni, hasikii, hajui jina lake—lakini ana hofu, huzuni au hamu ya kujificha kwenye kifua cha mama. Hisia hizi hazijafundishwa; ni mizizi ya kumbukumbu ambayo haikupitia kalamu ya dunia. Hii ni kumbukumbu ya nafsi, iliyo chini ya utambuzi, sehemu ya "subconscious" iliyo ya kale kuliko lugha, na pana kuliko fahamu ya kawaida.
kuna njia nyingi za mtu ku express hisia zake, na kitu pekee kwa mtoto mchanga anachoweza kufanya ku express hisia zake ni kulia, hivyo mtoto analia sababu anahisi amekuja kwenye mazingira ambayo hajazoea hivyo kulia ni kama njia yake ya kuongea, na animal instinct ni kuwa tukiwa na hofu tunafanya vitu viwili fight or flight, hawezi kupigana na hawezi kukimbia bali anahitaji kujificha na sehemu pekee salama ni kwa mtu anayehisi ndio alikuwa host wake, mtoto anasikia punde tu anavyozaliwa na my guess huwa huenda mapigo yake ya moyo na ya host wake huwa yapo sychronized hivyo anavyosikia mapigo ya moyo ambayo yupo familiar nayo hujihisi salama na amani.

Genetics haibebi tu tabia na sifa tofauti za mwanadamu toka kwa wazazi wake bali pia sifa zote za species jinsi gani species yake inavyo act and react, ingawa napenda sana idea ya genetic memory ila nahisi hizo huwa kushare kwa sifa na tabia za mtu toka kwa wazazi wake na ancestors wake pia na sifa zote species aliyozaliwa nayo wala sidhani kam ni kumbu kumbu
 
Binadamu hufikiri kuwa maisha huanza pale anapozaliwa, na hufa pale pumzi inapotoweka. Lakini mtazamo huu ni mwembamba. Kwa sababu, je, tungeuliza: ni kwa nini mtoto anapozaliwa hulia? Haoni, hasikii, hajui jina lake—lakini ana hofu, huzuni au hamu ya kujificha kwenye kifua cha mama. Hisia hizi hazijafundishwa; ni mizizi ya kumbukumbu ambayo haikupitia kalamu ya dunia. Hii ni kumbukumbu ya nafsi, iliyo chini ya utambuzi, sehemu ya "subconscious" iliyo ya kale kuliko lugha, na pana kuliko fahamu ya kawaida.

Kwa hiyo, kifo hakiwezi kuwa tu mwisho wa mwili, bali ni ukomo wa uwezo wa nafsi kuwasiliana kupitia mwili. Pale ambapo kumbukumbu ya fahamu (conscious memory) inapofifia kama vile kwa mzee anayeanza kupoteza kumbukumbu muunganiko wa nafsi na mwili huanza kuyeyuka. Huo ndio mwanzo wa mwisho.

Katika maana hii, maisha ni mwendelezo wa hisia zisizoandikwa; ni somo ambalo linaendelea kujifunza kupitia miili ya muda, hadi litatimiza ukamilifu wake. Kifo ni kuendelea kwa safari hiyo, si mwisho wake.

Nafsi haikumbuki kwa akili, inahisi kwa ukimya.
Hapa nadhani umeelezea vizuri lengo la hili andiko lako. Hii inamaana kwamba ubongo ambao ndio unaotunza kumbukumbu ndio ambao humuunga mtu na ulimwengu kwa ujumla katika namna ya mwili ila ukiachana na ubongo wenye kumbukumbu ila ipo nafsi au roho ambayo hii hubeba kumbukumbu za kale (hapa kwenye huo mfano wa mtoto mchanga na kujificha au kulia au kutabasamu na kadhalika ilihali hawana kumbukumbu yoyote ya kidunia).

So unaamini kwamba mwili unaweza kutengana na nafsi ila nafsi inaweza ikapata mwili mwingine na kurudi tena katika mzunguko wa kidunia?

Unaamini kwamba nafsi iliyondani ya mwili mpya inaweza ikawa na kumbukumbu za kale ndio maana mtoto licha ya kukosa kumbukumbu za kidunia ila bado anaweza kufanya hayo mambo tajwa hapo juu?
 
kuna njia nyingi za mtu ku express hisia zake, na kitu pekee kwa mtoto mchanga anachoweza kufanya ku express hisia zake ni kulia, hivyo mtoto analia sababu anahisi amekuja kwenye mazingira ambayo hajazoea hivyo kulia ni kama njia yake ya kuongea, na animal instinct ni kuwa tukiwa na hofu tunafanya vitu viwili fight or flight, hawezi kupigana na hawezi kukimbia bali anahitaji kujificha na sehemu pekee salama ni kwa mtu anayehisi ndio alikuwa host wake, mtoto anasikia punde tu anavyozaliwa na my guess huwa huenda mapigo yake ya moyo na ya host wake huwa yapo sychronized hivyo anavyosikia mapigo ya moyo ambayo yupo familiar nayo hujihisi salama na amani.

Genetics haibebi tu tabia na sifa tofauti za mwanadamu toka kwa wazazi wake bali pia sifa zote za species jinsi gani species yake inavyo act and react, ingawa napenda sana idea ya genetic memory ila nahisi hizo huwa kushare kwa sifa na tabia za mtu toka kwa wazazi wake na ancestors wake pia na sifa zote species aliyozaliwa nayo wala sidhani kam ni kumbu kumbu
Ingekua ni kumbukumbu nadhani zingekua na muendelezo kwasababu mtu ukimuonesha kitu ambacho yupo familia nacho ila ikatokea kuna namna amepoteza kumbukumbu juu yake kama aliinteract nacho hapo kabla kwa kadri unavyomkumbusha au kinavyobehave anakua anarudisha zile memory zake na kuanza kukumbuka na sometimes kutabiri hata next move ya kitu hiko ya kwamba itakua hii au ile.

Lakini kwa watoto hakuna hali ya namna hii so ni ngumu kuamini kama zile ni kumbukumbu za kale.
 
Ingekua ni kumbukumbu nadhani zingekua na muendelezo kwasababu mtu ukimuonesha kitu ambacho yupo familia nacho ila ikatokea kuna namna amepoteza kumbukumbu juu yake kama aliinteract nacho hapo kabla kwa kadri unavyomkumbusha au kinavyobehave anakua anarudisha zile memory zake na kuanza kukumbuka na sometimes kutabiri hata next move ya kitu hiko ya kwamba itakua hii au ile.

Lakini kwa watoto hakuna hali ya namna hii so ni ngumu kuamini kama zile ni kumbukumbu za kale.
Hakika 💯
 
kuna njia nyingi za mtu ku express hisia zake, na kitu pekee kwa mtoto mchanga anachoweza kufanya ku express hisia zake ni kulia, hivyo mtoto analia sababu anahisi amekuja kwenye mazingira ambayo hajazoea hivyo kulia ni kama njia yake ya kuongea, na animal instinct ni kuwa tukiwa na hofu tunafanya vitu viwili fight or flight, hawezi kupigana na hawezi kukimbia bali anahitaji kujificha na sehemu pekee salama ni kwa mtu anayehisi ndio alikuwa host wake, mtoto anasikia punde tu anavyozaliwa na my guess huwa huenda mapigo yake ya moyo na ya host wake huwa yapo sychronized hivyo anavyosikia mapigo ya moyo ambayo yupo familiar nayo hujihisi salama na amani.

Genetics haibebi tu tabia na sifa tofauti za mwanadamu toka kwa wazazi wake bali pia sifa zote za species jinsi gani species yake inavyo act and react, ingawa napenda sana idea ya genetic memory ila nahisi hizo huwa kushare kwa sifa na tabia za mtu toka kwa wazazi wake na ancestors wake pia na sifa zote species aliyozaliwa nayo wala sidhani kam ni kumbu kumbu
Asante kwa mtazamo wako mzuri wa kimaumbile na kisayansi. Ni kweli kabisa kwamba kumbukumbu hujengwa kadri mtu anavyoishi, huona, husikia, na kujifunza. Lakini falsafa huenda mbali zaidi ya kile tunachokiona au kupimika kwa akili ya kawaida.

Mtazamo wangu ni huu:
Kumbukumbu si lazima iwe ya tukio halisi lililowahi kutokea kwa mtu binafsi, bali inaweza kuwa ni miitiko ya ndani—hisia, msukumo, au maelekeo fulani ambayo yanamvutia mtu bila sababu ya moja kwa moja.

Mtoto anapolia anapozaliwa, hiyo sauti si tu kuonesha hofu au mshtuko wa mazingira mapya, bali ni ishara ya ndani ya nafsi kutambua kuwa imekatishwa na kitu kikubwa ilichokuwa sehemu yake kile ambacho wengine hukiita chanzo, kiini, au "home beyond time."

Tunapozungumzia "safari ya maisha kama kumbukumbu," hatumaanishi kumbukumbu ya kawaida ya akili ya mwanadamu, bali tunazungumzia kumbukumbu ya nafsi, ya ndani kabisa kama chembe ya uhai inayojua kuwa ipo kwa kusudi fulani.

Kwa hiyo hoja yako ni sahihi kwa upande wa akili, lakini kwa upande wa roho, mtu huweza kuwa na ukaribu na kitu ambacho hajawahi kufundishwa kukikumbuka.
Kumbukumbu ya kale haiwezi kupimwa kwa macho, bali huishi kwenye sauti ya utulivu, katika kilio cha kwanza, na katika ukimya wa nafsi.
 
Ingekua ni kumbukumbu nadhani zingekua na muendelezo kwasababu mtu ukimuonesha kitu ambacho yupo familia nacho ila ikatokea kuna namna amepoteza kumbukumbu juu yake kama aliinteract nacho hapo kabla kwa kadri unavyomkumbusha au kinavyobehave anakua anarudisha zile memory zake na kuanza kukumbuka na sometimes kutabiri hata next move ya kitu hiko ya kwamba itakua hii au ile.

Lakini kwa watoto hakuna hali ya namna hii so ni ngumu kuamini kama zile ni kumbukumbu za kale.
Ni kweli kwamba kumbukumbu nyingi hujengwa kupitia uzoefu unaorudiwa, na ubongo huitikia kwa mazoea hayo. Lakini hoja yangu haijiegemezi kwenye aina ya kumbukumbu inayoitwa "episodic memory" (yaani tukio kwa tukio), bali inachokoza wazo la kwamba nafsi ya binadamu huja ikiwa na hisia, mitazamo, au mwelekeo usio na msingi wa somo lolote alilowahi kusoma.

Kwa mfano: Kwa nini baadhi ya watu hujihisi nyumbani mahali wasipopajua? Kwa nini watoto wengine huogopa maji hata kabla ya kuogelea? Au kwa nini mtu akikiona kitu fulani cha kale labda muziki, maneno, au picha fulani huhisi kama amewahi kukutana nacho? Hii si kumbukumbu inayoishi katika ubongo wa kawaida, bali ni chembechembe ya nafsi inayobeba athari ya safari ndefu ya roho.

Kumbukumbu tunayoizungumzia hapa ni ya aina ya "intuitive knowing" ujuzi usiofundishwa wala kufundishika, bali unaoamshwa. Watoto wanaweza wasioneshe tabia za kuelewa jambo moja kwa moja, lakini bado kuna maeneo ya utambuzi wa ndani ambayo huja na wao kama vile huruma ya asili, hofu ya giza, au kuvutwa na sauti ya mama.
Kwa hiyo hoja yako iko sahihi kwenye uwanja wa neuroscience, lakini katika ulimwengu wa falsafa ya nafsi, tunaamini kwamba sio kila kumbukumbu ina ufuatano wa picha au matukio zingine ni hisia za kale zinazovuka akili ya kawaida.

Kumbukumbu hizi hazikumbukwi kwa macho, bali kwa hisia.
 
Nilichogundua kupitia huu mjadala ni kuwa inawezekana nafsi huingia ndani ya mwili pindi tu kichanga kinavyotoka tumboni na ndio sababu ya kulia kutokana na msukumo wa nishati mpya inayoingia na kustart maisha.
 
Kwa mfano: Kwa nini baadhi ya watu hujihisi nyumbani mahali wasipopajua? Kwa nini watoto wengine huogopa maji hata kabla ya kuogelea? Au kwa nini mtu akikiona kitu fulani cha kale labda muziki, maneno, au picha fulani huhisi kama amewahi kukutana nacho? Hii si kumbukumbu inayoishi katika ubongo wa kawaida, bali ni chembechembe ya nafsi inayobeba athari ya safari ndefu ya roho.
Hii kitu imeshajadiliwa sana humu na kama andiko lako limejikita upande huu basi pia unatakiwa utambue ya kwamba si Kila mtu duniani amewahi kupitia hali kama hii ila wapo watu wachache ambao wamewahi ku, vipi unasemaje hapo?

Sisi watu wa rohoni tunaamini kwamba zipo roho ambazo hutengana na mwili na kurudi tena kwenye mwili mwingine ili ziendelee kuwa katika mzunguko wa kidunia, lakini sio Kila roho au nafsi iliyo ndani ya mtu imewahi kuwa katika mzunguko wa kidunia hapo kabla.

Na kutokana na hiyo point basi utaona kuna ukinzani na hoja yako ya mtoto kulia anapoingia kwenye maji. Lakini kama bado unataka ubaki huko basi yapaswa tujiulize mtoto huanza kutengeneza kumbukumbu na kuhifadhi kwenye ubongo wake na vile vitu anavyo ingiliana navyo tangu wakati gani baada ya kuzaliwa?

Labda ukijibu hili swali tunaweza tukajua kwanini mtoto hulia pale anapowekwa kwenye maji au anapoexperience vitu vipya ambavyo hakupata kukutana navyo hapo kabla.

Kuna sehemu ya andiko lako inaingia moja kwa moja kwenye upande ambao Mimi nauamini ila sehemu pia ya hili andiko haikai na sehemu ambayo haikai ni hapo unapoamini kutokana na nafsi iliyomo ndani ya mtoto kuna kumbukumbu fulani za kale inakua imebeba ndani yake na ndizo hasa zinazopelekea haya mambo(hapa nasema sio kweli) na hii ni kutokana na hoja yangu kutoka hapo kwenye paragraph ya kwanza, lakini pia ukijibu swali nlilokuuliza hapo paragraph ya tatu nahisi tunaweza kuwa pazuri zaidi.
 
Nilichogundua kupitia huu mjadala ni kuwa inawezekana nafsi huingia ndani ya mwili pindi tu kichanga kinavyotoka tumboni na ndio sababu ya kulia kutokana na msukumo wa nishati mpya inayoingia na kustart maisha.
Nafsi ni nini? Labda tukianzia hapa ndio tutapata jibu na hii hoja yako mpya
 
Back
Top Bottom