Dhambi ya kikokotoo cha wastaafu ni mbaya kuliko dhambi ya mauti

kavulata

JF-Expert Member
Aug 2, 2012
12,317
12,617
Mishahara ya watumishi ni midogo saaana kuliko huduma/jasho wanayoitoa kipindi chote Cha ujana yao. Mishahara ya watumishi haiwatoshi kuishi, kuSomesha, na kujenga nyumba. Kima Cha chini cha mfanyakazi ni shilingi 4000 kwa siku nzima wakati kule Marekani ni dollar 8 (TSH 18,400) kwa saa TU. Hii inasababisha mtumishi ashindwe kuishi kwa mshahara lakini akatwe hela kidogo sana kwenye mifuko ya hifadhi ya jamii.

Wastani wa Umri wa kuishi (life expectancy) wa mtanzania ni miaka 55 tu lakini kikokotoo kinamtaka mstaafu anaestaafu akiwa na miaka 60 apewe 33% TU ya hivyo vijisenti vyake alivyokatwa na kuwekewa kwenye mifuko, kisha fedha nyingine apewe kila mwezi kama mshahara.

Kama ni kweli Wastanni wa Umri wa kuishi ni huu Ina maana aliyekuja na Wazo la kikokotoo hiki alidhamilia kuiba fedha za marehemu. Yaani kwa takwimu hizi za umri wa kustaafu ni kwamba watumishi wengi watakufa miaka michache kabla ya kustaafu na wengine watakufa ndani ya miaka 2 baada ya kustaafu. Maana yake wataziacha fedha zao za mafao na kubakia serikalini na kwenye mifuko au kuliwa na wategemezi ambalo sio kusudi la mfanyakazi.

Hii ni dhambi kubwa sana inayoonekana kwa macho, masikio na moyoni kuliko Ile dhambi ya baada ya kufa ambayo hujui kama IPO au haipo.

Hii Ina maana kuwa wastaafu watakaaoishi hadi miaka 80 ni asilimia ndogo sana kiasi cha kustahili kuhalalisha kikokotoo Cha 33%. Yaani huyu mtumishi ameibiwa mshahara halafu anaibiwa mafao yake pia.

Badala ya kutoa elimu kwa watumishi namna ya kujiandaa na kustaafu na namna ya kutumia mafao yake ya kustaafu mnaona njiia pekee ni kumuwekea hela zake. Hii sio sawa, ni dhuluma mbaya sana.

Lakini pia huwa ninajiuliza, kwani wale wastaafu wengine kutoka kwenye kilimo, ufugaji, uvuvi na biashara ambao ndio wengi sana huwa wanawekewa hela zao za uzeeni na nani wapi? Kwani hawa hawaadhiliki uzeeni kwa kukosa kipato? Kwanini huruma zenu ziwe kwa hawa tu wanaowadai hela zao? Hii ni njia ya kukwepa kuwalipa hela zao kwa kusaidiwa na kifo chao.

Wapeni hela zao buana wakafe nazo wenyewe. Na kama watazitumia hovyo basi wataishi kama wazee wenzao wengine wakulima, wafugaji, wavuvi, wakwezi na wawindaji wanavyoishi.
 
Linaonekana kana jambo la 'Ubunifu Uchwara'

Hata hivyo, serikali inapaswa kupunguza gharama, wanapaswa kujaribu njia kama hiyo, ikiwa wameshindwa kubuni na kupanua wigo wa ukusanyaji wa mapato. Wafunge mikanda.
 
Nimetoa machozi!!! Kuna Mzee mmoja alistaafu karibuni, alipoona mafao yake yalivo kidogo, alinyoosha mikono mbinguni mbele za watu. Akasema bora Mungu ungenichukua mapema kabla ya kulipwa senti hizi!
Kama Wana huruma sana na wazee wanaostaafu utumishi Mbona hawawaonei huruma hizo hizo wazee waliostaafu kulima, kufunga, kuvua, kufanya biashara na kukwea minazi?

Hizi ni huruma za wizi, wawape wastaafu hela zao, wapeni watumishi elimu ya kustaafu punde TU wanapoanza kazi wakiwa vijana badala ya kusubiri kuwaonea huruma kwa kuwawekea hela zao. TUCTA nao ni kama mazombie, hawana msaada hawana faida kwa watumishi.
 
Aliyebuni malipo haya ni raisi wa awamu ya ngapi?
Kikokotoo hiki kimebuniwa baada ya mifuko kukopwa sana na serikali, serikali kushindwa kupeleka makato ya watumishi wao kwenye mifuko na mifuko kuanzisha miradi yenye hasara. Dhambi hizi alizianzisha Kikwete. Magufuli alilikuta sakata, alipotaka kuhoji nadhani alionyeshwa gharama za uchaguzi zilizomuingiza madarakani, kimyaaaa!!! Lakini kwa hasira alikisikimamisha kikokotoo Cha 25% na kuwafukuza viongozi wa mifuko na kuitaifisha baadhi ya miradi ya mifuko. Lakini haya yote hayamsaidii mstaafu ambae alipunjwa mshahara na Sasa anapunjwa mafao yake.
 
Mm nadhani serikali imeamua kufanya hivi sababu ya hali ya mifuko yetu haiwezi kujiendesha na ilikuwa inafilisika.

Pia ilikosa pesa za kuwalipa wastaafu wengi.

Ingawa sioni mfumo huu mpya wa kikokotoo km utabadilishwa hivi karibuni sanasana watakuwa wanaongeza hizo percent kulingana na hali za mifuko husika.

NB. Madhara ya hiki kikokotoo cha sasa ni ufisadi na rushwa kwa wafanyakazi kuongezeka sana maan wote wanajua kabisa hata wakistaafu kiinua mgongo vyao havitawatosheleza hivyo wataforce kupata pesa mapema ili wajipange na maisha yao mapema.
 
Back
Top Bottom