Dewji: Hakuna Kitu kinaua Urafiki kama Mikopo!!

"Anakukopa pesa na anakuahidi, atakulipa siku fulani, siku ikifika humuoni! Siku utakayomwona anakueleza matatizo ya uongo! Matatizo ya uongo! Ya uongo eeh! Matatizo ya uongo! Kukopa chumbani kulipa polisi............."
ULALE PAHALA PEMA PEPONI DR. Remmy Ongala
 
Ila ukitaka rafiki asikukope tena, fanya hivi

Akikukopa laki moja, mwambie una 50k.

Alafu ukiona harudishi unamkumbusha akisema hana mpotezee.

Huyo hakukopi tenaaaaaaa!!

Mana akitaka kukopa anajua anadeni kwako.

Sometime natumia mbinu hii kwa wasumbufu
Mimi hutumia njia njia hii pia, imenisaidia kiasi....kiukweli haji kukopa kabisa
 
Sometimes haya maisha unaweza amua tu utafute hela ya kula na kubadili mboga tu af maisha yaendelee..sa kama bilionea moo anapta frustration kisa pesa si hatari.
 
Mimi nimeacha kukopesha. Kama nina nia ya kukusaidia nakwambia. Kwa kuwa umeomba laki mbili, hiyo pesa sina ila ipo laki moja hapa njoo tu nikupe hiyo bure wala sikukopeshi. Nikishakupa hiyo kilo, najua kwenye kumbu kumbu zangu itafutika kuliko nikukopeshe elfu hamsini alafu usinilipe nakuwa naiwazia full...
Mkuu nna shida na million moja, rejesho nitafanya kati ya tarehe 10-15 mwezi ujao. Nisaidie mkuu, nmekwama hela zangu zimechelewa kuingizwa!
 
Hakuna hata mmoja anayedaiwa ndani ya JF naona kila anayechangia hapa yeye anakopesha na kutoa tu
Hata sisi wengine uwa tunakopa lakini tunarudisha kwa uaminifu. Sasa wale wakopaji wasiorudisha wakiuona uzi huu hawana hata hamu ya kuufungua.
 
Kama unamfuatilia vzr Mo huwa ni inspirational speaker.
So kwa mtu anayejitambua sio jambo la ajabu Mo kupost kama hivyo.

La pili,Mo hawezi kuikopesha Simba coz yeye naye ni share holder,so hata kama anawadai nadhani kuna namna nyingine ya kupata hela zake kupitia shares zao
 
Mimi jamaa toka mwezi wa 5 mwaka Jana hadi Leo.
Nilimtishia kwenda Polisi akasema atalipa hii wiki ya pili sasa.
Juzi kati nimesikia kauza nguruwe wake 20 bado hata SMS hanitumii.
Yaani nikikumbuka jinsi huyu dogo tulikotoka basi tu.
Na kila siku anaenda home kwa mother kujidai anamsalimia na kuleta shobo kwa ndugu zangu
Pole sana brother! Kama ilivyo katika mambo ya "investments" wanasema You should invest something/money which you are willing to loose! Vivyo hvy katika kukopesha rafiki, hii kwa mtazamo wangu lkn...Ni vyema kwa rafiki ukamkopesha pesa ambayo hata asipokulipa hutoumia sana, marafiki mara nyingi hupeana ela kuliko kukopeshana. Usije mtupa au kumpotezea rafiki yako huyo sababu hajakulipa pesa (kama ni rafiki haswa), kuna siku isiyo na jina utakwama sana,narudia tena utakwama haswa, atakuja kukusaidia kwa pesa ndogo sana klk hata uliyomkopesha na ukamshukuru utafikiri kakupa ahadi ya kukuongezea kuishi miaka 150.

Angalia mfano huu wa kweli: kuna jamaa(chukulie anaitwa michael) alikua na rafiki (Shaban-sy jina halisi) walisoma wote shule ya boarding miaka ya nyuma, kuna siku Shaban alisafiri kwenda likizo na kumuachia Michael mabegi yake na vifaa vyake mhm, Michael hakwenda likizo. Baada ya Shaban kurudi baada ya likizo, hakumkuta Michael , kumbe alifanya mpango na kuhama shule na akaondoka na vitu binafsi vya Shaban ikiwemo nguo za gharama. Shaban akapotezea na ubaya au uzuri kipindi hicho hakukuwa na mawasiliano ya simu.

Miaka kadhaa ikapita, wote wakiwa na maisha yao lkn wakiwasiliana mara chache mno. Shaban alikwama, alikua anamsomesha mdogo wake chuo kikuu Dar, na huyo mdogo wake alikua mwaka wa mwisho chuoni na alikaribia mitihani yake ya mwisho ili amalize chuo, kwa bahati mbaya sana Shaban alikwama kumlipia dogo ada ya semester ya mwisho chuoni. Alifika hatua Shaban akamwambia dogo wake afanye utaratibu wa kuhairisha mwaka kwasababu amehangaika zaidi ya miezi 4 kutafuta hy pesa amekosa, na mipango yoòoote ya pesa iligoma, hakuna alietaka kumsaidia Shaban achilia mbali kumkopesha. Wote dogo na Shaban walikua ktk mawazo mazito, dogo aliwaza muda aliopoteza na akiangalia wanafunzi wengine wakijiandaa na pepa anazidi kudata....kwa upande wa Shaban anawaza pesa aliyotupa toka mwaka wa kwanza alafu Leo pesa ndogo sana inakuja kuharibu kila kitu, na pia aliwaza , Je akihairisha mwaka atakuwa na uhakika wa kumlipia pesa(ada) tena mwakani ikiwa hii ndogo imemshinda?..pia aliwaza huyu dogo akikaa bila elimu si atakuwa mzigo kwake? Basi mawazo yakawa juu ya mawazo.....zikiwa zimebaki siku 2 kabla ya mtihani wa mwisho wa dogo, Shabani akapekua kwenye phonebook yake akaona jina la Michael akiwa hana uhakika kama atafanikisha lengo lake , yani kama alikua anajaribu akampigia Michael simu na kumuelezea shida yake....unafikri Michael alichukua hata dakika 2? mzigo ukasoma kwa tigopesa na mwisho wa siku dogo akaenda shule.....na kutunukiwa shahada yake.

Moral of this story, ni kuwa maisha ni mzunguko Leo wwe unapata(kama unabidii lkn ya kutafuta ) kesho mwingine anapata........tusiwe watu wa kupenda kulaumu sana kwa yanayotokea katika maisha yetu, kila kitu hutokea kwasababu.
 
I wish I could help you...
Najua ni ngumu, ila ni swala la kibinadamu tu. Piga moyo konde nipige tafu mkuu, wanaume hatutupani. Tarehe zikifika nitakupatia kama nlivyoahidi maana pesa ipo kwa system ila ni malipo tu yamechelewa mkuu nami nahitaji instant cash.
 
Deni ndo linanigombanisha na Voda.
Wananidai 3864 toka mwaka juzi,sina mpango wa kuwalipa.
Wananitumia text daily.
Ndo deni pekee ninalodaiwa
 
Nilishaachaga kukopesha toka nipigwe mzinga na ndugu yangu wa damu pesa ndefu
 
Back
Top Bottom