Che mittoga
JF-Expert Member
- Mar 28, 2017
- 14,396
- 18,203
Kumekuchwa
Ngoja kuna mtu nimcheki then tuone itakuwaje.'Tangazo'
Natafuta mtu aliesoma Security Quality Control na OJT zake zote chap anicheki...mshahara kuanzia 1.5M
Nipo hapa accountssawa check me ukipata, na pia mtu aliseoma Accounts na HSE and Quality Assurance
Shusha vitu goma liisheDEVIL’S FAMILY (FAMILIA YA MASHETANI) 35
KILA KILICHO ANDIKWA KATIKA HADITHI HII NI UTUNZI HAKIENDANI NA KISA CHOCHOTE KILICHO WAHI KUTOKEA MAHALA POPOTE ASANTE
*************************************************************************************
ILIPOISHIA
“Uta waona shida yako ni nini mama?”
Jack alizungumza. Baada ya dakika tatu mlango ukafunguliw ana akaingia Valentina huku nyuma yake akifwatiwa na Rose.
“Amefwata nini huyu binti”
Mrs Tiger akataka kunyanyuka ila Sophia akamzuia na kurudisha kitandani alipo kaa. Taratibu Rose na Valentina kila mtu akasimama pembeni ya mume wake.
“Baba, mama huyu ni Rose mke wangu, mama wa wanangu. Mwanamke wa ndoto zangu ambaye nimefunga naye ndoa masaa kadhaa yaliyo pita. Poleni sana kwa kuto waalika hapo mwanzo kushuhudia ndoa yangu na mke wangu. Ila ilibidi nimuoe bila uwepo wenu ninyi ila mdogo wangu na mkewe walikuwa wasimamizi wa ndoa yetu.”
Mzee Tiger akamtazama Jack kwa sekunde kadhaa na mashine inayo hesabu mwenendo wa mapigo ya moyo ya mzee Tiger ikaanza kutoa mlio wa hatari huku asilimia za mapigo ya moyo zikionekana zikishuka kwa haraka sana.
ENDELEA
Mlango wa chumba ukafunguliwa na wakaingia madaktari wakikimbia kwani mfumo wa mashine ya oxygen anayo itumia mzee Tiger imeunganishwa na app zilizopo kwenye simu zao hivyo inavyo tokea dharura ya mgonjwa kwa haraka wana pata ujumbe.
“Sogeeni”
Daktari mkuu wa familia alizungumza. Wakasogea pembeni na kuanza kumpatia huduma ya kwanza mzee Tiger. Mrs Tiger akaendelea kulia huku akitazama madaktari wanavyo pambana kuyaweka sawa mapigo ya moyo ya mzee Tiger. Wakachoma sindano na taratibu mapigo yake ya moyo yakaarudi na kukaa sawa.
“Mzee amepata presha kama kuna mazungumzo yanayo muweka kwenye hii hali nina waomba yasiendelee”
Daktari alizungumza akimtazama James na wadogo zake.
“Na tuna hitaji kumfanyia upasuaji wa haraka kwani kwa hali ya presha anayo ipaa inazidi kuifanya damu kumwagika katka ubongo”
Daktari alizungumza.
“Mfanyieni”
James alizungumza.
“Maandalizi yafayike haraka”
Daktari aliwafahamisha wezake. Hapakuwa na muda wa kupoteza maandalizi ya kumfanyia upasuaji mzee Tiger yakaanza huku jopo la madaktari wengine likiaongezeka. Ikawalazimu James na wezake kusubiria nje ya chumba upasuaji ukiwa una fanyika.
“Endapo mume wangu akifa. Ninyi wawili sinto waacha hai haki ya MUNGU nina apia, sinto waacha hai”
Mrs Tiger alijiapiza akimtazama James na Rose.
“Mama nguvu unayo itumia kumtishia kaka na mkewe, ungeitumia katika kumuomba MUNGU amuepushe baba na kifo kwa maana jinsi anavyo sumbuliwa na hilo tatizo jipya pamoja na sataratani yake, sidhani kama ata toboa”
Maneno ya Jack yakamfanya Mrs Tiger kuondoka eneo hilo.
“Shem usiwe na shaka hakuna ambacho mama ata kifanya kwako sawa”
“Sawa shem”
“Tupo chumbani”
James alizungumza, akamshika mke wake mkono na akaelekea chumbani kwake.
“Mbona una shusha pumzi nyingi namna hiyo?”
“Mmmm nina wasiwasi mume wangu. Tusimchukulie mama yako poa ujue, ana weza kufanya chochote watu tuka mshangaa. Mulicho muonyesha mbele yake pamoja na mzee kime waumiza sana”
“Achana naye”
“Mume wangu tusipuuzie kila kaulia nayo izungumza mama yako. Kauli nyingine ana maanisha. Kama ni vipi tuondoke tu tuta pewa matokeo ya kinacho endelea”
Rose alizungumza akiwa amejawa na wasiwasi.
“Tafadhali”
“Sawa tuta ondoka na ili tuondoke kwa usalama ina tupasa tuwe na msaada wa dogo”
“Zungumza naye”
“Sawa. Walau ukione chumba changu ambacho toka nilipo kuwa mtoto mdogo nilikuwa nina ishi humu”
“Kizuri?”
“Japo now sio chumba changu tena.”
“Hizi ni picha zako za utotoni?”
“Ndio”
“Ulikuwa mzuri”
“Hahahahaa nimesha zeeka hivi sasa?”
“Wala hujazeeka. Una onekana kama kijana wa miaka ishirini na tano”
“Doooo”
“Ndio ukweli kipenzi changu”
“Asante babe”
James alizungumza na akaendelea kumuonyesha mke wake picha mbali mbali kipindi akiwa mtoto mdogo.
***
“Upo wapi?”
Mrs Tiger alizungumza machozi yakimwagika.
“Nakuja”
Mrs Tiger akakata simu na akabadilisha nguo. Akachukua pochi yake na funguo ya gari lake na akatoka chumbani kwake huku kichwani akiwa amevalia kofia kubwa ya duara pamoja na miwani nyeusi.
“Unakwenda wapi?”
Sophia alimuuliza mama yake.
“Nikuambie ninapi kwneda wewe ni mume wangu?”
“Mumeo amelala pale hivyo nina haki ya kukuuliza ni wapi unapo kwenda.”
Mrs Tiger akamsogelea Sophia.
“Koma mwanazo ni leo na mwisho ni leo usiniulize ni wapi ninapo kwenda”
“Okay safari njema”
Mrs Tiger akatembea kwa mwendo wa haraka na akatoka nje.
“Mama yako ana toka”
“Ana kwenda wapi?”
“Kwa madai yake hataki kuulizwa. Hembu mzuie ana ajenda zake za siri naona huu ndio muda ambao ana taka kuutumia kuzifanya”
“Poa siser”
Jack akakata simu na akapiga simu kwa walinzi wa getini.
“Ndio mkuu”
“Mama asitoke”
“Una sema?”
“Zuieni gari la mama lisitoke”
“Sawa mkuu”
Mlinzi akakata simu akitazama gari la Mrs Tiger linalo endeshwa kwa mwendo wa kasi kuelekea walipo getini. Mrs Tiger akakanyaga breki hadi tairi zikaburuzika kwani alitegemea walinzi wata fungua geti wakimuona akiwa mbali.
“Mbona hamufungui geti ninyi?”
Mrs Tiger alifoka.
“Samahani mkuu nimepewa maelekezo tusifungue geti”
“NINI nani kawapa?”
“Boss Jack”
“Ana wazimu. Ana jua nina kwenda wapi?”
“Tafadhali wasiliana naye”
Mrs Tiger akashusha pumzi nyingi zilizo changanyikana na hasira. Akampigia simu Jack.
“Mama”
“Una wazimu. Kwa nini una waambia walinzi wanizuie kufungua geti?”
“Baba ana fanyiwa upasuaji una kwenda wapi?”
“Nina kwenda kwa nabii kuiombea hii familia. Unataka baba yako afie kitandani eheee?”
“Muambie nambii aje hapa nyumbani”
“Jack umechanganyikiwa wewe?”
“Mama sija changanyikiwa. Ila hakuna mwana familia yoyote kutoka nje sawa mama”
Mrs Tiger.
“Hapa ni kwangu nina uhuru wa kutoka muda nitakao mimi na kurudi muda nitakao mimi”
“Mama elewa ninacho kuambia kwamba hakuna kutoka na ukilazimisha kutoka nita waambia walinzi wapige risasi gari lako usinilazimishe kufanya hayo maamuzi”
Mrs Tiger akamtazama mlinzi aliye simama pembeni ya gari lake ambaye ana sikia kinacho endelea.
“Tafadhali mama”
Mrs Tiger akakata simu, akageuza gari kwa mwendo wa kasi na kurudi katika maegesho ya magari yake. Akashuka akiwa na hasira akaingia ndani hadi nje ya chumba alichopo Jack na mke wake. Akamshika Jack mkono na wakaosega pembeni kutoka alipo kaa mke wake.
“Una tatizo gani wewe? Kaka yako amekulisha kitu gani wewe?”
Mrs Tiger alizungumza kwa sauti ya kunong’ona.
“Mama tafadhali sana nakuomba sana naomba ukaushe tupo kwenye kipindi ambacho wana familia wote tuna takiwa kuwa hapa. Kama mzee ata toboa basi tuwepo kama ata kufa basi sote tuwepo mambo ya kutoka toka ikiwa na wewe ndio mwenye mume una zingua. Mpigie nabii wako aje hapa kuomba”
Mrs Tiger akamtazama Jack kwa sekunde kadhaa.
“Sijapenda?”
“Hii haina swala la kupenda au kuto kupenda. Hili ni swala la kifamilia”
“Nataka huyo kama yako na mkewe waondoke”
“Una hisi ni na akili ndogo kama hiyo. Kwa sasa nahitaji familia kuungana. Sihitaji marafakano yasio ya sababu ya msingi ambayo wewe ndio chanzo”
“Mimi chanzo?”
“Ndio wewe ndio chanzo. Wewe ndio umeifikisha familia hapa. Kama mama ulikuwa na nafasi nzuri ya kumshawishi baba kumkubali Rose kwenye hii familia namaini leo baba asinge kuwa amelazwa pale. Ila ushawishi wako mbovu umesababisha leo hii hali kuwa kama ilivyo”
“Ila kumbuka baba yake ni adui yetu. Adui wa hii familia”
“Kumbuka ulivyo husika kumkata makend* yake na hivi viganja vyako mama. Umesahau?”
Mrs Tiger akakaa kimya.
“Sasa hivi kaushau, mtoto wa watu ana pitia magumu mama kausha basi”
“Una muonea huruma?”
“Sio namuonea huruma. Ila tunapaswa kuwa na haya. Wewe na mwenzio ndio muliwasukumiza katika bwawa la mamba wakiwa hai. Unajizima data?”
Mrs Tiger akaondoka eneo hilo na kuelekea chumbani kwake.
“Mama ana shida gani tena?”
“Kichwa chake kina pata moto”
“Sikutarajia kumuona mama akiwa kwenye hizi kelele. Nilikuwa nina muona mstarabu sana”
“Thubutu, huyo ndio mama yetu. Una paswa kuwa na digrii ya kumzoea”
“Itakuwaje kwa mke mwenzangu si atakuwa na woga”
“Naye ana paswa kuwa na moyo wa uvumilivu.”
Wakaendelea kusubiria oparesheni inayo endelea ndani ya ofisi. James na mkewe wakafika eneo hilo/
“Dogo sisi tuna hitaji kutembea”
“Kwa nini bro”
“Shemeji yako ana hofu”
“Shem kuwa na amani hakuna cha kukudhuru.”
“Namuogopa mama”
“Kuwa na amani mama hana tatizo”
“Kweli?”
“Yaah kweli hana tatizo. Tusubirie tuone mzee ana toboa au laa”
“Sawa shem”
“Baby nenda kamtembeze tembeze mwenzio ayaone mazingira ya nyumba”
“Sawa”
Valentina wakaondoka na Rose na kuwaacha James na Jack nje ya mlango wa chumba cha upasuaji.
“Shemeji yako yupo?”
“Ahaa amekwenda kwao kwanza, tulivyo rudi tu kesho yake akaenda kwao”
“Usianiambie mulivyo kuwa Dubai pia uli mla?”
“Weee acha tu. Mtoto mtamu yule aisee. Yaani ana pigo fulani hivi lazima uchanganyikiwe”
Wote wakacheka kwa nguvu.
“Yaani yule mtoto ana joto la kufa mtu”
“Kuliko dada yake?”
“Kuliko dada yake aisee.”
“Kuwa makini ni ndugu”
“Mmmm halafu hii game ya mwisho nilimwaga ndani”
James akamtazama Jack kwa mshangao.
“Tulikuwa tumelewa”
“Oya usije ukamjaza mimba”
“Naliwaza hilo sana mwanangu. Sijui akipata mimba itakuwaje?”
“Ni kipengele hicho ujue.”
“Ila akipata mimba fresh bwana kikubwa anizalie mwanangu”
“Ila ni mzuri hata akizaa sio mbaya.”
“Nimefikiria jambo moja”
“Jambo gani?”
“Hizi tabu zikisha isha nataka kumuoa”
“Umechanganyikiwa au?”
“Kaka sijachanganyikiwa. Nataka awe mke wangu. Siwezi kuruhusu mjinga mjinga mmoja akaja akamchukua”
“Sema umependa”
“Ni kweli nimempenda Vaileth”
James akatabasamu.
“Basi fanya kile kinacho kupa furaha. Usiogope”
“Shida ni kwamba dada yake akifahamu inakuwaje bro”
“Huo ndio mtihani aisee”
“Tena ngoja nimpigie”
Jack akampigia simu Valentina.
“Mke”
“Niambie kipenzi changu”
“Kipenzi na sio mume
“Jamani haya niambie mume wangu?”
“Njoo Dar”
“Lini?”
“Leo”
“Leo?”
“Ndio nakutumia pesa ya ndege. Njoo”
“Nikija nina muambia nini dada?”
“Ukija nita kuambia ni hoteli gani kwanza ufikie”
“Una nyegee ehee?”
“Zimefanya kujaa”
“Dadeki ngoja nijiandae kwa maana hatuto iba iba nitakuwa nina kupa kwa uhuru”
“Wacha weeee”
“Ndio nataka unifanye hadi pawake moto”
“Wachaaaa weee, nakutumia pesa uje”
“Sawa kipenzi changu”
Jack akakata simu na akamtumi pesa ya nauli ya ndege Vaileth.
“Kuna kitu nimegundua kwako”
“Kitu gani bro”
“Una furaha sana ukiwa na Vaileth kuliko Valentina”
“Yahaa na kuna kitu nimekijua nimekaa nacho moyoni na ndio kimenifanya niwe na Vaileth”
“Kitu gani dogo?”
Jack akamtazama kaka yake.
“Nimegundua mke wangu ana sagana na sister Sophia”
James macho yakamtoka kwa mshangao, japo ana fahamu mdogo wake Sophia ana mahusiano ya kimapenzi na wifi yake ila hakutarajia kama mwenye mke Jack aana weza akawa ana jua swala hilo na akawa kimya kama vile hajui chochote kile.
ITAENDELEA
Mchaka mchaka mpya umeanza. Jack na ndugu zake bado wana mkabia juu mama yao hadi kutoka nje ya nyumba wamemzuia. Jack ana fahamu ukweli mkewe Valentina ana mahusiano ya kimapenzi na Sophia dada yake kwa nini amekaa kimya? Ungana nami katika stori hii ya kusisimua sehemu ya 36.