DEVIL’S FAMILY(FAMILIA YA MASHETANI) 30
ANGALIZO: KAMA UPO CHINI YA UMRI WA MIAKA 18. TAFADHALI USISOME HII HADITHI.
ILIPOISHIA
“Babe”
“Mmm…umerudi?”
“Yaa nimerudi una endeleaje?”
“Nipo poa mume wangu. Umempata shem?”
“Bado”
Jack akavua nguo zake na akaelekea nafuni. Akaoga haraka haraka na akarudi kitandani na akajilaza pembeni ya Valentina.
“Mbona una onekana uma mawazo sana”
“Hakuna”
“Sijakuzoea hivyo”
“Nipo sawa mke wangu pumzika”
“Kama kuna tatizo naomba uniambie mume wangu”
“Hakuna tatizo babe. Pumzika”
Taratibu Valentina akajivuta juu kidogo na akakilaza kichwa chake juu ya kifua cha Jack na kuendelea kulala huku Jack akiwa hana furaha kabisa kwani aliyo kutana nayo baharini yameshangaza na kinacho muumiza kichwa zaidi ni kazi aliyo pewa ya kumuua kaka yake anaye mpenda.
ENDELEA
‘Nawezaje kumua James?”
Jack aliendelea kuwaza na kujiuliza maswali yaliyo kosa majibu.
***
Ndani ya siku mbili za James kukaa hospitalini akaruhusiwa kutoka huku hali yake ikiwa imeimarika.
“Una waza nini mume wangu?”
Rose alizungumza huku akimtazama James ambaye muda wote macho yake yapo nje ya gari akitazama vitu wanavyo vipita barabarani.
“Eti mume wangu?”
“Siwaza kitu mume wangu”
“Najua una pitia kipindi kigumu cha mawazo”
“Rose”
“Abee”
“Najua una biashara nyingi za wazazi wako unazo paswa kuzitazama kwa ukaribu. Je utaweza kuziacha na kuandamana nami kwenda kule ninapo pataka?”
“Nipo tayari”
James akamtazama Rose aliye jibu swali alilo ulizwa bila hata ya kufikiria mara mbili.
“Una uhakika?”
“Ndio babe. Nimeishi maisha yangu kwa asilimia kubwa nje ya nchi. Hivyo kwa hivi sasa naweza kwenda na kuishi nje ya nchi popote upatakapo mume wangu”
James akakishika kiganja cha mkono wa kulia cha Rose.
“Nakupenda snaa James sitanii kweye hili. Mwanzoni sikuwahi kujua nini maana ya mapenzi ila baada ya kukutana na wewe nimejua nini maana ya upendo. Unanipenda kweli James nami nina kupenda sana”
“Asante nahitaji kuanzisha familia na wewe”
“Hata mimi James”
Rose taratibu akambusu James mdomoni hadi anko Ally anaye endesha gari hilo akatabasamu. Wakafika nyumbani kwa wazazi wa Rose.
“Karibu na ujisikie huru”
“Asante mpenzi”
“Hichi ndio chumba changu ninacho ishi toka nikiwa binti mdogo”
“Asante sana mpenzi”
James alizungumza akitazama picha ukutani zinazo muonyesha Rose akiwa na wazazi wake.
“Picha hii nilipiga nikiwa na miaka mitano”
“Ulikuwa mrembo”
“Sana yaani, nilikuwa pis kali”
Wote wakacheka.
“Umefanana sana na mama yako”
“Yaah mama mama aliacha chata yake duniani”
“Kwa kweli, unataka tukaishi nchi gani?”
Rose akamtazama James kwa sekunde kadhaa.
“Nchi yoyote uitakayo wewe”
“Wewe ndio useme”
Rose akashusha pumzi taratibu.
“Kuwa huru”
“Brazil”
“Una papenda?”
“Sana napenda maisha yao wanayo ishi. Naamini tukienda kuanzisha maisha yetu pale tuta ishi kwa aamani”
“Kazi yako ya upelelezi?”
“Haina maana kwa sasa”
“Kwa nini?”
“James upelelezi ni kazi ninayo ipenda. Na nilijiunga kwa kuifanya kwa mapenzi yangu tu. Ila nilicho kuja kukigundua katia mataifa haya ya giza ambayo viongoz wake walio wekwa madarakani hawana nguvu juu ya wale walio waweka madarakani basi huwa nina ona hakuna haja ya mimi kuwa mpelelezi kwani kama walishindwa kunisaidia ukweli kwenye kupotea kwa baba yangu na kaka zangu una hisi kuna kitu gani wata weza kunisaidia?”
Rose alizungumza kwa uchungu akimtazama James usoni mwake.
“Jibu nililo pewa na mkuu wangu ni kuwa siwezi kuipeleleza familia yako nikaona kuna haja gani ya mimi kuendelea kuwa mpelelezi”
“Katika familia mbaya na hatari sana kwenye hii n hi basi ni familia yangu. Baba na mama yangu ni watu hatari sana. Nitofauti sana na jinsi vile watu wanavyo waona kwenye tv au jamii. Wale ni Chui walio jivisha ngozi za kondoo.”
“Una mpango gani dhidi yao?”
Rose aliuliza swali la kimtego.
“Kwa sasa nahitaji mimi na wewe tukawe sehemu salama. Baada ya hapo nitajua nini cha kufanya”
“Sawa mume wangu”
“Tuta tumia ndege yangu kuondoka Tanzania?”
“Una ndege?”
“Ndio ila hakuna mwanafamilia anaye tambua”
“Una muda gani toka umeimiliki?”
“Miaka miwili hivi sasa.”
“Wee”
“Kitu ambacho MUNGU alinipa akili ni kujitengenezea maisha nje ya familia yangu. Nilikuwa naishi maisha ambayo wana familia wangu waliyaona ni maisha yasiyo na future yoyote hivyo nilikuwa nina jiwekeza na nina fungua kampunia za teknolojia duaniani pasipo wao kujua. Hata hili la kuwaua walinzi wenye mafunzo ya hali ya juu itakuwa ni meseji tosha kwao kuwa sikuwa kama vile wanavyo nichukulia. Kwani waliniona mimi ni kama lover boy fulani hivi sina nguvu na hata majukumu mazito alikuwa ana kabidhiwa mdogo wangu”
“Waoooo”
“Ndio hivyo mpenzi. Nahitaji tuondoke ikiwezekana leo”
“Leo naomba niweke mambo sawa ndani ya kapumni hizi za baba. Kuna baadhi ya vitu ni lazima niviweke kwenye mstari ulio nyooka”
“Sawa mke wangu”
“Ngoja nimuambia anko Ally awaite wakurugenzi wote hapa nyumbani kwa ajili ya mkutano”
“Katika kampuni za baba yako kuna mfumo ambao una weza kuwasimamia wakurugenzi hata kama wewe upo mbali?”
“Upo ila wengi wana uchezea kwenye mahesabu”
“Naweza kuuona?”
“Ndio twende ofisini”
Wakatoka chumbani na wakaingia ofisini kwa mzee Chiko.
“Baba alikuwa ana tumia mfumo huo kupata taarifa za kampuni zake”
Rose alizungumza huku akiwasha computer ya baba yake. Akamuonyesha James mfumo huo.
“Mbona ni mfumo wa kizamani”
“Kumbe?”
“Ndio ni mfumo wa kizamani sana mpenzi. Ndio maana hata wakurugenzi wenu wana weza kuchepusha pesa za kampuni vile wanavyo jisikia wao. Ngoja nikutengenezee mfumo ambao hakuna ambaye ata weza kuuchezea hata awe na mdukuzi wa aina gani. Kila kifaa electron kinacho tumia mfumo ndani ya kampuni zako utakuwa una weza kufwatilia taarifa zake”
“Inawezakana kufanyika hivyo?
“Kwa asilimia mia moja. Tenknolojia ipo juu sana hivi sasa na sio tu utaweza kufwatulia taarifa za kikazi bali hata cctv zilizo fungwa kwenye maofisi zote na kila kitakacho kuwa kina zungumzwa ndani ya ofisi kitanaswa kupitia laptop, simu za ofisi, kamera za ofisi au tablet za ofisini. Hakuna ambaye ata kuwa salama kwenye mfumo mpya nitakao uunda”
“Mmmmm mume wangu ina wezekananaje simu au computer ikanasa sauti za watumishi?”
“Mke wangu sasa hivi hivi vifaa tunavyo vitumia sio salama unapo kuwa na mazungumzo nyeti. Nitafutie simu mpya nikuonyeshe”
“Kuna simu nilinunua ngoja nikaichukue”
Rose akaondoka na baada ya dakika akarudi akiwa na simu.
“Niliohofia kukupa simu ukiwa hospitalini kwa maana ungehatarisha ualama wako”
“Hahahaaa hakuna kitu kama hicho.”
“Hofu yako ndio ilikuwa ina niogopesha babe”
James akajisajili katika simu mpya, akaingiza mfumo wake wa udukuzi ambao ameuunda yeye mwenyewe.
“Mfumo huu niliuunda kwa ajili ya shirika lenu la ujasusi. Ila nikaona uta tumiwa vibaya sana na maafisa wake kwani utawezesha siri nyingi kuvuja”
James akaingia katika rekodi za vifaa vinayo tumika katika nyumba ya wazazi wake ikiwemo hadi simu za mikononi kuanzia ya baba yake, mama yake, Jack, Sophia, Valentina na watumishi wote wa ndani.
“Kwa hiyo hata nikiwa offlien nina weza kusikiliza mazungumzo yao waliyo yafanya simu zao zikiwa karibu na wao”
“Wana jua kuwa una wafwatilia?”
“Hapana huu mfumo ni mimi mwenyewe ndio ninao ujua”
James akatazama mazungumzo yaliyo rekodiwa na simu ya Jack siku mbili zilizo pita majira ya saa tisa usiku. James akajifikiria kwa sekunde kadhaa kisha akaifungua audio hiyo. Wakaanza kusikiliza mazungumzo ya Jack na baba yake kuanzia wakiwa sebleni hadi kufika eneo la katikati ya bahari na mazugumzo hapo yakakatika.
“Ina onekana baba yako ana kuchukia sana kwa kutaka kunioa mimi”
“Nikuulize jambo?”
“Niulize”
“Upo tayari kufunga ndoa na mimi?”
“Ndio nipo tayari mume wangu”
“Kweli?”
“Ndio mume wangu”
“Nakuoa leo mbele ya wafanyakazi wako”
“Leo?”
“Ndio leo”
“Mbona una harakisha?”
“Kwa sababu nikikuoa kuna vitu hawato weza kutufanyia”
“Vitu gani?”
James akashusha pumzi taratibu huku akimtazama Rose.
“Ipo hivi kuna siri ya utajiri wetu. Siri za nguvu za giza ambazo ndio zinazo linda huu utajiri ambao kila siku una kuwa una ongezeka.”
“Sasa ukiniona mimi mambo gani wata shindwa kutufanyia?”
James akanyanyuka na kumtazama Rose.
“Mtoto wa kwanza kwenye ukoo wetu huwa hapaswi kuoa. Endapo ata oa utajiri utaingia katika anguko ambalo waanzilishi wake hawapendi kitu kama hicho kiweze kutokea. Mbili nikikuoa hawato weza kuniua kwa nguvu za giza kwani kila mtoto wa kwanza kwenye ukoo wetu akisha fikisha miaka arobaini na mbili ana kufa. Hapa nina arobaini kamilia hivyo nimebakisha miaka miwili nife”
“Tatu kila mimba anayo ipata mwanamke ambaye sija muoa wana itoa. Ndio maana una weza kukuta hadi leo nimetembea na wanawake wengi sana ila sijafanikiwa kuwa na hata mtoto mmoja. Si kwamba nilio kuwa nina tembea nao walikuwa hawapati mimba? Walikuwa wana pata mimba ila walikuwa wana zito”
“Mmmmm! Baba yako ni mtoto wa ngapi kwao?”
“Wa pili. Kaka yake alifariki akiwa na miaka miwili tu. Ndio maana una weza kuona kuwa yeye ana onekana ni kama wa kwanza kwao”
“Umejuaje hizo siri zote mume wangu?”
“Kuna kitabu kipo katika library iliyopo chini ya ardhi katika makazi ya mzee pale. Mimi kwetu ndio nilikuwa nina penda kusoma hivyo nilibahatika kukisoma hicho kitabu nikiwa nimerudi chuo. Kuanzia hapo nikawa makini sana na kujitengenezea maisha yangu nje ya pesa ya familia. Pesa ambayo imejaa laana ya damu na pia nilipambana nihakikishe nina kuwa na ujuzi mkubwa katika tenkonolijia ili niweze kuapata pesa ndefu.”
“Nimekuelewa mume wangu. Nipo tayari kufunga ndoa na wewe”
“Mapigia mchungaji pamoja na sonara ninaye mfuamu atupe picha za pete kisha azilete”
“Sawa mpenzi wangu. Nakupenda sana”
Rose akamyonya denda James kwa hisia kubwa na James akaanza kuwasiliana na sonara ambaye ni rafiki yake na akatuma picha kadhaa za pete na wakaanza kuchagua.
***
“Siku ya tatu hii hadi leo mumeshindwa kujua ni wapi alipo eheee….Nina walipa pesa zote za nini nina wapa saa ishirini na nne muwe mumempata tunaelewana?”
Mzee Tiger alizungumza kwa kufoka, akakata simu huku akimtazama Jack akaingia ofisini kwake.
“Watu wako wamefikia wapi?”
“Bado wana mtafuta”
“Ina maana James amewazidi akili ninyi eheee?”
Mzee Tiger akazidi kufoka.
“Tuta mpata. Nimetega watu wangu kila mahala na hata pale nyumbani kwa Chiko, kuna watu tumewatega kufwatilia na kujua kama yupo pale au laa”
Mzee Tiger akaka katika kiti chake cha kuzunguka. Galfa hali ya hewa ikabadilika na manukano ya harufu nzuri yakatawala ofisi nzima.
“Kuna nini baba?”
“Bibi yako”
Mzee Tiger alizungumza akitazama ukuta wa upande wake wa kulia. Jack akashtuka kumuona bibi yake ambaye alikutana naye siku mbili zilizo pita. Mzee Tiger akampa ishara ya kunyanyuka Jack na kafanya hivyo, wakainama kidogo kama ishara ya heshima.
“Nyanyukeni”
Wakanyanyuka.
“Jack bado hujanizoea tu”
“Aaaaha….”
Jack akapata kiguumizi.
“Ina bidi unizoee”
“Sawa bibi”
“Sema mkuu”
Mzee Tiger alizungumza kwa sauti ya kunong’ona.
“Wala hana haja ya kuniita mkuu. Huyu ndio mjukuu wangu pendwa hivyo ana weza kunita bibi tofauti na ninyi”
“Mumefikia wapi kwa swala la James?”
“Kusema kweli hadi sasa hatujampata mkuu. Hatujui ni wapi alipo. Tumetumia hadi maafisa wa serikali kumtafuta ila hatujampata kabisa. Tuna omba msaada wenu”
“James ana oa leo. Ana muoa Rose leo”
Mzee Tiger akatazamana na Jack kwa mshangao.
“Na endapo ata muoa Rose basi Jack kuna malipo uta paswa kuyalipa kwani kazi itakuwa ni ngumu zaidi ya leo”
“M…amalipo?”
“Ndio kila jambo huwa lina utaratibu wake na kanuni zako. Baby yako mzaa baba yako, alimuua mwanaye wa kwanza alipo kuwa na miaka miwili tu kuepusha adhabu kama hizi ambazo wewe uta kutana nazo”
Jack akamtazama baba yake huku akitetemeka.
“Wewe ndio umekalia kiti cha utajiri wa familia yako. Hivyo kama kiongozi una beba majukumu yote ambayo kiongozi hubeba kwa watu wake anao waongoza. Endpo James akamuoa Rose basi ia tulazimua kumtoa kafara mke wako Valentina. Ndoa ya Rose na James ina fungwa baada ya masaa mawili yajayo. Ukichelewa kuizuia na kumuua James na Rose basi leo usiku mke wako atakufa”
Jack na mzee Tiger macho yakawatoka kwa mshangao huku wakishuhudia bibi akipotea mbele yao na kumfanya Jack akae kwenye kiti chake huku akitetemeka kwa woga.
ITAENDELEA
Mchaka mchaka mpya umeanza. James ameamua kumuoa Rose. Ndoa yake na Rose ita sababisha kifo cha Valentina je ni kitu gani ambacho Jack ata kifanya kuyaokoa maisha ya mkewe ambaye hawana hata wiki mbili toka wamefunga ndoa? Ungana nami katika stori hii ya kusisimua sehemu ya 31.