Devil’s family(familia ya mashetani) 01

Devil’s family(familia ya mashetani) 01

DEVIL’S FAMILY(FAMILIA YA MASHETANI) 36

KILA KILICHO ANDIKWA KATIKA HADITHI HII NI UTUNZI HAKIENDANI NA KISA CHOCHOTE KILICHO WAHI KUTOKEA MAHALA POPOTE ASANTE
*************************************************************************************

ILIPOISHIA
“Wacha weeee”
“Ndio nataka unifanye hadi pawake moto”
“Wachaaaa weee, nakutumia pesa uje”
“Sawa kipenzi changu”
Jack akakata simu na akamtumi pesa ya nauli ya ndege Vaileth.
“Kuna kitu nimegundua kwako”
“Kitu gani bro”
“Una furaha sana ukiwa na Vaileth kuliko Valentina”
“Yahaa na kuna kitu nimekijua nimekaa nacho moyoni na ndio kimenifanya niwe na Vaileth”
“Kitu gani dogo?”
Jack akamtazama kaka yake.
“Nimegundua mke wangu ana sagana na sister Sophia”
James macho yakamtoka kwa mshangao, japo ana fahamu mdogo wake Sophia ana mahusiano ya kimapenzi na wifi yake ila hakutarajia kama mwenye mke Jack aana weza akawa ana jua swala hilo na akawa kimya kama vile hajui chochote kile.

ENDELEA
“What! Umelitambua hilo lini?”
“Kabla hata sijamuoa?”
James akazid kushangaa.
“Dogo”
“Haki ya nani na pia nilichukua namba ya simu kutoka kwa sister”
“Duuu. Kwa hiyo pigo za dada yako una zijua muda?”
“Nazijua na huyu ni demu wake nimempenda na nikaona nimuoe”
“Yeye ana jua kuwa unajua tabia yake?”
“Hapana na nimejikausha”
“Una kifua aisee”
“Unaambiwa ukipenda boga penda na ua lake”
“Una moyo aisee….Haya kama umeamua kuyaishi hayo maisha ya ku share na dada yako basi endelea nayo”
“Ila leo ameombewa naona kasha mpiga sister kibuti”
“Umejuaje?”
“Kuna staili yao wakitazamana una ona kabisa ni kama glasi imesha vunjika”
Mlango wa chumba anacho fanyiwa upasuaji mzee Tiger ukafunguliwa na akatoka daktari wa familia. James na Jack wakasimama huku daktari akivua barakoa.
“Upasuaji wa mgonjwa una endelea. Ni upasuaji wa taratibu ambao uta chukua masaa nane mbeleni”
“Duuu”
“Ila tuna matarajio makubwa ya upasuaji huu kufnaikiwa. Nimeona nije kuwapa update ya kile kinacho endelea”
“Je kuna chochote muta hitaji kama chakula au vinywaji?”
James aliuliza.
“Hapana. Tuta endelea na upasuaji hadi pale tutakapo maliza”
“Sawa daktari kaendeleeni”
Jack alizungumza na dakatri akarudi ndani.
***
“Hivi una jua tuna mbuga ya wanyama”
“Weee ipo wapi?”
“Kutoka hapa hadi ilipo ni kama kilomita moja na nusu huko kwenda ni hadi tutumie gari”
“Tuna weza kwenda?”
Rose aliuliza akiwa na shahuku kubwa.
“Mmmm sio salama sasa hivi usiku umesha ingia kesho tuta kwenda.”
“Naogopa sana kulala hapa”
“Kwa nini?”
“Si unamuona mama mkwe alivyo tuwakia mimi na mume wangu”
“Mama mkwe wetu ni mtu wa kupanic sana. Hivyo ana mahasira yake tu hawezi kukufanya chochote”
“Mmm”
“Twende tukajue kinacho endelea”
Wakarudi ndani na kuwakuta James na Jack wakiendelea kupiga stori.
“Bado?”
Valentina alimuuliza mume wake
“Bado. Jamani nina njaa munaonaje mukaenda kuandaa chakula eti shem?”
“Sawa”
“Katupikieni warembo wetu”
“Sawa shem”
Rose alizungumza akimtazama James aliye mpa ishara ya kumruhusu kwenda kupika. Wakaondoka.
“Hivi maana ana tolea wapi nguvu ya ukataa pisi shameji yangu Rose?”
“Hata sijui mwenyewe ana waza nini?”
“Dishi lake halisomi signal”
Wakacheka kwa nguvu.
“Unajua hata mzee akitoboa kwenye hii oparesheni sidhani kama ata kuwa hai?
Jack alizungumza.
“MUNGU ndio anaye jua?”
“Kwa staili ya kukutana na majini una hisi kuna msaada wa MUNGU…..Weeee”
“Yana weza kumsaidia, kama yamemp utajiri yatashindwa kumpa afya?”
“Angesha pona saratani kama ni hivyo”
Sophia akawashangaa Rose na Valentina walio ingia jikoni.
“Vipi wifi zangu?”
“Salama tumekuja kuandaa chakula cha usiku”
“Wapishi wamesha anza kupika hivyo kapumzikeni tu”
“Tubaki baki humu huku jikoni”
Valentina alizungumza akimtazama Sophia.
“Sawa tujumuike kwa pamoja”
Sophia alizungumza na wakaendelea kuandaa chakula kwa pamoja.
***
“Nimeshindwa kutoka”
“Kwa nini?”
“Kijana wangu mdogo ndio mtu ambaye ana madaraka makubwa baada ya baba yake. Hivyo amenizuia kuto kutoka”
Mrs Tiger alizungumza akiwa maekaa bafuni.
“Kwani ulikuwa unataka kuzungumza nini?”
“Hali ya mume wangu ina zidi kuwa mbaya. Sidhani kama ata pona na ninavyo ona hawa watoto wana weza kunipiga kata funua. Nataka uangalie uwezekano wa mimi kumiliki hizi mali zote. Wanangu wamesha oa wanawake wapumbavu najiona kabisa nina kwenda kupata asilimia ndogo”
“Mmmm ila mfumo wa kurithi mali za familia ya Tiger upo wazi. Kuubadilisha ni ngumu”
“Umekuwa mwanasheria wa hii familia. Kuna makampuni yameanzishwa kipindi nimeolewa na yana mchango wangu. Tafadhali fanya jambo”
Mwanasheria akashusha pumzi nyingi.
“Ngoja niangalie kama kuna mwanya. Ila tambua kwamba wanao ni wasomi”
“Ndio ni wasomi ila una weza kufoji wosia na wosia wa mume wangu ukazungumzia mimi ndio mmiliki wa mali zote”
“Nitapata nini?”
“Asilimia kumi ya utajiri itakuwa yako”
“Kumi na tano”
“Kumi, hiyo ndio ofa yangu”
“Sawa mzee atakapo kufa nifahamishe nije hapo na wosia.”
“Usijali”
Mrs Tiger akakata simu.
“Wapuuzi hawa wananiona mimi mjinga ikiwa wote nimewaweka tumboni mwangu miezi tisa. Hawawezi kunishinda akili.”
Mrs Tiger akabadilisha mavazi aliyo kuwa ameyavaa kwa ajili ya kutoka na kwenda kukutana na mwana sheria wa familia. Akatoka chumbani na kuelekea nje ya chumba anacho fanyiwa upasuaji mumewe.
“Madaktari hawajasema chochote?”
Mrs Tiger aliwauliza wanaye kwa sauti ya upole.
“Wenge limekuisha bi mkubwa”
“Jack kwa hiyo mimi nina wenge”
“Unajiona upo sawa mama?”
“Dogo usimuongeleshe bi mkubwa hivyo”
“Ahaa mama ana zingua uje”
“Naombeni munisamehe. James nimejitafakari na kuona nimekosea sana sipaswi kukufanyia kile ambacho nilikifanya. Naomba unisamehe”
“Ukiona shetani ana omba msamaha ujue ni mtego huo”
Jack alizungumza akicheka.
“Mama una mpango gani kwa bro na mkewe?”
“Tafadhali Jack sihitaji kugombana na wewe?”
“Hahahaa mama sisi ni wanao. Hadi una omba msamaha ujue kuna mpango, una mpango gani?”
“Nimeamua kubadilika na kuungana na familia yangu. Hatuna haja ya kugombana”
“Mmmm bro akili kichwani mwako”
“Mama nimekuelewa.”
“Umenisamahe….Naomba hata mkeo nizungumze naye”
“Tuta zungumza wakati wa chakula cha usiku.”
“Sawa ila naomba unisamehe kwanza wewe”
“Mama nakuelewa hivyo kuwa na amaani”
“Asante mwanangu”
“Madaktari wana sema tuna masaa nane ya kusubiria toka walivyo zungumza hadi sasa hivi yamesha pita masaa mawili hivyo bado masaa sita”
James alimjibu mama yake.
“Sawa tuendelee kumuomba MUNGU”
“Nabii wako amepeperuka?”
Jack alimuuliza mama yake akimtazmaa machoni.,
“Amepata dharura?”
“Dharura…..?”
“Ndio”
“Ni nabii gani?”
“Kwani kuna haja gani ya kumjua”
“Mmaa kwani huyo nabii wako ni malaika kwamba hapaswi kujulikana? Wewe sema ni nani tumtime vijana wamlete hapa apige fire. Hii nyumba ina mashetani wengi sana”
Jack alizungumza akicheka.
“Sitaki Jack sitaki utani wako”
“Sio utani mama. Aje nabii hapa aseme mzee Tiger nyanyuka na mzee ana nyanyuka na ana pona hapo hapo”
“Mmmm”
James akaguna
“Si manabii wana fanya miujiza. Akifnaya muujiza huo nakuambia nitakuwa mwanafunzi wake kama mwanafunzi wa Yesu”
James akashindwa kujizuia na kucheka.
“Kwa akili zako wewe utakuwa Yuda”
Mrs Tiger alizungumza huku akitabasamu.
“Kwa kweli nikiona nabii ana zingua nina muuza tu ana kwenda kusulubishwa”
Wote wakacheka. Sophia akashangaa kuwaona kaka zake na mama yao wakicheka.
“Dada”
Jack alizungumza.
“Kuna nini mbona muna cheka sana?”
“Nataka kuwa mwanafunzi wa nabii wa mama yako halafu ninakuwa Yuda nina msaliti nabii naye ana kwenda kusulubishwa”
“Chizi kweli wewe.”
Sophia alizungumza akicheka.
“Chakula tayari twendeni tukale”
Wakanyanyuka na wakaongozana pamoja hadi katika meza ya chakula. Wakawakuta Valentina na Rose wakiwa tayari wamesha kaa. James na Jack wakakaa pembeni ya wake zao.
“Chakula mbona kina nukia sana?”
Jack aliuliza.
“Wake zenu ndio wapishi”
“Ahaa….”
“Ndio nina mawifi wapishi sana”
“Tusali”
Mrs Tiger alizungumza. Valentina na Rose wakamtazama kwa mshangao. Mrs Tiger akaombea chakula. Wakaanza kula huku sauti ya vijiko ikiwa ndio ina sikika.
“Tusikilizane”
Mrs Tiger alizungumza na kila mtu akaacha kula.
“Rose”
“Abee”
“James”
“Naam mama”
“Kwanza Rose karibu sana kwenye familia ya Tiger. Naomba unisamehe pale nilipo onyesha tabia ambayo haikuwa rafiki kabisa kwa upande wako”
Sophia na Jack wakatazamana kwa mshangao.
“Kama mama unapo faya makosa basi yana weza kupelekea mpasuko mkubwa wa familia hivyo nina waomba sana tena sana munisamehe kwa kila aina ya tabia ambayo nimewaonyesha”
“Usijali mama mimi kwa upande wangu nimekusamehe”
Rose alizungumza akitabasamu.
“Mama una maanisha?”
Jack aliuliza.
“Ndio nina maanisha kuomba msamaha kwa tabia yangu mbaya niliyo ionyesha.”
“Usijali mama nimekusamehe”
James alizungumza.
“Nawashukuru”
Wakaendelea kula.
‘Mama kuna kitu ana kipanga sio mjinga kuomba msamaha huyu mwanamke ana roho ngumu kuliko kawaida’
Jack aliwaza akilini mwake akimtazama mama yake.
‘Ana mpango gani ambao ana taka kutufanyia suprize?’
Jack alizidi kuwaza. Jack akawa wa kwanza kumaliza kula chakula kisha James naye akafwatia. Jack akampa ishara James na wakatoka nje.
“Kuna nini dogo?”
“Bro namjua mama. Hichi alicho kifanya leo hakijatoka moyoni, ana tumia mbinu ya kutuliza moto huku mkono wa kushoto ameshika kidungu cha petroli muda wowote ana weza kuilipua hii familia”
“Una waza an ampango gani?”
“Sijui ila sio mtu wa kujishusha vile mama. Kama ana uwezo wa kumuua mtu ana wezaje kuomba msamaha kirahisi namna hii bro huu ni mtego. Si wewe wala mkeo munao paswa kuuamini msamaha wake. Naona kabisa ana mpango wa ajabu”
Jack na James kila mmoja akawaza kwa upande wake ni mpango gani ambao mrs Tiger ana upanga dhidi yao.
ITAENDELEA
Mchaka mchaka mpya umeanza. Mrs Tiger amesha muandaa mwana sheria kwa ajili ya kuchukua mali zote za familia endapo mume wake ata fariki ana jipendekeza mbele ya wanaye ila Jack haamini kujishusha huko kwa mama yao je nini kita tokea? Ungana nami katika stori hii ya kusisimua sehemu ya 37
 
DEVIL’S FAMILY(FAMILIA YA MASHETANI) 37
.
KILA KILICHO ANDIKWA KATIKA HADITHI HII NI UTUNZI HAKIENDANI NA KISA CHOCHOTE KILICHO WAHI KUTOKEA MAHALA POPOTE ASANTE
*************************************************************************************

ILIPOISHIA
James alizungumza.
“Nawashukuru”
Wakaendelea kula.
‘Mama kuna kitu ana kipanga sio mjinga kuomba msamaha huyu mwanamke ana roho ngumu kuliko kawaida’
Jack aliwaza akilini mwake akimtazama mama yake.
‘Ana mpango gani ambao ana taka kutufanyia suprize?’
Jack alizidi kuwaza. Jack akawa wa kwanza kumaliza kula chakula kisha James naye akafwatia. Jack akampa ishara James na wakatoka nje.
“Kuna nini dogo?”
“Bro namjua mama. Hichi alicho kifanya leo hakijatoka moyoni, ana tumia mbinu ya kutuliza moto huku mkono wa kushoto ameshika kidungu cha petroli muda wowote ana weza kuilipua hii familia”
“Una waza an ampango gani?”
“Sijui ila sio mtu wa kujishusha vile mama. Kama ana uwezo wa kumuua mtu ana wezaje kuomba msamaha kirahisi namna hii bro huu ni mtego. Si wewe wala mkeo munao paswa kuuamini msamaha wake. Naona kabisa ana mpango wa ajabu”
Jack na James kila mmoja akawaza kwa upande wake ni mpango gani ambao mrs Tiger ana upanga dhidi yao.

ENDELEA
“Nitadukua simu yake ili kufwatilia mazungumzo yake au unaonaje hilo?”
“Fanya hivyo bro kwa maana bi mkubwa haeleweki huyu ni mtu wa kupiga mishe za siri sana namjua sana mama kuliko ninyi wote kwa maan amadhambi yake mengi nimeyafukia fukia mimi”
“Poa ngoja katika huu mwanya wa kujifaya ana tupenda na mimi nidukue simu yake”
“Nikuletee?”
“Wala hauna haja. Naidukua kwa kutumia simu yangu”
Wakarudi ndani na wakawakuta wake zao wakiwa nao wamesh amaliza kula.
“Wamekwenda wapi hawa mama?”
Jack aliuliza akikaa kwenye kiti alicho kuwa amekalia.
“Wametoa vyombo wapo jikoni”
James akaa kiti cha pembeni na mama yake, kwa kutumi app ya udukuzi aliyo itengeneza na kuihifadhi katika simu yake, akaidukua simu ya mama yake iliyopo mezani bila ya mama yake kufahamu.
“Leo si mutalala hapa na mkeo?”
“Tutaangalia kama tuta lala au tuta ondoka”
“Ila ni usiku ni bora mukalala”
“Sawa bi mkubwa”
“Nimeshiba jamani ngoja nikasubiria watakacho kizungumza madaktari”
Mrs Tiger akanyanyuka na kuwaacha wanaye mezani
“Shetani siku zote hawezi kuwa makini. Kuwa makini bro”
Sophia alizungumza akimtazama James.
“Usijali dada”
Sophia akachukua glasi yake ya juisi na akanyanyuka.
“Umefanikiwa?”
Jack aliuliza.
“Ndio. Hivyo kuanzia hivi sasa, simu na meseji zote zitakazo kuwa zina toka na kuigia nitakuwa nina zipata”
“Hapo sawa”
Jack akafungua picha aliyo tumiwa na Vaileth.
“Mtoto amesha panda ndege”
Jacka akamuonyesha James picha ya Vaileth.
“Una mpelekea hoteli gani?”
“Sijajua ila nita pata tu kwa kwenda kumficha”
“Mkeo una muagaje?”
“Nita muambia kuna dharura ya kikazi”
“Sawa”
Wakaelekea nje ya chumba anacho fnayiwa upasuaji mzee Tiger na wakamkuta Mrs Tiger akiwa maekaa peke yake. Wakajumuika naye katika kusubira masaa yaliyo salia. Valentina n aRose nao wakajumuika na wana famila kuendelea kusubiri habari watakayo pewa.
Majira ya saa nane usiku madaktari wakatoka katika chumba walicho kuwa wana mfanyia upasuaji mzee Tiger. Kila mtu akanyanyuka alipo kuwa amekaa kwa jaili ya kuwasikiliza madaktari.
“Poleni kwa kusubiria kwa kupindi kirefu sana”
“Tumesha poa. Mzee hali yake vipi?”
Jack aliuliza.
“Tumefanikiwa kuondoa damu iliyo kuwa imeganda katika ubongo na pia tumefanikiwa kuuziba mshono ambao ulikuwa una mwaga damu kichwani mwa mzee.”
“Kwa hiyo mume wangu atakuwa salama?”
“Kwa sasa tuna weza kusema kuwa kweka salam ni kwa asilimia thelathini. Jinsi atakavyo kuwa ana endelea kupatiwa matibu na uangalizi wa karibu basi asilimi ahizo zita panda taratibu.”
“Tuna weza kumuona?”
James naye aliuliza.
“Ndio ila kwa sasa hato hitaji kupata kelele kwani ubongo uja jaribu kurudi kwenye mfumo wake wa kawaida wa utendaji kazi. Pia hadi aje kuzinduka na kufumbua macho yake ita mchukua wiki kadhaa”
“Je ugongwa wake wa saratani?”
James alihojini.
“Nao tunaendelea kuufanyia utaratibu hadi aweze kupona”
“Asante sana dokta”
“Nawashauri kwa sasa mumuache mzee ajiuguze”
Jack akatoa simu mfukoni mwake, akasoma ujumbe wa meseji alio tumiwa kisha akuirudisha/
“Tunaweza kuingia na kumuona?”
“Ndio ingieni”
Wakaingia na kumuangaliza mzee Tiger aliye lala kitandani huku kichwa chake kikiwa kimefungwa na bandeji na anaendelea kupumua kwa msaada wa mashine ya oxygen. Jack akampa ishara Valentina na wakatoka nje.
“Kuna ishu nina kwenda kuishuhulikia. Hivyo ninatoka”
“Muda huu?”
“Ndio mke wangu kama unavyo jua mimi ndio nimechukua nafasi ya baba hivyo kila kitu ina bidi nikifanye mimi”
“Sawa ila kuwa makini”
“Usijali nipo makini mke wangu”
Wakarudi walipo simama wengine.
“Mimi nina toka kuna ishi nina kwenda kuifanya”
“Sasa hivi!?”
Mrs Tiger alimuuliza Jack kwa mshangao.
“Ndio mama”
“Poa mimi nipo nita angalia mazingira”
James alizungumza.
“Sawa bro nakuamini”
James na Jack wakepeana tano.
“Shem kuwa na amani. Lala vyema”
“Sawa shemeji”
Jack akatoka chumbani hapo.
“Mimi naenda zangu kulala nimechoka”
Sophia naye alizungumza na akatoka chumbani hapo.
“Kama kuna mtu atakuwa amechoka akapumzike. Mimi nita endelea kuwa na mgonjwa hadi kupambazuke”
“Sawa mama usiku mwema”
Valentina akaaga na kutoka chumbani hapo.
“James mwanangu mpeleke mwenzako akalale. Ni usiku sana sasa hivi”
“Eti umechoka?”
Rose akatingisha kichwa. Wakatoka na kumuacha Mrs Tiger na madaktari ambao wana peana zamu na wezao ili kuendelea kuifwatilia hali ya mzee Tiger ili chochote kitakacho tokea basi waweze kumsaidia.
“Umefunga vizuri mlango?”
Rose alimuuliza James.
“Ndio mbona muoga sana mke wangu?”
“Mmmm chochote kina weza kutokea”
“Ina maana huamini kama mama amebadilika?”
James alimuuliza Rose swali la kimtego.
“Kwa taaaluma yangu ya upelelezi niliyo somea. Ukiona adui yako amebadilika na kukufanya uwe rafiki kwake basi jua ndio wakati unao paswa kuwa makini zaidi ya pale mulivyo kuwa maadui kwani kukuvuta kwake ni maandalizi ya kukuua kwa kushtukiza. Hivyo kama ni umakini ina bidi tuuongeze kwenye kila kitu. Kuanzia vyakula, vinywaji kwani ana weza kupanga na mpishi yoyote kutuwekea sumu. Ndio maana nilimshauri Valentina tukaandae chakula wenyewe”
“Usemacho ni kweli mke wangu hivyo tutaongeza umakini mara dufu”
“Nashukuru sana mume wangu kwa kunielewa”
“Umechoka pumzika. Kuna kazi nahitaji kuifanya”
“Kwenye computer au?”
“Ndio kuna mifumo ya usalama katika akaunti za benki za familia ina bidi niziongezee. Kwani chochote kina weza kutokea”
“Bado una jali kuhusiana na mali za familia yako ambazo zilitaka kukutoa roho mume wangu?”
“Namsaidia Jack. Jack ni mzuri katika kuendesha oparesheni za kibiashara na kuyafanya mambo yaweze kutokea na kuwa vile anavyo taka yawe. Ila linapo kuja swala kimifumo ya kiuchumi hayupo vizuri. Namsaidia ili hata pale mama atakapo taka kufanya mapinduzi basi ashindwe”
“Sawa mume wangu”
“Kuwa na amani. Pesa niliyo nayo mimi ina nitosha mimi na watoto wetu kula hadi kufa kwetu”
“Sawa nimekuelewa”
Rose akambusu James mdomoni, akavua nguoa zake, akaingia bafuni na kuoga.
***
“Wifiiiii”
Valentina alishtuka mara baada ya kumuona Sophia akiwa amesimama mlangoni mwa bafu la chumbani kwake.
“Kipi kinacho kushangaza”
“Mume wangu ana weza kurudi muda si mrefu. Akikukuta humu ana weza ku…..”
“Sitaki kusikia kuhusiana na Jack hivi sasa. Una hisi una weza kuniacha kirahisi namana hiii”
Sophia alifoka huku akimsogelea Valentina aliye uchi.
“Una hisi ni rahisi kukuacha wewe eheeee?”
“Ila mimi nataka nitoke kwenye haya maisha. Nimesha olewa”
“Nani aliye fanya hadi ukutane na Jack? Ni mimi”
Sophia akambana Valentina ukutani.
“Umempenda Rose ehee?”
“Hapana Rose namuheshimu kama mke mwenzangu”
“Kwa nini umeniacha nimi niambie”
“Wifi nahitaji kuwa huru sihitaji maisha ya kusagana tena”
“Kuna mtu amekusukuma uniache si ndio”
Sophia akamshika Valentina kooni ila hajamkaba.
“Niambie ni nani ambaye amekufanya uniache”
“Mama ana jua mimi na wewe tuna mahusiano. Naipenda ndo yangu bado changa una hisi nikiachika hivi sasa itakuwaje”
“Una muogopa Jack”
“Ndio nina muogopa ni mume wangu. Mwanaume aliye nioa Sophia…..Naachaje kuto kumugopa hembu niambie nina patia wapi huyo ujasiri”
“Nita mueleza ukweli Jack”
“Nini?”
“Ndio siwezi kukucha. Sina mwanamke mwengine zaidi yako na nipo tayari ndoa yenu ivunjike ili tuwe pamoja”
“No no no unanikosea Sophia. Siwezi kuachana na Jack, una taka wazazi wangu wafe kwa presha kwa kusikia kuwa nimeachika kwenye ndoa yangu kwa sababu mimi ni msagaji hapana. Ni heri nife kuliko kuipata hiyo aibu au aibu hiyo kuileta kwenye familia yangu tafadhali”
Valentina alizungumza huku akilia.
“Naomba unielewe Rose nampenda Jack”
“Mimi hunipendi si ndio”
Sophia aliuliza kwa uchungu.
“Niambie ukweli, hunipendi mimi eheee?”
“Nakupenda ila naomba tu…..”
Sophia hakumpa nafasi Valentina ya kumalizia sentensi yake na akaanza kumnyonya denda. Kwa sababu ana ujua udhaifu wa Valentina kaanza kumtomasa maeneo yana mpagawisha Valentina na ndani ya muda mfupi Valentina akaanza kutoa ushirikiano wa Sophia huku akimvua Sophia nguo alizo zivaa na wote wakabaki kama walivyo zaliwa.
***
Jack akaminya akagonga mlango wa chumba alichopo Vaileth, haukupita muda mrefu mlango ukafunguliwa. Jack akamtazama Vaileth aliye valia bikini na sidiria.
“Nimekusubiria hadi usingizi umenipitia mpenzi”
Valeileth alizungumza huku akitembea mbele na kumfaya Jack ashuhudie makalio jinsi yanavyo tingishika. Jack kwa haraka akaingia ndani na akafunga mlango kwa ndani.
“Au dada yangu alikuwa ana kupa utamu”
“Wala”
“Ila”
“Mzee ana umwa hivyo tulikuwa tuna subiria tupewe majibu na madaktari”
“Majibu gani?”
“Amefanyiwa upasuaji wa kichwa hivyo nisinge weza kuondoka hadi nijua hali yake. Vipi umekula?”
“Nimekula, nimekunywa. Nakusubiria wewe tu unikule”
Vaileth akakaa kitandani na akaipanua miguu yake.
“Waoooo…….”
Jack kwa haraka akavua nguo zake na akapanda kitandani huku mzuka wa mapenzi ukiwa umepanda. Hakutaka hata kuivua bikini ya Vaileth alicho kifanya ni kuisogeza tu pembeni na kuanza kumpelekea moto Vaileth.
Mipinduano ikazidi kurindima ndani ya chumba walichopo huku kila mmoja akihakikisha ana mpatia mpenzi wake kitu roho ina penda.
Dakika ishirini za kwanza zikawatosha kila mmoja kumaliza mzunguko wa kwanza.
“Hembu ongeza AC kwa maana uta niua wewe mtoto”
“Hahahaaa”
“Ndio una jua mambo sana kuliko dada yako”
“Ina maana Valentina hakupi show kali kama hii?”
“Hanipi aisee…..Wewe ni moto wa kuotea mbali”
“Asante mwaya”
“Nyumbani umeagaje?”
“Nimewaambia kuna kazi nimeiomba Dar nimepigiwa simu asubuhi niwahi kwenye majaribio asubuhi hivyo huko kila mtu ana jua nimekuja kwa ajili hiyo. Waliniambia nifikie kwa dada nikamuambia ni mbali na ninapo hitaji kufanyiw ainterview”
“Sawa nahitaji usirudi home tena”
“Weee”
“Ndio nahitaji uwe mke wagu. Nataka kukuoa kisheria, sihitaji mwaname yoyote kukuchukua mikononi mwangu. Nimechanganyikiwa kwa penzi lako Vai sijiwezi, na nipo tayari kwa lolote ili mradi uwe mke wangu”
Vaileth macho yakamtoka kwa mshangao huku akiwa haelewi jibu la kumfa Jack ambaye anaonekana anacho kizungumza ni kitu anacho kimaanisha.
ITAENDELEA
Mchaka mchaka mpya umeanza. James amedukua simu ya mama yake je ata ata fanikiwa kujua mipango anayo panga mama yake? Jack amepagawa na penzi la Vaileth shemeji yake na ametangaza ndoa je Vaileth ata kubalian ana ombi la shemeji yake? Ungana nami katika stori hii ya kusisimua sehemu ya 38
 
DEVIL’S FAMILY(FAMILIA YA MASHETANI) 38

KILA KILICHO ANDIKWA KATIKA HADITHI HII NI UTUNZI HAKIENDANI NA KISA CHOCHOTE KILICHO WAHI KUTOKEA MAHALA POPOTE ASANTE
*************************************************************************************

ILIPOISHIA
“Ina maana Valentina hakupi show kali kama hii?”
“Hanipi aisee…..Wewe ni moto wa kuotea mbali”
“Asante mwaya”
“Nyumbani umeagaje?”
“Nimewaambia kuna kazi nimeiomba Dar nimepigiwa simu asubuhi niwahi kwenye majaribio asubuhi hivyo huko kila mtu ana jua nimekuja kwa ajili hiyo. Waliniambia nifikie kwa dada nikamuambia ni mbali na ninapo hitaji kufanyiw ainterview”
“Sawa nahitaji usirudi home tena”
“Weee”
“Ndio nahitaji uwe mke wagu. Nataka kukuoa kisheria, sihitaji mwaname yoyote kukuchukua mikononi mwangu. Nimechanganyikiwa kwa penzi lako Vai sijiwezi, na nipo tayari kwa lolote ili mradi uwe mke wangu”
Vaileth macho yakamtoka kwa mshangao huku akiwa haelewi jibu la kumfa Jack ambaye anaonekana anacho kizungumza ni kitu anacho kimaanisha.

ENDELEA
“Nakupenda sana Vaileth.”
“Jack kuolewa na wewe…… kuta nifanya nigombane na familia yangu. Familia yangu kama unavyo jua ni ya watu wacha MUNGU. Sidhani kama nitapewa baraka hizo na wazazi”
“Sikuharakishi mpenzi wangu fikiria na tafakari”
“Daaa unaniweka kwenye wakati mgumu Jack”
“Nita subiria jibu lako. Sawa mpenzi wangu?”
“Tumuombe MUNGU asaidie kipenzi kwa maana nina kigugumizi
“Kwa sasa usiharakishe kunipa jibu”
“Sawa”
“Unanipenda?”
“Ndio nina kupenda ila wewe ni mume dada yangu na ndo yetu haina hata wiki tatu”
“Kila kila kutu niachie mimi”
“Ila tafadhali usimuache dada yangu”
“Siwezi kumuacha”
Jack akazinyonya lipsi za Vaileth. Hawakupoteza muda mzunguko wa pili wa mechi ukaanza huku mzunguko huu ukichukua muda mrefu hadi kumalizika, huku wote wakiwa hoi. Hapakuwa na aliye na hamu ya kupiga stori wote wakalala.
***
“Mbona umeamka alfajiri mke wangu”
James alimuuliza Rose anaye jinyoosha viungo vyake.
“Nataka nifanye mazoeiz mume wangu. Sijazoea siku yangu kuanza na kulala”
“Kuna gym. Nguo sasa za mazoezi itakuwaje?”
“Ngoja nijaribu kumpugia Valentina nina weza kuvaliana naye”
“Yaah mjaribu yeye”
Rose akampigia simu Valentina. Simu ya Valentina ikaita hadi ikakatika, akampigia tena na kumfanya Valentina kufumbua macho yake, akamshtuka kumuona Sophia akiwa amelala pembeni yake huku wote wakiwa uchi.
“Wifi wifi”
“Mmmm”
“Kumesha kucha….amkaa”
Sophia akakurupuka. Akashuka kitandani n akuanza kuvaa nguo zake haraka haraka. Akatoka chumbani kwa Jack na akaelekea chumbani kwake.
“Saa kumi na mbili na dakika tano, ana taka nini?”
Valentina alijiuliza na akaipokea simu ya mke mwenzie.
“Valentina pole nimekuamsha asubuhi asubuhi”
“Usijali kipenzi, vipi kwema?”
“Kwema. Samahani naomba guo za mazoezi kama huto jali”
“Ohoo njoo uchukua”
“Nashukuru”
Rose akakatasimu akimtazama James aliye jilaza kitandani.
“Ngoja nikafanye fanye mazoezi hadi saa mbili hivi”
“Sawa mke wangu, mimi ngoja nilale kwa maana sina hata dakika ishirini toka nilivyo panda kitandani”
Rose akambusu James mdomini kisha akaelekea chumbani kwa Valentina, akagonga mara moja mlango na Valentina akamruhusu kuingia.
“Pole kwa kukusumbua”
“Asante”
“Kwanza shemeji yupo?”
“Hapana toka alivyo ondoka usiku hajarudi”
“Umelala mwenyewe”
“Weee acha tu baridi yote ya usiku nimeniishia mwenyewe”
“Pole”
“Ahaa asante nimesha zoea.”
“Naomba unisaidie nguo za mazoezi”
“Tena kuna ambazo nimezinunua dubai, ngoja nikuonyeshe”
Valentina akafungua kabati la nguo na kutoa nguo kadhaa mpya za mazoezi pamoja na raba za mazoezi.
“Chugua utakazo kwa maana niliziona sehemu nikazipenda nikanunua za kutosha”
Rose akachuagua suruali ya mazoezi na koti pamoja na raba.
“Zina nitosha hizi”
“Kweli?”
“Ndio. Twende basi tukafanye wote mazoezi”
“Mmmmm leo nimechoka ila kwa ajili yako ngoja niende tu”
“Asante”
“Ngoja nikaoge”
Valentina akaingia bafuni kisha akarudi na akavaa nguo za mazoezi. Wakaelekea katika jengo la gym.
“Kwenye ile mbuga tuta kwenda wote?”
Rose aliuliza huku wakitembea kwa mwendo wa taratibu katika treademil.
“Ndio tukimaliza twende ukapaone”
“Sawa”
“Ila itabidi twende na walinzi hata wawili”
“Si umezoeana nao?”
“Sio kivile ila kwa kuwa wana nijua hivyo tuna weza kuwaambia na kwenda”
“Sawa”
Rose akatabamu huku akilini mwake anacho kiwaza ni bwawa ambalo gprs ya baba yake ilionekana kwa mara ya mwisho. Sakika sabini zikawatosha kufnaya mazoezi huku wote wakiwa wamelowana na jasho.
“Tubabadili nguo au twende hivi hivi?”
“Hapana hivi hivi”
“Sawa”
Wakatoka nje ya gym.
“Tuna taka kwenda zoo. Nahitaji gari”
“Sawa madam”
“Utupeleke”
“Post yangu nimepangiwa hapa”
“Wasiliana na mkuu wako”
“Mkuu, wakwe wa familia wana hitaji kuelekea kwenye mbuga”
Mlinzi anaye lina eneo la gym aliwasiliana na mkuu wao wa kazi kwa kutumia redio maalumu za kuwasiliana.
“Sasa hivi?”
“Ndio.”
“Wapeleke hakikisha wana kwenda salama na kurudi salama.”
“Sawa boss. Mkuu ameniruhusu hivyo naomba nikachukue gari”
“Poa”
Mlinzi akaondoka.
“Hivi hili kasri lina ukubwa gani?”
“Mmmmm huyu mzee nahisi alinunua mji. Unajua ni kubwa sana jana tumetembea tu eneo la nyumbani. Ila hii fukwe nzima kwende kule mbele ni eneo lao. Kule kuna minazi kuna mashamba. Ni mbali”
“Duuu na walinzi?”
“Walinzi hapa sijui wapo wangapi ila wapo wengi sana. Na wana badilishana shift.”
“Unajua harusi yangu ilifanyika hapa”
“Kumbe?”
“Ndio hatukwenda hata kanisani kila kitu kilifanyika hapa hapa. Hadi raisi wan chi alikuja”
“Raisi?”
“Ndio. Hii familia nina sikia ina nguvu sana sio tu kwenye jamii hadi kwenye mambo ya kiutawala wa nchi na wana maamuzi kwenye mambo kadhaa kadhaa yanayo husiana na hii nchi”
“Mmmm”
“Tuna bahati ya kuolewa na vijana wao”
“Kwa kweli ila nikuulize kitu?”
“Niulize?”
“Mama mkwe kwa jinsi alivyo kuwa hanipendi na akaja kubadilika galfa hivi una ona ni ana mpango gani?”
“Kwa kweli huyu mama mimi pia simuelewi kwa maana na kuna ishu yangu moja hivi anaifahamu. Ishu ambayo kwa mara ya kwanza alinichimba mkwara kwa hasira sana ila ndani ya muda mchache akatabasamu na maisha yakaendelea. Hivyo kuna muda tuna paswa kuwa makini shosti yangu na mama mkwe”
“Ulifanya ishu gani?”
“Ahaa….tuiache tu ila ni mtu ambaye kwa muda huu mchache nilio kaa naye, ana kasirika na anakuoyesha wazi ana kasirika ila baadae muna kaa na kucheka kama vile hakuna kilicho tokea”
“Duuu”
Mlinzi akafika na gari eneo walipo simama. Wakaingia na kukaa siti za nyumana taratibu wakaondoka eneo la Gym.
“Katika eneo la mbuga ya wanyama mta waangalia tu mukiwa ndani ya gari, kwa asubuhi hii ni hatari kutembea mbugani kwani wanyama ndio wana toka kwenda kujitafutia malisho yao ya kila siku”
Mlinzi aliuliza.
“Nikajua wana fugwa?”
Rose aliuliza kwa mshangao.
“Kufugwa wana fugwa ila kwa asubuhi wana achiwa kuwinda na baadae kuna maeneo yao huwekewa vyakula kutokana na jamii ya wanayama”
“Ohooo hapo sawa kuna wanyaama wa aina gani?”
“Wa kila aina wapo”
“Kumbe?”
“Ndio”
Wakafika katika katika geti la kuingilia bugani.
“Kumbe wametengenezewa na uzio?”
Rose aliendelea kuuliza maswali ya kudadisi.
“Ndio kwa ajili wasitoke eneo hili na kuja eneo la makazi”
Wakafika hadi katika nyumba iliyo jengwa mbugani.
“Hapa ni wapi tena?”
Rose aliuliza.
“Hapa ni kama hoteli. Wageni wanao hitaji kuja kutembelea na kulala hapa mbugani wana fikia hapa.”
Walinzi wawili wakatoka ndani ya nyumba.
“Karibuni”
“Asante sana. Huyu ni mke mwenzangu anaitwa Rose”
“Karibu sana”
“Asante.”
Amenisumbua toka jana ana hitaji kuona mbuga.”
“Karibu naitwa Ramanadhani. Ndio mkuu wa usimamizi wa mbuga hii.”
“Nashukuru kukufahamu”
“Tuna magari ta kutembelea mbugani hivyo tuna weza kwenda nikawatembeza”
“Sawa”
Wakaingia katika gari maalumu ambalo hutumiwa katika matembezi ya Mbugani. Mkuu wa mbuga akawataembeza maeneo mbalimbali ya mbuga na kuwaeleezea historia ya eneo hilo.
“Kumbe hii mbuga ipo kwa muda mrefu?”
“Ndio toka muanzilishi wa huu ukoo. Ikaendelezwa na baba yake Tiger kisha mzee wa sasa naye ana iendeleza.”
“Kwa hiyo hawa wanyama wamezaana vizazi na vizazi?”
“Ndio”
“Ni wanyama tu wa ardhini ndio wana fugwa?”
“Hapana kuna bwawa kubwa sana lenye mamba na samaki”
“Weeee, unajua sijawahi kuona mamba”
Rose alizungumza.
“Hujawahi?”
Valentina aliuliza kwa mshangao.
“Haki ya nani nina waona kwenye tv tu. Ila kuwaona hivi kwa macho sijawahi”
“Kutoka hapa tulipo hadi kufika kwenye bwana ni kama dakika ishirini hivi. Tutaelekea hapo”
“Nitafurahi kuwaona”
Rose alijibu huku mapigo ya moyo yakimuenda kasi. Wakaendelea kuzunguka katika mbuga ambayo ni kubwa na ipo pembezoni mwa bahari. Wakafika eneo la bwawa lenye mamba wakali.
“Naruhusiwa kushuka?”
“Ndio ila musisogelee karibu na bwana”
Rose akashuka huku Valentina naye akashuka kwenye gari. Mlinzi waliye ongozana naye, akashuka ndani ya gari.
“Mbona una tetemeka?”
Valentina alimuuliza Rose.
“Hawa wadudu wa tisha hivi?”
Rose alijibu kwa kudanganya.
“Ndio, yaani hapo mtu ukiingia wana kuralua chap una potea”
Valentina alizugumza wakitazama jinsi mamba hao wanvyo katiza katiza ndani ya maji. Ramadhani akashuka ndani ya gari.
“Kwa sasa hawa mamba madam ana mpango wa kuwavuna na kuwauzia wachina kama chakula”
“Wana liwa?”
Rose alijifanya kuuliza swala la kishamba.
“Ndio wana liwa na ni nyama tamu sana. Wapo wengi sana hadi kuna mpango wa kuliongeza hili bwawa”
“Narushusiwa kupiga picha?”
“Ndio nyinyi ni wana familia”
Rose akapiga picha kadhaa kwa simu yake.
‘Ina maana baba yangu na ndugu zangu walivyo waua wakaja kuwatupa hapa.’
Rose aliwaza akilini mwake. Akazidi kujizuia hasira yake yake isionekane na wengine. Akawa mtu wa kwanza kurudi ndani ya gari na kila mtu akarudi ndani ya gari.
“Usiowaope”
Valentina alimfariji Rose akimshika kiganja.
“Nina amani kidogo nimerudi ndani ya gari. Eti huwa wana toka ndani ya bwawa?”
“Tungekuja mida ya mchana tusinge simama tulipo kuwa tumesimama kwani hutoka na kuota jua.”
“Ohooo. Nimefurahi sana kuiona hii mbuga”
“Umeridhika? Kwa maana kuna maeneo hatujatembelea?”
Valentina alimuuliza Rose akimtazama usoni.
“Maeneo gani?”
“Maeneo ya kufugia majoka yale makubwa. Huko ndio kuna tisha mwenyewe nilishindwa kuvumilia”
“Ina tosha kwa leo”
Rose alizungumza huku moyoni mwake kukiwaka moto, wa kulipa kisasi kwa wahusika walio husika na kifo cha baba yake na kaka zake.
ITAENDELEA
Mchaka mchaka mpya umeanza. Rose amefanikiwa kufika katika bwawa ambalo kaka zake na baba yake walitupwa wakiwa hai na kuuliwa na mamba. Hasira na hamu ya kulipiza kisasi imamejaa moyoni mwake je kuwepo ndani ya Familia yam zee Tiger ita msaidia kulipa kisasi? Ungana nami katika stori hii ya kusisimua sehemu ya 39
 
DEVIL’S FAMILY (FAMILIA YA MASHETANI) 39


KILA KILICHO ANDIKWA KATIKA HADITHI HII NI UTUNZI HAKIENDANI NA KISA CHOCHOTE KILICHO WAHI KUTOKEA MAHALA POPOTE ASANTE
*************************************************************************************

ILIPOISHIA
“Usiowaope”
Valentina alimfariji Rose akimshika kiganja.
“Nina amani kidogo nimerudi ndani ya gari. Eti huwa wana toka ndani ya bwawa?”
“Tungekuja mida ya mchana tusinge simama tulipo kuwa tumesimama kwani hutoka na kuota jua.”
“Ohooo. Nimefurahi sana kuiona hii mbuga”
“Umeridhika? Kwa maana kuna maeneo hatujatembelea?”
Valentina alimuuliza Rose akimtazama usoni.
“Maeneo gani?”
“Maeneo ya kufugia majoka yale makubwa. Huko ndio kuna tisha mwenyewe nilishindwa kuvumilia”
“Ina tosha kwa leo”
Rose alizungumza huku moyoni mwake kukiwaka moto, wa kulipa kisasi kwa wahusika walio husika na kifo cha baba yake na kaka zake.

ENDELEA
“Vipi umefurahi kuwaona wanyama?”
Valentina alimuuliza Rose.
“Sanaa”
Wakafika walipo liacha gari, wakaagana na msimamizi wa mbuga, wakapanda gari walilo toka nalo nyumbani na kuanza kurudi katika nyumba ya mzee Tiger.
“Asante eheee”
Valentina alimuaga mlinzi waliye ongozana naye kisha wakashuka ndani ya gari na kuingia ndani.
“Nimewatafuta mulikuwa wapi?”
Mrs Tiger aliwaulizaza akiwatazama Rose na Valentina.
“Kwanza shikamoo mama”
“Marahaba”
“Shikamoo mama”
“Marahaba Rose. Ehee mulikuwa wapi?”
“Tuliwenda Mbugani mama. Nilimpelekea Rose akashangae shangae wanyama”
“Ohooo kumbe?”
“Ndio mama Valentina alinieeleza kuhusiana na mbuga ya wanyama hivyo nikawa na hamu kubwa sana ya kuona kinacho endelea eneo hilo”
“Mama huwezi amini mkweo ana ogopa mamba”
“Mamba!?”
Mrs Tiger alijifanya kuuliza kwa mshangao.
“Ndio mama. Amewaona mambo hadi ana tetemeka”
“Dooo si muliwaona kwa mbali?”
Mrs Tiger alimuuliza Rose, akimtazama machoni.
“Ndio mama tulisimama mbali”
Valentina alijibu kwa furaha, ila Rose uso wake una tabasamu akijitahidi kuificha hasira yake.
“Wale mamba wamezaliana sana hivyo nina mpango wa kuwauza kwa watu wana penda kula nyama yao”
Mrs Tiger alizungumza akijaribu kumdadisi Rose.
“Ohoo ni wazo zuri mama”
“Okay tuachane na stori za mamba kaogeni, tuje kula kuna mahala nina taka twende pamoja by saa nne hivi”
“Sawa mama”
Valentina alijibu.
“Rose nawe pia?”
“Sawa mama”
Rose akatabasamu na akawa wa kwanza kuondoka huku Valentina akimfwata kwa nyuma.
‘Atakuwa amegundua jambo au?’
Mrs Tiger alijiuliza swali lililo kosa jibu. Rose akaigia chumbani, akamkuta James akiwa bado hajaamka. Akavua viatu na nguo na kuelekea bafuni, akaufunga mlango wa bafuni kwa ndani, akafunuga bomba la maji, akakaa kwenye kona ya bafu na kuanza kulia kwa uchungu sana. Kwa picha ya hisi akawaza jinsi ndugu zake na baba yake walivyo kuwa wana rushwa ndani ya bwawa la mamba.
‘Relax kisasi chako kita fika. Taratibu endelea kuaminka Rose’
Rose aliwaza akilini mwake, akajifuta machozi, akanyanyuka, akasimama mbele ya kioo na kuutazama uso wake.
‘Muda uta fika wa kuwafanya walipe kwa kile walicho kifanya ni lazima walipe’
Rose alizidi kujiapiza.
“Babe”
Sauti ya James ikamtoa kwenye ndimbwi la mawazo.
“Babe”
“Abeee”
“Mbona umejifungia”
Kwa haraka Rose akajipitisha kwenye bomba la mvua na mwili ukalowana maji kisha akafungua mlamgo na James akaingia ndani.
“Upo sawa?”
“Yaa nimechoka tu mume wangu”
Rose akachukau sabuni ya maji na kuanza kujimwagia mwilini mwake. James akajisaidia haja ndogo.
“Babe”
“Naam”
“Mama ametuambia tunywe chai na tutoke naye”
“Utoke na mama yangu?”
“Ndio ila nipo na Valentina”
“Kwenda wapi?”
“Hajatuambia”
“Eheee?”
“Yaa hapa nina oga, kisha nishuke huko chini, nikanywe chai ndio tutoke pamoja”
“Mama yangu simuamini, ngoja nikamuhoji kwanza”
“Tafadhali mume wangu hii ni asubuhi, sitaki marafakano na mama yako, acha niongozane naye”
“Oya hapa tuna zungumzia usalama wako”
“Una hisi ata nidhuru nikiwa nimetoka na yeye? Sidhani kama ana weza kuwa na akili mbaya namna hiyo”
James akamtazama Rose.
“Hawezi kuwa na amani”
“Usimuamini kwa chochote”
“Usijali mume wangu. Bado una endelea kulala?”
“Nilitaka nikalale ila kwa ulicho niambia nimeishiwa usingizi”
Rose akamshika mkono James na akamvuta katikati ya eneo la maji ya bomba la mvua yanapo mwagika. Akamkumbatia kwa nguvu James.
“Nakupenda mume wangu”
Rose alizungumza kwa uchungu na hisi kali.
“Nakupenda pia mke wangu. Una jua nina weza kufanya chochote kwa ajili yako”
Rose akakingiza kiganja cha mkono wake wa kulia ndani ya boxer ya James na kuanza kumtomasa jogoo wa James na taratibu akaanza kusimama. Kuongeza hisia ya anacho kifanya, akaanza kuyonyana dena na James na hisia kali za mapenzi zikaongezeka kati yao. Akamvua boxer James na wakajikuta wakipiga show wakiwa bafuni.
***
Valentina akajifuta maji na taulo kwnai ametoka bafuni kuoga, akaichukua simu yake kitandani na akampigia Jack. Simu ya Jack ikaita hadi ikakata, akarudia kumpigia kwa mara ya pili na simu ikapokelewa.
“Mke wangu”
“Mbona nina kupigia hupokei mume wangu?”
“Nipo kwenye kikao. Vipi umeamkaje?”
“Nimeamka poa. Umelala kweli?”
“Nilale nina raha gani mke wangu. Hapa nimechoka mwili hadi akili”
“Unarudi saa ngapi?”
“Mmm mchana. Kwa maana nikimaliza kikao baadae nina wafanyakazi nina taka kukuaa nao na kufanya nao kikao pia”
Jack alizungumza huku akiyatomasa makalio ya Vaileth aliye lala kifudifudi pembeni yake.
“Sawa mume wangu. Naomba ruhusa mama ameniambia nitoke naye?”
“Muna kwenda wapi?”
“Hajasema”
“Leo?”
“Ndio natoka naye na Rose”
“Mmmmm!”
Jack akakaa vizuri kitandani.
“Sawa”
“Mbona umeguna?”
“Hamna. Kikubwa kuweni makini”
“Sawa mume wangu”
Jack akakata simu. Akajifikiria kwa sekunde kadha.
‘Mama ana wapeleka wapi hawa watu?’
Jack alijiuliza. Akataka kumpigia mama yake ila akasita. Akampigia mlinzi mkuu wa familia.
“Boss”
“Upo nyumbani?”
“Ndio”
“Mama ana toka na wake zetu. Naomba uhakikishe wana kwenda na kurudi salama huko waendapo”
“Nitazingatia hilo”
“Umebahatika kuangalia afya ya mzee?”
“Ndio nimeingia chumbani asubuhi hii hali yake ipo vile vile”
“Sawa. Walindwe hao, kama unavyo elewa mishe za bi mkubwa huwa hazieleweki”
“Nimekuelewa boss”
“Asante”
Jack akakata simu. Akampigia simu James ila haikupokelewa, akampigia kwa mara ya pili na haikupokelewa.
“Mbona humuamini mama yako?”
“Mmmmm?”
“Mbona humuamini mama yako?”
Vaileth alimuuliza Jack huku akijigeuza na kulala chali.
“Ahaa kuna mambo ya kifamilia yana endelea hivyo hatumuamini”
“Mama yenu wa kumzaa?”
“Ndio”
“Mbona yule mama ni mtu mwema”
“Kuwa mwema hamaanishi una aminika mpenzi. Tuachane na hayo, nina wazo”
“Wazo gani?”
“Nahitaji kukupa nyumba na gari, uishi hapa Dar kisha uta waambia nyumbani kwenu kwamba umepewa hivyo vitu na kampuni.”
“Jack jamani mbona una nipeleka haraka mpenzi wangu. Una jua fika kwamba mimi ni mwizi wa penzi la dada yangu”
“Achana na dada yako. Mimi nina zungumzia kuhusiana na wewe na maisha yako.”
Jack alizungumza kwa msisitizo.
“Au una taka niwe na kutomb** tu kisha maisha yako yawe sifuri si ndio?
“Hapana mpenzi usikasirike”
“No kwa maana hapa najaribu nikuwekee wewe maisha yako sawa ila una waza tu dada dada…..Hujui kama dada yako ana mahusiano ya kimapenzi na dada yangu eheee?”
Jack alifoka.
“Ngoja kwanza umesema?”
“Achana na hiyo mada”
Jack akaingia bafuni na kumfanya Vaileth kushuka kitandani na kumfwata bafuni.
“Tuzungumze….umesema dada yangu ana mahusiano ya kimapenzi na dada yako?”
Jack akamtazama Vaileth kwa sekunde kadhaa.
“Ndio”
“Ina maana ni msagaji?”
“Ndio”
“MUNGU wangu!”
Vaileth akajifanya kushangaa.
“Nisikilize nina lijua hilo kabla ya kumuoa ila sitaki ajue kuwa nina jua unanielewa?”
“Ahaa…”
“Unaielewa?”
“Ndio mpenzi
“Nahitaji mwanamke wa kwangu peke yangu ndio maana nipo na wewe”
“Nimekuelewa mpenzi wangu”
“Yaa hivyo tulia nikutengenezee maisha na ikiwezekana nikuoe kabisa. Kama ni kuzungumza na wazazi wako mimi ndio nitakaye zungumza nao”
“Sawa.”
Vaileth alijibu kumridhisha Jack ila moyoni mwake ana ona hatari kubwa kwake, kwani familia yake ina weza hata kumtenga kwa usaliti anao mfanyia dada yake wa tumbo moja.
***
“Shikamoo mama”
“Marahaba. Karibu unywe chai”
James akavuta kiti na kukaa, akawatazama Rose na Vaileth ambao wamesha pendeza kwa ajili ya safari.
“James nataka kutoka na wakwe zangu”
“Munakwenda wapi?”
“Tuta kuwa na mizunguko mingi leo. Ila moja nataka kuwapeleka kwenye kampuni ya vipodozi, nikawatambulishe kwa wafanyakazi. Nina mpango wa kuwapa share na usimamizi wa kampuni hiyo”
Rose na Valentina wakamtazama Mrs Tiger kwa mshangao.
“Mimi sasa hivi nazeeka, dunia ipo kasi kuna ushindani wa kila mahali. Rose wewe una ujuzi mkubwa wa biasharaha hivyo nimeona kila mmoja nimpe share ya asilimia ishirini na tano za kampuni yangu. Mimi nitabaki na asilimi ishirini. Sasa kazi kwenu, mujitahidi kunipatia wajukuu kabla sijakufa”
“Asante sana mama”
Rose na Valentina walijikuya wakijibu kwa pamoja.
“Upo seriously, mama?”
James aliuliza.
“Ndio. Tuta pita kwa mwana sheria wa familia. Ata andaa taratibu zote za kutoa share zangu kwa wakwe zangu baada ya hapo wata saini. Hivyo wote kama hamto jali mutakuwani wakurugenzi wasaidizi wa kampuni. Nahitaji kila mmoja uwezo wake ufanye kazi”
“Nakuahidi mama nita tumia uwezo wangu wote kufanya kazi uliyo nipa”
Rose laijibu akimtazama Mrs Tiger kwa furaha.
“Hata kuleni sasa twende tuna long day”
Mrs Tiger akaendelea kula. James akamtazama mama yake na kuendelea kula taratibu. Mrs Tiger na wakwe zake wakamaliza kula. Wakatoka nje na kuingia katika gari moja aina ya Cadilic Escalade mbele zikatangulia gari mbili za walinzi aina ya Land Cruiser LC 300 an nyuma yao zikafwatia gari nyingine mbili za aina hiyo na safari ya kuelekea katika kampuni kubwa ya Mrs Tiger inayo jishuhulisha na vipodozi ya kila aina ikaanza. James akatoka nje na kutazama msafara huo jinsi unavyo ondoka nyumbani kwake. Akampigia simu Jack.
“Bro nimekupigia hujapokea”
“Nilikuwa bafuni.”
“Wife ameniambia wana toka na mama?”
“Ndio ana kwenda nao katika kampuni yake ya vipodizo na taarifa ni kwamba ana kwenda kumpa kila mkwe wake asilimia ishirini na tano ya share zake katika kamouni”
“Asilimia ishirini na tano?”
“Ndio dogo”
“Mmmm mama ana mpango gani aisee mboa gafla sana.”
“Nashindwa kuelewa aisee. Ina tupasa kuwa makini kwani hizi asilimia ishirini na tano anazo zitoa zina weza kurudi kwa kitu kikubwa zaidi ya hizo. Tuwe macho dogo”
James alizungumza akiwa haamini kabisa kama mama yake ana toa asilimia hamsini ya hisa za kampuni yake na kuwapa wakwe zake hususani Rose ambaye ni mtoto wa adui ya familia ya mzee Tiger.
ITAENDELEA
Mchaka mchaka mpya umeanza. Mrs Tiger ana toa asilimia hamsini za kampuni yake na kuwapa wakwe zake, je ana mpango gani wa siri ambao ana taka kuutekeleza? Ungana nami katika stori hii ya kusisimua sehemu ya 40.
 
DEVIL’S FAMILY(FAMILIA YA MASHETANI) 40


KILA KILICHO ANDIKWA KATIKA HADITHI HII NI UTUNZI HAKIENDANI NA KISA CHOCHOTE KILICHO WAHI KUTOKEA MAHALA POPOTE ASANTE
*************************************************************************************

ILIPOISHIA
“Bro nimekupigia hujapokea”
“Nilikuwa bafuni.”
“Wife ameniambia wana toka na mama?”
“Ndio ana kwenda nao katika kampuni yake ya vipodizo na taarifa ni kwamba ana kwenda kumpa kila mkwe wake asilimia ishirini na tano ya share zake katika kamouni”
“Asilimia ishirini na tano?”
“Ndio dogo”
“Mmmm mama ana mpango gani aisee mboa gafla sana.”
“Nashindwa kuelewa aisee. Ina tupasa kuwa makini kwani hizi asilimia ishirini na tano anazo zitoa zina weza kurudi kwa kitu kikubwa zaidi ya hizo. Tuwe macho dogo”
James alizungumza akiwa haamini kabisa kama mama yake ana toa asilimia hamsini ya hisa za kampuni yake na kuwapa wakwe zake hususani Rose ambaye ni mtoto wa adui ya familia ya mzee Tiger.

ENDELEA
“Kuna walinzi nimewaambie wapeleleze hicho wanacho kwenda kukifanya kisha wanipatie ya kile kinacho endelea”
“Sawa unipanga”
“Poa bro”
James akakata simu akimtazama mmoja wa walinzi akimfwata.
“Mkuu”
“Mimi sio boss wenu bwana. Niambie Martin”
“Salama una muda tukazungumza?”
“Ndio”
“Kuna jambo lina endelea una paswa kulifahamu”
“Jambo gani?”
“Walinzi wengi wamechukizwa na kitendo cha mauaji uliyo yafanya kwa wezetu. Baadhi wana jiapiza kulipa kisasi kwako. Hivyo kuwa macho usiwamini”
James akamtazama Martin.
“Ilitolewa amri na wazee ya wao kuniua. Sikuwa na jinsi zaidi ya kupambana maisha yangu na sikutaka kuwaua ila wao walionyesha dhamira ya kuniua”
“Ina eleweka ila baadhi ni marafiki zetu hivyo kuwa makini”
“Nita jaribu kuzungumza nao”
“Sidhani kama ni wazo zuri. Mtu peke anaye msikiliza hivi sasa ni Jack”
“Sawa nitajua cha kufanya. Nashukuru kwa hiyo taarifa”
“Usijali boss”
James akarudi ndani. Akaelekea moja kwa moja chumbani kwake na akaendelea na majukumu yake.
***
“Mama mkwe”
Rose alita akimtazama Mrs Tiger.
“Abee”
“Naomba kuuliza swali”
“Uliza tu mkwe wangu”
“Kwa nini umefanya maamuzi kama haya?”
“Nimesha waeleza kuwa nafanya hivi kwanza umri wangu umesha kwenda nahitaji kupumzika na kumuuguza mume wangu. Pili nahitaji ninyi kama wakwe zangu nanyi mujisikie kuwa ni wana familia wa familia ya Tiger.”
“Ila una hisi wifi Sophia ata furahia maamuzi haya ikiwa yeye ndio binti wa kike kwenye fmailia?”
“Sophia yeye ana urithi wake ana mali zake hivyo haingii kwenye mali zangu. Kuwa na amani Rose sawa”
“Sawa”
Wakafika katika jengo la gorofa ishirini ambalo lina milikiwa na kampuni ya Mrs Tiger. Wakakuta wafanyakazi kadhaa wakiwasubiria nje ikiwamo viongozi wote w akampuni.. Wakapokelewa kwa heshima na moja kwa moja wakaingia ndani ya jengo hilo. Mrs Tiger akawatambulisha Valentina na Rose kwa wafanyakazi kisha kikao cha viongozi wa ngazi ya juu wa kampuni kikafanyika na Mrs Tiger akawatangaza Rose na Valentina kama wamiliki wenza wa kampuni hiyo huku kila mmoja akiwana asillimia ishirini na tano za umiliki. Hapakuwa na aliye biasha ujui wa wakurugenzi wapya ambao ni Rose na Valentina.
“Ninacho waomba ni kuwapa ushirikiano kama ule mulio kuwa muna nipatia mimi”
Mrs Tiger mara baada ya kufanya utambulisho akamaliza kikao na wakaelekea ofisini kwake na kumkuta mwana sheria akiwa tayari amesha andaa mikataba ya makabidhiano ya hisa. Akawatambulisha kwa mwna sheria kisha kila mmoja akapewa mkata unao fanana kila kitu kasoro ya majina ya wao wanao kabidhiwa.
“Pitieni mikataba yote vyema kabla hajatia sahihi.”
Mwanasheria alisisitiza na kila mtu akapitia mkatabasa wake wa kukabidhiwa hisi asilimia ishirini na tano. Rose akapitia kipengelea kwa kipengele, neno kwa neno, mstari kw amstari hadi akamaliza mkataba huo.
“Nimeuelewa”
Rose alizungumza akiuweka mkataba juu ya meza. Akamtazama Valentina ambaye tayari amesha tia sahihi katika mkataba wake. Rose naye akaweka sahihi ya maandishi pamoja na sahihi ya dole gumba.
“Karibuni sana kwenye familia yangu”
Mrs Tiger alizungumza akiwa na furaha.
“Asante mama”
Rose alizungumaza akipeana mkono na Mrs Tiger.
“Inabidi niwapelekeae kiwandani muka shuhudie jinsi vipodozi vinavyo zalishwa kwa ubora wa hali ya juu. Mmimi katika uongozi wangu nmefanikiwa kufanya soko labidhaa zetu kufika hadi nchi kubwa kama Marekani na China. Mission yenu ninyi wawili ni kuhakikisha tuna endelea kubaki ndani ya soko la kimataifa na kufungua branch kubwa zaidi kila kona ya dunia hii. Tunaelewana warembo wangu?”
“Ndio mama”
“Muambieni mlinzi awatembeze maeneo munayo taka kuweka ofisi zenu kwa ajili ya kuanza kazi mara moja”
“Sawa mama”
Valentina aliitikia, wakanyanyuka na kutoka ofisini kwa Mrs Tiger. Wakawatazama.
“Naweza kukuuliza una mpango gani kwa maana nimshtushwa ulivyo niambia niandae mkataba kama huu?”
Mrs Tiger akatabasamu.
“Mbona una ogopa?”
“Kuogopa ni lazima kwa jinsi ulivyo pigania hii kampuni halafu galfa tu una kabidhi kiasi kikubwa cha hisi kama hivyo ina niogopesha”
“Tazama mkataba wa Rose”
Mwanasheria akaufungua mkataba wa Rose na kutazama.
“Umegundua nini?”
Mwanasheria akausoma mkataba huo.
“Mbona upo kama wa Valentina tu”
“Unajua kwa nini nimefanikiwa kwenye maisha yangu?”
“Ahaa…haa….hapana”
“Kwa sababu nina toa kidogo na kuingiza kikubwa. Kwa kuzitazama asilimi ishirini na tano ni mamilioni ya dollar ila ninacho kwenda kukipata ni mabiloni ya dollar”
“Kuzipata wapi?”
“IQ ya Rose katika biashara ni kubwa sana she is so smart, genius. Ana endesha makampuni ya baba yake kwa kipindi kifupi alicho take over kampuni zao zimepanda. Hujaliona hilo?”
“Nimeliona”
“So ubongo wake nita utumia kuifikisha kampuni hii juu zaidi. Mbili ni sahii yake kwenye huo mkataba, nita weza kutumia kuweza kufoji kwenye mahitaji yangu ya kibiashara hivyo ni win win situation”
“Daaa wewe ni genius?”
“Wanangu hawaniamini kuhusiana na mali za familia na endapo nita foji chochote na yule kichaa Jack akijua ata tuua. Kwa maana sasa hivi akili yake ime chachuka sana tena sana hivyo kupitia mlango wa uwani wa huyu aliye kuja kwenye family yangu basi nita hakikisha nina jipatia vikubwa zaidi. Ninacho kitengeneza sasa hivi kwao ni kuaminiwa. Waniamini, wanipende, wajue mimi ni mwenzao ila akilini mwangu, nina mission yangu”
“Nimeipenda hiyo. Vipi mzee ana endeleaje?”
“Hali yake bado ni mbaya. Hakuna mang’azo”
“Chanzo cha yeye kuparalaizi ni nini??”
“Imetokea tu, ameanguka na nilimkuta ofisini kwake akiwa chini basi mambo yamekwenda kama yalivyo kwenda”
“Una hisi Jack ana tosha kwenye kuongoza makampuni yote?”
“Jack peke yake hatoshi. Kaka yake ndio genius tuna lijua hilo ila tuna jizimaga data. Hivyo nime wakaribisha nyumbani kwa upendo wa kuigiza ili tusije tukaanguka chini”
“Kuna jambo asubuhi hii mwanao ameniambia”
“Mwanangu gani?”
“Jack”
“Jambo gani?”
“Ila usimuambie”
“Siwezi kumuambia”
“Ana tafuta jumba la kifahari Masaki hivyo ana hitaji niandae mkataba wa kuinunua jumba hilo”
“Ahaa…Jack ni kawaida yake kununua nunua majumba. Uzuri wa Jack ana wekeza kwenye ardhi”
“Ni kweli nilitaka tu ujue”
“Muandalie afanye anacho taka kukifanya. Kwanza baadae nataka fujo zipungue nyumbani kwangu, nibaki na wafanyakazi wangu tu”
Mrs Tiger hakuwaza zaidi ya alicho elezwa na mwana sheria wao.
“Mimi nita chagua hapa napenda kuangalia eneo la barabarani”
Rose alizungumza huku akitazama ofisi kubwa ya vioo.
“Mimi nitakuwa jirani yako”
“Hahahaa”
“Nikishindwa jambo basi nakuja kukuuliza”
“Mutapendelea zipambwe na vitu vya rangi gani?”
Maneja wa kampuni aliwauliza. Kila mmoja akaachagua jinsi muonekano wa ofiis yake anavyo taka uwe.
“Sawa kuanzia leo jioni mafundi wataanza kufanya kazi”
“Tuna shukuru sana”
Velentina alizungumza.
“Ngoja nimpigie video call mume wangu nimpe ubuyu”
Valentina alizungumza na akaelekea ofisini kwake. Akampigia simu Jack ikaita hadi ikakata, akaipiga kwa mara nyingine, ikaita hadi ikakata.
“Mmmm mbona hapokei hajamaliza vikao?”
Kabla hajapiga tena, Jack akampigia.
“Mama mtu”
“Mume wangu mbona unaniogopesha”
“Naendesha bwana nilikua nina ingia barabarani ningepokea ingekuwa ni hatari”
“Una kwenda wapi?”
“Nakuja hapo ofisini”
“Bora uje unishauri ni jinsi ganinna weza kuipangilia ofisi yangu”
“Ina maana mumesha dondsosha wino?”
“Kitambo tu mpenzi”
“Ohooo hongera sana. Kama baada ya dakika kumi nitakuwa hapo”
“Sawa mume wangu nakusubiria”
Valentina akkaata simu.
“Upo salama?”
“Nipo salam mume wangu. Tumesha ingia mkataba wa kukabidhiwa asilimia ishirini na tano kila mmoja”
Rose alizungumza akitazama kinacho endelea barabrani.
“Umeusoma vizuri mkataba?”
“Ndio na kuuelewa na hapa nimesha kabidhiwa ofisi yangu”
“Mmmm! Mbona vitu vimekwenda spidi hivyo?”
“Sijui labda mkono wa MUNGU umemtembelea si una jua mzee ni juzi alikuwa mzima ana jimuda ila leo hii yupo kitandani na hajitambui”
“Ni kweli ila sawa”
“Una fanya nini?”
“Namalizia ule muundo wa code nilio kuwa nina utengeneza jana”
“Hujachoka?”
“Sijachoka nipo vizuri tu”
“Tukitika hapa tuna kwenda kiwandani, Kiwanda kipo wapi?”
“Kiwanda cha mama?”
“Ndio”
“Kipo Bagamoyo”
“Ohoo sawa mume wangu baadae”
“Poa”
Rose akakata simu akimtazama Valentina anaye ingia ofisini kwake.
“Shosti mume wangu ana kuja”
“Hapa?”
“Ndio ana kuja kunisaidia kuwapanga muundo wa ofisi yangu. Nataka iwe ni ofisi ya kisasa sana yaani ivutie kile atakaye ingia”
Rose akatabasamu.
“Wewe umechagua vitu vichache kwa nini?”
“Mmmmm kama unavyo niona mimi nipo simpe. Sipendi vitu vingi”
“Sawa”
Mrs Tiger akaingia ofisini.
“Warembo wangu tuondokeni twende kiwandani”
“Ahaa….mama Jack ana kuja”
“Sasa hivi?”
“Ndio ana kuja kunisaidia kupanga muonekano wa ofisi, ameniambia kama dakika kumi atakuwa hapa?”
Mrs Tiger akatazama saa yake.
“Hembu mpigie”
Valentina akampigia simu Jack.
“Mke”
“Mama anataka kuzungumza na wewe?”
“Mpe simu”
“Upo wapi?”
“Nipo mataa hapa nimekwama kwenye foleni”
“Sasa sisi tuna taka kuwahi kiwandani, tuna mizunguko mingi una onaje mukakutana tukimaliza mizunguko?”
“Sawa wahini”
“Poa mwanangu baadae”
“Ngoja mama. Hivi umefanya haya maamuzi ukiwa sawa na utimamu kabisa kabisa au?”
“Ndio mbona hamuniamini jamani”
“Haya”
“Lazima wakwe zangu wajifunze biashara. Hamujaoa wanawake kuja kuwa wamama wa nyumbani, kuwapikia na kuwzalia. Lazima wajue kufanya biashara, wata warithisha watoto wenu. Kama baba yenu alivyo niwezesha mimi na toka mukiwa wadogo mulikuwa muna nishuhudia nikitoka kwa ajili ya kufanya biashara zote za familia. Hivyo warembo wangu hawa ni lazima wachakarike tu”
“Sawa mama nimekuelewa”
“Haya baadae”
Mrs Tiger akamrudishia Valentina simu yake.
‘Mrs Tiger umefanya kosa kubwa kuniweka kwenye kampuni yako. Kama una tarajia mimi niwe chanzo cha kukuongezea utajiri basi sahau kwani nita chukua hata hizo asilimia hamsini zako na hii kampuni itakuwa ni yangu kaa suburie huto amini mama’
Rose alizungumza kimoyo moyo huku uso wake ukiwa umetawaliwa na tabasamu lililo jaa furaha ambayo sio rahisi kwa mtu kuweza kuelewa kilichomo ndani ya moyo wake.
ITAENDELEA
Mchaka mchaka mpya umeanza. Game on Mrs Tiger matarajio yake ni kumtumia Rose kumuingizia kipato kikubwa sana kwenye kampuni yake ila Rose mpango wake ni kuichukua kabisa kampuni ya Mrs Tiger nani ata kuwa mshindi kwenye hii game? Ungana nami katika stori hii ya kusisimua sehemu ya 41.
 
Hakika inavutia sana sema unaweka vipande vichache fanya hata mbili[
 
Back
Top Bottom