DEVIL’S FAMILY (FAMILIA YA MASHETANI) 26
ANGALIZO: KAMA UPO CHINI YA UMRI WA MIAKA 18. TAFADHALI USISOME HII HADITHI.
ILIPOISHIA
“Hayupo ndani ya gari lake”
“Fuc****”
Mzee Tiger akakata simu na kumuita mlinzi wake.
“Ndio mkuu”
“Mtafuteni James kila mahali na hakikisheni muna mkamata. Akileta kipingamizi, hakikisheni munampatia tocha hadi alainike”
“Sawa mkuu”
“Mume wangu…..”
“Shiii…kaa kimya. James ni laizma alipe kwa using** wake wote anao taka kuufanya….Una hisi nimetumia miaka mingapi kuijenga heshima yah ii familia halafu shahawa zangu tu ambazo ningewez akupigia punyeto na kuzimwaga chooni zina kuja kunisaliti……nita muua. Nakuambia nita muua akiendelea na ukum** wake”
Mzee Tiger alizungumza kwa ukali na msako wa kumsaka James ukaanza eneo zima la makazi ya familia ya mzee Tiger huku walinzi wakiwa na amri ya kumkamata na kama ata kataa basi ashushishiwe kipigo kitakatifu.
ENDELEA
Taa za jumba zima zikazimika kiasi cha kumfanya mzee Tiger na mke wake kwani katika jumba hilo umeme huwa haukatiki na hata ikitokea umekatika basi kuna nifumi miwili ya kuwasha umeme katika nyumba hiyo. Mufmo wa umeme wa jua pamoja na umeme wa jenereta.
“Kwa nini umeme umakatika?”
Mzee Tiger alimuuliza mlinzi wake aliye simama pembeni yao.
“Umesahau kuwa James ndio mwenye kuongoza mifumo ya nyumba nzima…..”
Mrs Tiger akawasha tochi ya simu yake na kuondoka eneo hilo na akamuacha mzee Tiger na mlinzi wake ambaye alikuwa ana mlinda toka akiwa kijana hadi sasa wamezeeka pamoja na ndio mshauri wake mkubwa.
“Tomas”
Mzee Tiger akamtazama mlinzi wake ambaye mara nyingi humuita kwa jina lake la ubazito na sio jina la ukoo la Tiger.
“Sidhani kama umetumia busara kudili na tatizo la kijana wako”
Mzee Tiger akashusha pumzi nyingi.
“Na usijaribu kuingia kwenye vita isiyo na sababu na ukitegemea huto pata faida zaidi ya hasara kubwa”
“Niache nikapumzike”
“Zuia walinzi kumtafuta James”
“Acha atafutwe nimfunze adabu”
Mzee Tiger akaondoka eneo hilo na kumfanya mlinzi wake kumtazama na kumfwa kwa nyuma kuingia naye ndani.
***
“Hawa jamaa kuku wao wana wapika vizuri”
Sophia alizungumza wakiwa wana pata chakula cha usiku.
“Wana wapisha bora sana”
Jack alizungumza akiendelea kula. Simu ya Jack ikaanza kuita, akatazama video call kutoka kwa baba yake.
“Baba ana taka nini usiku?”
“Mpokelee”
Valentina alizungumza. Jack akapokea simu anayo pigiwa na baba yake.
“Baba shikamoo”
“Rudini Tanzania”
“Kuna nini baba?”
“Kesho muwe hapa. Umenielewa?”
Mzee Tiger akakata simu.
“Mmm mbona gafla?”
Sophia alizungumza akitazama Jack.
“Hata sijui ila wakao tupo dukani mama alinipigia simu akimlalamikia James”
“James amefanya nini?”
“Ana toka kimapenzi na Rose”
“Rose ndio nani?”
“Mtoto wa mzee Chiko”
“Fuc** ana akili?”
“Na mbaya ana sema ata muoa”
“Msen*** anataka atukatishie starehe zetu kwa ujinga wake…..”
Sophia akachukua simu na kumpigia James ila siku ya James haikuweza kuita.
“Haiiti”
“Ngoja nimpigie mimi”
Jack akampigia James kupitia whasapp call ila pia simu ya James haikuita.
“Haiti”
“Mfarakano una weza kuwa ni mkubwa sana”
“Sijui sister hembu mpigie bi mkubwa muna weza kuzungumza vizuri”
“Bi mkubwa nilipishana naye dakika za mwisho”
“Mmmm”
“Tutajua tukirudi bwana”
“Andaeni mizigo yenu kesho tuna rudi Tanzania”
“Sawa”
“Wifi mbona umejibu kinyonge”
“Hamna wifi.”
“Tutakuja wakati mwengine”
Sophia alizungumza akitanasamu.
***
“Nishushe hapo”
James alimuambia dereva pikipiki aliye mkodisha na akasimamsha pikipi karibu na ukuta wa makazi ya mzee Chiko. Akamlipa kiasi alicho kubaliana na dereva pikipiki na akamuacha dereva pikipiki kuondoka eneo hilo. Akatembea hadi getini. Mlinzi mmoja akatoka nje ya geti akiwa na bunduki.
“Samahani naomba nionane na Rose”
“Wewe ni nani kwake?”
“Rafiki yake”
Mlinzi akamtazama James aliye vimba usoni huku jicho lake moja likiwa limevilia damu. Majera yake yana onyesha ni jinsi gani alivyo pigwa.
“Nimuambie ni nani?”
“James”
Mlinzi akarudi ndani ya geti, James akainama kidogo kwani ana hisi maumivu ya tumbo na mbavu zake. Mlinzi akawasiliana na anko Ally. Anko Ally akaelekea chumbani kwa Rose na akamgongea.
“Nani?”
“Ni mimi”
“Anko saa saba hii vipi?”
“Kuna mgeni wako”
Rose aapiga niyayo ya uchgovu kwani show aliyo pewa na James mchana kutwa imemfanya achoke sana mwili.
“Ni nani?”
“Amejitambulisha kwa jina la James”
Rose kusikia ni jina la James kwa haraka akashuka kitandnai, akafungua kabati lake na kuvaa suruali ya kitambaa pamoja na tisheti. Akatoka chumbani.
“Una uhakika ni James”
Anko Ally akamuonyesha katika simu video ya kamera ya ulinzi ya getini jinsi James aliye chuchumaa chini.
“MUNGU wangu ana nini!?”
Rose akatimua mbiio kuelekea getini huku anko Ally akimfwata kwa nyuma.
Fungua geti”
Rose alimuambia mmoja wa walinzi huku akikimbia. Amlinzi akafungua geti dogo na akawa wa kwanza kutoka huku Rose akifwata.
“James”
James akakohoa na damu zikamtoka mdomoni na puani kitendo kilicho mchnaganya Rose.
“Nisaidie kumnyanyuaaa”
Rose alizungumza kwa ukali na wakamyanyua James aliye nyong’onyea. Wakaanza kutembea naye kwa mwendo wa taratibu kuelekea ndani.
“Kimeokea nini mpenzi wangu?”
James hakujibu chochote zaidi ya kumtazama Rose huku nguvu za mwili zikiendelea kumuishia.
“Anko Ally mpigie daktari”
“Sawa”
Wakamfikisha eneo la kupumzikia na kumlaza James katika sofa.
“Kimetoka nini mume wangu”
Rose aliuliza akiwa amevurugwa kwani James ana majeraha usoni, mwake akamfungua shati lilio chafuka na akazidi kushangaa majera ya kuvilia damu mwilini mwa James ambaye masaa machache wametoka kuachana kila mtu akiwa mzima.
“Ni majambazi walio kuvamia?”
James akatingisha kichwa.
“Hali yake ni mabaya mkuu tumpeleke hospitali”
“Ha….ha…pana”
James alizungumza kwa kujikaza, akakohoa tena na kutema mate yenye damu.
“Mukinipeleka baba ata niua”
James alijikaza kuzungumza Rose macho yakamtoka.
“Una maanisha nini?”
“Najisikia vibaya”
“Anko huyo dokta hafiki tuuuu”
Rose alizungumza kwa ukali.
“Ngoja nimpigie tena”
Anko Ally akasogea pembeni na akamapigia simu Eddy.
“Usifumbe macho usifumbe macho mpenzi wangu”
Rose alizungumza machozi yakimwagika. Kadri muda unavyo zidi kwenda ndivvyo jinsi James anavyo ona mawenge mawenge. Hazikuisha dakika kumi akazimia na kumfanya Rose kutokwa na macho ya mshangao. Daktari akafika akaanza kumfanyia James vipimo.
“Hajafariki. Amezimia. Kwa hali yake hii ina bidi timuwahishe hospitali kwa ajili ya vipi kama CT Scan”
“Ila amesema kuwa akipelekwa hospitalini ata uwawa?”
“Boss akikaa hapa ata kufa. Ni maamuzi yako”
“Nahitaji mazingira ya usiri kuingizwa hospitalini na kupatiwa matibabu”
“Tufanya hivyo”
“Mungizeni kwenye hari haraka haraka”
Hapakuwa na muda wa kupoteza zaidi ya kumuwahisha James hospitali huku Rose akiwa amekaa siti ya nyuma huku kichwa cha James kikiwa kimemlalia mapajani mwake.
***
“Mkuu kuna habari ambayo sio nzuri”
Mzee Tiger akamtazama mlinzi wake.
“Kuna nini?”
“Tumekuta walinzi sita eneo la kusini wakiwa wameuwawa”
“Sita?”
“Ndio na tulicho kikuta ni hii simu ya James”
Mzee Tiger macho yakamtoka kwa mshangao.
“James ana wezaje kuua walinzi wenye mafunzo sita ikiwa hata kuku hawezi kuchinja?”
Mzee Tiger alizidi kushangaa. Mke wake akaingia ndani ya ofisi ya mzee Tiger huku ikiwa ni saa kumi ikielekea saa kumi na moja alfajiri.
“Hamjampata kwa maana usingizi sijapata kabisa mume wangu”
“Hajapatokana ila ameua walinzi sita”
“Hahahahaa….James ameua walinzi?”
“Hata mimi nina shangaa. Wameuliwa na bundukia au?”
“Hapana. Wameuliwa kwa mapigano makali na tena mapigano yanayo onekana ni makali sana.”
“Toka lini James amejifunza ngumi?”
Mzee James alimuuliza mke wake.
“Mimi sijawahi kufaahamu kabisa. James hawezi kupigana”
“Twendeni mukainonyeshe hizo maiti”
Wakatoka ofisini na wakaongozana hadi eneo zilipo hifadhiwa maiti za walinzi sita huku wezao wakiwa na wasiwasi mwingi kwani katika historia ya ufanyaji wao kazi katika jumba hilo hapajawahi kutokea shambulizi lililo ua hata walinzi wawili.
“Walinzi wote wameuwawa kwa vpigo na aina ya uuaji woa wote ni wa kuvunjwa shingo”
Mzee Tiger na mkewe wakatazamana kwa mshangao.
“Hawa mafunzo yao yana karibia kwa ukaribu mafunzo ya makomandoo. Kitendo cha wao kuuwawa ni kitendo cha kushangaza sana”
“Tulimdharau sana James ila kwa hichi alicho kifanya mkuu ni wakati wa kumtazama James kama tishio halisi”
“Kweli ina bidi iwe hivyo”
Mzee Tiger akatoa simu yake mfukoni.
“Unataka kufanya nini?”
Mke wake aliuliza.
“Niwapigie wakuu wa majeshi watume vijana wao kumtafuta”
“Hapana. Mume wangu hili ni swala la kifamilia. Hatupaswi kushirikisha watu kutoka nje.”
“Kama ameua walinzi wote hawa una hisi mimi na wewe tupo salama”
Mrs Tiger akashusha pumzi nyingi.
“Mume wangu tafadhali. Naomba unielewe”
Mzee Tiger akamtazama mke wake kwa sekunde kadhaa.
“Nakuomba sana”
“Poa. Hakikisheni munatoa ripoti kwa vijana wetu wote na wahakikishe wana mtafuta James popote alipo na atakaye mpata waambie kuna zawadi ya shilingi milioni ishirini”
“Aje akiwa hai au amekufa?”
Mlinzi mmoja aliuliza swali lililo mfanya Mrs Tiger kumtazama kwa macho makali. Akapiga hatua hadi alipo mlinzi huyo.
“Uliza tena swali lako?”
“Samahani madam”
“Asitokee mpumbavu yoyote akamuua mwanangu. Mkamateni kama munaweza na mulete kwetu. Hakuna anaye jua uchungu nilio upitia kumzaa”
Mrs Tiger akaondoka kwa hasira huku akizidi kujutia moyoni mwake kwani maamuzi ya kumchochea mume wake aliyo yafanya yameleta madhara makubwa sana si kwao tu hadi kwa walinzi ambao wana familia.
***
“Rose kaa utulie”
“Natuliaje ikiwa mwanaume ninaye mpenda anapigania uhai wake eheee…..Toka tulivyo mleta hapa usiku hadi sasa hivi saa mbili hii hatujui kinacho endelee eheee?”
Anko Ally akaka kimya.
“Haki ya MUNGU James akifa nakuambia sinto waacha salama ile familia. Nilikubali kuweka hasira na kisasi changu pembeni kwa ajili ya James kwa kuwa nimempenda ila sasa hivi haki ya nani nita washuhulikia, akifa wata juata kwa maana ni familia ya ajabu sana inaweza kumuua mtoto wao.”
Rose alizungumza kwa uchungu akilia na kumfanya Anko Ally kukaa kimya kwani toka James ameingizwa chumba cha upasuaji bado hajatoka.
ITAENDELEA
Mchaka mchaka mpya umeanza. Imekuwa ni jambo la kushangaza kwa kila mtu baada ya James kuhusika katika vifo vya walinzi sita wanao linda nyumba ya baba yake. Ila hali ya James ni mbaya sana je ata fanikiwa kutoka salama katika chumba cha upasuaji? Ungana nami katika stori hii ya kusisimua sehemu ya 26.