DEVIL’S FAMILY(FAMILIA YA MASHETANI) 55
KILA KILICHO ANDIKWA KATIKA HADITHI HII NI UTUNZI HAKIENDANI NA KISA CHOCHOTE KILICHO WAHI KUTOKEA MAHALA POPOTE ASANTE
*************************************************************************************
ILIPOISHIA
“Nenda tutazungumza baadae”
“Mama zungumza kama na wewe una taka ulazwe jua mimi sina uwezo wa kuwaangalia wote watau mukiumwa. Zungumza kama una jambo la kushauriwa ushauriwe”
“Kati ya baba yako una chagua nani aendelee kuishi”
“Jack. Mzee kashakula chumvi namambo aliyo yafanya yana tosha aisee. Mika sabini ni mingi sana muache apumzike kwa amani”
“Yaani baba yako ndio una mchukia kiasi hicho”
“Mama tuache unafki hilo swali nikuulize wewe. Kati ya Jack na mzee nani ambaye una taka abaki hai duniani?”
Mrs Tiger akakosa jibu na akabaki akimtazama Sophia na akilini mwake ana waza endapo bibi wa familia akimtokea kwa mara ya pili ni nani atakuwa tayari afe ikiwa mume wake ana mpenda na Jack mwanaye ana mpenda.
ENDELEA
“Twende tukanywe chai bwana”
Sophia akamshika mkono mama yake na akatoka naye katika chumba alicho lazwa mzee Tigera. Wakajumuika mezani na kuendelea kunywa chai. Ukimya ukatawala huku kila mmoja akiwa kimya akionekana kuwaza anacho kiwaza.
“Mimi narudi hospitalini”
Valentina alizungumza huku akinyanyuka.
“Subiri twende wote”
Sophia alizungumza.
“Na mimi pia nina kuja”
Vaileth alizngumza.
“Mimi nitakuja baadae nahitaji kulala kidogo”
Mrs Tiger alizungumza akiendelea kuywa chai taratibu. Valentina akaelekea chumbani kwake, akaanda nguo chache na akaziweka katika kibegi kidogo. Vaileth akaingia ndani ya chumba cha dada yake.
“Vipi mbona mnyonge”
“Hamna”
“Una nini unataka kuongea?”
“Hamna dada. Shem kweli ata pona?”
“Moyo wangu una matumaini sana juu ya kuwa mume wangu ata nyanyuka tena pale kitadani.”
“Sawa. Ila nimeanza kuiogopa hii familia”
Vaileth alizungumza kwa sauti ya chini.
“Kwa nini?”
“Maadui ni kama hawa unavyo waona. Wana ilenga fmailia hii na sisi tupo ndani ya hii familia itakuwaje?”
“Mdogo wangu. Familia za kitajiri zina mambo yao. Mambo yao ndio kama haya, haiwezi kutokea watu wakaenda kuvamia familia za chini. Hivyo kuna nyakati ina bidi tumshukuru MUNGU kwa kila jambo mdogo wangu. Sawa”
“Sawa dada”
“Kuwepo kwenye hii familia pamefungua milango ya kiuchmi katika familia yetu. Tulivyo kuwa hapo mwanzo na hivi sasa ni tofauti. Au wewe mwenzangu hujaona tofauti?”
“Nimeiona”
“Basi kama ni hivyo sisi tutumie akili kuishi nao. Kwenye mambo yao ya ajabu tuachane nayo na kwenye mambo ambayo tuna ona yana manufaa kwetu basi tuyafwate. Good news ni kwamba nimepewa hisi asilimia ishirini na tano katika kampuni ya mama mkwe”
“Hisa asilimia ishirini na tano?”
“Ndio na mimi ni mkurugenzi”
“Zina thamani gani?”
“Mmmmm pesa nyingi sana mdogo wangu. Kwa maana kampuni kila siku ina panda. Hapa ninacho kiwaza ni kujitafutia eneo nikajenga jumba langu la kufahari, nikafungua biashara ambazo zitakuwa chini yangu na maisha yakaendelea”
“Hongera sana dada”
“Asante. Niambie ni biashara gani una taka kufanya nikuweke kwenye bajeti kwa maana nafasi ndio hii”
“Nitakuambia dada”
Sophia akaingia.
“Nipo tayari tuondokeni”
Valentina akabeba kibegi kidog chenye ngo. Wakatoka nje na wakangia katika gari moja na wakaondoka na walinzi wawili huku mmoja akiwa ni dereva.
***
“Hivi navyo ni sh ngapi?”
Dokta Boaz aliuliza funga la viatu vitabu. Macho ya mwana mama wa pembeni anaye muangalia kwa kuiba iba.
‘Fuc**’
Dokta Boaz alizungumza kimoyo moyo akishtuka kwani angalia ya mwana mama huyo ina asihria kuwa ana mfwatilia.
“Nifungie mafungu mawili”
Dokta Boaza alizungumza huku akimpa mwana mama anaye muuzia viazi noti ya shilingi elfu kumi.
“Nikuwekee kwenye mfuko wa shilingi mia tano au mia tatu?”
“Mia tano”
Akatazama wauzaji wawili wanao uza matunda, akagundua wauzaji hao nao ni wapelelezi na wana mfwatilia yeye.
“Samahani….hapa ni wapi kwenye vyoo vya kulipia”
‘Nenda upande ule wa kulia, kunja kushoto utaona vyoo”
“Asante”
Dokta Boaz akatembea kwa mwendo wa kuchechemea huku macho yake yakiwa makini kutazama wanao mfwatili.
‘Hawa wapuuzi wamenijuaje?’
Dokta Boaz alizungumza hukua akiendelea kuwatazama wanao mfwatilia.
“Vipi?”
Aliye pewa jukumu la kumfwatilia dokta Boaz alimuuliza bodaboda mara baada ya kushuka ndani ya gari
“Yupo ndani ya soko”
Bodaboda alijibu. Afisa w ashirika la X kwa mwendo wa haraka akaingia ndani ya soko. Akapewa ishara na afisa mwengine ambaye ni muuzaji ndani ya soko na akaanz akutembea kwa mwendo wa haraka na wenye tahadhari kuelekea eneo la vyooo. Akafika eneo la vyoo, akatoa ishara kwa mpokeaji pesa kukaa kimya, akachomoa bastola kiinoni mwake. Akaingia katika vyoo vya kiume, akaanza kukagua mlango mmoja baada ya mwengine. Akafika choo cha saba ambacho mlango wake umefungwa kwa ndani. Akajaribu kuusukuma ila haukufunguka. Akagonga mara mbili, ila hapakuwa na jibu lolote. Akarudi nyuma kwa garaka na akaupiga kwa teke na mlango ukafunguka. Akaingia na kuona eneo la juu ya bati la choo kukiwa limefunguliwa ikishiria aliye ingia ndnai ya choo hicho ametokea kupitia katika bati. Akachomeka bastola kiunoni mwake, akatoka.
“Umemuona huyu mzee?
“Ndio ameingia humo ndani”
Akazunguka upande wa nyuma wa vyoo. Hakumuona mtu yoyote, akawatumia meseji maafisa wote walipo ndani ya soko ambao ni wapelelezi wa siri. Msako wa kumtafuta dokta Boaz kimya kimya ukaendelea ndani ya soko ila hapakuwa na aliye weza kumuoana. Akampigia simu Rose.
“Nipe ripoti?”
“Hatujafanikiwa kumpata. Ametoroka ndani ya vyoo vya sokoni alipo ingia’
“Sokoni?”
“Ndio”
“Soko gani?’
Afisa akataja soko alilopo. Rose akaata simu.
“Katika hilo soko kuna kamera una weza kupata video zake”
“Ngoja”
James akadukua kamera zilizo fungwa ndani ya soko. Akafanikiwa kupata rekodi inayo muonyesha dokta Boaz jinsi anavyo ingia ndani ya soko hilo. Wakafwatilia mizunguko yake ndani ya soko.
“Huyu mama ndio kamfanya agundue”
Rose alizungumza kwa hasira.
“Anafanya naye kazi au?”
“Hapana jinsi alivyo kuwa ana mtazama kwa muhalifu anaye weza kusoma macho ya mtu ana gundua kabisa kuwa na afwatiliwa.”
“Huyu jama ana ana onekena ana uwezo mkubwa”
“Kijinga tu wameshindwa kumpata”
“Video yake ya mwisho ni hii kuingia bafuni”
“Huwezi kuangalia eneo la pembeni hapo kama kuna maduka yana kamera?”
“Ngoja”
James akaendelea kukagua eneno la jirani na soko kama kuna maduka yanye kamera.
“Hamna na kamera zilizopo ni kamera za ndani ya maduka yao”
“Ndio tumesha mpoteza kizembe tu”
Mlango ukafungulia, akaingia Sophia akiwa ameongozana na mawizi zake.
“Mbona mumerudi mapema. Tukajua mtakaa hadi mchana”
“Mmmm shem mimi nimeshindwa kuvumilia. Nimekosa kabia amani ya kukaa nyumbani.”
Valentina alizungumza akiweka kibegi chake juu ya meza.
“Umekuja na begi kabisa”
“Ndio shem sirudi nyumani hadi mume wangu awe sawa”
“Ohooo sawa”
“Wifi Rose upo sawa?”
Sophia alimuuliza Rose.
“Yaa nipo vizuri wifi”
Rose alizungumza huku akitazama simu yake inayo ita.
“Ndio”
Rose alizungumza huku akitoke nje.
“Tumefwatilia na kuuliza kuna walio muona akipanda bajaji”
“Fwatilieni sasa hiyo bajaji”
“Kwa bahati mbaya boss si bajaji ya eneo hilo. Ni bahaji aliyo isimamisha barabarani”
“Hilo eneo halina kamera?”
“Tumechunguza na halina”
“Muna wezaje kumuacha mtu akaondoka kirahisi nama hiyo, ni uzembe wa aina gan hiyo eheee?”
Rose alizidi kufoka. Akakata simu huku akimtazama James.
“Wanasemaje”
“Wanasema kapanda bajaji”
“Bajaji ya kwenda wapi?”
“Sijui ni bajaji aliyo pita barabarani”
“Ata kwenda kubadilisha muonekano wake na kuwa katika muonekano mpya”
“Ndio anacho kwenda kukifanya”
“Inabidi twende Morogoro”
“Kufanya nini?”
“Kwenye hicho kituo chake cha watoto. Naamini hapo tuna weza kupata taarifa zaidi”
Rose akajifikiria.
“Naamini kuna polisi watakuwa wamesha kwenda kuchukuru ripoti katika kituo chake”
“Sasa tuna fanyaje mke wangu”
“Ngoja niulizie”
Rose akapiga simu kwa mkuu wa jeshi la polisi na akaulizia kuhusiana na taarifa za dokta Boaza akafamishwa walicho kipata makachero wa jeshi la polisi mara baada ya kuhojiwa wafanyakazi na baadhi ya watoto walipo katika kituo hicho.
“Nashukuru sana mzee wangu”
Rose akakata simu.
“Wanasema wamesha kwenda kuwahoji. Walezi wa kituo hicho wana sema Boaz naye alilelewa katika kituo kingine cha watoto yatima ambacho kipo chini ya kanisa la Katoliki. So baada ya kusomeshwa na kukua, akapata mafanikio naye akafungua kituo chake cha kulea hao watoto”
“Hicho kituo cha Kanisa Katoliki kipo wapi?”
“Morogoro”
“Twende huko mke wangu. Tuna weza kujua mengi kuhusiana na yeye. Masaa matatu hadi manne yana tosha sisi kufika Morogoro”
“Sawa”
Wakarudi ndani ya chumba alicho lazwa Jack.
“Tuna toka, kuna mahali tuna elekea. Kuna jambo tuna kwenda kulishuhulikia”
“Sawa”
Sophia alijibu.
“Chris na wezake wataendelea kuimarisha ulinzi”
“Sawa bro”
James na Rose wakaondoka na hospitalini na kuianza safari ya kuelekea Morogoro huku Rose akiwa ndio dereva wa gari.
***
“Eheee mbona umerudi tofauti na ulivyo kweenda”
“Wajinga wamenistukia”
“Kivipi?”
“Sijui aisee”
“So ulikuwaje ukatoroka”
“Ngoja ni nywe maji aisee hili jua litaniua”
Dokta Boaz akafungua friji, akachukua chupa ya maji na kuanza kunywa. Akaongeza upepo wa AC.
“Kwanza umehakikisha kuwa hufwatiliwi?”
“Ndio.”
“Imekuwaje?”
“Hospitalini kila kitu kimekwenda vizuri. Nimetoka pale nikachukua boda hadi sokoni, kuna chakula nilihitaji kuja kukipika. Sasa nikiwa pale kuna mama mmoja akawa ana nitazama ile ya kupeleleza hapo ndipo nikajua kuwa nipo kwenye mtego kwani kulikuwa na maafisa wengine wakinifwatilai kwa umakini sana”
“Eneo nilio kuwa njia, pekee ya kutoka mule ilikuwa ni kupitia chooni. Niliingia chooni ikanilazimu kutoka kupitia paa la choo”
“Ina maana hapakuwa na gypsum?”
“Haikuwepo zaidi ya bati tu. Nikaruka na kutokea upande wa piili. Nikatembea kwa haraka hadi barabarani ambapo nikapa bajaji iliyo nipeleka hadi maeneo madukukani, nikanunua nguo nilizo vivaa na nikaenda kubadilisha muonekano katika chochoro moja.
“Hawajakuona watu ukivua sura yako ya bandia?”
“Hawajaniona”
“Sasa wamekujuaje?”
“Mimi nahisi ni yue mwanamke niliye kutumia picha yake na kosa nililo lifanya ni kumsogelea”
“Kumsogelea kivipi?”
“Pale hospitalini kuna friji la kununua vijanywaji hivyo nilitaka kumchunguza vizuri hapo ndipo nilipo chnaga karata zangu vibaya”
“Na wakakuacha utoke nje ya hospitali”
“Ndio na naamini walitaka kunifwatilia hadi ninao ishi”
“Boaz usije ukaniletea matatizo”
“Huwezi kupata matatizo kuwa na amani. Hujapta taarifa zake?”
“Hapana”
“Daaa. Yule binti ni nani ina bidi nimshuhulikie aisee”
“Kwa nini usiachane na huu mpango”
“Nimesha chukua pesa ya watu. Siwezi kuacha hii kazi na mimi sio mtu wa kukatishwa tamaa na changamoto ndogo kama hizi. Ni lazima nikamishe mission yangu”
“Wewe niambie uta zikwa wapi? Morogoro au hapa hapa Dar. Hawa watu wapo seriously na wamesha kuweka kwenye mabado. Kama leo umeweza kupotea chupu chupu basi kesho wata kukamata rafiki yangu. Nakushauri achana na huu mpango. Hii ngoma unayo taka kuicheza ni nzito kuliko uwezo wako. Jizime data rafiki yangu ila naona mwisho wako una kuwa ni mbaya”
Dokta Boaz akatulia kwa sekunde kadha akiufikiria ushauri anao pewa na rafiki yake, japo ana jiamini kweye kazi yake ya uuaji ila anacho elezwa na rafiki yake ni kitu cha maana na asipo kuwa makini ata kufa.
ITAENDELEA
Mchaka mchaka mpya umeanza. Rose na James wana elekea Morogoro, je wata fanikiwa kupata taarifa za Dokta Boaz? Dokta Boaz amepewa ushauri wenye ukweli ndani yake ja ata uzingitia au ataendelea kushupaza shingo akiamini katika uwezo wake? Ungana nami katika stori hii ya kusisimua sehemu ya 56.