DEVIL’S FAMILY(FAMILIA YA MASHETANI) 57
KILA KILICHO ANDIKWA KATIKA HADITHI HII NI UTUNZI HAKIENDANI NA KISA CHOCHOTE KILICHO WAHI KUTOKEA MAHALA POPOTE ASANTE
*************************************************************************************
ILIPOISHIA
“Tulia hapa”
James akashuka ndani ya gari, akakimbilia lilipo lori la mafuta. Akafika eneo lilipo lori na akamkita dereva akiwa amebanwa ndani ya gari huku akilia.
“Fungua mlango”
Alimuambia dereva kwani mlango ameifunga kwa ndani. Dereva kwa jinsia livyo banwa akashindwa hata kufungua mlango. James kwa kutumia kitako cha bastola akavunja kioo cha upande wa dereeva. Akafanikiwa kuufungua mlango kwa ndani.
“Fuc**”
James alizungumza hukua akishindwa kumchomoa dereva alipo banwa. Kwa haraka akashuka kwenye ngazi za gari. Macho yakamtoka mara baada ya kuona mataki mawili yanayo vutwa na kichwa cha lori yakimwaga mafuta huku cheche cheche zikiwa zikiwa zina jitokea kwenye nyaya zilizo katika.
“Spana una weka wapi?”
“Kwenye toolbox”
Akavunja kuvulia kwa kutimia kitako cha bastola kisha akachkua spana kubwa akapandisha ngazi za lori na kuanza kutanua eneo ambalo dereva amebanwa. Taratibu Rose akashuka ndani ya gari, akatazama eneo alilo elekea James. Akazima gari na akalifunga kitendo cha kupiga hatua mbili tu kuelekea lilipo Lori, mlipuko mkubwa ukatokea kitendo kilicho mshtua sana Rose na mbaya zaidi James yupo eneo la mlipuko.
ENDELEA
Kwa haraka Rose akaanza kukimbia kuelekea eneo ambalo lori la mafuta limelipuka. Kabla hajafika mlipuo mwengine wa ukatokea na kumfanya Rose kujificha katika moja ya mti mkubwa kwani mlipuko huo una nguvu kubwa sana iliyo ambatana na upepo.
“Usiinue kichwaa”
James alizungumza huku akikiinamisha kichwa cha dereva chini kwenye korongo walipo angukiwa sekunde chache kabla ya lori kulipuka.
“Asante sana”
Dereva alizungumza huku akimtazama James ambaye baada ya kumchomoa kwenye mskani ulio kuwa ume mbana alimbeba begani mwake na kukimbia naye kwa mwenzo wa haraka sana kwa zaidi ya mita arobaini na akadumbukia naye kwenye gema.
“Jamesss”
Rose aliita kwa sauti ya juu sana na kumfanya James kunyanyuka walipo lala.
“Nipo huku, toka hapo bado lina endelea kulipuka”
James alizungumza kwa sauti ya juu na kumfanya Rose akimbilie walipo.
“Mupo salama?”
“Mimi nipo poa ila jamaa mguu umepata shida”
Rose akatazama mguu wa kulia wa dereva ulio vunjika mara mbili.
“Ngoja niombe msaada kwa jeshi la zima moto.”
Rose akapiga simu kwa mkuu wa Wilaya wa eneo walipo. Akaomba masaada na kuelekeza eneo ajali ilipo tokea. Wakasikia sauti za mashuhuda wa ajali. Ikamlazimu James kunyanyuka eneo walip[o jificha.
“Jamani sogeeni bado yana lipuka hayooooooo”
James alizungumza kwa sauti ya juuu kuwapa tahadhari watu wanao sogelea eneo la ajali. Mzinga mwengine ukatokea na kuwafanya watu kukimbia.
“Wameudhurika?”
Rose aliuliza.
“Wamewahi kukimbia”
Dereva akaanza kulia kwa maumivu makali kwani ganzi aliyo kuwa ameipata.
“Jikaze broo soon jamaa wana kuja”
“Naumiaa brooo……maumivu makali”
“Pole una tokea wapi wewe na familia yako?”
“Nimetokea Mtwara ndio ilipo familia yangu”
“Sawa nitajie jina la lako kamili, mke au mtu yoyote wa familia yako tunaye weza kumpatia taarifa ya ajali yako. Garama na matibabu yote mimi na mke wangu tutasimamia matumizi yote na wakifika waokoaji tuta waeleza ni hospitali gani upelekwe”
“Sawa kaka shukrani, nikutajie namba ya kaka yangu”
Dereva akataja namba ya kaka yake na James akainakili katika simu yake.
“Nitampigia uokozi ukisha malizika”
“Nashukuru”
Ving’ora vya gari mbili za zima moto zikafika eneo hilo na kuanza kuzima moto wa eneo hilo. Kwa kusaidiana na wananchi pamoja naa askari wa jeshi la polisi. Dereva akabenwa kutoka eneo la ajali hadi barabarani ambapo akapakizwa ndani ya gari la wagonjwa. James akamuomba dereva wa gari la wagonjw ani wapi kwa kumpeleka mgonjwa.
“Ila ina bidi ahawahishwe hospitali ya wilaya”
“Natambua ila mpeleke katika hospitali niliyo kutajia. Nitajie namba yako ya simu”
James akaingia katika app ya simu ya mtandao wa pesa. Dereva akamtajia namba ya simu.
“Nimekuingizia milioni, laki mbili ongeza mafuta nyingine kama bonus yako ya udereva. Ukimfikisha hospitali niliyo kuambia utapata pesa nyingine ya ziada kama shukrani imekaaje hiyo”
“Asante sana kaka. Chap ana fika Dar”
Dereva alizungumza mane yote thelathini na mbili yapo nje. James akarudi eneo la nyuma ya gari hiyo ya wagonjwa aina ya Land Cruiser Mkonga ambayo ni mali ya hospitali ya wilaya.
“Muangalieni, ikiwezekana mchomeni sindano ya kutuliza maumivu. Ana kwenda mbali”
“Sawa”
“Bro sijakuuliza jina lako unaitwa nani?”
“Suleimani”
“Nesi una kalamu na karatasi”
“Hapana sina”
“Sawa tuna wafwata kwa nyuma tutafika wote hospitalini”
“Asante kaka”
James akaelekea lilipo gari.
“Vipi?”
“Nimepa dereva chochote kitu ili apelekwe hospitali aliyo lazwa dogo”
“Ila Tanzania bwana. Watu hawawezi kufanya kazi bila ya chochote kitu”
“Hapana mke wangu. Ni kumpa nguvu dereva kumbuka ana fanya kazi za humu ndani ya wilaya yake safari za nje ya mkoa ni chache”
“Endesha hapa mwili mzima umechoka”
James akaingia upande wa dereva huku Rose naye akipanda upande wa abiria, taratibu wakaondoka eneo hilo ambalo tayari limesha jaa watu wanao shuhudia kinacho endelea. Ukimya ukatawala ndani ya gari huku wakilifwata gari kwa nyuma.
“Mchungaji Kimaro, MUNGU amempatia karama ya kipekee sana”
“Kwa nini?”
“Si una ona ajali imetupunyua punyua. Kwa maana isinge kuwa hivyo sasa hivi ingekuwa tuna ongea mambo mengine”
“Ndio hivyo mke wangu. Kila mtu na karama yake. Hapa ina bidi dogo akapatie matibabu nyumbani”
“Kwa nini?”
“Una hisi yule mshenzi ata kubali kushindwa kazi. Ni lazima ata fanya mpango wa kubadili sura kwa mara nyingine na kudili ana adui wa aina hiyo sio jambo dogo. Leo kaja kama mzee, kesho ana weza kuja kama mwanamke”
“Ila ni kweli”
“Akiwa nyumbani ulinzi utakuwa ni imara zaidi”
“Sawa mume wangu. Zungumza na Sophia hilo wazo”
“Poa”
James akakata simu na akampigia simu Sophia na akaweka loud speaker.
“Bro”
“Upo wapi?”
“Hospitalini?”
“Dogo hali yake?”
“Ni ile ile hakuna mabadiliko”
“Sasa hali ya kiusalama kwa dogo haipo vyema. Una onaje tuka mrudisha nyumbani”
“Nyumbani?”
“Ndio madakatri wawe wana muhudumia hapo. Nazungumza na mmiliki wa hospitali kisha utaratibu wa kumuondoa hapo ufanyike”
Sophia akatoka ndani ya chumba alicho lazwa Jack.
“Kuna nini kianendelea bro”
“Naamini una jua kuwa kuna mtu alipanga kumuua tena dogo”
“Ndio”
“Nina hofu huyo mtu ana weza akarudia tena na kutaka kumuua. Mbaya ana badilisha sura yake hivyo ana weza kutumia munekano mwengine na akaja kumuua dogo. So zungumza na Chris aondolewe hapo hospitalini”
“Sawa bro”
“Wamuondoe kimya kimya. Nyumbani itakuwa salama kwakwe”
“Poa bro ngoja nimcheki Chris wewe mpigie huyo mmiliki wa hospitali madaktari watakao kuwa wana muangalia”
“Poa poa
Sophia akakata simu.
“Yupo wapi Chriss”
“Ameshuka chini”
“Mcheki aje chap”
Mlinzi akawasiliana na Chris. Baada ya dakika mbili Chris akafika eneo.
“Broo ina bidi tumuhamishe dogo hospitalini tumrudishe nyumbani”
“Kwa nini boss?”
“Kaka kasema hivyo. Yule muuaji ana weza kurudi na kumua dogo tena”
“Sawa”
“Ngoja ana fanya mpango wa madaktari. Wewe andaa msafara wa kumrudisha nyumbani”
“Ina bidi mufanye mazungumzo na madakatri kujua kama kuna uwezekano wa kumsafirisha kwa helicopter au gari. Mimi nita andaa mazingira yote”
“Hakuna tatizo”
Sophia akarudi ndani.
“Kuna nini wifi?”
Vaileth aliuliza huku akimtazama Sophia.
“Ina bidi tumrudishe nyumbani kwa ajili ya usalama wake. Kama munavyo fahamu kuwa mazingira ya hali yake yana tokana na kutaka kuuliwa. Tuna hofia ana weza kutaka kuuliwa tena hivyo ina bidi tumrudishe nyumbani”
“Sawa wifi”
Sophia akamtazama Valentina aliye fumba macho hukua kiomba.
***
“Boss kuna mwana mama yupo nje ya geti”
“Mwana mama”
“Ndio ana hitaji kuonana na wewe”
Mwanamama bilionea akamtazama mlinzi wake.
“Tumemzuia kuingia kwa maana hatumtambui hana kitambilisho chochote”
“Kama ana omba msaada mpeni pesa aondoke”
“Amesema ana hitaji kuonana na wewe ni muhimu”
“Mkagueni na mumuingize ndani akae eneo la kupumzikia”
“Sawa”
Mwana mama bilionea akanyanyuka na akatembea hadi kwenye kibaraza cha gorofa lake. Akatazama jinsi mwana mama aliye valia vitenge akikaguliwa na mlinzi wa kike kisha akasindikzwa hadi kwenye eneo la kupumzikia.
“Anaitwa nani?”
Alimuuliza mlinzi wake aliye simama pembeni.
“Mama Bite”
“Ndio nani?”
“Labda ukazungumze naye”
Mwana mama bilionea akaongozana na mlinzi wake hadi kwenye eneo la kupumzikia alipo mama Bite.
“Karibu”
“Una walinzi wa hovyo sana”
“Boaz”
“Yaani nimevalia hivi na hakuna aliye nitambua aiseee. Kama ni mtu angetaka kukuua si angesha kamilisha kazi yake”
Dokta Boaz alizungumza huku akivua sura ya bandia aliyo ivaa na kuwafanya walinzi wawili wa mama bilionea kushangaa.
“Nendeni nina mazungumza na boss wenu”
Walinzi wakamtazama mwana boss wao. Akawapa ishara ya kuondoka na walinzi wake wakaondoka.
“Kuna nini kimetokea mbona upo hapa na muonekano kama mwanamke”
Dokta Boaz hakujibu kitu, akaendelea kutoa maziwa ya bandia aliyovaa kifuani mwake, akavua makalio ya bandia ambayo ameyavaa.
"Madude. Wanawake muna wezaje kutembea na makalio makubwa na maziwa kama hivi"
"Ndio maana tumekuwa wanawake. Vipi?"
“Poa ilibidi nitumie njia hii kuondoka Dar es Salaam kwa maana huko kote nina sakwa kama dhahabu”
“Imekuwaje”
Dokta Boaz akamuelezea mwana mama huyo jinsi Rose alivyo haribu mipango yake.
“Una picha ya huyo binti?”
“Ni mkwe wa hiyo familia. Mke wa James ila yule dada ni afisa ambaye ana jicho moja kali sana la kuweza kujua mtu huyu ni mwema au si mwema”
“Tuna fanyaje?”
“Ina bidi kuandaa kikosi kazi”
“Kikosi kazi kivipi?”
“Sasa tuna paswa kwenda usoni kwa uso kutumia nao. Wamesha block mianya yote ya kumdhuru mwana yeyote yule”
“Hao watu tunao watafuta ni kina nani na tutawapatia wapi?”
"Nina timu ya x specila force watano. Nina watumia mara kadhaa katika mission za kuhita and run"
"Watano watatosha ikiwa Tiger ana vikosi kabisa"
“Ni kweli ila jamaa wana mziki mkubwa Jamaa wana uwezo wa kufanya utume ngumu.
"Walikuwa ni macho wan chi hii?"
“Ndio”
“Una uhakika wata ifanya hiyo kazi?”
“Asilimia mia moja Na ikikupendeza hili swala langu nina omba ulizime Nimesha ingia kwenye rekodi za vyombo vya usalama, si polisi wala si shirika la X wana nisaka sana”
Mwana mama bilionea akajirikiria kwa muda kidogo.
"Sawa nitajua jinsi ya kulimaliza hili na kulifuta. Ila kumbuka tuna weza kulifuta kwenye vyombo vya ulinzi na usalama ila kwa ile familia"
"Najua"
"Kumbuka wale ndio wameshikilia nchi hii. Endapo tukiwasambaratisha itakuwa ni nafasi yangu nzuri ya kugombania kiti cha urais. Siwezi kugombania endapo wapo hai"
“Kwa nini una taka kumuua Tiger na familia yake”
“Unataka kujua?”
“Ndio”
“Leo nitakuambia ni kwa nini nilijiapiza kumuua Tiger na familia yake nzima”
Mwanamama bilionea alizungumza na kumfanya dokta Boaz kukaa vizuri ili kumsikiliza.
ITAENDELEA
Mchaka mchaka mpya umeanza. Wameamua kumrudisha Jack nyumbani ili kumuepusha na muuaji ambaye ni dokta Boaz. Ila dokta Boaz amekuja na mpango mwengine wa kutumia makomandoo kwenda kuivamia familia ya Tiger je nini kitatokea? Ni nini mwana mama bilionea alicho fanyiwa na mzee Tiger? Ungana nami katika stori hii ya kusisimua sehemu ya 58.