Mawazo kama haya daima hayawezi kulisaidia taifa hili zaidi ya kulisambaratisha.
Mawazo kama haya ya kuanza kumbagua huyu na yule kwa kabila lake ama dini yake ni mawazo mufilisi yasio na chembe ya msaada wowote kwa hali mbaya ya kiuchumi inayowakabili watanzania hususani vijana.
Ieleweke, viongozi BAVICHA wanapatikana kwa misingi ya kidemokrasia na hawa waliokp sasa hivi waligombea wakashindana na vijana wengine na wao wakashinda na sasa wanawahudumia vijana kwa nafasi zao.
Ieleweke mkutano mkuu wa BAVICHA unaundwa na vijana kutoka majimbo, wilaya na mikoa yote ya Tanzania kama ilivyo kwa Kamati Tendaji ya BAVICHA taifa inayoundwa na vijana wa mikoa yote Tanzania. Vyombo hivi ndio vilivyowachagua wakina Munishi na Heche kuongoza BAVICHA. Sasa kama wasukuma, wakurya, wabena, wangoni, wasambaa, wanyakyusa, wamwera, wahaya, wanyamwezi wamakonde n.k siku hizi ni wachaga, basi wachaga hao wanastahili pongezi.
Huyo Munishi (Katibu Mkuu wa BAVICHA) unayelia lia alishindana na watu tisa. (Taarifa tu)
Huyo Munishi na Mallyawanazungumza kuhusu tatizo la boda boda ambalo Chama Chenu cha CCM na serikali yake imelisababisha. Wanazungumza kuhusu tatizo la ajira ambalo serikali yenu ya CCM imelisababisha na kushindwa kulitatua.Wanazungumza kuhusu tatizo la elimu mbovu ambayo serikali yenu ya CCM imekua ikiwapa vijana hawa na hivyo mwisho wa siku wanashindwa kujiajiri na hata kuajiriwa.
Hizi ndio hoja za msingi za kujadili kama zina mashiko kwa mustakhabali wa vijana wa taifa hili na sio aliyetoa hoja ni kabila gani.
Uchaga wao unahusiana vipi na kukosekana kwa ajira kwa vijana nchi hii?
Uchaga wao unahusiana vipi na kuporomoka kwa kiwango cha elimu nchini?
Uchaga wao unahusiana vipi na kutokuwepo kwa mapinduzi ya viwanda nchi vitakavyoajiri mamilioni ya vijan wetu?
Uchaga wao unahusiana vipi na kutokuwepo kwa mapinduzi ya kilimo nchini ili kuajiri vijana wengi ?
Uchaga wao unahusiana vipi na kukosekana kwa uongozi bora nchi?
Vijana wa CHADEMA hawajali makabila ya viongozi wao kwani hawatambiki.
Vijana wa CHADEMA wanajali uwajibikaji, uongozi bora, umakini, utu na sio kabila la mtu.
Asanteni kwa kuelewa (Kama umeelewa)