jamaani naangalia ukurasa-EATV nimeona viongozi wa bavicha Dar wakilalamikia waendesha pikipiki kuingia katikati ya jiji. lakini naombeni mnisaidie kunitoa tongotongo jamani. hivi hakuna makabila mengine zaidi ya wachaga wanaoweza kuongoza huko chadema? nimeshangaa jiji la Dar lililojaa makabila mbalimbali lakini nafasi zote muhimu zinaongozwa na wachaga tu kuanzia mwenyekiti wa mkoa henry kileo kumbe mpaka bavicha mwenyekiti na katibu ni mnishi na malya.
msaada tafadhali, kulikoni wachaga na chadema?
Mtoa mada una makengeza ya ubongo! Wewe umewahi kugombea nafasi yoyote ya uongozi ndani ya CDM ukatoswa kwa sababu tuu wewe si mchaga? Usijaribu kurusha mateke kuelekea CDM huku ukiwa ndani ya CCM.
Kwa taarifa yako ukitaka kupenya kwenye uongozi CCM kuanzia ngazi ya wilaya ni lazima uwe mtoto angalau wa mwenyekiti wa CCM wilaya. Watoto wa makapuku wote watabaki kuwa wenyeti wa vijiji na mitaa ndani ya CCM na wengine kuwa mabalozi wa nyumba kumi. Ukitaka kuwa DC, Mjumbe wa NEC, mbunge kupitia CCM lazima uwe na backup ya wazazi, wajomba, shangazi n.k. Akiwa binti inabidi awe nyumba ndogo wa kigogo wa CCM.