Daraja2
JF-Expert Member
- Jul 10, 2017
- 285
- 346
Habari watanzania wenzangu,
Jioni ya leo ningependa tujadili suala hili la deni letu kwa heshima,unyenyekevu,busara na hekima tulizo jaaliwa na Mwenyezi Mungu (mwingi wa rehma mwenye kurehemu).
Kwanza napenda kuipongeza serikali yetu kwa kuliweka wazi kwetu sote.
USHAURI WANGU.
1. Uandaliwe mkeka maalumu wa Taifa ili Kila Mmoja aweze kulipa deni lake kikamilifu bila kificho (1.7m)
2. Serikali iiombe Bank ya Dunia itutengenezee A/c maalumu kwa ajili ya malipo ya deni la Tanzania.
MAELEZO MUHIMU.
1.Mtu akilipa deni jina lake lijitokeze mara Moja kwa umma wa Watanzania.
Wataalamu wa mambo ya fedha wapendekeze hata malipo ya kidogo kidogo kuanzia 10,000 na kuendelea kwa Tshs. Kama itawezekana mbali na Dola.
2.Tuwekeane muda maalumu ikiwezekana miezi 18 kuanzia makubaliano yatakapokubalika kwa mchakato kuanza.
3.Tukubaliane kwa ujumla hakuna kukopa Tena kuanzia Sasa.
4.Baada ya deni kuisha Kama Taifa itungwe Sheria mpya namna bora ya kukopa Kama itahitajika kwa kushirikisha Watanzania wote.
MWISHO KABISA INGAWA SI KWA UMUHIMU.
Nipo tayari kumlipia Mtanzania mwenzangu Mmoja.
Ahsanteni.
Jioni ya leo ningependa tujadili suala hili la deni letu kwa heshima,unyenyekevu,busara na hekima tulizo jaaliwa na Mwenyezi Mungu (mwingi wa rehma mwenye kurehemu).
Kwanza napenda kuipongeza serikali yetu kwa kuliweka wazi kwetu sote.
USHAURI WANGU.
1. Uandaliwe mkeka maalumu wa Taifa ili Kila Mmoja aweze kulipa deni lake kikamilifu bila kificho (1.7m)
2. Serikali iiombe Bank ya Dunia itutengenezee A/c maalumu kwa ajili ya malipo ya deni la Tanzania.
MAELEZO MUHIMU.
1.Mtu akilipa deni jina lake lijitokeze mara Moja kwa umma wa Watanzania.
Wataalamu wa mambo ya fedha wapendekeze hata malipo ya kidogo kidogo kuanzia 10,000 na kuendelea kwa Tshs. Kama itawezekana mbali na Dola.
2.Tuwekeane muda maalumu ikiwezekana miezi 18 kuanzia makubaliano yatakapokubalika kwa mchakato kuanza.
3.Tukubaliane kwa ujumla hakuna kukopa Tena kuanzia Sasa.
4.Baada ya deni kuisha Kama Taifa itungwe Sheria mpya namna bora ya kukopa Kama itahitajika kwa kushirikisha Watanzania wote.
MWISHO KABISA INGAWA SI KWA UMUHIMU.
Nipo tayari kumlipia Mtanzania mwenzangu Mmoja.
Ahsanteni.