DED wa Mtama na Mkurugenzi wa umwagiliaji wamkimbia Waziri mkuu na kuzima simu, mh Majaliwa awataka kuripoti Dsm kesho asubuhi

johnthebaptist

JF-Expert Member
May 27, 2014
83,968
141,976
Mkurugenzi wa halmashauri ya mji wa Mtama ( Lindi vijijini) na mkurugenzi wa umwagiliaji kanda ya kusini wametakiwa kuripoti ofisini kwa waziri mkuu kesho asubuhi bila kukosa.

Viongozi hao walitakiwa kuwepo kwenye msafara wa waziri mkuu alipokuwa akikagua mradi wa ujenzi wa scheme ya umwagiliaji pale Mtama unaogharimu zaidi ya sh milioni 700.
Imeelezwa kuwa zaidi ya sh milioni 400 zimeshatumika lakini katika eneo la mradi hakuna kilichofanyika. Ndipo mh Majaliwa akawaita DED na boss wa umwagiliaji ili watoe maelezo lakini wote wawili hawakuwepo na simu zao zilikuwa zimezimwa.

Ndipo waziri mkuu akaagiza watafutwe na wamfuate uwanja wa ndege na wasipomuwahi basi wamfuate Dsm kesho asubuhi.
Hadi waziri mkuu anaondoka wakurugenzi hao walikuwa hawajafika na simu zao hazikupatikana, ndipo mh Majaliwa akarudia maagizo yake kuwa wamfuate Dsm kesho asubuhi bila kukosa vinginevyo atachukua maamuzi tarajiwa.

Source Channel ten !
 
Viongozi hao walitakiwa kuwepo kwenye msafara wa waziri mkuu alipokuwa akikagua mradi wa ujenzi wa scheme ya umwagiliaji pale Mtama unaogharimu zaidi ya sh milioni 700.
Imeelezwa kuwa zaidi ya sh milioni 400 zimeshatumika lakini katika eneo la mradi hakuna kilichofanyika.


Wamejichoka yawezekana wapo wengi wa aina yao hao wametangulia
 
Mkurugenzi wa manispaa ya Mtama na mkurugenzi wa umwagiliaji kanda ya kusini wametakiwa kuripoti ofisini kwa waziri mkuu kesho asubuhi bila kukosa.

Viongozi hao walitakiwa kuwepo kwenye msafara wa waziri mkuu alipokuwa akikagua mradi wa ujenzi wa scheme ya umwagiliaji pale Mtama unaogharimu zaidi ya sh milioni 700.
Imeelezwa kuwa zaidi ya sh milioni 400 zimeshatumika lakini katika eneo la mradi hakuna kilichofanyika. Ndipo mh Majaliwa akawaita Ded na boss wa umwagiliaji ili watoe maelezo lakini wote wawili hawakuwepo na simu zao zilikuwa zimezimwa.

Ndipo waziri mkuu akaagiza watafutwe na wamfuate uwanja wa ndege na wasipomuwahi basi wamfuate Dsm kesho asubuhi.
Hadi waziri mkuu anaondoka wakurugenzi hao walikuwa hawajafika na simu zao hazikupatikana, ndipo mh Majaliwa akarudia maagizo yake kuwa wamfuate Dsm kesho asubuhi bila kukosa vinginevyo atachukua maamuzi tarajiwa.

Source Channel ten !

Huyo PM na rais wanacheza mazingaombwe ya siasa nyepesi, washauriwe tu warudi Dar kuja kupanga wizi wa kura maana wananchi washawastukia ni wasaka sifa binafsi. Wana miaka minne madarakani wameshindwa kujenga mifumo imara ya uwajibikaji mpaka wao waende kwenye miradi ndio wajue upigaji. Mtu asiyejua lolote anaweza kuamini rais na waziri mkuu ni wachapa kazi, kumbe kwa sehemu yenye mifumo imara hao viongozi ni futuhi. Waambiwe watu wamegoma kupiga kura maana wamegundua hata wao sio wasafi bali ni wanajisi box la kura.
 
Kazi nzuri, lakini ni wakati huu tu ?? Au tutaendelea hivi

Wanacheza siasa za futuhi, hapo katikati hamna watendaji wa ngazi husika, kama mkuu wa mkoa, watu wa TAKUKURU mpaka PM aende ndio ajue wizi? Huo ni ushahidi kuwa mifumo haifanyi kazi bali watu wameamua kusaka sifa. Kwa maneno marahisi wezi huko serikalini wamekuwa digital huku viongozi wa juu walibaki analogia.
 
Back
Top Bottom