Dean of student na deputy provost of academic affairs wafukuzwa kazi kcmc-tumaini un

kcmc-students

Member
Sep 9, 2010
15
0
Aibu kubwa imeikumba tena GSF kwa kupitia uozo uliopo madarakani wa bodi ya chuo cha udaktari kcm college chini ya uonozi wake ajiitae bishop martin shao.
kweli huku ni kukosa maarifa yale aliyoandikwa kwenye vitabu vitakatifu na kukumbatia uovu na uonevu juu ya waongea ukweli na utetezi juu ya haki za msingi za kibinadamu na kiroho pia.

kuachishwa kazi dean of student kwa kisingizio eti ameshindwa kutatua migogoro ya wanafunzi na pia kusema anakula rushwa kweli ni kosa la jinai kumsingizia mama yetu mchungaji martha massawe tutapata hukumu kubwa machoni kwa bwana siku ya hukumu na majoho yetu ya kiaskofu.
inakuwaje ufanisi wa mtu hauonekani tokea siku ya kwanza aingiapo ofini na kuja kumevaluate siku ya mwisho itokeapo dhoruba kali na isiyomhusu.

nduli wetu provost amekuwa mtu mwenye kushindwa kutimiza majukumu ya watendaji waliopo chini ya ofisi yake.
dean ameshindwa kupata hata kompyuta na printer hata ya kumsaidia kutunza rekodi katika majadala na wakati wote amekuwa akitumia ya idara ya research na kutokana na kero na kuelemewa kwa kutoa msaada huku nduli akishindwa kutoa mafungu kwa idara hiyo muhimu ya kijamii.

wakati mwingi dean amekuwa akiomba hata simu awasiliane na bodi ya mikopo ili kutatua matatizo ya wanafunzi wafikapo ofisini kwao na wakati mwingine inambidi atumie simu ya mkononi mwake personal phone ili kuepuka mikwaruzo hiyo na huyo bi mdogo wa provost amela(provost personal secretary).
kwa upande mwingine provost mwenyewe amediriki kufuta safari za dean na kuunganisha na trip zake binafsi aendapo mjini akidai atapitia loan board kitu ambacho amekuwa hafanyi hivyo na kula allowance za bure ambazo ilikuwa ni stahiki za dean.huu ni ubinafsi na kuwaumiza watoto wa watanzania wategemeao chombo nyeti kuweka hali ya watoto wao vyema wasomapo.

serikali ya wanafunzi kupitia ofisi ya dean wamekuwa na mikutano mingi ya kiutendaji na wakati mwengine wamekuwa wakimwomba mkuu wa chuo hiki aka nduli na kuishia kupewa ahadi na visingizio lukuki kitu kinajulikana siku zote ni kwa mkuu huyu kukimbia majukumu yake hasa pale aombwapo kukutana na wanafunzi.leo unasemaje mama huyu hakuwa na jitihada ,shame on you ..sometime i real doubts how come you guys have become bishops and proffesors na kulitumia jina la kristu vibaya.

tatu ni aibu kubwa kusema hadharani leo dean of student analipwa mshahara ulinganao na waden wa hosteli ya wanafunzi kweli......huku ni kudhalilishana na wizi usiovumulika na unyonyaji wa damu .
mi sijui kweli huyu mzee ana dementia ama hajui kada za watendaji ofini kwake na hata kusoma kwa majirani wenzake wanalipaga shilingi ngapi kweli
na mwisho swala la rushwa serikali lina vyombo vyake vya kisheria kutenda haki juu ya madai kama hayo leo hii ikiwa hakuna dai lolote limewafikia ofisi hizo na hakuna ushahidi wowote uliopatikana hata hapa chuoni iweje useme dean anaomba hongo ili kutratua matatizo ya wanafunzi .

tetesi za chuo hiki kupewa hadhi ya kuwa chuo kikuu kamili na siyo tegemezi kwa tumaini university kimemtisha mkuu aliyeko sasa madarakani takribani miaka 16 bila mafanikio. hii ni kweli kwamba mkuu huyu endapo chuo hiki kitapewa hadhi hiyo basi aliyestahili ni prof.mallya ambaye alikuwa ni deputy provost in academic affairs kipenzi cha wanafunzi na waajiriwa wote hapa chuoni .hii ni kutokana na umahiri wake katika utendaji na kuchapa kazi bila uvivu na majungu na kutokuwa na mahusiano na watumishi wengine hasa yalee ya kimapenzi kama aliyepo.
mkuu huyu pia amekuwa akiaminika na kutumika katika mabaraza mbalimbali ya kitaifa kutokan ana na shule aliyokuwa nayo.
kumkosa hapa chuoni ni pengo kubwa sana .
madai ya kuondolewa kwake yamekuwa si ya msingi na kuficha ukweli na chuki aliyokuwa nayo huyu nduli wetu provost.
kusema mallya anawaunga mkono wanafunzi madai yao na kukimbia utawala hii imekuwa si jambo la kustajaabisha kwani ni muda mrefu wamekuwa wakilikumbatia jahazi la provost na bodi yote likiwa limebeba uozo usiovumilika harufu yake na hakuna asiyeacha kujua kuanzia maspecialist mpaka walinzi wa chuo na hospitali.

huyu baba amekuwa mstari wa mbele kujikomba na kujikosha kwa sauti yake nyembamba kwa mheshimiwa askofu malasusa akidai mambo yamekuwa yakienda sawa kumbe moto unawaka na kutumia ubabe wa kizee kusulubisha watu wasiokuwa na hati ahasa akishirikiana na vice chancellor wa tumaini aka cheupe ,wakiendeleza uozo kwenye taasisi hii.

kama kuna kitu mheshimiwa askofu malasusa utakachokarimiwa milelele juu mbingu na kuwa mmoja wa mtakatifu hapa duniani ni kuto wafungia macho mkuu wetu wa chuo na vice chancellor wa tumaini mh,shayo kweli tunaomba wastaafu tu kwa manufaa ya watanzania wote na GSF kwa ujumla.hii ni kero kubwa nastahili kuiita dhambii kubwa isiyovumilika machoni kwa watu waliostarabika kichwani na kiroho pia.

ombi la pekee ni kwa tumaini university itupe viongozi wapya wa bodi ya chuo kwa waliopo wameshindwa kutenda wajibu wao hayta hatua ndogondogo za kuwajibisha watu unaanza kuwafukuza moja kwa moja na kuacha karipio thenn written letter na mwisho ndo barua .
pia uteuzi wa dean hauzingatiwi vigezo kwani huchukua wachungajii tuu bila hata kujua cv zao za form 4 na kuleta vituko wakati wa presentation kwenye bodi mbalimbali za kitaifa.uchaga na ulutheri usitumike vibaya katika kutetea maslai binafsi ila kutetea mission na vision ya tumaini
 
Back
Top Bottom