DC Richard Kasesela alishiriki kuzima moto kituo cha watoto Yatima Mgongo

figganigga

JF-Expert Member
Oct 17, 2010
25,717
55,819
Mkuu wa wilaya ya Iringa Mh Richard Kasesela alishiriki katika kuzima moto uliounguza bweni wanalo kaa watoto yatima katika kituo cha Mgongo. Moto huo ilioanza kwa hitalafu ya umeme umeteketeza bweni 3 na kuunguza mali za watoto hao ikiwemo nguo, madaftari magodoro. Kikosi cha zimamoto chini ya Mrakibu Komba kilifanya kazi ya ziada kuzuia moto huo usieneee majengo mengine. Wananchi wa eneo la Mgongo wamefanya kazi kubwa wakisaidiana na jeshi la zima moto.

Akizungumza na wananchi Mh Kasesela ameahidi kuomba wahisani pia kuangalia uwezekano wa kuwasaidia waathirika wa janga hili la moto. Inakadiriwa watoto zaidi ya 45 wameathirika na moto huu ingawaje hamna majeruhi hata mmoja. " Pongezi ziwandee jeshi la Zimamoto pamoja na changamoto walifanikiwa kuzima moto huo" aliesema Mkuu wa Wilaya. Mkuu wawilaya alikutana na watoto na kuwapa matumaini serikali ipo pamoja nao.
13626572_254431508262846_2936083836126775549_n (2).jpg
13606570_254432064929457_2115382045518832961_n.jpg
13599851_254431974929466_7290609759724204951_n.jpg
13592217_254431571596173_4213212812631906787_n.jpg
13620950_254431908262806_8005360221201806857_n.jpg
 
mbona alikuwa kama hayuko busy sana na moto anaonekana yuko busy sana na camera? au macho yangu?
 
Ukitazama picha hizi utaona kuwa harakati hizi zimefanyika wakati moto umeshazima, kwa mbali naziona hizi picha za maigizo ya kutaka kuonekana fulani kafanya kitu fulani,
 
Mzee wa makamera kama kawaida hasa ukizingatia mtukufu rais mwema Pombe alimsifia juzi ikulu kwa makamera haya-haya.
 
Vuta vuta kwa nguvu. Twanga foto, waaaah! hapo sijui walikuwa wanazima moto upi? Lakini picha imepigwaaa! Maigizo mengine balaa.

13606570_254432064929457_2115382045518832961_n-jpg.363612
 
Ukitazama picha hizi utaona kuwa harakati hizi zimefanyika wakati moto umeshazima, kwa mbali naziona hizi picha za maigizo ya kutaka kuonekana fulani kafanya kitu fulani,

Na ni hayo maigizo yamemfikisha hapo alipo, na uteuzi mpya mkuu amesema anamuacha hapo hapo Iringa kwakuwa watuwanamsemasema juu ya hizo picha za maigizo.

Sasa,anaanzaje kuacha kufanya maigizo hayo kwa mfano...?
 
kweli richard ana roho nzuri ya kusaidia na ni mchapa kazi kweli kweli...good job richard
 
Back
Top Bottom