DC Mrisho Gambo wa Arusha amhujumu mkuu wa mkoa

DC Mrisho Gambo wa Arusha amhujumu mkuu wa mkoa

Ukichukiwa na mtani wako ujue unafanya vizuri...ukipendwa/sifiwa na mtani lazima ujiangalie umejikwaa wapi.
 
Dah! Yaleyale ya Makonda kupewa barua ya kusimamia jiji lote la Dar wakati yeye ni D.C. wa Kinondoni! In Magufuli tik takas are so many!
 
Katika hali ambayo haikutarajiwa mkuu wa wilaya ya Arusha Mrisho Gambo ameanza kumhujumu mkuu wa mkoa Bwana Ntibenda. Hali hiyo imetokea leo eneo la nane nane Arusha,leo ndio siku ya uzinduzi rasmi wa siku ya nane nane ambako ilitegemewa watumishi wa halimashauri kuhudhuria sherehe hizo ambazo mgeni Rasmi ni Mkuu wa mkoa

Katika banda la halimashauri ya jiji la Arusha hakukuwa na mtendaji hata mmoja baada ya kuitwa kwenye kikao kingine na mkuu w wilaya ya Arusha bwana Gambo katika ukumbi wa chuo cha ufundi Arusha. Haikuweza kufahamika mara moja sababu ya mkuu wa wilaya kumtoroka bosi wake na kuitisha kikao kisicho na tija wakati akijua kuwa sherehe za nane nane ni za muhimu zaidi.

Baadhi ya watumishi walioenda kwenye kikao cha DC wamekerwa na tabia ya DC kujisifu kuwa yeye ndie mteule sahihi wa Rais na kuwa siku si nyingi atapandishwa cheo kuwa RC hivyo watumishi wote wamsikilize yeye vinginevyo atawahamishia Tandahimba au Chato.

Kitendo cha leo ni mwendelezo wa mgogoro wa chini kwa chini unaondelea kati ya mkuu wa wilaya na mkuu wa mkoa unaosababishwa na tabia ya DC kumuhujumu waziwazi RC na wakati mwingine kuongea maneno ya kashfa dhidi ya RC
Hongera mkuu
 
Tunaenda kushuhudia kiwango cha juu cha unafiki,fitina, majungu, umbeya na kujikomba kwa wateule mbalimbali katika serikali
Hakika ni hivyo.....ndani kwa ndani kwenye Ccm na serikalini wanamalizana
 
Watu wanapeana vitengo tu wanakula maisha!..khaaa
 
Katika hali ambayo haikutarajiwa mkuu wa wilaya ya Arusha Mrisho Gambo ameanza kumhujumu mkuu wa mkoa Bwana Ntibenda. Hali hiyo imetokea leo eneo la nane nane Arusha,leo ndio siku ya uzinduzi rasmi wa siku ya nane nane ambako ilitegemewa watumishi wa halimashauri kuhudhuria sherehe hizo ambazo mgeni Rasmi ni Mkuu wa mkoa

Katika banda la halimashauri ya jiji la Arusha hakukuwa na mtendaji hata mmoja baada ya kuitwa kwenye kikao kingine na mkuu w wilaya ya Arusha bwana Gambo katika ukumbi wa chuo cha ufundi Arusha. Haikuweza kufahamika mara moja sababu ya mkuu wa wilaya kumtoroka bosi wake na kuitisha kikao kisicho na tija wakati akijua kuwa sherehe za nane nane ni za muhimu zaidi.

Baadhi ya watumishi walioenda kwenye kikao cha DC wamekerwa na tabia ya DC kujisifu kuwa yeye ndie mteule sahihi wa Rais na kuwa siku si nyingi atapandishwa cheo kuwa RC hivyo watumishi wote wamsikilize yeye vinginevyo atawahamishia Tandahimba au Chato.

Kitendo cha leo ni mwendelezo wa mgogoro wa chini kwa chini unaondelea kati ya mkuu wa wilaya na mkuu wa mkoa unaosababishwa na tabia ya DC kumuhujumu waziwazi RC na wakati mwingine kuongea maneno ya kashfa dhidi ya RC
Ndo hivyo tena jamaa ameshalamba dume.Wenye karata namba Saba mikononi mpungieni mkono.
 
asante Mkuu kwa Uzi murua kweli tunapata mambo mazuri kwa kuwa "be the first to know"
 
Back
Top Bottom