Kwani Raia Mwema nalo pia mwana harakati Generali Ulimwengu kaliuza kama Rai na mengine?????????????
CCM ndo imejaaaa wahuni,wez,wajinga wanaoendelea kuvimbisha mitumbo yao bila kujua kuna wananchi wanalala njaa.Nangushangaa sana kuwa anti-maendeleoHalafu tukisema CHADEMA kimejaa wahuni kuanzia viongozi wake....Wapuuzi wengine humu wanaendelea kubisha. aaakhkhkhkh...puh!
Godfrey Dilunga tuambie ni njaa au ushabiki ndio unaokusumbua? Hii ni mara ya pili unatoa uchambuzi hafifu uliojaa ushabiki usiona maana. Nakumbuka ulitoa mada ya kupinga hotuba ya Lema bungeni aliyotoa kama waziri kivuli wa Mambo ya Ndani. Leo bila aibu unarudia upupu mwingine. Mbona unalidharirisha gazeti ambalo linaheshimika sasa hapa nchini!
sinunui Raia Mwema tena
Pamoja na uhuni huu walio uonesha Igunga inashangaza bado Chadema kinajiita ni Chama Makini! Chadema wanatumia akili za makalio kufikiria!
Wewe ndugu si ulisema ni mtumishi wa Mungu au siyo wewe nakosea? Mbona maneno yako siyo. Wewe kwa simple mind chadema ndo wenye makosa?Pamoja na uhuni huu walio uonesha Igunga inashangaza bado Chadema kinajiita ni Chama Makini! Chadema wanatumia akili za makalio kufikiria!
Mkuu umezungumza mengi sana kuonyesha udhaifu wa Chadema lakini pia umefanya makosa makubwa kuhusisha tukio hilo na chama lakini aliyoyafanya Dc kwa niaba ya chama hayahusiani na CCM isipokuwa unatazama haki ya Dc na sii ile ya wasimamizi wa kura wa Chadema jimbo la Igunga.DC Igunga amefichua udhaifu wa CHADEMA?
Godfrey Dilunga, Raia Mwema, 21 Sep 2011 Toleo na 204.
JE, kitendo cha Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kutokemea udhalilishaji dhidi ya Mkuu wa Wilaya (DC) ya Igunga, Fatuma Kimario, uliofanywa na ‘wahuni' wanaodaiwa ni wafuasi wa chama hicho, ni udhaifu? Je, ni udhaifu, hata kama hiki ni kipindi cha kampeni za uchaguzi wa ubunge Jimbo la Igunga?
Je, CHADEMA kujidai ‘kutoona' udhalilishaji ule eti tu kwa sababu DC naye anayo makosa yake ni udhaifu? Je, ni udhaifu katika misimamo ya kifalsafa au kimtazamo? Je, ni matukio gani mengine kuhusu CHADEMA yanayothibitisha udhaifu huu? Tujadili.
Kimsingi, CHADEMA kimeonyesha udhaifu. Ni udhaifu wa kujitetea kwa gharama yoyote ikiwamo kufumbia macho makosa yake dhidi ya raia wengine. Kuna hatari au dalili, chama hiki kinaanza kulewa. Ni ulevi wa kuamini wakati fulani kinaweza kuwa juu ya sheria kwa kauli mbiu ya ‘nguvu ya umma' isiyo halisi.
Wahuni wanaodaiwa wafuasi wa CHADEMA wamevamia kikao cha DC, Fatuma Kimario. Wakamkamata, wakampekua na kumdhalilisha (kwa maelezo ya awali). Vitendo hivi vimefanyika baada ya wahuni hao kuhisi hujuma. Eti siku hizi ukihisi tu, basi sheria zinakuruhusu kuvamia, kukamata na kupekua, tena bila kibali cha mamlaka husika? Hisia tu? Vipi, siku wahuni wengine wakihisi, kitu cha ovyo ofisi za CHADEMA na kuvamia?
Hisia ambazo ni chanzo cha uvamivi huo dhidi ya DC kujengewa uhalali au kutetewa kwa sababu tu karatasi ya ajenda za kikao cha DC zimehusisha agenda ya uchaguzi mdogo wa Igunga, ni jambo la kushangaza. Je, mkuu wa wilaya ambayo imo kwenye uchaguzi mdogo, anakatazwa kwa sheria gani kujadili suala hilo katika muktadha wa kiutawala? Sidhani kama hii ni sababu ya msingi.
Lakini ipo sababu ya muda wa mkutano, Mkuu wa Kitengo cha Ufuatiliaji na Tathmini wa Jeshi la Polisi, Issaya Mungulu, anasema CHADEMA walichelewa ratiba yao iliyokuwa kati ya saa nne hadi saa sita na DC mkutano wake ulikuwa saa nane. Hapa, nakala ya ratiba ndiyo muamuzi bado sijaipata na hivyo, sitajadili.
Hata hivyo, kuna udhaifu ndani ya CHADEMA. Tunaelezwa na Mungulu katika tukio hilo, DC alivuliwa hijabu, viatu, alikatiwa mkufu, achilia mbali simu yake kupotea. Inadaiwa pia DC alidhalilishwa kwa kutukanwa.
Kwa maelezo haya, ambayo ni dhahiri DC alifanyiwa vurugu kama ambavyo baadhi ya picha za magazeti ya zilivyoonesha tukio hilo, CHADEMA walipaswa kuonyesha ujasiri wa kimaadili, nidhamu, mila na desturi za kitanzania, kinyume chake wameonyesha udhaifu.
Walipaswa kueleza makosa ya DC lakini wakati huo huo, nilitaraji waombe radhi kwa vitendo vingine visivyo vya kimaadili wala vya kisheria dhidi ya DC huyo.
Tukumbushane. Wakati Mwenyekiti wa CHADEMA, Freeman Mbowe, alipotuhumiwa kudharau Mahakama mkoani Arusha ambako anayo kesi, Mahakama hiyo ilitoa amri akamatwe. CHADEMA kilipinga amri hiyo ya Mahakama kuwa, utekelezaji wake unakiuka sheria, mila na desturi za miaka mingi zinazohusu kinga, haki na madaraka ya Bunge.
Lakini katika taarifa iliyotolewa na Tundu Lissu, kwa upande mwingine,CHADEMA kwa kutumia jina la Kambi ya rasmi ya Upinzani, ililalamika kwa nini Mbunge wa Busega, Dk. Titus Kamani, alikamatwa baada ya taratibu za kisheria kufuatwa na Mbowe akamatwe bila taratibu hizo?
Kwamba, Dk. Kamani ambaye anatuhumiwa kupanga mauaji kwanini kabla ya kukamatwa, polisi walifuata utaratibu kwa kuomba kibali cha Bunge, wakati Mbowe anataka kukamatwa bila kibali cha Bunge?
Mantiki hapa ni kwamba, Lissu alikuwa akisisitiza umuhimu wa kufuata sheria na taratibu. Kwamba, utaratibu wa kumkamata mbunge ni lazima uwe na idhini ya Bunge, ingawa pia uongozi wa Bunge ulifafanua suala hilo kwa maelezo ya kina.
Kwa kuzingatia mantiki hiyo ya Lissu kusisitiza utiifu wa sheria na taratibu tujiulize. Je, hatua ya kuvamia mkutano wa DC, kumkamata, kumpekua (kwa kutumia vijana wa kiume) kumezingatia taratibu kisheria? Je, ni halali kuvunja taratibu za kisheria kwa sababu tu, DC naye amezivunja?
Lakini kama taratibu za kisheria hazikuzingatiwa katika kumvamia DC, kwa nini CHADEMA leo hii inakosa ujasiri wa kuomba radhi kwa makosa yake? Na kama haiombi radhi, kwa nini isiwakane wahusika? Kwa kuzingatia tukio la DC kuvamiwa na hili la Mbowe kutaka kukamatwa bila kibali; Je, uzingatiaji wa sheria na taratibu ni muhimu wakati gani kwa upande wa CHADEMA?
Mungu ibariki Tanzania, Mungu ibariki Afrika
JAMANI MAMBO HAYO NA reserve comment zangu kwa sababu naweza kua bias wenzangu semeni
Halafu tukisema CHADEMA kimejaa wahuni kuanzia viongozi wake....Wapuuzi wengine humu wanaendelea kubisha. aaakhkhkhkh...puh!
Godfrey Dilunga tuambie ni njaa au ushabiki ndio unaokusumbua? Hii ni mara ya pili unatoa uchambuzi hafifu uliojaa ushabiki usiona maana. Nakumbuka ulitoa mada ya kupinga hotuba ya Lema bungeni aliyotoa kama waziri kivuli wa Mambo ya Ndani. Leo bila aibu unarudia upupu mwingine. Mbona unalidharirisha gazeti ambalo linaheshimika sasa hapa nchini!