DC adai talaka mbili kwa mpigo mahakamani

Mkuu kwa mantiki ya maelezo ni kwamba, baada ya kushindwana ndiyo akaoa mke mwingine bomani ambaye naye wameshindwana pia.

Kwa maelezo ya mdai talaka na maswali ya mdaiwa, yananivuta kuwa upande wa dc.
Unaambiwa hapo alipo anaishi na mwanamke mwingine. Labda akifanikiwa kawapa hawa wawili talaka ndo atafunga ndoa nyingine na huyo anaeishi nae kwa sasa.
 
Hivi Kuna MaDC wa Aina hii wapo hapa Tz na serikali yetu Pendwa,SADC inaisha lini jamani??
Maana tunatamani iishe ili twende Town tukale bata.

Hawa MaDC wakumbuke uchaguzi mwakani,na newly DC watakuja kwenye hizo nafasi.
Nahisi huyo mama kapiga hesabu za mwakani.
 
Hayo mengine tusimuhusishe sana Mungu, kwa sababu inaonesha kwa maelezo ya hapo mahakamani, huyo mwanamke ni maruhuni na kuna mtu kamkochi ujinga.
Point hapo ni kwamba, hawa viongozi wanatakiwa kuwa kioo cha jamii.
Hatakiwi kuonesha missbehave ya aina yoyote ile ama dalili, ama kuhisiwa tu.
Hii kesi inatafsiri mbovu sana kwa huyo dc, tafsiri ya kushindwa kuicontrol familia yake.
Mtu anayeshindwa kuongoza vizuri familia yake ambayo ni kikundi kidogo cha watu, je kundi kubwa la kijamii kama wilaya?
Huyo moja kwa moja kajinyang'anya sifa mwenyewe na hastahili kupewa uongozi hata wa kitongoji.
Watu wa maadali ama mwajiri wake, waliangalie hili, ili hatua madhubuti za kimaadili zichukuliwe mapema dhidi yake,hata kabla kesi hii haijafikia ukomo.
Kwenye kada ya uongozi hafai hata kulumangila, aondolewe akafanye kazi nyingine.
Wakati mwingine ni heri kuongoza watu 1000 kuliko kuongoza mke mmoja mwenye dharau kali,aliyepata kijamaa kinachomvimbisha kichwa na kumjaza matumaini ya uongo na kipumbavu.
:-Apewe talaka yake atembee mbele,ameshapa mke mwenye heshima mnyenyekevu na mwenye adabu.
 
Kuna mambo mawili hapa inabidi DC uyatazame kwa makini
1. Mwajiri wako hapendezwi na kitendo cha kutumia muda mwingi mahakamani wakati watu wake wakikosa mtatuzi wa kero zao.
2. Haya ni maisha tu, kuendelea kuishi na huyo mama hakukugharimu chochote, ni kweli inawezekana ana mapungufu yote hayo, fikiria kwanini mwanzoni ulishauriwa utoe talaka ukakataa na leo wewe uliyekataa kutoa talaka ndiye unaomba talaka, tafakari kwa kina Mungu anaongea nawe jipe nafasi ya kutafakari jambo hilo
Namba 1, ipo sawa ila namba 2 haipo Sawa, hata kama haimgarimu chochote hapo hakuna mapenzi tena na huenda tukashuhudia ukatili wa wazi kama ule wa kigamboni na gunia mbili za mkaa. Cha msingi aachane kesi akashughulikie shida za wananchi Wake, kama ana nia thabiti ya ndoa zake abadili dini awe muislamu, huko atapata ufumbuzi sahihi wa ndoa, ktk uislamu kilichofungwa duniani kinamalizikia hapa hapa duniani.
 
Kumbe talaka ni ngumu kuipata
Achana nayo hiyo kitu ni ngumu na huwezi kuitoa kirahisi rahisi hasa ndoa za kikristo. Kwa waislamu haina ugumu ni rahisi sana. Tena kwa maelezo hayo kwa imani ya kiislamu hapo hakuna ndoa
 
Sasa hamuishi pamoja toka 2003 halafu hutaki mtalakiane ili kumkomoa asione tena au upumbavu tu?

Maana inaonekana huyo mke ndiyo chanzo cha kutengana sasa anag'ang'ania?
 
Unaambiwa hapo alipo anaishi na mwanamke mwingine. Labda akifanikiwa kawapa hawa wawili talaka ndo atafunga ndoa nyingine na huyo anaeishi nae kwa sasa.
Mkuu chama chetu hiki pendwa, chama chenye wanachama wengi kuzidi wanachama wa ccm, ni kigumu sana.
 
Kisheria kama wanandoa wametengana kwa miaka mitatu mfululizo kwa uamuzi wao wenyewe, basi ndoa haipo tena. Hata hivyo, huyo mke anang'ang'ania ndoa na kusema haivunjiki wakati haishi na mumewe maana yake nini? Hivi hajui mumewe anaweza kusema amekubali warudiane halafu akanunua magunia mawili ya mkaa akafanya kile yule jamaa alichofanya kwa mke wake akamchomelea mbali?
Itakuea anataka kuwa mama DC........
 
Back
Top Bottom