DAWA YA UPWEKE NI NDOA

DAWA YA UPWEKE NI NDOA

Sawa umesema pesa haimfanyi mwanamke kuwa juu ya mwanaume ila naomba nikuulize swali kwani ni kipi kinachomfanya mwanaume kuwa juu ya mwanamke?
Kulingana na imani imani za kikiristo .
Biblia katika kitabu cha Mwanzo kinasema Eva aliumbwa kutoka katika ubavu wa adamu baada ya Adamu kuwa katika usingizi mzito..na kusudi la kuumbwa kwa Eva ni kuwa msaidizi wa Adamu

Swali 1.Je hapo nani yuko juu ya Mwenzake?
2.Je nani anapaswa kusikiliza na kufuata maelekezo ya mwenzake? Je ni Mwanamke au Mwanaume

Nb:Nadhan umepata Mwanga kidogo kwamba Mwanamke anapaswa kuwa chini ya Mwanaume kwa usalama wake na furaha yake
 
Sawa umesema pesa haimfanyi mwanamke kuwa juu ya mwanaume ila naomba nikuulize swali kwani ni kipi kinachomfanya mwanaume kuwa juu ya mwanamke?
Nature.. Sir God alisema wazi, sijui hata kwa nini mnalumbana kwa vitu visivyo na msingi. Unataka kuwa juu ya mume? Unataka usawa? Nini kinafanya utake usawa ndani ya nyumba, ni kazi/pesa? You'll doomed to think so!!
 
Wewe, hakuna anayewachukia wanaume wala anayetaka kushindana na wanaume ila ninachotaka ujue ni kwamba wanawake wenye mitazamo kama yangu wapo wengi tu tena wengi kuliko mnavyodhani ila tofauti ni kwamba wengine hawana ujasiri wa kuyaongea humu mitandaoni ila mimi sioni aibu kuyaongea

Kwahiyo nimegundua ninyi siyo kwamba hamjui kuwa wanawake wa aina hiyo wapo mnajua sana ila hamtaki tu wajionyeshe yaani mnataka waende na ninyi kinafiki ndo maana mnanishangaa mimi kujionyesha

Sasa mimi unafiki siwezi ndugu yangu mimi miaka mia unafiki ulishanishinda muogope sana mtu mnafiki na hata maandiko yanasema unafiki ni dhambi kwahiyo wanawake wa hivi tupo wengi ila tofauti yetu ni kwamba wengi hawajionyeshi wengine tunajionyesha

Sasa wale wasiojionyesha ndo wanaonekana wastaarabu wakati mioyoni mwao wanawaza kama sisi tu yaani kama unanibishia wewe jiulize kwanini ndoa nyingi siku hizi hazidumu wewe tulia bado haujatujua wanawake vizuri kama tunavyojijua sisi wenyewe.
Pitia nyuzi zote za mahusianoi/ndoa uone anavotiririka nao mpaka mwisho akiwa negative tu
 
Nashukuru umesema kuwa mwanamke aliumbwa kama msaidizi tu kwa mwanaume sasa ndugu yangu hebu nisaidie unakuta kwenye familia nyingi baba anatafuta pesa na anahudumia watoto tu hafanyi kazi za nyumbani wala halei watoto ila mama anatafuta pesa anahudumia watoto anafanya kazi za nyumbani na analea watoto

Hivi hapo ni nani anayefanya majukumu mengi kuliko mwenzie na hapo nani anakuwa mkuu na nani msaidizi? Maana kumbuka kikawaida msaidizi hatakiwi kufanya majukumu mengi kumzidi mkuu yaani ni sawa useme makamu wa rais afanye majukumu mengi kuliko rais hiyo inaleta picha kweli?
Kulingana na imani imani za kikiristo .
Biblia katika kitabu cha Mwanzo kinasema Eva aliumbwa kutoka katika ubavu wa adamu baada ya Adamu kuwa katika usingizi mzito..na kusudi la kuumbwa kwa Eva ni kuwa msaidizi wa Adamu

Swali 1.Je hapo nani yuko juu ya Mwenzake?
2.Je nani anapaswa kusikiliza na kufuata maelekezo ya mwenzake? Je ni Mwanamke au Mwanaume

Nb:Nadhan umepata Mwanga kidogo kwamba Mwanamke anapaswa kuwa chini ya Mwanaume kwa usalama wake na furaha yake
 
Nature.. Sir God alisema wazi, sijui hata kwa nini mnalumbana kwa vitu visivyo na msingi. Unataka kuwa juu ya mume? Unataka usawa? Nini kinafanya utake usawa ndani ya nyumba, ni kazi/pesa? You'll doomed to think so!!
Sijui kwanini wanaume wengi mnashindwa kunielewa hapa na matokeo yake mnalazimisha kuwa nataka usawa na wanaume hakuna anayetaka kuwa sawa na wanaume ila kama baadhi ya wanaume hawatimizi majukumu yao unafikiri ni nani wa kulaumiwa hapo?

Kumbuka Mungu alipomwambia mwanaume kuwa atamtawala mwanamke pia alimwambia huyo huyo mwanaume kuwa atakula kwa jasho lake sasa inakuwaje leo hii kuna wanaume hawataki kula kwa jasho lao wanakula kwa jasho la wake zao halafu bado wanataka wawatawale wake zao? Kwahiyo wanachagua maandiko ya kuyafuata na ya kuyaacha au? Yaani kwamba wanaamua kufuata andiko la kuwatawala wake zao tu ila la kula kwa jasho lao hawalifuati?
 
Nashukuru umesema kuwa mwanamke aliumbwa kama msaidizi tu kwa mwanaume sasa ndugu yangu hebu nisaidie unakuta kwenye familia nyingi baba anatafuta pesa na anahudumia watoto tu hafanyi kazi za nyumbani wala halei watoto ila mama anatafuta pesa anahudumia watoto anafanya kazi za nyumbani na analea watoto

Hivi hapo ni nani anayefanya majukumu mengi kuliko mwenzie na hapo nani anakuwa mkuu na nani msaidizi? Maana kumbuka kikawaida msaidizi hatakiwi kufanya majukumu mengi kumzidi mkuu yaani ni sawa useme makamu wa rais afanye majukumu mengi kuliko rais hiyo inaleta picha kweli?
Swala la kutafuta pesa ni suala mtambuka binadamu wote wanatafuta pesa iwe mwananke au mwanaume wote lazima watafute pesa ili kuendesha maisha yao ..imagine mwanamke ambaye ajaolewa asitafute pesa eti kwa sababu ni jukumu la mwanamume(mpenzi)kutafuta pesa..ndio maana mwanamke wa haina hiyo anadharaulika kwa utegemezi na Mara nyingi wanaishia pabaya

Na ndio maana wazazi wako walichukua jukumu la kukupa elimu ili ujitegemee ..kijamii na kiuchumi

Katika suala la usaidizi wa mwanamke kwa mwanaume ..nashawishika kusema kuwa hata utafutaji wa pesa ni uthibitisho wa usaidizi wa mwanamke kwa mwanaume.. Sababu inawezeka mshahara(kipato) cha Mwanaume kinaweza kikawa hakitoshi na kipato cha mwanamke kikaokoa jahazi..na maana ya neno msaidizi likatimia(na hayo ndio mapenzi)

Kuhusiana na mwanamke kuonekana ana shughuli nyingi wakati ni msaidizi(kulingana na Maandiko) nadhani maana ya neno msaidizi haliku maanisha kuwa mwanaume afanye kazi zote huku mwanamke akiwa ame starehe na kusidia mwanaume pale panapo hitajika..ili maanisha mgawanyiko wa majukumu(division of labor) kulingana na ufanisi ..maana Mimi siwezi kwenda kupika jikoni wakati sina interest na upishi so huyo kazi ni ya mwanamke(au kulea mtoto,kupiga deki) Mimi nipe kazi kama kukata kuni ,na zingine za kiume ambazo Niko interested Nazo

Mbona simba jike anaenda kuwinda na kumletea nawindo simba dume na wanakula wote lakini jike halalamiki kuwa Mimi nafanya kazi ngumu wa kawati ni msaidizi?? (Joke)

Nampenda mwanamke mwenye uwezo wa kutafuta pesa kwa sababu moja tu:::siku nikifa watoto wangu wabaki katika mikono salama..na wapate malezi yote sawa na Yale ambayo ningewapa kama ningekuwa hai
 
Ukiona ndoa imedumu anzia miaka mi 5 kwenda mbele ujue kuna bwege mmoja ndani ya hiyo ndoa...YES nasema bwege kwasababu hata akikosewa yeye atakubali kujishusha na kuomba msamaha yeye.

Ndoa itadumu kama TU kuna ataekubali mwenzake awe JUU yake siku zote na muda wote ila sisi tunaotaka EQUALITY ndo zkijitahid sana ni miaka 3.

OA halafu ukutane na yule mwanamke wa kutaka USAWA yani hataki umuoneee anataka haki bin haki Lazima urudi hapa uanzishe thread kutushauri ambao hatujaoa TUSIOE.
Huyo mwanamke ambae hataki kuonewa ndo mzuri.Anatambua Thamani yake.Na kwa nini umuonee mtu unaempenda?
 
Ndoa haiwezi kuwa mbadala wa upwekeeeee... Tafuteni chanzo kingine
 
Utaweza kuwa na mwanamke wa aina hiyo!!!...yupo corrupt,labda upige usepe
Try Me! Hebu nijaribu uone nitakavyokufurahisha unadhani kila mwamamke ni malaya wa kupiga na kusepa kama wa kwako hao?

Dharau zangu juu ya baadhi ya wanaume ndo zimenifanya hadi leo hii niwe na mwanaume mmoja tu vinginevyo ningekuwa naikubalia kila takataka inayonitongoza wanaume malaya mixer wahuni wote hao kwangu ni takataka tu
 
Unadhani nin kimemfanya awe na mtazamo hasi juu ya wanaume ?
Wala hata sina mitazamo hasi juu ya wanaume mbona naamini wapo wanaume wengi tu wastaarabu na wanaojielewa ila ninachojaribu kuwaambia hawa ni kwamba waache kuwafanya wanawake waonekane kama ndo chanzo cha maovu mengi kwenye mahusiano kuliko wanaume wakati jinsi zote zina maovu yake halafu mbaya zaidi wanasisitiza kwamba wanawake ndo wabadilike ila wanaume wasibadilike waendelee hivyo hivyo sasa hapo lengo lao ni nini?

Si maana yake wanataka wanaume ndo wafurahie maisha ya mapenzi huku wanawake wanahuzunika? Eh wanawake wameteseka vya kutosha jamani sasa itabidi tu tubadilishe mitazamo tutafute uelekeo mwingine siyo tena kutaka tuishi maisha kama ya babu zetu na bibi zetu kwa kisingizio cha kuwa ndoa zao zilidumu bila kujua jinsi gani bibi zetu waliteseka sana hadi hizo ndoa zao kudumu huku babu zetu wakifurahia maisha sasa ndicho wanaume wengi wanachokitaka hadi leo hicho yaani kwao mwanamke kukubali kuteseka kwenye ndoa ndo unyenyekevu
 
Swala la kutafuta pesa ni suala mtambuka binadamu wote wanatafuta pesa iwe mwananke au mwanaume wote lazima watafute pesa ili kuendesha maisha yao ..imagine mwanamke ambaye ajaolewa asitafute pesa eti kwa sababu ni jukumu la mwanamume(mpenzi)kutafuta pesa..ndio maana mwanamke wa haina hiyo anadharaulika kwa utegemezi na Mara nyingi wanaishia pabaya

Na ndio maana wazazi wako walichukua jukumu la kukupa elimu ili ujitegemee ..kijamii na kiuchumi

Katika suala la usaidizi wa mwanamke kwa mwanaume ..nashawishika kusema kuwa hata utafutaji wa pesa ni uthibitisho wa usaidizi wa mwanamke kwa mwanaume.. Sababu inawezeka mshahara(kipato) cha Mwanaume kinaweza kikawa hakitoshi na kipato cha mwanamke kikaokoa jahazi..na maana ya neno msaidizi likatimia(na hayo ndio mapenzi)

Kuhusiana na mwanamke kuonekana ana shughuli nyingi wakati ni msaidizi(kulingana na Maandiko) nadhani maana ya neno msaidizi haliku maanisha kuwa mwanaume afanye kazi zote huku mwanamke akiwa ame starehe na kusidia mwanaume pale panapo hitajika..ili maanisha mgawanyiko wa majukumu(division of labor) kulingana na ufanisi ..maana Mimi siwezi kwenda kupika jikoni wakati sina interest na upishi so huyo kazi ni ya mwanamke(au kulea mtoto,kupiga deki) Mimi nipe kazi kama kukata kuni ,na zingine za kiume ambazo Niko interested Nazo

Mbona simba jike anaenda kuwinda na kumletea nawindo simba dume na wanakula wote lakini jike halalamiki kuwa Mimi nafanya kazi ngumu wa kawati ni msaidizi?? (Joke)

Nampenda mwanamke mwenye uwezo wa kutafuta pesa kwa sababu moja tu:::siku nikifa watoto wangu wabaki katika mikono salama..na wapate malezi yote sawa na Yale ambayo ningewapa kama ningekuwa hai
Lakini kumbuka maandiko yamesema mwanaume atakula kwa jasho lake? Haya sawa haina shida inawezekana kabisa mwanamke akafanya hayo majukumu yote lakini je mwanaume una uhakika kwamba kweli unastahili kufanyiwa yote hayo na mkeo yaani kwamba haumsaliti wala haumnyanyasi?
 
MMungu alishatupangia majukumu na mgawanyo wa kazi!
Kwa ujuaji na upotofu wetu.... tukayapindua...sasa kinachoendelea ndio hicho...
ndoa ...zinaelekea kufa na ule upendo wa maisha ya familia utaondoka...hakutakuwa na mapenzi tena bali maamuzi!
 
Wala hata sina mitazamo hasi juu ya wanaume mbona naamini wapo wanaume wengi tu wastaarabu na wanaojielewa ila ninachojaribu kuwaambia hawa ni kwamba waache kuwafanya wanawake waonekane kama ndo chanzo cha maovu mengi kwenye mahusiano kuliko wanaume wakati jinsi zote zina maovu yake halafu mbaya zaidi wanasisitiza kwamba wanawake ndo wabadilike ila wanaume wasibadilike waendelee hivyo hivyo sasa hapo lengo lao ni nini?
Si maana yake wanataka wanaume ndo wafurahie maisha ya mapenzi huku wanawake wanahuzunika? Eh wanawake wameteseka vya kutosha jamani sasa itabidi tu tubadilishe mitazamo tutafute uelekeo mwingine siyo tena kutaka tuishi maisha kama ya babu zetu na bibi zetu kwa kisingizio cha kuwa ndoa zao zilidumu bila kujua jinsi gani bibi zetu waliteseka sana hadi hizo ndoa zao kudumu huku babu zetu wakifurahia maisha sasa ndicho wanaume wengi wanachokitaka hadi leo hicho yaani kwao mwanamke kukubali kuteseka kwenye ndoa ndo unyenyekevu

Naweza kukuchumbia mkuu ?
 
Back
Top Bottom