DAWA YA UPWEKE NI NDOA

DAWA YA UPWEKE NI NDOA

Kumbe unajua kuwa kinachotakiwa ni haki sasa kama kinachotakiwa ni haki unaona ni haki mwanaume kumkosea mwanamke halafu anataka amvumilie ila mwanamke akimkosea mwanaume anaadhibiwa?

Kwani mwanaume anapokosea anaadhibiwa na nani? Huo mnaouita ni usawa ndo njia pekee za kufanya wote mfurahie ndoa ila wanaume mnataka kufanya vile vitu ambavyo vitawafurahisha nyie tu wanawake wasipofurahi nyie haiwahusu
Wewe inaelekea uliolewa na ukawa unalipiza kila kosa analofanya mumeo..akakuacha,umejenga mambo mengi sana akilini mwako
 
Namaanisha heshima au utii wa mwanamke kusikiliza na kufanya kila kitu anachosema au anachotaka mwanaume
Mwanaume gani alifanya hivyo?!...mimi babu yangu alikua anamkabidhi bibi mshahara
 
Suala la kusameheana ni suala la wahusika na si kwamba wanawake hawakosei na wakakosa kusamehewa kwenye ndoa zao..labda yalikukuts peke ysko
Labda nikupe mfano tu mwanaume akifumaniwa na mkewe anachepuka atataka mkewe amsamehe na amvumilie ila huyo huyo mwanaume akimfumania mkewe anachepuka anaweza akampiga, akamuacha, akamuongezea mke au hata kumuua kabisa sasa hiyo ni haki?

Naomba usiniambie habari za sijui mwanaume kaumbwa na tamaa sijui mwanaume kuchepuka ni kawaida huo upumbavu haupo kwenye maandiko (mimi naongelea amri za Mungu na siyo mila na desturi za mababu na mabibi zetu kwa sababu wao hawakuwa Mungu bali walikuwa binadamu kama sisi)
 
Naona haujanielewa nimesema kama wote na mkeo mnafanya kazi zinazotumia akili nyingi na wote mnarudi nyumbani usiku mmechoka halafu bado mke akirudi nyumbani anafanya kazi za nyumbani peke yake haumsaidii hilo unaona ni sawa kweli? Kumbuka WOTE mnafanya kazi siyo wewe peke yako
Mfano wa hizo kazi za kutuchosha wote kiasi hiko? maana kama tunafanya kazi za aina moja yawezekana kabisa mwanamke ukawa unachoka zaidi yangu.

ndio mana kuna wasaidizi wa nyumbani,ila kama tunaishiwawili tu asee kama mke/mpenzi wangu umechoka na nakuona mimi sioni shda kukufulia,kufanya usafi kukubeba kukuogesha na kukurudsha bed.

Najua kuna sku miili yetu itatofautina mimi ntakua sinanguvu kabsa so nawewe uta play ile part kama mimi ninavyofanyaga..lakini kama dada yupo ntahakikisha kila kitu chako unaandaliwa on time ili uwahi kupumzka.

Ki ufupi kwa wafanyakazi wa aina moja mnatoka saa 11 mnarudi saa mbili usku wote Hamna wa kumtegea mwenzake wote mkifika home mnashuhulika..wakat unaandaa chakula mimi napasi nguo za kazini za kesho..

Siwezi toka kazini na mke wangu nifikiekitandani yeye aendelee na kazi(siwezi) kwa wanaoweza ambao labda ndio unaowalenga kwa haya maswali..Jibu ni kwamba wanahitaji tu elimu kuna kitu bado hakijatoka kichwani mwao.
 
Labda nikupe mfano tu mwanaume akifumaniwa na mkewe anachepuka atataka mkewe amsamehe na amvumilie ila huyo huyo mwanaume akimfumania mkewe anachepuka anaweza akampiga, akamuacha, akamuongezea mke au hata kumuua kabisa sasa hiyo ni haki?

Naomba usiniambie habari za sijui mwanaume kaumbwa na tamaa sijui mwanaume kuchepuka ni kawaida huo upumbavu haupo kwenye maandiko (mimi naongelea amri za Mungu na siyo mila na desturi za mababu na mabibi zetu kwa sababu wao hawakuwa Mungu bali walikuwa binadamu kama sisi)
Hapo mfumaniaji ndiye mwenye maamuzi..kwa muislam mungu anamshauri aachane na mwenza akimfuma akifanya uchafu(zinaa,kusagana,kufillana)..
 
Wewe inaelekea uliolewa na ukawa unalipiza kila kosa analofanya mumeo..akakuacha,umejenga mambo mengi sana akilini mwako
Ndivyo mlivyo wanaume wa jf kwa kukariri hamjambo yaani haya ninayoongea umeshajipa uhakika kuwa yamenitokea kwenye maisha yangu utafikiri unanijua vile yaani mtu akitetea vilema basi na yeye kashakuwa kilema

Kwa taarifa yako nimeolewa na ndoa yangu ina amani na sina mume mwenye mitazamo ya kijinga kama ya kwenu hiyo ila kamwe sitaacha kuwasemea wanawake wenzangu

Hata mniite majina yote duniani sijui feminist sijui activist na mengine mtaongezea ila huo ndiyo ukweli na nimegundua wanaume kuambiwa ukweli huwa hampendi

Hasa kama huo ukweli unatoka kwa wanawake na badala yake ndo mnabaki mnatoa kauli kama hizo kuwa sijui tunapenda usawa sijui tunataka kushindana yaani hiyo huwa ndiyo defensive mechanism yenu
 
Ndivyo mlivyo wanaume wa jf kwa kukariri hamjambo yaani haya ninayoongea umeshajipa uhakika kuwa yamenitokea kwenye maisha yangu utafikiri unanijua vile yaani mtu akitetea vilema basi na yeye kashakuwa kilema

Kwa taarifa yako nimeolewa na ndoa yangu ina amani na sina mume mwenye mitazamo ya kijinga kama ya kwenu hiyo ila kamwe sitaacha kuwasemea wanawake wenzangu

Hata mniite majina yote duniani sijui feminist sijui activist na mengine mtaongezea ila huo ndiyo ukweli na nimegundua wanaume kuambiwa ukweli huwa hampendi

Hasa kama huo ukweli unatoka kwa wanawake na badala yake ndo mnabaki mnatoa kauli kama hizo kuwa sijui tunapenda usawa sijui tunataka kushindana yaani hiyo huwa ndiyo defensive mechanism yenu
 
Mwanaume gani alifanya hivyo?!...mimi babu yangu alikua anamkabidhi bibi mshahara
Kwani babu yako alikuwa anafanya majukumu gani kwenye familia na bibi yako alikuwa anafanya majukumu gani kwenye familia?
 
Kwani babu yako alikuwa anafanya majukumu gani kwenye familia na bibi yako alikuwa anafanya majukumu gani kwenye familia?
 
Labda nikupe mfano tu mwanaume akifumaniwa na mkewe anachepuka atataka mkewe amsamehe na amvumilie ila huyo huyo mwanaume akimfumania mkewe anachepuka anaweza akampiga, akamuacha, akamuongezea mke au hata kumuua kabisa sasa hiyo ni haki?

Naomba usiniambie habari za sijui mwanaume kaumbwa na tamaa sijui mwanaume kuchepuka ni kawaida huo upumbavu haupo kwenye maandiko (mimi naongelea amri za Mungu na siyo mila na desturi za mababu na mabibi zetu kwa sababu wao hawakuwa Mungu bali walikuwa binadamu kama sisi)
umeshawahi muona mwanaume aliyechepuka akafumaniwa anavyokuaga mdogo kama pini? hata ukiamua kumpga mangumi ya uso hawezi kukurudishia...ki ufupi hutambua kua lile ni kosa wamefanya ndio mana wananyweaga kiasi kile.

SASA BASI : nyie kinachowanyima kutuzibua makofi,kutupiga kama watoto,kutupa adhabu yyte ni kitu gani? mnatufumaniaga lakini mnaishia kuongea tu na kulalamika,nani kawanyima kutupiga hata vibao kama tunavyofanyaga sisi tukiwafumania?

Hamna mwanaume anaetaka kusamehewa akifumaniwa kachepuka ila ni nyie wenyewe na huruma zenu,kwa mfano mimi nikikosea hua natamani mpenzi wangu anizabue hata KOFI ndio naonaga ananipenda nakweli kakasirika..ila nakosea hunifanyi kitu,unalalamika tuu

Mwanaume ukikosea halalamiki anakuzabua tena ipasavyo...nyie kama mnashindwa kutuadhibu tunapokosea n shauri yenu ila sisi mkikosea tunazibua tena vizuri tu...

Labda unambie ni mwanamke gani kamfumania mume wake akaamua kumuacha Jamiii ika mua attack au mume akamfata akamlalamikia kwanini umeniacha...HURUMA ZENU ndio zinawaponza..wanaume wako real ila nyie mnakerwa mnakasirika badala muonyeshe hisia kwa vitendo mnaongea tu..

kwenye swala la adhabu tusilalamikiane ni uzembe wenu wenyewe.
 
Kwani babu yako alikuwa anafanya majukumu gani kwenye familia na bibi yako alikuwa anafanya majukumu gani kwenye familia?
Babu kuhudumia familia(kujenga,mkate wa kila siku) bibi kulea familia
 
Sasa mbona uongo unaouongelea wewe ndo huo huo uliomkataza mkeo? Wa kukudanganya kuwa alikuwa dukani kumbe alikuwa kwa jirani? Hata yeye si anakuwa amekudanganya ili kunusuru ndoa yenu?
Ruksa kunipa adhabu utakayo kama utagundua nimekudanganya..maana mimi ukinidanganya na ukweli naujua nakuzibua kofi..so kama wewe ukiamua kuni flash ni wewe hiyo.
 
Mfano wa hizo kazi za kutuchosha wote kiasi hiko? maana kama tunafanya kazi za aina moja yawezekana kabisa mwanamke ukawa unachoka zaidi yangu.

ndio mana kuna wasaidizi wa nyumbani,ila kama tunaishiwawili tu asee kama mke/mpenzi wangu umechoka na nakuona mimi sioni shda kukufulia,kufanya usafi kukubeba kukuogesha na kukurudsha bed.

Najua kuna sku miili yetu itatofautina mimi ntakua sinanguvu kabsa so nawewe uta play ile part kama mimi ninavyofanyaga..lakini kama dada yupo ntahakikisha kila kitu chako unaandaliwa on time ili uwahi kupumzka.

Ki ufupi kwa wafanyakazi wa aina moja mnatoka saa 11 mnarudi saa mbili usku wote Hamna wa kumtegea mwenzake wote mkifika home mnashuhulika..wakat unaandaa chakula mimi napasi nguo za kazini za kesho..

Siwezi toka kazini na mke wangu nifikiekitandani yeye aendelee na kazi(siwezi) kwa wanaoweza ambao labda ndio unaowalenga kwa haya maswali..Jibu ni kwamba wanahitaji tu elimu kuna kitu bado hakijatoka kichwani mwao.
Now we are communicating na ninaowalenga ndiyo hao ambao wake zao wanawasaidia majukumu yao ila wao hawataki kusaidia majukumu ya wake zao na kama wewe kweli upo hivyo kama unavyosema basi HONGERA KUBWA
 
We
Ndivyo mlivyo wanaume wa jf kwa kukariri hamjambo yaani haya ninayoongea umeshajipa uhakika kuwa yamenitokea kwenye maisha yangu utafikiri unanijua vile yaani mtu akitetea vilema basi na yeye kashakuwa kilema

Kwa taarifa yako nimeolewa na ndoa yangu ina amani na sina mume mwenye mitazamo ya kijinga kama ya kwenu hiyo ila kamwe sitaacha kuwasemea wanawake wenzangu

Hata mniite majina yote duniani sijui feminist sijui activist na mengine mtaongezea ila huo ndiyo ukweli na nimegundua wanaume kuambiwa ukweli huwa hampendi

Hasa kama huo ukweli unatoka kwa wanawake na badala yake ndo mnabaki mnatoa kauli kama hizo kuwa sijui tunapenda usawa sijui tunataka kushindana yaani hiyo huwa ndiyo defensive mechanism yenu
We huoleki na hupo ndoani...we ni lazima utalilia zamu za kupika na kupiga deki
 
Now we are communicating na ninaowalenga ndiyo hao ambao wake zao wanawasaidia majukumu yao ila wao hawataki kusaidia majukumu ya wake zao na kama wewe kweli upo hivyo kama unavyosema basi HONGERA KUBWA
Kusaidia isiwe deni..maana unavyosound ni kidenideni..lazima pawe na mgawanyo wa majukumu
 
Hapo mfumaniaji ndiye mwenye maamuzi..kwa muislam mungu anamshauri aachane na mwenza akimfuma akifanya uchafu(zinaa,kusagana,kufillana)..
Hata kwa wakristo iko hivyo lakini dunia ya leo mwanaume akimfumania mke wake jamii inamshauri amuache lakini mwanamke akimfunia mume wake jamii inamshauri amvumilie

Kwa kisingizio cha kwamba kila mwanaume anachepuka (kitu ambacho siyo kweli) na hii mitazamo ndo inawapa kichwa sana wanaume na kuwafanya mzidi kuchepuka na kuona kama vile ni jambo la kawaida

Hadi imefikia hatua mmejibadilishia na jina kabisa eti mwanaume anayechepuka haitwi malaya bali anaitwa kidume ila mwanamke anayechepuka ndo malaya ndugu zangu umalaya ni umalaya tu haijalishi unafanywa na jinsia gani

Kwa sababu kwenye maandiko ya dini zote hakuna sehemu Mungu aliyomruhusu mwanaume kuwa malaya amekataza umalaya kwa jinsia zote sasa na hapo napo mtambishia Mungu mtasema ni usawa?
 
Back
Top Bottom