Dawa ya malaria kwa mama mjamzito

Dawa ya malaria kwa mama mjamzito

kunywa tena kesho halafu unapokunywa unywe maji mengi hata glass nzima moja kubwa.
 
Mama mjamzito chini ya miezi mitatu dawa anayotakiwa kupewa ni Quinine na siyo dawa nyingine yeyote, hii ni kwa usalama wa kile kiumbe kilichopo tumboni. Kwa hiyo mama aliyekupa hizo dawa kakosea sana, sijui umeenda hospitali gani wasiojua dawa unayostahili kupewa. Au inawezekana hukuwaambia kwamba wewe ni mjamzito?
 
nimewaeleze kila kitu #chakii

nafikiri CHAKIi apo juu amejaribu kukuelezea vizuri...mimba ya chini ya miezi 3 only drugs of choice ni quinine....baada ya tremister ya kwanza ndo dawa zngine utakazo elekezwa...jitahd uwe una enda RCH(clinic) kwa ushauri zaidi juu ya mtoto kwani uko mtaani wengi wa wafanyakazi wa afya siyo wataalamu unaweza adi pew mseto wa ALU usipo jiangalia...!!!

pia nirudi kwwnye swala la malaria kila sku najitaidi waambia amna mtu anaweza kuwa na malaria chini ya 10-20 lazma iwe kuanzia hapo...ukiona mtu kakwambia una malaria 2,3,5 uyo kakutapeli...jitahdi uende hosptal zenye hadhi kama itashindikana jitahd uwambie wakupme na MRDT japo mda mwngine nacho kinakuwa na complication za antbodys.
 
Mke wangu ana ujauzito wa mwezi mmoja na siku kama saba, siku mbili zilizopita alikuwa analalamika maumivu ya kichwa na uchovu lakini amepima amekuta hana malaria lakini kwa namna alivyojieleza kwa daktari ameelezwa kuwa huenda ana malaria lakini haijaonekana hivyo akashauriwa atumie dawa MSETO

Alizotakiwa kuanza kumeza palepale hospitalini na Amoxilini kwa sababu ya mkojo mchafu. Sasa mke wangu kagoma kuendelea na dozi kwa madai kuwa alishawahi kusoma vijalida mbalimbali vya wataalamu wa afya wakionya juu ya matumizi ya dawa hizo kwa wajawazito kuwa zina uwezo mkubwa wa kudhuru ukuaji wa kiumbe wakati wa ujauzito au kuharibu kabisa ujauzito. Lakini nafahamu pia kuwa malaria ni mbaya sana hasa kwa kina mama wajawazito isipotibiwa ipasavyo mapema.

Tafadhali naombeni ushaurini wenu, dawa hizo kweli zina madhara kama hayo? Na kama ni kweli, itakuwaje wakati kasha anza dozi? Nimejaribu kuwauliza wataalamu wa afya, nao maelezo yao yanatofautiana. Wengine wana sema hazina madhara lakini wengine wanaishia kusema "Mara nyingi wajawazito wa umri huo hawashauriwi sana kutumia MSETO".... Tuko njia panda hasa ukizingatia SP(dawa inayokubalika kitaalamu kwa wajawazito inashauriwa kuanza kutumika kwa wajawazito wenye mimba ya miezi mitatu tu)

Naombeni ushauri wenu tafadhali.

NB. Hospitali aliyoenda ni ya serikali yenye hadhi ya hospitali ya wilaya na iko mjini

Mzizi mkavu, nakutegemea sana mkuu na wengine wote wenye utaalamu wa mambo haya au uzoefu na mambo ya kina mama wajawazito
 
Dawa ya Alu haishauriwi kutumika kipindi cha miezi mitatu ya mwanzo sababu inauwezo wa kupita kwenye placenta ,kipindi cha miezi 3 ya mwazo ndo kipindi cha uumbwaji wa kiumbe hivyo dawa hii ikitumika kipindi hiki itaingilia uumbwaji wa kiumbe hicho
DAWA HII INAWEZA KUTUMIKA KIPINDI HICHO(MIEZI 3 YA MWANZO) PALE AMBAPO FAIDA KWA MAMA ITAKUA KUBWA KULIKO KWA MTOTO
NB:-dawa hii haitumiki kwa mama anayenyonyesha mtoto mwenye uzito chini ya kilo 5
 
Je ni kweli kuna kinga ya malaria kwa mama mjamzito?
Kuna umuhimu wa kumeza SP kwa mama mjamzito hata kama hana malaria?
Je SP zinajumuisha makundi gani ya dawa za malaria?
Hizi SP hazina side effect kwa mama mjamzito? Mfano mama huyu akiwa hajawahi kutumiwa hizo dawa kabla ya ujauzito?
 
Ni mhimu ni kinga dhidi ya malarai mimi kabla sijaanza kuzitumia niliumwa sana malaria nilipoanza SP kila nikipima sina. Mimi sio nurse ila nakumbuka zamani hizo SP zilikuwa dawa za malaria.
Pia zinatakuwa hazina madhara coz mama mjamzito haruhusiwi kutumia dawa bila kushauriwa na doctor so hawawezi toa dawa ambazo ni risk kwa pregnant woman.
 
Mchumba wangu amepewa dawa za malaria akiwa na ujauzito wa miezi mitatu na wiki moja. Je ujauzito utapata matatizo? Ni ujauzito wake wa kwanza.
 
Amepewa dawa aina gani? Miezi mitatu ya kwanza haruhusiwi kumeza dawa aina ya ALU kwa sababu sio safe kwenye ujauzito ila akiwa kweny 2nd na 3rd trimester anaruhusiwa kumeza ALU inakuwa safe pia inakuwa inategemea kama ni complicated Malaria au sio complecated.
 
kama alipewa hospitali basi daktari alilizingatia hilo, labda kama hakuwa na kadi ya mama mjamzito au hata kujieleza tu.
 
Amepewa dawa aina gani? Miezi mitatu ya kwanza haruhusiwi kumeza dawa aina ya ALU kwa sababu sio safe kwenye ujauzito ila akiwa kweny 2nd na 3rd trimester anaruhusiwa kumeza ALU inakuwa safe pia inakuwa inategemea kama ni complicated Malaria au sio complecated.
alikuwa haumwi na amepewa sp
 
ahaaaa! atakuwa ameanza clinic huyo,hivyo amepew za chanjo (vaccine) ya malaria
 
Miezi mitatu anakunywa sp...
Hata Mimi nilikutwa Na malaria wakati nna ujauzito wa wk 12,Na nikapewa sp
 
Back
Top Bottom