Malaria ni maambukizi ya seli nyekundu za damu inayosababishwa na parasiti iitwayo Plasmodiumu. Plasmodiumu hawa husambazwa na mbu aina ya Anofelesi. Mbu hutoa parasiti za malaria katika damu ya mtu aliyeambukizwa anaponyonya damu 'chakula', na kisha kupitisha parasiti anapomwuma mtu mwingine. Parasiti hukua na kukomaa katika seli nyekundu za damu na mamilioni ya parasiti hukusanyika katika plasenta ya mjamzito.
Malaria inaweza kuwa kali zaidi kwa kina mama walio na magonjwa mengine. Malaria ni hatari zaidi kwa wajawazito kuliko watu wengine.
Dalili za malaria
Mama mjamzito anakuwa na dalili kama wagonjwa wengine ambao sio wajawazito. Dalili hizo ni kama vile
Baridi (kuhisi baridi isiyo ya kawaida) na kutetemeka (vipindi vikali vya kutetemeka kwa dakika kadhaa na hudumu hadi saa 1), hii huwa dalili ya kwanza ya maambukizi
Maumivu ya kichwa na udhaifu mara nyingi huandamana na baridi
Joto jingi mwilini (halijoto ya juu); Joto jingi mwilini mara nyingi hufuatwa na baridi, na joto linaweza kwenda juu sana hivyo mtu anakabiliwa na deliriumu (kutokuwa katika hali sawa kiakili, kuona au kusikia mambo yasiyohalisi)
Kutokwa na jasho joto lishukapo
Katika baadhi ya hali zingine kuhara/kutapika kunaweza pia kushuhudiwa
Dalili nyingine ya kawaida ni maumivu ya misuli/viungo.
Hata hivyo magonjwa mengine yanaweza kusababisha dalili kama hizi.
Vipimo vya malaria
Malaria huweza kugundulika kwa kutumia vipimo vya haraka au hadubini
Matibabu ya Malaria kwa Mama mjamzito
Ni muhimu kwa wajawazito kuepukana na malaria - au kutibiwa haraka wakiwa wagonjwa. Dawa za kutibu malaria zinaweza kuwa na madhara, lakini ni afadhali kuliko kupatwa na malaria. Ikiwa mama ana dalili za malaria, anapaswa kutibiwa mara moja.
Wiki 12 za awali za ujauzito
Kwa kina mama wajawazito ambao hawana malaria kali dawa inayotumika kutibu malaria katika kipindi hiki ni Kwinini na Clindamycin au Kwinini pekee iwapo Clindamycin haipatikani. Dawa hizi zikishindwa kutibu Artesunate hutumika katika matibabu kwa muda wa siku saba.
Muhula wa pili na watatu.
Dawa mseto jamii ya Artemisin zinaweza kutumika katika vipindi hivi kutibu malaria ambayo sio kali.
Madhara ya Malaria kwa Mama mjamzito
Mjamzito aliye na malaria yuko katika hali ya kupata anemia, kuharibika kwa mimba (kutoka kwa mimba pekee yake kabla ya wiki 24 za ujauzito), kuzaa mapema, kupata mtoto mdogo zaidi, kuzaa mtoto aliyekufa (mtoto kuzaliwa akiwa amekufa baada ya wiki 24 za ujauzito) au kufa yeye mwenyewe (kifo cha mama).
Kukinga na Malaria
Kukinga malaria inapaswa kuwa wajibu wa mtu binafsi na jamii.Mama mjamzito afanye kila awezalo kuepuka kuumwa na mbu.Hata hivyo matumizi ya vyandarua pamoja na kuangamiza mazalia ya mbu hupunguza kuenea kwa ugonjwa wa Kukinga malaria inapaswa kuwa wajibu wa mtu binafsi na jamii