Dawa ya kuua huyu mdudu

Dawa ya kuua huyu mdudu

Hizo zinaitwa kamera za wachawi kila unachofanya ndani wanaona
Baada ya kuelezewa hivyo na kuambiwa dawa yake nilijaribu dawa niliambiwa kama nikitia hiyo dawa wakiondoka nijue ni wakichawi kweli waliondoka mpaka leo sipendi mijusi

Naishi msela kwa hiyo ndani kwangu walikuwa huru sana
kukaa na kuona wajusi watano wapo maukutani wamerelax ilikuwa ni kawaida sana
Nikiondoka kurudi usiku kwa hivyo walikuwa huru
Dawa niliyotumia niliambiwa nichukue majani ya kisamvu niweke katika pembe za chumba hata mawili mawili kila kona
Alafu nichukue mbegu za kitunguu saumu nizitumie kusugulia sehemu mbalimbali ambapo huwa nawaona
Unatumia zile mbegu kuchorea maeneo wanayokaa
Baada ya kufanya hivyo kesho yake tu sikuona hata mjukuu wao nilishangaa sana
Huenda hivyo vitunguu swaumu ni sumu kwao ndivyo viliwafukuza hao mijusi, hakuna uchawi hapo
 
Mijusi uliyoyaamua kuifuga mwenyewe imeanza kukusumbua .Ikifika hatua ya kukupandia kitandani na kukutambalia wakati upo usingizini utujulishe tukupe dawa
Dogo una roho mbaya si mchezo aisee🤣
 
House Gecko,

wajusi wa ndani...inategemea na imani yako ila kwa wazungu wa Marekani wanaamini hao wajusi wakiingia ndani kwako basi kuna ugeni utakuja kwako, Baraka au Maongezeko flani

Watu wengine wanaamini ni wanaleta mkosi, hasa watu weusi
 
House Gecko,

wajusi wa ndani...inategemea na imani yako ila kwa wazungu wa Marekani wanaamini hao wajusi wakiingia ndani kwako basi kuna ugeni utakuja kwako, Baraka au Maongezeko flani

Watu wengine wanaamini ni wanaleta mkosi, hasa watu weusi
Dah!! Sijui nofanyeje
 
Mi huwa nawaacha tu, naishi nao na wenyewe wananichukulia kama mwenzao hivi 😁😁😁. Ila siku wakijichanganya wakakaa kweye frame ya mlango, wanakula kiminyo
 
Mijusi oyeeeee!! Mijusi oyeeee! Hata kwenye bible imeandikwa kuwa mjusi anaingia hadi kwenye jumba la mfalme. Hawana sumu wala hawatumiwi na wachawi.
 
Hao ni kawaida tu hawana madhara mi kwangu wanapita hata madirishani nawafukuza tu basi lkn siwaui
 
Back
Top Bottom