Dawa ya kuondoa msongamano Dar...

The boss wazo lako sio baya sana ila mimi ninachoona tatizo la foleni ni tatizo la mipango miji ambalo kama utalitazama vizuri basi utaweza kubaini kuwepo kwa mgawanyo mbovu uliopo katika mgawanyo wa huduma za kijamii zilizopo jijini Dsm.Dsm kama ilivyo ina manispaa tatu(3)yaani Ilala,Temeke & Kinondoni na katika Manispaa hizi kiukubwa kwa eneo ni Temeke ikifuatiwa na Kinondoni na mwisho ni Ilala ndio ndogo kieneo kuliko zote.Cha ajabu huduma zote za kibiashara,maofisi ya Serikali,Hospitali kubwa,Soko kubwa la Kariakoo,Wizara nyingi kama si zote,ikulu,Airport, maduka yote makubwa,mahoteli yote makubwa,mahukumbi makubwa yote na nyinginezo nyingi zipo katika Manispaa ya ilala.Kuwepo kwa huduma hizi tu katika eneo moja tena dogo kieneo ukilinganisha na manispaa nyingine hilo ni tatizo kubwa.Nini kifanyike,kwanza ni kuhamisha huduma zote muhimu kubwa katika manispaa ya ilala na kwenda katika manispaa nyingine za kinondoni na temeke,huduma kama vile kuwepo kwa shopping malls kubwa zenye kuchukua maeneo makubwa mf.century city iliyopo cape town,kuwepo kwa masoko ya kariakoo mengine katika manispaa hizi mbili,baadhi ya ofisi za Serikali kubwa zinatakiwa kuhamishwa hapo mjini(uchambuzi ufanyike zipi zihamishwe na zipi zibaki) etc
Pia kuanzishwe huduma ya kutoza kodi kwa magari yanayoingia mjini,hii itapunguza baadhi ya magari kuingia mjini na bila kusahau watu wahimizwe kutumia public transport kama dbrt itakapoanza.huo ni mtizamo wangu
 
Pia huduma nyingi za kijamii zianzishwe pembezoni mwa hzi manispaa mbili ili kupunguza idadi ya watu kuja katikati ya mji bila sababu za msingi
 
The Boss, dawa ya kuondoa foleni ni KUYAONDOA MAGARI barabarani. Hili ni suala la MIUNDOMBINU. Nilikwishamuelimisha Mwakyembe kuhusu solution. Hebu Google "Kuala Lumpur Monorail" kisha nenda kwenye "images" uone jinsi wenzetu walivyofanikiwa. Kwao foleni wanaisikia kwenye vyombo vya habari tu!

kuala-lumpur-monorail.jpg
Mkuu hebu acha masihara Bana...
Hivi kama TRL ilitushinda hii project si tunatafutiana tu lawama?
Mi nadhani solution ya kila kitu nchini ni kuondoa kwanza huu mfumo Ovu wa Uongozi kisha tuanze upya..
Chini ya Uongozi tulionao hamna tunachoweza kufanya kama nchi, Trust me..
 
Mji unakatisha tamaa, na foleni zitazidi kuongezeka ikiwa serikali itaendelea kuwa kama ilivyo sasa. Ujenzi wa Morogoro rd mi nadhani hautasaidia sana kupunguza foleni, itakuwa kama pale feri wakati kilipoletwa kivuko cha MV Magogoni ilionekana kuwa ni mtatuzi wa tatizo lakini hadi sasa tatizo liko pale pale, kilasiku foleni hadi ikulu.

Jambo lingine ni ujenzi wa maofisi;
Kuna minara miwili inajengwa pale mtaa wa Mission na Sokoine drive kila moja lina zaidi ya floor 30 na kwa chini (upande wa pili wa Sokoine drive kuna kitu kinakuja na kinategemewa kuwa na floor 40
Hebu fikiria hii minara miwili kuwa kila floor ina mpangaji mmoja hivyo una wapangaji kama 30x2=60, fanya tu 50 na kila floor kuna wafanyakazi watatu (kwa kiwango cha chini) wenye magari (50x3 =150),
Kila ofisi kuna watu 5 wamekuja kwa wakati mmoja kwa magari kupata huduma (5x30 = 150)

Hivyo magari 150 ya wafanyakazi na 150 ya walokuja kupata huduma =300

Ile Sokoine drive sikuhizi jioni ni balaa kwa foleni majengo yote mawili yakikamilika huenda kwenye hiyo foleni pataongezeka magari mengine kama 300x2 =600

TUENDELEE KUJENGA MAJENGO YA KISASA, MAREFU SANA ILI KUPENDEZESHA MJI NA SIO KUJENGA BARABARA.
ASWANTE!
 
- Eneo la Kariakoo liwe na bidhaa moja tu ya biashara, mfano bidhaa za nguo.

- Maduka ya simu na vifaa vya simu yahamishwe, mfano Pugu.

- Maduka ya vifaa vya ujenzi yote yahamie mfano Tegeta.

- Vipodozi yote yaende mwenge.

- Vifaa vya kilimo Tandika. Posta yoote kusiwe na maduka zaidi ya maofisi na maduka ya nguo tu.
maduka ya furniture yote yaende Keko..

Tukiweza hili misongamano na foleni zitakwisha Dar. Tuige nchi zingine basi, ingawa Madiwani na mameya wote waliopo ni mizigo.
Hili siyo suluhisho 100%, kwa sababu miundo mbinu ya barabara iliyopo Keko,Tandika,Pugu etc bado ni finyu kuweza ku-accomodate pilika za biashara ulizotaja,suluhisho la uhakika ni uwepo wa barabara za kisasa na serikali kufungua maeneo ya biashara mchanganyiko(siyo aina moja kama unavyoshauri) kwenye njia kuu zinazoingia Dar kutokea mikoani,ili wajipatie huduma zote muhimu huko huko pembezoni,
 
- Eneo la Kariakoo liwe na bidhaa moja tu ya biashara, mfano bidhaa za nguo.

- Maduka ya simu na vifaa vya simu yahamishwe, mfano Pugu.

- Maduka ya vifaa vya ujenzi yote yahamie mfano Tegeta.

- Vipodozi yote yaende mwenge.

- Vifaa vya kilimo Tandika. Posta yoote kusiwe na maduka zaidi ya maofisi na maduka ya nguo tu.
maduka ya furniture yote yaende Keko..

Tukiweza hili misongamano na foleni zitakwisha Dar. Tuige nchi zingine basi, ingawa Madiwani na mameya wote waliopo ni mizigo.
Umesahau Bar kubwa kubwa zinahamishiwa wapi?
 
- Eneo la Kariakoo liwe na bidhaa moja tu ya biashara, mfano bidhaa za nguo.

- Maduka ya simu na vifaa vya simu yahamishwe, mfano Pugu.

- Maduka ya vifaa vya ujenzi yote yahamie mfano Tegeta.

- Vipodozi yote yaende mwenge.

- Vifaa vya kilimo Tandika. Posta yoote kusiwe na maduka zaidi ya maofisi na maduka ya nguo tu.
maduka ya furniture yote yaende Keko..

Tukiweza hili misongamano na foleni zitakwisha Dar. Tuige nchi zingine basi, ingawa Madiwani na mameya wote waliopo ni mizigo.

THE BOSS...mawazo yako ni mazuri sana,wasiwasi wangu ni nani wa kuyafanyia kazi haya mawazo yako! na kumbuka mwlm nyerere alikwisha sema kitambo,kwa uongozi huu wa ccm,tanzania ijayo mbele ni giza.....
 
Mawazo haya ni mazuri sana lkn wahusika wanapita huku jamvini kuyasoma?coz viongozi wengi wa kibongo hawashauriki kwakuwa wamejaa dharau na kiburi
 
Hiyo haiwezekani, tena itasababisha usumbufu wa hali ya juu. Mtu anunue vipodozi mwenge, aende kkoo kuchukua nguo. hyo ndo maanake nn? usumbufu. dawa ya msongamano ni kupanua barabara na kuwa na feeder roads.
 
huu utaratibu unaoshauri utasaidia vipi kupunguza foleni ya posta-mwenge-tegeta,posta-ubungo-kimara,posta-chang'ombe-g/mboto,magomeni-kigogo-chang'ombe wakati wa asubuhi na jioni??hawa nao wanaenda kariakoo/posta madukani??au umekusudia kupunguza foleni kariakoo tu.

Jiulize hili
mbona jumamosi wafanyakazi hawaendi makazini
lakini foleni mara mbili zaidi?
jibu very simple
waajiriwa wa serikali jiji hili hata asilimia kumi hawafiki
wengi ni biashara ,na biashara center ni Kariakoo...
ukii fix Kariakoo ume fix jiji hili
 
Kaka;

Wengine tulishapiga kelele hadi tukachoka. Mpaka wakubwa wanaohusika tuliwaona na maoni yetu tuliwapa, lakini "sikio la kufa halisikii dawa". You may get a modern complete solution package kwa kupitia hapa: Traffic congestion - Wikipedia, the free encyclopedia

Mkuu hatupaswi kuchoka
wenye jukumu hili ni madiwani zaidi na Meya
jiji lina mameya 5 now,soon wataongezeza wengine
badala ya kutatua kero hii
 
Dawa ni moja tu serikari wahamie Dodoma Hakika msongamano utakwisha

Mbona Jumamosi watu hawaendi makazini msongamano ndo unazidi?
na siku hizi hadi jumapili?

Na utashi wa wao kuhamia Dodoma hakuna
bora hili ni rahisi kulikazania
 
ndugu wazo si baya, linalenga kutatua, lakini swala nalo liona mimi ni kuhusu mfumo wa nchi una katisha tamaa , siwezi miaka yote ni kauza simu naweza badili biashara sasa serikali itanihamisha na kama ujuavyo itakuwa mbinde na umaskini ndipo utakapoanza, mimi sasa hivi ndani ya miaka 7, nimebadili biashara za aina 5 kazi yangu ni kuangalia fursa iko wapi . nafikiri maofisi ya serikali yahame kwanza yaende dodoma nalo hilo litapunguza msongamano .

Kukiwa na maeneo maalumu hata kibiashara utafanikiwa
ni sawa leo ukifungua duka la spare za magari Mtaa wa Msimbazi
utafanikiwa kirahisi,sababu watu wote Dar wanaanzia hapo wakiwa na shida ya Spare
maduka ya bidhaa moja yakikusanyika pamoja
biashara ni guarantee
 
Hili siyo suluhisho 100%, kwa sababu miundo mbinu ya barabara iliyopo Keko,Tandika,Pugu etc bado ni finyu kuweza ku-accomodate pilika za biashara ulizotaja,suluhisho la uhakika ni uwepo wa barabara za kisasa na serikali kufungua maeneo ya biashara mchanganyiko(siyo aina moja kama unavyoshauri) kwenye njia kuu zinazoingia Dar kutokea mikoani,ili wajipatie huduma zote muhimu huko huko pembezoni,

Nimesema swala la kupanga aina za bidhaa na mji
linatumika nchi nyingi mno za kiiashara
sasa wewe ukisema sio solution sijui unatoa mifano wapi..
hili halina gharama,likiamuliwa ni miezi tu,foleni zinakwisha
hilo lako ni miaka na pesa nyingi linahitajika
 
Hiyo haiwezekani, tena itasababisha usumbufu wa hali ya juu. Mtu anunue vipodozi mwenge, aende kkoo kuchukua nguo. hyo ndo maanake nn? usumbufu. dawa ya msongamano ni kupanua barabara na kuwa na feeder roads.

usumbufu utatoka wapi na foleni itakuwa hakuna
halafu sio lazima ununue vitu vyote siku moja
mbona unaweza leo kwenda hospitali aga khan ukatumia siku nzima
na kesho ndo ukaenda kariakoo kununua vitu?
na ukapitia mlimani city bank?
 
Pia huduma nyingi za kijamii zianzishwe pembezoni mwa hzi manispaa mbili ili kupunguza idadi ya watu kuja katikati ya mji bila sababu za msingi

huduma kama mabenki zinafuata biashara ilipo
so maduka yakihamia Pugu na benki zote zitafungua matawi Pugu
ndo maana Kariakoo kuna matawi mengi mno ya Bank zote...
 
Jiulize hili
mbona jumamosi wafanyakazi hawaendi makazini
lakini foleni mara mbili zaidi?
jibu very simple
waajiriwa wa serikali jiji hili hata asilimia kumi hawafiki
wengi ni biashara ,na biashara center ni Kariakoo...
ukii fix Kariakoo ume fix jiji hili

hio foleni ya jumamosi iko kariakoo tu??sio kweli uki fix kariakoo umefix jiji zima.....
 
Tatizo ni moja atu na liko wazi, hakuna barabara za kutosha na zilizopo ni nyembamba sana. Kwa waliotembelea nchi za jirani wataona jinsi gani wenzetu wanajitahidi kuwekeza katika barabra ambayo ni moja ya msingi wa maendeleo ya kila siku.

Nchi ya TZ haina vision (hakuna hata vision 20200 wala vipaumbele kwahivyo kila anaeingia madarakani anatumia uwezo wake mfinyu wa kufikiria na kujituma kufanya maendeleo hafifu yasisyo natija....kama huyu wa sasa wa bara bara za kasi ambazo kimsingi ni suluhisho la muda mfupi kama sio tatizo la muda mrefu.

Mpaka sasa hakuna 3 lane hata moja, hakuna overpass, hakuna barabara za kutosha....hakuna umeme wa uhakika, hakuna viwanda, hakuna jambo lolote lianloonyesha nia ya dhati ya kusonga mbele kiamendeleo...isipokuwa ku-omba omba kuogopa ushindani wa nchi jirani......Mara nyingine unatamani mjerumani arudi kuisaidia Tanganyika yake kufikiri na kuchukua hatua.....umimi na ulafi usio na mipaka kila walio wengi wako bize kutengeneza kesho yao na kuhakikisha'monarchy' inanendelea.....


Nhi ngumu sana Tanzania....sijui lini itafika...

Mfano wa bara bara za watani wa jadi tunazohitaji na sio speed lane (jokes) za bongo...

Blind_Spot.jpg Blind_Spot2.jpg thika.jpg
 
Jiulize hili
mbona jumamosi wafanyakazi hawaendi makazini
lakini foleni mara mbili zaidi?
jibu very simple
waajiriwa wa serikali jiji hili hata asilimia kumi hawafiki
wengi ni biashara ,na biashara center ni Kariakoo...
ukii fix Kariakoo ume fix jiji hili

jiulize hili
asubuhi kuna foleni tegeta-mwenge-posta,kimara-ubungo-posta,gongolamboto-posta,mnyamala-kino-posta utafix vipi hii kwa kufix kariakoo??hawa wote wanaenda kariakoo???
na jioni kuna foleni posta-mwenge-tegeta,posta-ubungo-kimara,posta-mbagala na hii utafix kwa kufix kariakoo???
 
Back
Top Bottom