Dawa ya CHADEMA yapatikana

Dawa ya CHADEMA yapatikana

Labda 'peponi' Dar, huku kwetu mikoani CCM mnatuona kama misukule
 
Hii ndo hekima na ndo njia sahihi. Hakuna sababu ya kupambana na wapinzani, wala kuwabambikia ugaidi feki. CCM ina sera na ilani ambayo ndio kinga yake. Ukiwaonyesha wananchi uliyotenda, na CCM inayo mengi na ukiwaeleza sera nzuri za CCM watakuunga mkono tu. Mabomu na kutumia polisi havisaidii. Asanteni wazee kwa busara zenu!
 
Ccm hawana cha kuonyesha tofauti na makaburi ya mwangosi, majaburi ya na bomu ya kwenye mkutano wa arusha na risasi za 5/1/2011. mia
 
Huo mradi wakuonyesha mafanikio walishauanza tangu mwaka jana lakini naona ulifeli,

Walijikuta wanaingia gharama kubwa sana kulipia matangazo yao kwenye vyombo vya habari huku wananchi wanazidi kuwakataa,

Tunawasubiri tena karibuni!

Kamanda Yericko umesema ukweli mtupu. Namkumbuka waziri Lukuvi alivyokuwa anaupigia debe huo mpango mkakati wa kuwaonyesha wananchi mafanikio ya serikali yao.
Kila wizaea ililipia na kurusha vipindi katika vituo vyote vya television nchini lakini hakuna chochote cha maana walichokionyesha zaidi ya mipango iliyopo kwenye makaratasi.
 
Wanasema wazee ni hazina ya hekima lakini hili, namhurumia huyo mzee. Au ni mbinu mbadala tena hiyo. Anataka kutuonyesha nini? Kweli hii ni enzi ya Bigi rizalti naooo! Lo! Ataonesha nini jamani? Mashimo ya Bulyanhulu au Mererani kwa Sendeka? Big Results Now yako mzee ni kuwapiga watu nyumbani kwao na kuwatisha na vifaru vyetu watu wasio hata na mshale? Ya leo kali ngoja nikajilalie. Namwambia, Siku hazigandi, kufumba na kufumbua tutasikia ni 2014. Hapo kwa madiwani tu kutamfanya huyo mzee akajifiche ajuako. Labda China kwa ufadhili wenu wa gesi-ntwara. B/up Big Result Now!!! Tumekumbuka shuka nako kumekucha. Laiti siku zingerudi nyuma.
 
alietoa wazo kama hilo kapinda kiupeo
kuna mafanikio yapi ya kuonyesha?
kama ni barabara,mashule nk hizo ni kodi za wananchi na sio CCM
kama alivosema Nape wazee wanasubiri kufa na kweli akili zao zimeanza kufifia
:A S-fire1::A S-fire1::A S-fire1::A S-fire1:😛izza:😛izza:😛izza::A S-fire1::A S-fire1::A S-fire1::frog::frog:
 
Ningemwelewa kama angeshauri waanze kutekeleza ilani na kutatua kero za wananchi, baada ya hapo wananchi tutajionea wenyewe na kuwapa haki yao, hatuhitaji kuonyeshwa maendeleo, chema chajiuza ilihali kibaya chajitembeza.
 
Miaka 50 ya ccm hamjaweza kutekeleza ilani zenu ndo itakuwa hii miwili mliobakiza huyo mzee anajisumbua
 
Dawa ya CHADEMA na wapinzani wengine imepatikana. Mjumbe mmoja wa Baraza la Wazee la CCM Taifa amependekeza kikaoni Dodoma kuwa dawa kuu ya wapinzani ni kuwaonesha wananchi mafanikio ya chama tawala kwa matendo. Mjumbe huyo ambaye alikuwa Makamu wa CCM Tanzania Bara amesema kuwa wapinzani kama CHADEMA hawatakuwa na la kusema ikiwa wananchi wataona mafanikio yaliyoletwa na CCM kwa macho yao wenyewe.

'Hakuna haja ya kutumia nguvu. Kuonesha tu kutatosha. Tukifanya hivi,chama chetu kitaimarika zaidi na kuzoa kura kwenye uchaguzi wowote. Tuachane na propaganda...tuitekeleze Ilani kwa matendo' alisema Mjumbe huyo

Ni matumaini yangu kuwa hata matumizi ya vyombo vya dola kuimarisha chama na kuusumbua upinzani sasa yatapungua au kukoma kabisa. Hakuna haja ya kukamata wala kushtaki wapinzani.CCM yetu yaweza kufanya jambo la kuonesha mafanikio kwa manufaa makubwa.Ni wakati sasa wa kufanya siasa kwa vitendo. Vyombo vya dola(kama alivyowahi kusema Mwenyekiti wa Taifa) havitakisaidia chama chetu cha Mapinduzi

Mzee Tupatupa wa Lumumba,Dar es Salaam

mafanikio yapi??? wizi mtupu, chama kinanuka hata mkikisafisa na jiki hakifai tena,
 
Mafanikio mpaka yaoneshwe. Kama hayo ndio mawazo ya wazee wanaoaminiwa kuwa na busara na washauri, CCM kwisha habari yake.

We wa Sumbawanga hata hapo kwa Aishi hamyaoni mafanikio ya CCM? Tehe....tehe.....sisi huku Mpanda Tunayaona mafaniko ya Said Arf....wala hata hatuhitaji kuoneshwa....yanaonekana yenyewe.....Posuta....!
 
Mnakuwa kama man city bana mpaka dk za mwisho ndio mnazinduka. Imeshakula kwenu hiyo. Mipango mizuri hupagwa ndani ya zaidi mitano ndio upate big results.
 
Mafanikio hayaonyeshwi, bali yanajionyesha yenyewe. Mafanikio sio uchawi, bali ni tunu au nuru uchanua. Watanganyika sio vipofu, ni watu welevu, wenye macho na kufuatilia mambo.
 
Huo mradi wakuonyesha mafanikio walishauanza tangu mwaka jana lakini naona ulifeli,

Walijikuta wanaingia gharama kubwa sana kulipia matangazo yao kwenye vyombo vya habari huku wananchi wanazidi kuwakataa,

Tunawasubiri tena karibuni!

of course walianzisha mradi huo ukashindwa kabla haujafika mbali. Bila shaka wafuatiliaji watakumbuka harakati za kutangaza mafanikio ya CCM kwenye runinga ya Taifa pamoja na safari za Mh. Kinana akiambatana na viongozi waandamizi wa CCM na mawaziri 'nyota'
 
PIA CCM IANGALIE NI JINSI GANI ITAONDOA HAO VIJANA 2 WENYE PROPAGANDA za VIJIWENI UNLESS OTHERWISE NOTHING GONNA HAPPEN THEY DONT HAVE WISEDOM
 
kuonyesha mafanikio ya chama cha mateja aka CCM, Tanzania - ni sawa na kumuonyeha a mutilated victim of war mafanikio ya VITA - how many neurons do you have, stinking bull shit of Lumunba??

I hate you!!
 
Back
Top Bottom