Dates za siku hizi

Dates za siku hizi

Nyani Ngabu

Platinum Member
Joined
May 15, 2006
Posts
97,070
Reaction score
136,458
Jumapili njema raia.

Sasa bana, neno la leo ni kuhusu miadi ya makutano ya watu wawili walio na raghba ya kuja kuweza kuwa wenza hapo baadaye.

Mkaka na mdada wanawasiliana kwenye simu. Wanapanga muda na sehemu ya kukutana ili waweze kujuana vizuri.

Siku ya siku inafika na kila mmoja wao anajiandaa vile awezavyo. Mara nyingine hao wawili huongozana na rafiki zao huko kwenye miadi. Nadhani wadada ndo hupenda zaidi kufanya hivyo, jambo ambalo mimi huliona ni la kishenzi.

Mimi na wewe ndo tumepanga tukutane. Wewe unaleta gurudumu la tatu la nini? Ni ushenzi tu.

Hata hivyo, hiyo si hoja yangu kwa leo. Nilikuwa nachomekea tu kama Anko Magu.

Basi bana...mnafika sehemu ya mkutano wenu...mnasalimiana. Kama ni vinywaji mnaagiza halafu mnaendelea na yenu.

Cha kustaajabisha sasa....unakuta kila mtu ana simu....iwe ki Tecno (sijui ndo inaandikwa hivyo), Samsung kuukuu, au ki iPhone cha ajabu ajabu ambacho pengineo ni cha bandia.

Baada ya maongezi kidogo unastukia kila mtu kajiinamia na kibyongo chake. Kila mtu kama si anachati kwenye magrupu ya Whatsapp basi yuko sijui Instagram huko au Snapchat.

Unakuta mtu yuko kwenye rundo la magrupu. Hapo alipo kwenye kideti chake lakini huko kwenye magrupu anatongozana na wengine.

Au unakuta mwingine yupo kwenye hicho kideti lakini yupo kwenye magrupu huko anagombana na wenzake.

Ambacho sikielewi sasa...kwa nini watu muende kwenye miadi yenu halafu badala ya kuongea na kujuana vizuri mnaishia kuchati kwenye magrupu ya Whatsapp?
 
Bora kuchat utamwaambie aache ili muongee mbaya ni pale anapokujia na kundi la wanawake ka wamekuja kukusuta. Enyi wadada mnawanyima wanaume kuwapa yaliyo moyoni nenda mwenyewe umpe uhuru wa kukufunulia yaliyomo mwoyoni mwake.Mkiwa wengi hawezi.
 
Huo ni ujuha kweli, mtu labda hamjaonana Muda halafu mmefunga safari kuitafuta sehemu nzuri ya maongezi, baada ya kufika mtu kajiinamia kwenye kuchati
 
Huu ni uraibu unaokua taratibu na unazidi kuwa kilevi kikali kuliko sembe,tutafika mahali tutafungua vituo vya kusaidia kuondokana na uraibu wa matumizi ya cm.
Kuna siku nilivunja kidate kwa ajili ya upuuzi huu,nimefika eneo la appointment nikasubiri akaja na kisindikizo pembeni tukaagiza vinywaji na kila nikijaribu tuongee nakuta wako deeply wanachart nikaona isiwe tabu nikawaaga.
 
Huu ni uraibu unaokua taratibu na unazidi kuwa kilevi kikali kuliko sembe,tutafika mahali tutafungua vituo vya kusaidia kuondokana na uraibu wa matumizi ya cm.
Kuna siku nilivunja kidate kwa ajili ya upuuzi huu,nimefika eneo la appointment nikasubiri akaja na kisindikizo pembeni tukaagiza vinywaji na kila nikijaribu tuongee nakuta wako deeply wanachart nikaona isiwe tabu nikawaaga.

Hahahaa pole sana.

Halafu unadhani hata walikuwa wanachati ya maana basi?

Usikute ulikuwa umbea tu.
 
Jumapili njema raia.

Sasa bana, neno la leo ni kuhusu miadi ya makutano ya watu wawili walio na raghba ya kuja kuweza kuwa wenza hapo baadaye.

Mkaka na mdada wanawasiliana kwenye simu. Wanapanga muda na sehemu ya kukutana ili waweze kujuana vizuri.

Siku ya siku inafika na kila mmoja wao anajiandaa vile awezavyo. Mara nyingine hao wawili huongozana na rafiki zao huko kwenye miadi. Nadhani wadada ndo hupenda zaidi kufanya hivyo, jambo ambalo mimi huliona ni la kishenzi.

Mimi na wewe ndo tumepanga tukutane. Wewe unaleta gurudumu la tatu la nini? Ni ushenzi tu.

Hata hivyo, hiyo si hoja yangu kwa leo. Nilikuwa nachomekea tu kama Anko Magu.

Basi bana...mnafika sehemu ya mkutano wenu...mnasalimiana. Kama ni vinywaji mnaagiza halafu mnaendelea na yenu.

Cha kustaajabisha sasa....unakuta kila mtu ana simu....iwe ki Tecno (sijui ndo inaandikwa hivyo), Samsung kuukuu, au ki iPhone cha ajabu ajabu ambacho pengineo ni cha bandia.

Baada ya maongezi kidogo unastukia kila mtu kajiinamia na kibyongo chake. Kila mtu kama si anachati kwenye magrupu ya Whatsapp basi yuko sijui Instagram huko au Snapchat.

Unakuta mtu yuko kwenye rundo la magrupu. Hapo alipo kwenye kideti chake lakini huko kwenye magrupu anatongozana na wengine.

Au unakuta mwingine yupo kwenye hicho kideti lakini yupo kwenye magrupu huko anagombana na wenzake.

Ambacho sikielewi sasa...kwa nini watu muende kwenye miadi yenu halafu badala ya kuongea na kujuana vizuri mnaishia kuchati kwenye magrupu ya Whatsapp?
Ki. iPhone ? Au ulitaka kusema iPhone 4
 
Kwani bar ndo sehemu za kujuana jamani????

Nyani Ngabu nafikiri neno "DATE" unalitumia vibaya.

Ili watu wafahamiane vizuri na kujuana lazima watembeleane kwenye makazi yao na cyo bar au pub.

Bar ni sehemu ya drinks tu.
 
Kwani bar ndo sehemu za kujuana jamani????

Nyani Ngabu nafikiri neno "DATE" unalitumia vibaya.

Ili watu wafahamiane vizuri na kujuana lazima watembeleane kwenye makazi yao na cyo bar au pub.

Bar ni sehemu ya drinks tu.

Kuna sehemu nimetaja bar mimi?

Na mtu ambaye unakutana naye kwa mara ya kwanza au ambaye humjui vizuri utaruhusu aje unapoishi?

Where dey do dat at?
 
Mimi nipoteze muda wangu nije tuonane alafu ushike simu. WTF? HELL TO THE NO. HAO WANAOFANYA HIVYO NI WAKO KTK FASTRUATION. EXPECTATIONS ZAO ZILIKUWA TOFAUTI
 
Kuna mdada nlikuwa na ahadi nae tumeenda sehem aliyopendekeza nakuta kuna shoga yake kumbe alikuwa kafika tayari...vidada hivi vya kimjini vina mambo sana
 
Hapa mtaani kwangu kuna kona hairuhusu utumiaji wa cmu, tab na mazagazaga mengine kwa muda wote utakao kuwa ndani ya kona hiyo. .... Ni kona pouwa kwa kwenda kwenye kidate.....
 
Hili limekuwa swala sugu sana, labda ndo tunachipukia kwenye matumizi ya simu.

Siku hizi unaweza kukuta mmetoka na washkaji kwenda kubadili mawazo huku mnapata drinks, sasa katika hali ya kushangza unakuta kila mtu yuko bize na simu na story zinakata kabisa.

Mimi kiukweli huwa sikai nalo rohoni nawaeleza tu au naaga zangu.
 
Hapa mtaani kwangu kuna kona hairuhusu utumiaji wa cmu, tab na mazagazaga mengine kwa muda wote utakao kuwa ndani ya kona hiyo. .... Ni kona pouwa kwa kwenda kwenye kidate.....

Huku kwetu wanataka kupiga marufuku kutembea kwa miguu huku una text kwenye simu.

Kuendesha na ku text tayari ni kosa.
 
Back
Top Bottom