Darasa: Chakula cha akili (Mental food)

Darasa: Chakula cha akili (Mental food)

Mwl ulisema weekend hii tutapata somo jipya na weekend sio mda inakwisha naomba ufafanuz wako kwenye hili

brain is like parachute it work when u open
 
Mwl ulisema weekend hii tutapata somo jipya na weekend sio mda inakwisha naomba ufafanuz wako kwenye hili

brain is like parachute it work when u open
Ni kweli mwalimu alitarajia kufanya hivyo, lakini aliamua kuandaa somo lingine upya kutokana na michango ya wanadarasa alipowauliza kuwa wangependa nini azungumzie kabla ya kuufunga utangulizi. Lakini pia mwalimu ametingwa kidogo kwa ajili ya kuandaa masomo ya upande wa pili, "patience is bitter but its fruits is sweet" likikamilika atalitoa.

Lakini hicho siyo cha muhimu sana, cha muhimu ni hiki;

"Most people think they are going to read book ONE time and change. But the problem is that the subconscious mind does not work that way. There are so many things competing for the attention of your subconscious mind.
Its when you read it OVER and OVER that it manages to cut through the noise and your subconscious realizes".

This is important.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ni kweli mwalimu alitarajia kufanya hivyo, lakini aliamua kuandaa somo lingine upya kutokana na michango ya wanadarasa alipowauliza kuwa wangependa nini azungumzie kabla ya kuufunga utangulizi. Lakini pia mwalimu ametingwa kidogo kwa ajili ya kuandaa masomo ya upande wa pili, "patience is bitter but its fruits is sweet" likikamilika atalitoa.

Lakini hicho siyo cha muhimu sana, cha muhimu ni hiki;

"Most people think they are going to read book ONE time and change. But the problem is that the subconscious mind does not work that way. There are so many things competing for the attention of your subconscious mind.
Its when you read it OVER and OVER that it manages to cut through the noise and your subconscious realizes".

This is important.

Sent using Jamii Forums mobile app
Nimekuelewa sana!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ni jumatatu nyingine tena hii, amani kwenu wanadarasa popote mlipo, wengine mkiendelea kuwepo na wengine kuishi na wale wengine ambao mko hai.

Leo mwalimu amekuja na suala jipya kidogo. Umsikilize kwa makini, tayari mpaka sasa ameweka masomo mawili yenye jumla ya sehemu 12 (twelve sub-lessons). Kwa yule anaesoma kwa kuzingatia na si kutaka kuwahi kumaliza amejifunza mengi na anaendelea kujifunza tena na tena kwa kuyarudia kusoma. Kama mwalimu alivyosema huo ni utangulizi tu na bado somo moja la tatu lenye sehemu nne (four sub-lessons) ili kukamilisha sehemu ya utangulizi na sehemu hizo tayari mwalimu ameshamaliza kuziandaa. Alikuwa anafwatilia utaratibu wa kutoa nakala (hardcopy) utakaokuwa na huo utangulizi ukiwa umekamilika ukiwa na masomo yote na baadhi ya sehemu (sub-lessons) za somo la kwanza na la pili zikiwa zimehaririwa (edit).

Mwalimu alisema hataendelea kutoa mtiririko wa masomo unaofwatana hapa kama alivyotoa baadhi ya sehemu kadhaa za masomo yaliyopita. Ni pamoja na huo mwendelezo wa masomo ya utangulizi yaliyobaki hautaonekana hapa, lakini kuanzia kesho mwalimu ataanza kuutoa huo mwendelezo kwenye group na bado una nafasi ya kujiunga. Hapa darasani atakuja kurudi akikamilisha somo lolote litakalogusa nyanja yoyote atakayoanza nayo lakini Mwalimu yupo hapa kujibu maswali yoyote kuhusu masomo aliyoyatoa na kutoa ufafanuzi wowote atakapohitajika.

Tukiacha yote hayo kubwa ni hili Mwalimu anahitaji wanadarasa baadhi watakaokuwa wawakilishi katika sehemu mbalimbali hapa nchini kwa ajili ya kusambaza nakala za Mwalimu. Mwalimu anahitaji kila mkoa watu watatu na ni vzuri wawe wilaya tofauti.

Sifa za hao mabalozi (hapa ndo kasheshe mwalimu sijui aweke ada kabisa ya kumsajili huyo balozi maana huyu binadamu).
1. Uwe mwaminifu.
Mwalimu anaposema mwaminifu anamaanisha, balozi usiye na tamaa ya pesa ambae utakuwa mwaminifu kuisambaza hiyo nakala bila kuzidisha kiasi atakachopanga Mwalimu.
•Iko hivi kutaka kuibadilisha jamii tuliyonayo, tufanyike msaada kwa ajili ya matunda ya vizazi vijavyo yatupasa kujitolea na ndio maana Mwalimu ameamua kutoa masomo haya BURE (free of charge) hamna hela itakayofikia thamani ya maarifa (knowledge) ambayo Mwalimu anaitoa hivyo hata nakala zake zitauzwa gharama iliyotumika kuiandaa nakala hiyo.
•usije ukaniambia Mwalimu kitu nilichokiona kwenye ubongo wangu ni kusambaza nakala zako hahaha mwalimu hataki kusikia kitu hicho.
•mwalimu umri umeenda hawezi kuzunguka Tanzania yote hivyo anataka uwe balozi hapo ulipo kikubwa maarifa haya yawafikie wengi hata wale walio ndani vijijini.
Hiyo ni sifa kubwa ya balozi zingine mwalimu atazipata atakapomfanyia usahili.

Hivyo tumia namba ya mwalimu ili kupata utaratibu wote.

Kesho tutaendelea na mwendelezo lakini upande wa pili lakini nitakuwepo hapa kutoa ufafanuzi juu ya masomo yote yaliyopita na maswali mengine.

<H.Faraday> 《0625934471》.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mwalimu. Sikitiko langu kubwa ni kwamba, utapokuwa unaendelea na masomo katika group la whatsap mimi sitaweza kuhudhuria.

Kumbuka mimi ni mfwatiliaji no.1 na kifaa ninachotumia ni NOKIA 2700 CLASSIC.

Moyo wangu unalia kwa kuwa nitakosa mengi saana.
 
Habari zenu wanadarasa! Kesho mwalimu atatuletea chakula hapa kaa mkao wa kula.

Sent using Jamii Forums mobile app

Nakala za masomo haya ya mwalimu pia zinapatikana, tumia namba yake kuwasiliana nae popote ulipo.
 
LESSON; MAPINDUZI YA MISINGI NA MIFUMO.

Ni siku nyingine tena tunapoianza weekend yetu, mwalimu aliahidi kuwa ataendelea kutoa baadhi ya masomo na ndivyo ambavyo anaenda kukuletea somo mujarabu kabisa lenye kichwa tajwa hapo juu.

Kupata mfululizo wa masomo haya unakaribishwa tena kujiunga kwenye group letu la WhatsApp masomo na mijadala kuhusu elimu hii vinaendelea kutolewa. Lakini pia nakala za masomo haya zinatolewa hivyo ukihitaji popote ulipo Tanzania hii wasiliana na mwalimu kupitia namba yake hiyo chini mwisho wa somo.


Twende moja kwa moja tukalianze somo letu hili la leo, umakini na utulivu unahitajika lakini pia ukweli ni mchungu jitahidi tu uuelewe ndio sifa ya dawa ilivyo “"The art of medicine consists in amusing the patient while nature cures the disease." -By Voltaire.

Katika masomo yaliyopita mwalimu aliweza kugusia msingi kawaida, kuwa watu wengi wamejengwa katika huo wakiamini katika kufanya kile tu kilichozoeleka kufanywa katika jamii. Mwalimu alisema wengi wao hufanya hivyo kwasababu ya kujitengenezea ulinzi kuwa hata akifeli hataonekana yeye wa kwanza kufeli, au akikwama mahali atakimbilia kuuliza wafanyaji wengine wa hicho kitu na si kutaka akili yake ipambane yenyewe katika kutatua hilo. Mwalimu akasema kinatengenezeka kitu kinachoitwa utumwa wa kifikra kwamba unaona jambo fulani haliwezekani pasipo mawazo/fikra za mtu fulani. Hapa huchagizwa sana na kitu kinachoitwa kujiamini (self confidence), kulipata somo hili la self confidence wasiliana na mwalimu. Mwalimu alikuja kumalizia kuwa kinachobaki ni kusubiri kwanza superior afanye ndipo nasisi tuige. Na mengine mengi ambayo mwalimu ameweza kuzungumzia katika masomo yaliyopita kama mizizi, shina na matawi, kama umesahau jikumbushe masomo yaliyopita.

Leo twende tukaangalie misingi mingine ambayo hupaswi mwanadarasa kwenda nayo, msingi wa pili msingi maumivu uwe makini hapa, watu wengi wanakosa tafsiri na maana sahihi ya vitu wanavyovisikia na kufanyika, matokeo yake watu huteseka huku wakifurahia utofauti wa mateso yao. Utulize akili kwelikweli hapa kuna kazi kubwa mpaka kufikia ngazi ya superior. Baada ya waafrika ama watanzania kuupata uhuru wa bendera kwamba tujitawale wenyewe kuna utumwa tulioachiwa ambao huo kuuona ni ngumu kwasababu tumeweka kuwa msingi wa maisha na kuonekana ndo uhalisia wa namna ya kuyafikia mafanikio.

Wanadarasa walio wengi wamekuwa watumwa wa shughuli wanazozifanya kila siku shughuli za kuwaingizia kipato na kuwafikisha kwenye mafanikio. Kuna baadhi ya kauli na misemo iliyozoeleka kabisa katika jamii, mojawapo ikiwa ni ili uweze kufanikiwa ni lazima uumie (upate maumivu) ama uteseke, msemo wa pili ili uweze kufanikiwa lazima uvuje jasho haswa “hahaha” ngoja tu mwalimu acheke kidogo maana kitu kinachoenda kufanyika hapo watu wanaenda kuumiza ama kutesa mwili maskini ya Mungu na si kuumiza akili. Watu wanaenda kuvuja jasho la mwili mpaka likikauka ngozi inabaki na chumvi “hahaha” na si kuvuja jasho la akili. Usichanganye maneno kuna mazoezi na kazi

Ukiachilia mbali vitu vinavyofanywa na kazi vinavyohusisha nguvu ya mwili, kwa mfano mtu anaweza kuwa mchezaji na vitu vingine ambavyo hata akienda kwa daktari hatashauriwa kufanya mazoezi kwasababu mazoezi ndiyo namna ya ufanyaji kazi wake. Lakini kuna kazi ambazo huyu daktari kabla hajafahamu ufanyaji wako atakuagiza ufanye mazoezi kwasababu hiyo kazi si ya kutumia nguvu, lakini cha ajabu wewe ndio kazi ambayo jasho linakauka na kuacha chumvi juu ya ngozi. Mpaka leo kazi zinazopaswa kufanywa na mashine bado zinafanywa na nguvu ya mwili, lakini cha ajabu kabisa hata kazi ambazo zinatakiwa kufanywa na wanyama nazo zinafanywa na nguvu ya mwili wa binadamu, kazi anayopaswa kufanya punda cha ajabu inafanywa na wewe mwanadarasa “hatari sana hii” Mungu wanaemwamini hawa wanadarasa awasaidie kuweza kuielewa hii elimu.

Mwalimu anakupa homework kidogo nenda kafanye utafiti (research) kati ya wale wanaotumia nguvu nyingi ya mwili na yule anaetumia nguvu nyingi ya akili katika kutekeleza shughuli yake yupi anamafanikio. Mungu kaumba uwezo mkubwa ndani yako mwanadarasa wa kuweza kuvitawala viumbe vingine tofauti na wewe, lakini cha ajabu hauvitumii hivyo viumbe na vimekuwa kwenye level moja ya maisha na wewe. Katika ufanyaji wa shughuli mbali mbali akili na nguvu ni lazima vitumike lakini kwa uwiano gani? Mtu atakwambia mwalimu najua ili niweze kulima na kufanikiwa nisitumie tena jembe la mkono, mwalimu najua ili niweze kufanya kwa uharaka na ufanisi inanipasa nitumie msumeno wa mashine wa kuchania mbao na si kuchana kwa msumeno wa mkono, lakini tatizo mwalimu ni kwamba sina uwezo wa kuwa na hizo mashine. Sasa tunafikaje kote huku!

Moja ya kitu ambacho kila mwanadarasa anakijua basi ni suala la muda, mwanadarasa anaamini kwamba ili uweze kufanikiwa ni lazima ujali muda, ni kweli lakini huyuhuyu mwanadarasa ukimuuliza ni jinsi gani unavyopoteza muda hawezi kukuelezea. Kupoteza muda namba moja hapa duniani ni kufanya kitu ambacho unaijua picha ya mwisho wake kuwa hutofikia mafanikio ya kutosha lakini unajipa moyo na kauli za kijinga kabisa kwamba lolote linaweza kutokea mbele ya safari. Utaanzaje kilimo kwa namna ambayo mwenyewe ukiangalia unaona hata ufanye kwa miaka mitano mfululizo bado hautafanikiwa? Utaanzaje kazi ambayo unaona hata ukiifanya kwa miaka sita bado utakuwa unahangaikia tu tumbo lako? Huku ndo kupoteza muda.

Sehemu kubwa ya wanadarasa wengi wanapokosea ni mwanzo, mwanzo wa ufanyaji wa kila shughuli wengi wao hawaanzii mwanzo kwanini, kwasababu hawaujui mwanzo na kwanini hawaujui huo mwanzo sababu kuu ni hii hapa;

Wanadarasa wengi wamefumbwa hapa, leo mwalimu anaenda kukufungua, wengi wa watu kabla ya kufanya shughuli yoyote ile iwe biashara ama kilimo au kitu chochote, kitu cha kwanza anachoumiza kichwa ni kupata mtaji, kosa moja kubwa sana kumbe kitu cha kwanza ambacho ulitakiwa uumize kichwa kuwa utakipataje ni maarifa (knowledge) inayoihusu kitu hicho. Tofauti yako na superior ni kwamba wewe unawaza kwanza upate mtaji ndipo uanze kuuliza kuwa kitu fulani kinafanyikaje ndio maana kundi kubwa la watu hujikuta wanafeli. Ni kawaida mtu kusikia anaomba msaada wa fedha ili aweze kufungua genge lakini mwalimu na utu uzima huu hajawahi kusikia mtu akiomba msaada aweze kupata fedha ya kumuwezesha kupata maarifa ya biashara ya genge, sikiliza vizuri mwanadarasa hakuna kitu kinachofanyika bila ya kuhitaji maarifa juu ya ufanyaji wa hicho kitu hata kama kinaonekana ni kidogo kiasi gani.

Kwanini wanaoupa mtaji kipao mbele na si maarifa ya kutosha kwanza wanafeli ni kwasababu, moja hulka ya milango ya fahamu kivipi ni kwamba mwili wa binadamu umeumbwa na matamanio (desire) haya matamanio huzaa tamaa, mtu akishapata mtaji tamaa yake kubwa nikuona kashaanza kufanya hiyo shughuli, kuna kitu kimoja anachokimbizana nacho ambacho ni hofu (fear). Anahisi huo mtaji ataweza utumia kwa kitu kingine ambqcho ni tofauti na hicho anachokipanga hivyo hana budi kuanza kufanya haraka iwezekanavyo.

Sifa ya yule anaeanza na maarifa kwanza hatahitaji mtaji mkubwa kwasababu hata akipata shilingi mia tano anajua sehemu yake husika ya kuipeleka. Na hata akianza na kiasi kidogo sana ana malengo ya kufika kwenye umilionea kwasababu anaijua njia anayopita. Kwanini watu ni ngumu kuanza na kutafuta maarifa kwanza, sababu ya kwanza ni kushindwa kujiamini. Wanaofanikiwa siku zote huanzia kwenye hamna kwenda kwenye kuwanacho (from nothing to something). Picha iliyojengeka kwetu sisi wanadarasa hatuamini katika nothing. Hivyo kutafuta maarifa kwa kitu ambacho haujui hata mtaji utatoka wapi ni kumletea masihara huyu mwanadarasa.

Kwasababu hiyo utamkuta mwanadarasa anakifanya kitu kwa njia ile ile zaidi ya miaka 10. Inakuwaje unajisifu mbele za watu kabisa kuwa mimi nimekuwa muunga pancha za baiskeli kwa mwaka wa nne huu. Lakini kwanini hali iko hivyo ni kwasababu watu wamejengwa hivyo, hawajajengwa katika mfumo wa maarifa kwanza.asilimia 70% ya wanadarasa wanafanya vitu ambavyo hawana uelewa navyo wa kutosha.

Maarifa mengi yamejaa kwenye nakala mbalimbali lakini kutokana na desturi tuliyojiwekea ya kutoyatafuta, hizo nakala huwa tunazifungia maandazi. Acha ujinga wa kutotaka kuuacha ujinga jifunze kutoa gharama kwa ajili ya kupata maarifa. Kitu ambacho ulitakiwa kukiandalia gharama ya kutosha ni elimu juu ya vitu mbalimbali na sio kuweza kugharamikia ili uweze kujua ugomvi wa jirani yako, kuna watu wawili kuna atakaeweka vocha ili apige kujua misha ya jirani yake na huku mwingine akiweka bundle aweze kuingia mtandaoni asome kupata maarifa.

Hivyo tafuta kuwa na mwanzo sahihi wa kitu chochote unachopanga kukifanya na huo mwanzo ni ngumu kuujua isipokuwa umetafuta maarifa ya kutosha kukihusu hicho kitu. Usianze kufanya kitu ili mradi, kijue kwanza ndo ukifanye. Jitoe gharama kwa ajili ya kutafuta maarifa na maarifa yote yanapatikana kwenye maandishi. Una macho ya kuweza kuona yatumie ipasavyo yasiishie kuona vitu vya kijinga ama kukesha kusoma vitu vya kijinga ambavyo hata mwanao au mjukuu wako akikuuliza nini unasoma utashindwa kumjibu. Soma kitu kitakachokufanya uweze kujua yale ambayo huyajui lakini ukayajua utakuwa faida kwa watoto wajukuu na vitukuu vyako pia.

Ukianza kufanya kitu cha kufanywa na mashine kwa kufanya kwa mkono baada ya miezi kadhaa hakikisha unafanya kwa kile inachostahili kufanywa nacho.

Principal ni moja tu “to know a lot, read a lot”.

Masomo haya yanaendelea mtafute mwalimu kupata mwendelezo wake na kupata nakala za masomo haya.


<H.FARADAY> (0625934471).
 
Back
Top Bottom