Darasa: Chakula cha akili (Mental food)

Darasa: Chakula cha akili (Mental food)

Mwalimu nilikua na swali

Kwa hyo imani ya upili inapata mafunzo kutoka kwenye dini zote mbili yaan dini ya awali na dini ya upili?

Lakini kwa kusoma hapo nimebaini mfumo wa ndani ambao unajikita kwenye dini na imani (kwa maana ya imani zote mbili ya awali na ya upili)una kusudi la kuandaa mfumo wa nje mi niuite mfumo wa mazoea kujiandaa kwa chochote kitakachotokea iwe ni kibaya hama kizuri

Kwa nini kwa sababu mfumo wa mazoea hauwezi kubadilika kwa haraka kwa kuwa ulishazoeleka hivyo utachukua muda mrefu kufanyia assessment mfumo wa ndani kuzoeleka kwa sababu ya jambo moja kutokuipa kipaumbele japo sijafahamu kiundani nini hasa kilichomo ndani zaidi ukiachilia mbali vitu vilivyoweza kuunda mfumo wa ndani ambao ni dini na imani ya upili

Swali langu mwalimu hapa mwalimu ni kwamba mifumo hii yote ya ndani na nje inamjengaje mwanadarasa kutambua nafasi aliyonayo na kutengeneza strategies za kujikomboa yeye na kizazi chake

Sent using Jamii Forums mobile app
Naomba nijibu kama ifuatavyo, umeambatanisha maswali mawili, swali la kwanza nanukuu aya yako ya kwanza "kwahiyo imani ya upili inapata mafunzo kutoka kwenye dini zote mbili yaan dini ya awali na dini ya upili" jibu ni hapana imani ya upili inajengwa kwa kujifunza lakini masomo yake yanatolewa na nguvu ya ubongo kwa kutumia akili. Rejea aya ya 10 katika somo.

Swali la pili ambalo umeuliza katika aya yako ya mwisho ni kuhusu "application" ya somo lakini hususani mfumo wa ndani. Jibu la hapo lipo utaliona part B ya somo letu kwasababu somo linaendelea hapo lipo mwanzo kuuhusu mfumo wa ndani.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kweli Chakula cha akili... Nimesoma kwa mara ya kwanza nikatoka Kapa nikaona ngoja nirudie tena.. Hapo ndipo ubongo wangu ukufunguka sasa na nikaelewa kwa kiasi Kwani natakiwa kurudia tena na tena. Kwa ufupi mwal nimeelewa kama ifuatavyo:
1. Baada tu ya kuzaliwa binadamu anakuwa na imani ya awali ambayo inahusu uumbaji au inayohusu Mungu wake kutokana na anavyoamini yy..ambayo imani hii hasa hujengwa juu ya misingi ya dini ya upili ambayo ni ukristo, budha, uislamu, na dini nyingine zaidi ya 2000 zilizopo.
2. Baada ya kuwa na imani ya awali huyu binadamu anakuwa na imani ya upili ambayo misingi yake ipo Kwenye dini ya awali ambayo hutokana na kutumika kwa ubongo na mafundisho yake hasa hujengwa Kwenye saikolojia na filosofia.
3. Imani Zote hizi mbili zinamajukumu tofauti... Imani ya awali ni Kwa ajili ya kumtambua muumba wako. Imani ya upili ni kwa ajili ya kujitambua ww mwenyewe jinsi ulivyo au ulivyoumbwa.
4. Imani Zote mbili hukaa ndani na zinamatokeo yake katika maisha yako ya nje kama mwanadamu.
5. Imani Zote hizi mbili yaani ya awali na upili tunao Uwezo wa kuzi "control" na zikatupa matokeo chanya katika ulimwengu wa nje.
6. Imani hizi ndo chanzo pia cha mifumo tuliyonayo katika ulimwengu wa nje.
7. Tukiweza Ku "control " hizi imani hata mifumo ya nje pia tunaweza kuu "control ".
Ni hayo tu kwanza mwal wangu.. Bado naendelea kulipitia somo Ingawaje linahitaji akili itulie kweli kweli... Ila sasa naanza kupata mwanga ni Wapi tunakoelekea... Ila pia Kama Kuna makosa sehemu kwa namna nilivyoelewa Naomba unirekebishe mwal. Nitakie Usiku mwema na Jumatano njema maana naona imeshaanza siku mpya... Ingawaje huu mfumo nao Huwa siuelewagi hata kidogo....

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Neno la leo.

"Aliyekufanya uishi ndiye aliyekupa utashi, kakupa utashi ili uweze kuishi kumbe wewe na utashi mna thamani sawa, lakini kinachotakiwa kuanza ni utashi ili uweze kuishi, lakini ukitangulia kuanza wewe badala ya utashi hautaishi bali UTAKUWEPO. Utashi ni MAARIFA"

BY H.FARADAY.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
LESSON THREE~sehemu ya kwanza
KUJIAMINI (self confidence).

Amani iwe nawe mwanadarasa popote ulipo, mwalimu anaamini u mzima wa Afya ya mwili na unaendelea kuwepo ama kuishi chini ya jua hili. Kabla hatujafunga masomo yetu ya utangulizi na kuanza kuzichambua nyanja mbalimbali twende tukajifunze kitu muhimu kabisa kukijua ambacho ni kujiamini ama ujasiri binafsi. Hili suala linagusa kila nyanja iwe ni Elimu, biashara, kilimo ama uchumi na nyanja mbalimbali, hapa tutaenda kuangalia kwa ujumla (in general). Tutakuja kuongelea tena kwenye kila nyanja tutakayoichambua. Mwalimu anakwambia bado haujachelewa kutuma namba yako ili akuongeze kwenye list kwa ajili ya masomo yanayokwenda kuchambua nyanja mbalimbali yatakayokuwa yanaendelea huko whatsapp.

Twende tulianze somo letu, moja ya sababu kubwa ya watu kuwa hivyo walivyo ni kukosa/kushindwa kujiamini, tungelikuwa bado tupo kwenye kipindi kama cha karne zilizopita lisingeonekana umuhimu sana, lakini kwa karne tuliyopo sasa iliyojaa USHINDANI ni muhimu sana tena sana kulifahamu hili. Tunapozungumzia kujiamini tunamaanisha nini, tumaanisha hivi uthaminishaji chanya juu yako mwenyewe katika kuweza kufanya jambo fulani (your positive self-assessment in performing a task). Kwa lugha rahisi ni kuamini katika uwezo wako binafsi (to believe in your own abilities).

Sote tunajua kuwa vitu vyovyote vipya vinagunduliwa na binadamu na si paka wala mjusi bali binadamu, na huo ugunduzi huanza na binadamu mmoja (a single person). Kabla ya kutekeleza ugunduzi huo aliwaza kwanza kama tulivyosema kwenye masomo yaliyopita kuwa kila kitu huanzia ndani (kama wazo) ndipo huja kujidhihirisha kwa nje (kama kitendo). Baada ya kupata wazo kilichofwata kwa mtu huyo ni kujiuliza je nitaweza/staweza kufanya? Na nitafanikisha? Hapa hakuwa na jibu alijiambia kuwa nitapata jibu baada ya kufanya, kitendo cha kuchukua hatua ya kufanya hujificha chini ya neno kujiamini.

Kuchukua hatua ya kufanya ndiko tunakoita kujiamini, unaamini katika uwezo wako kwamba unaweza kufanya bila kujalisha matokeo yatakuwaje, uwe makini hapa, hamna njia yoyote ya kujua/kuhakikisha kama unaweza au hauwezi jambo fulani pasipo KUFANYA. Kuna msemo wa kawaida kabisa wenzetu wanasema “when you start the journey of your professional life, have confidence in your abilities. Because you have not proven your abilities yet.” < unapoianza safari ya utashi katika maisha yako, jiamini au kuwa jasiri katika uwezo wako kwasababu haujauhakikisha (not proven) uwezo wako bado.

Mwalimu anakwambia tuliza akili uweze kupaelewa hapa, moja ya kosa kubwa ambalo wanadarasa wanalifanya ni kushindwa kutofautisha au kushindwa kufuata hatua za msingi kuanzia ndani (kwenye kufikiri) mpaka nje (kwenye vitendo). Kushindwa ama kukosa kujiamini kunakuja baada ya kukosa mpangilio kuanzia kifikra mpaka nje (vitendo). Twende tukaangalie tunapokosea, ni hivi;

Unapowaza kufanya jambo lolote hata liwe kubwa kiasi gani, hakikisha hauvuki hatua ya kwanza ni hatua gani hiyo hii hapa, hatua ya kwanza inakuwa kati ya mawazo (idea) na kutenda, mawazo hubeba maarifa (knowledge) juu ya hicho unachowaza kukifanya, huwezi kuwaza kufanya kitu chochote bila kuwa na maarifa (haijalishi maarifa ya kutosha au laah) juu ya kitu hicho. Mwalimu aliwahi kusema kuwa kila kitu kipya tunachokiona huanza kama jaribio lakini nyuma ya jaribio kuna kitu kinaitwa nadharia (hypothesis), hivyo katika hatua ya kwanza ambapo ni mawazo na kutenda humaanisha nadharia na jaribio (hypothesis and experiment). Hivyo hupaswi kuvuka hapo kwenye mawazo na vitendo. Hupaswi kuvuka kwenda wapi? Twende tukaiangalie hatua ya pili;

Hatua ya pili, uchunguzi na matokeo (observation and results) baada ya kuwaza na kufanya (to take an action) kinachofwata ni uchunguzi wa nini kinachoendelea katika kitendo hicho, Je kinachoendelea kinakupa mwanga wa kuyafikia matokeo uliyoyawaza? Na bila kujalisha ulichokutana nacho wakati wa uchunguzi ulipokuwa unafanya jambo hilo je mwisho umepata matokeo gani?. Kuvuka ama kuruka hatua kunakuwaje ambako ndiko mwalimu anakwambia ni kosa kubwa na kunapelekea ushindwe kujiamini na kisha unashindwa kufanya kabisa jambo hilo ni hivi;

Mwanadarasa anapokuwa katika hatua ya kwanza ya mawazo huruka hatua zingine zote zinazofwata na kwenda moja kwa moja kwenye hatua ya matokeo, yaani yeye hujipa hatua mbili tu (mawazo na matokeo) “hahaha, hatari sana! Wala Mwanadarasa hataki kusumbua akili yake anajirahisishia na kujipa hatua mbili tu anaamua kupita short cut” kinachofanyika hapo ni Mwanadarasa kujipa matokeo mwenyewe kwenye kichwa chake bila kitendo kufanyika, ana heri yule anaejipa matokeo chanya kabla ya kitendo maana huyo ndiye aliyejaa kujiamini (Over confidence) lakini huyu tunaemzungumzia hapa yeye matokeo ambayo hujipa ni hasi. Hivyo hushindwa kabisa kukifanya hicho kitu kwasababu ya kujipa matokeo mwenyewe.

Anauona uwezo wake hauwezi kufanya jambo hilo pasipo hata kuujaribu, matokeo yake jamii inakosa ugunduzi wa vitu mbalimbali, jamii inakosa uanzishwaji wa vitu vipya tunarudi kulekule tunaishia kuiga tu. Hivyo mwalimu wako anakwambia mwanadarasa HAUNA UHAKIKA JUU YA UWEZO WAKO KWAMBA UNAWEZA AU LAAH NI MPAKA UMEFANYA. Kiuhalisia ni ngumu kuanza kuyatekeleza mawazo yako kwa kuanza na 100% za kujiamini (confidence), kujiamini huimarishwa na kuanza kuchukua hatua ya kufanya. Unaweza ukawa shuhuda hapa ukamsikia mtu anasema nilikuwa nakihofia tu bure kukifanya hiki kumbe kirahisi tu.

Kuna mwanafilosofia mmoja anaitwa Plato anasema “The beginning is the most important part of the work” kumbe kitu cha kwanza kabisa katika kufanya jambo lolote ni KUANZA (beginning). Au kwa lugha nyingine tunaweza kusema uthubutu na ni hatua moja muhimu sana ya kujenga kujiamini (self-confidence). Aina ya pili ya kutokujiamini ambayo pia ina wanadarasa wengi ambao wengi wameiweza ile ya uthubutu wa kuanza kufanya jambo ni hii hapa twende tukaiangalie;

Aina hii ya pili huja baada ya mtu kuanza kufanya, anapoianza hatua ya pili ya uchunguzi juu ya mwelekeo wa kile alichokikusudia, uchunguzi wake ukibeba hasi nyingi basi kujiamini kote kunatoweka, anaishia hapo na hiyo hujijenga na kuwa TABIA huyu jamaa Michael Jordan anasema “if you quit once it becomes a habit. Never quit” ndio maana utamsikia mtu anasema nimejaribu kufanya vitu vingi kwenye haya maisha lakini ukimwangalia hana hata kimoja mkononi. Watu wanashindwa kusimamia kile wanachokiamini. Watu wanashindwa kuwa wavumilivu jean Jaques anasema “patience is bitter but its fruits is sweet”. Mtu anatamani aanze kufanya jambo leo kesho aone mafanikio.

Mwalimu anakwambia safari ya mafanikio katika maisha ni kama kilimo cha miti tena ya mbao huwezi kupanda na ukatarajia kuvuna ndani ya miezi miwili au mitatu ijayo. Lakini kuna sababu kadhaa zinazopelekea watu kushindwa kujiamini au kupoteza kujiamini, tutaenda kuziangalia chache ambazo ni muhimu sana. Tukianza na ya kwanza misingi uliyojengwa nayo mwanadarasa hapa mwalimu aliongelea sana katika masomo yaliyopita, watu wamejengwa kwenye msingi kawaida ama mazoea, mwanadarasa haamini kama anaweza kufanya jambo ambalo halijazoeleka katika jamii, mwanajamii amejengwa katika msingi wa kutokuwa na uthubutu hivyo haamini kama anaweza kuthubutu na kufanya kitu tofauti na wengi walivyozoea.

Wanadarasa walio wengi wanaishi maisha ya kuwapendeza watu (to please people), kabla ya kufanya chochote mwanadarasa anakuwa na maswali ya kijinga kabisa kichwani, mwalimu lazima awe mkali kidogo hapa, maswali yenyewe ni kama haya moja wengine watasemaje (what will others say?) Mbili je Watu watanicheka (will people laugh at me)? Tatu nitawatazamaje watu endapo hili jambo litafeli (how can I face others if fail?) Na maswali mengine mengi mwalimu anayaita ya kijinga. Kuna msemo mujarabu kabisa unasema “Dont be afraid to stand for what you believe in, even if that means standing alone” <usiogope kukisimamia kile unachokiamini hatakama unaona umesimama peke yako hamna anaejali> hivyo ndivyo mwanadarasa inatakiwa uwe na mwalimu anakwambia tena kama alivyokwambia kwenye masomo yaliyopita toka kabisa kwenye msingi kawaida unaokuongoza ujiwaze katika kufeli kuna huyu jamaa anaitwa Bill Cosby anasema “In order to succeed, your desire for success should be greater than your fear of failure” <ili kuweza kufanikiwa, matamanio ya kufanikiwa yanapaswa yawe makubwa zaidi kushinda hofu ya kushindwa>.

Kwanini mwalimu anazungumzia zaidi wanadarasa kushindwa kujiamini katika kufanya mambo mageni/mapya, kwasababu wengi wa wanadarasa hawapati taabu sana kujiamini kufanya mambo yaliyozoeleka katika jamii. Kwanini watu hujiamini kufanya mambo ambayo tayari yamezoeleka kwasababu wanajiona kupata ulinzi wa jamii kwamba kwa sehemu yoyote mwanadarasa atakayokwama basi hatakosa wa KUMUULIZA, lakini kwenye kufanya jambo jipya anajiona ataonekana kichaa mbele ya jamii na ni kweli mwanafilosofia mmoja anaeitwa Aristotle anasema “no great genius has ever existed without some touch of madness”. Hivyo usiogope watu watakuonaje ni wajibu wako kuwashangaza watu (to prove them wrong).

Sababu ya pili ya watu kushindwa kujiamini, kukosa maarifa na ufahamu wa kutosha juu ya kitu wanachopanga kukifanya, (lack of enough knowledge and good understanding). Mwalimu anakwambia kwamba watu wengi hushindwa au hukosa kujiamini kwasababu hawana uelewa wa kutosha juu ya kufanya kitu fulani, kwasababu wapo kwenye msingi wa kuiga, basi kila atakachotaka kukifanya hawezi kuwa na uelewa wa kutosha juu ya hicho kitu, wengi wao husita kufanya kabisa lakini wale ambao hulazimisha kufanya basi hufeli vibaya kiasi kwamba wanashindwa kuinuka tena kisha mtaani watu huwapachika majina kuwa mkurupukaji. Hata iwe biashara tutakuja kuangalia vizuri tukifika kwenye nyanja ya biashara, kabla ya kuanza biashara yoyote hakikisha unataarifa zote muhimu (details) za kuihusu biashara hiyo. Moja ya kitu wanadarasa walio wengi wanashindwa kukizingatia na ni kitu muhimu basi ni kutenga muda wa kutosha wa kutafuta kukijua (doing research) juu ya hicho anachotaka kufanya na kuruhusu hisia za kukuona ukifanya hicho kitu zikikuongoza.

Sababu ya tatu kushindwa kuuishi wakati uliopo, watu wengi miili yao inaishi wakati uliopo huku mawazo na fikra zao zinaishi wakati uliopita (past). Wengi wao kipindi fulani kilichopita walijaribu kufanya vitu viwili vitatu na viliwaletea matokeo mabaya sana, ile hali ikawaharibu kisaikolojia na wakakubali kuishi nayo. Bado mwanadarasa anajiona ni yuleyule aliyeshindwa kipindi kile, bila kujalisha sababu zilizofanya ashindwe kipindi kilichopita, bila kujalisha kuwa kwasasa ufahamu umeongezeka kiasi gani. Mwalimu anakwambia mwanadarasa uishi usasa achana na ukale. Maarifa uliyonayo kwasasa ni tofauti na yale yaliyopita kale haina cha kufanya nawewe, historia haibadilishi chochote juu yako (past has nothing to do with you). Karl marx anasema “it is not history which uses men as a means of archiving-as if it were an individual person- its own ends. History is nothing but activity of men in pursuits of their ends”.

Kataa kabisa kuishi kutokana na historia mwanadarasa “Stop being a prisoner of your past. Become the architect of your future”. By Robin.

Mwalimu anasema tumaangalia kwa uchache tu kuhusu kujiamini (self-confidence) tutakuja kuangalia tena kwa kila nyanja tutakayoigusa.

<H.FARADAY> (0625934471)
.​
 
Mwl nipo hapo nimekuelewa cha msingi nikuwa positive katika kila jambo unalojaribu kufanya namalizia kwa kusema knowledge is the power

brain is like parachute it work when u open
 
Mwalimu mimi ni mwanadarasa wako niliyechelewa kukipata kipindi hiki lakini nashukuru nimekipata. Nimesoma na kuelewa lakini pia nimejifunza kitu hapa. Labda kwa uchache moja ya kitu nilichojifunza ni kwamba akili zetu zinatumika kiasi kidogo sana (20%) ili tu ku sustain maisha huku (80%) zikiwa idle.

Jambo lingine elimu tulizozipata hatuzitumii ipasavyo. Tunaishia kuungana na misingi ya kawaida iliyopo kwenye jamii zetu badala ya kama msomi kuwa huru (free) na kuitumia akili ipasavyo katika ku-reason ili kutatua matatizo ya kijamii.

Kimsingi ni mengi sana nimejifunza lakini kwa sababu simu yangu inakaribia kuzima chaji ngj ni-pause nitakuja kuelezea tena ila tu OMBI langu moja kwako mwalimu, kwakuwa umesema kuna whatsapp group unapoendeleza somo la "chakula cha ubongo" huko na kwakuwa kwa somo hili sihitaji kukosa hata mini-subtopic yake, ninaomba uniunganishe na group hilo na nitashkuru kama utanipatia na vipindi vyote ambavyo mimi mwanadarasa nimevikosa.

Asante sana kwa hili pindi lako lenye manufaa ya hali ya juu na Mungu akubariki sana.

Sent using Jamii Forums mobile app

 
Mwalimu mimi ni mwanadarasa wako niliyechelewa kukipata kipindi hiki lakini nashukuru nimekipata. Nimesoma na kuelewa lakini pia nimejifunza kitu hapa. Labda kwa uchache moja ya kitu nilichojifunza ni kwamba akili zetu zinatumika kiasi kidogo sana (20%) ili tu ku sustain maisha huku (80%) zikiwa idle.

Jambo lingine elimu tulizozipata hatuzitumii ipasavyo. Tunaishia kuungana na misingi ya kawaida iliyopo kwenye jamii zetu badala ya kama msomi kuwa huru (free) na kuitumia akili ipasavyo katika ku-reason ili kutatua matatizo ya kijamii.

Kimsingi ni mengi sana nimejifunza lakini kwa sababu simu yangu inakaribia kuzima chaji ngj ni-pause nitakuja kuelezea tena ila tu OMBI langu moja kwako mwalimu, kwakuwa umesema kuna whatsapp group unapoendeleza somo la "chakula cha ubongo" huko na kwakuwa kwa somo hili sihitaji kukosa hata mini-subtopic yake, ninaomba uniunganishe na group hilo na nitashkuru kama utanipatia na vipindi vyote ambavyo mimi mwanadarasa nimevikosa.

Asante sana kwa hili pindi lako lenye manufaa ya hali ya juu na Mungu akubariki sana.

Sent using Jamii Forums mobile app

Kuna namba ya mwalimu mwisho wa somo mtafute ili akuunganishe.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Shukran san mwalim vtu adhim san hvi ni ile bas tu watanznia maandsh n adui yetu lakin kwa mwnye akil atatafuta kujua zaid juu ya hya. Ngja nkutafut mwalm naiman sijachelew.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ndo kusema mwl alishawakimbia wanafunzi wake duuuuh ni hatari

brain is like parachute it work when u open
 
[QUOTE="Haber Faraday,
Vipi masomo haya tukiyaandalia mfumo mwingine rafiki kwa wanafunzi kama vile PP? Wabongo wengi wanapenda kuangalia maandishi yalochanganywa na picha. Niko tayari kufanya kazi hiyo ili kuwafikia walio wengi.
 
Back
Top Bottom