Daraja la Kigamboni ni White Elephant Project, Hatulihitaji!

Daraja la Kigamboni ni White Elephant Project, Hatulihitaji!

Mkuu, labda tueleweshane, ni mji gani mkubwa duniani ambao unaufahamu ambao uko kando ya bahari kama Dar es Salaam wenye metro? Nafikiri tabia ya nchi, udongo na miamba una nafasi kubwa sana katika hilo la kujenga metro. Halafu huo umeme wa kuendesha hayo ma train hatunao bado. Labda unachosema wewe ni kwamba tuanze kwa kuangalia upper stream devlelopmental investments?

Ndugu yangu twaweza jadili kuhusu umeme wa uhakika labda, lakini kuhusu bahari halina maana,
Nchi kama uingereza, Japan ni visiwa kabisa, zina metro za kutosha, mji kama dubai wamepitisha train juu ya bahari kabisa kuunganishia upande wa pili wa mji wa sharjah, vipi wameweza!?
 
Mi siungi mkono kujengwa kwa mradi wa kuunganisha coco beach na daraja la salenda. Kwa umbali (km 7 kama sikosei) alioutaja JPM ni dhahiri huu mradi utahitaki pesa nyingi.Pamoja na kwamba unagharimiwa na Korea basi tungeomba hizo pesa tujenge flyovers kwenye major road juntions kama Banda la ngozi, Kamata, ilala soko l machinga, magomeni, mwenge na nyingine hapa mjini. Hii ingeweza kuondoa jam mji mzima kuliko kuweka nguvu zote kwenye sehemu moja ya Masaki. Hizi.pesa zitakuwa nyingi sana kiasi kwamba zingeweza kumaliza jams za hapa Dar kwa kujenga flyovers mji mzima.
 
Naunga mkono ujenzi wa daraja la Kigamboni maana umbali ni mfupi na kuna karaha kubwa kwenda huko siku za weekend.
 
mtoa post mbona uko shallow hivo???population dar inakua sana ni vizuri wamejenga hilo daraja kwasababu demand ya vivuko itakua kubwa na haitoweza kidhi mahitaji ya wananchi,na there is a maximum number ya vivuko vinavyoweza kufanya kazi eneo husika lakini sio daraja....daraja muda wote lipo na litaokoa muda kwa wake waenda kasi plus halitasumbua kama vivuko....watu wamekaa wametafakari na wameliona hilo binafsi nawapongeza sana
 
Oh My God! Siwezi hata kufikiri kwamba kuna kiumbe anaye weza kuja na hoja kama hii. It's a total embassment. I thought hii forum ni ya Great Thinkers. What a waste of time!

Think about congestion ya traffic in the inner city. Think about mafuta yanayo potea bure kwenye hizo foleni, think about kuboresha sehemu zingine za jiji, think about maendeleo ya satellite cities, etc. Halafu eti unasemaje???
Well..tell us kwa uhalisia namna gani daraja litapunguza congestion na kuboresha jiji..dont speak of hearsay na projection ambazo ni unrealistic like flyovers ambazo hadi sasa ziko kwenye plan...tusaidie tujue kwa sasa lita add value gani ili hata mtoa hoja ajiridhishe kua thats not about prestige n blue print..otherwise i see more of blame games
 
wewe ndio huna unachoelewa, kiuchumi daraja la kigamboni sio kipaumbele chetu kabisa ni ujenzi wa sifa tu, kigamboni ina watu wangapi? na hata wao watu wakija mjini bado njia za mjini hazijaboreshhwa so foleni iko pale pale, kigamboni bridge is a white elephant project, period
Ni wazi kwamba wewe na wenzio wote mnahitaji operation ya ubongo mara kadhaa ili kuelewa kwamba already tumechelewa na tunahitaji madaraja mengine zaidi kama hilo moja linalo kamilika sasa. Mna ubishi mfirisi usiokuwa na mashiko. Hujui hata kitu kiitwacho socio-economic assessment iloyofanywa na wataalamu kabla ya mradi haujaanza. Ni ule ubishi wa kinafiki kuonekana kwamba angalao na wewe umechangia hoja. Data zenu za uvunguni na kubabsisha. Kama huoni umuhimu wa hilo daraja, je ujenzi wa mji mpya kigamboni si utakutia wazimu! Mambo ya wasomi waachie wasomi wenyewe. Siyo size yenu.
 
Nilisikiaga mwaka 2011 Marekani wanachimba visima vikubwa kwaajili ya kuhifafhi mafuta ambayo yangetumika baada ya miaka 100 kutoka na utafiti wao baada ya miaka hiyo dunia itakuwa na upungufu mkubwa wa mafuta
 
Ni wazi kwamba wewe na wenzio wote mnahitaji operation ya ubongo mara kadhaa ili kuelewa kwamba already tumechelewa na tunahitaji madaraja mengine zaidi kama hilo moja linalo kamilika sasa. Mna ubishi mfirisi usiokuwa na mashiko. Hujui hata kitu kiitwacho socio-economic assessment iloyofanywa na wataalamu kabla ya mradi haujaanza. Ni ule ubishi wa kinafiki kuonekana kwamba angalao na wewe umechangia hoja. Data zenu za uvunguni na kubabsisha. Kama huoni umuhimu wa hilo daraja, je ujenzi wa mji mpya kigamboni si utakutia wazimu! Mambo ya wasomi waachie wasomi wenyewe. Siyo size yenu.



Ujenzi wa Mji wa Kigamboni na wewe unaamini kabisa hizo Sarakasi? Kama kuzoa taka tu hatuwezi au hata kubandika tu kibao cha Mtaa ambao upo tangu enzi za ukoloni hatuwezi, leo hii ukitaka kufika mahali ni lazima useme karibia na kontena fulani nyumba hazina namba hilo pia hatuwezi halafu unaongelea kujenga Mji mpya?

Zaidi ya asilimia 70 (70%) ya wakazi wa Dar wanaishi kwenye makazi yasiyo rasmi na hawana maji kwa maana haiwezekani kuwafikishia wala Zimamoto haiwezi kufika nyumba ikiwaka moto kwa maana hakuna br. yakufika sasa kama vitu vidogo na vya msingi kama hivi hatuwezi kufanya iweje tuweje kujenga Mji mpya?
Hiyo miujiza itatoka wapi? Acha kujidanganya mtoto hawezi kuanza kukimbia kabla ya kutambaa!
 
Lisingejengwa bado mngepiga kelele, vipaumbele ni vingi sana, ukitazama karibu huwezi kuelewa logic ya bandari ya bagamoyo, na ukishaiweka akili ikawa katika mtazamo wa kupinga, unaweza kujikuta unapinga hata yale mambo ambayo unatakiwa kupewa shule ili uweze kuyajua vizuri. Mpeni Rais muda wa kufanya kazi na sio kuishi kukosoa kila kitu. Hata posho kubwa za wabunge na zenyewe ni mzigo kwa taifa kama unaliangalia kila jambo katika fikra hasi.
 
Well..tell us kwa uhalisia namna gani daraja litapunguza congestion na kuboresha jiji..dont speak of hearsay na projection ambazo ni unrealistic like flyovers ambazo hadi sasa ziko kwenye plan...tusaidie tujue kwa sasa lita add value gani ili hata mtoa hoja ajiridhishe kua thats not about prestige n blue print..otherwise i see more of blame games
Impact analysis ya project ilikwisha weka hadharani tangu miaka ile kabla mradi haujaanza. Kwa sababu ya ufilisi wenu na uzembe wa kutotafuta facts ndo maana leo five years later na project kukamilika mnaleta hoja za kipuuzi. Nenda sehemu husika usome projections za mradi. Ni public documents. Nina hakika utapewa na next time usishabikie kitu bila facts.
 
Lisingejengwa bado mngepiga kelele, vipaumbele ni vingi sana, ukitazama karibu huwezi kuelewa logic ya bandari ya bagamoyo, na ukishaiweka akili ikawa katika mtazamo wa kupinga, unaweza kujikuta unapinga hata yale mambo ambayo unatakiwa kupewa shule ili uweze kuyajua vizuri. Mpeni Rais muda wa kufanya kazi na sio kuishi kukosoa kila kitu. Hata posho kubwa za wabunge na zenyewe ni mzigo kwa taifa kama unaliangalia kila jambo katika fikra hasi.


Sasa kama unafahamu kwamba Vipaumbele ni vingi je hilo Daraja lilifaa liwe hata Kipaumbele?
Kwa lipi hasa? Kwa ajili tu ya watu kwenda club na kushinda beach ndiyo tutumie bilioni 200?
 
Mimi siyo Great thinker na wala sijawahi na sitowahi kujitambulisha hivyo ila kama wewe unaona unastahili kuitwa hivyo hiyo ni juu yako!

Haya niambie hili daraja litapunguza msongamano wa kiasi gani kwenye huu Mji? Ni asilimia ngapi ya wakazi wa Dar watalitumia kila siku kwenda na kurudi kazini ikilinganishwa na gharama iliyotumiwa kulijenga?
Mmh, my friend
Usiirudishe nchi katika enzi za fikra ambazo mitambo ya TV ilionekana kama luxury. Please.[/QUOTE]
Mimi Binafsi Nimekuelewa sana tu. uwekezaji wa Mabilion kama hayoulitakiwa hapahapa feli siyouko mafichoni. Mkeka ungetandikwa hapa hata watalii wangeongezeka kuja kusha ngaa hilo daraja. FANYA VITU VINAVYOSHANGAZA WENGINE PESA ITARUDI TU.
 
Mabilioni yaliyowekezwa kwenye Ujenzi wa hili Daraja ni kama yamepotea bure kwa maana halihitajiki, halina umuhimu mkubwa kiasi hicho kwa maana ya kwamba halitasaidia kuboresha maisha ya wakazi wa Dar kwa walio wengi ukilinganisha na gharama ya Ujenzi wake hii ni prestige project ambayo kwa nchi masikini na yenye kila aina ya shida inayojulikana na binadamu hapa Duniani hatukupaswa kulijenga badala yake hizi fedha zingewekezwa kwenye miradi mikubwa kama DART kwa mfano hii fedha ingetosha kujenga DART nyingine kutoka Mwenge mpaka Kivukoni hivyo kuwa na DART mbili ambazo zingesadia sana wakazi wa Dar, kuliko hili Daraja!

Itatuchukuwa muda sana sisi Watanzania kuja kuendelea, mpaka tuje tuweke vipaumbele vyetu sawa tuna safari ndefu sana, mradi mwingine ambao nasikia uko mbioni na namwomba Rais Magufuli auzuie huu mradi kama ule wa bandari ya Bagamoyo ni wa kujenga daraja baharini ktk daraja la Salenda kuunganisa na Coco Beach, hili daraja hatulihitaji badala yake hizi fedha ziende kujenga DART nyingine labda ya Br. ya Mandela- Buguruni -Kariakoo!
Mtoa post anastahili kutumia haki yake ya kutoa maoni. Lakini maoni yawe na mshiko; yamebebe hoja za kutetea msimamo wake kwa facts and figures, siyo kubwabwaja tu.
 
Impact analysis ya project ilikwisha weka hadharani tangu miaka ile kabla mradi haujaanza. Kwa sababu ya ufilisi wenu na uzembe wa kutotafuta facts ndo maana leo five years later na project kukamilika mnaleta hoja za kipuuzi. Nenda sehemu husika usome projections za mradi. Ni public documents. Nina hakika utapewa na next time usishabikie kitu bila facts.
Umemaliza???? Tanzanians are good in plans ..theories,processes and projections...paper work as usual...adios amigos!
 
Kila mradi unaofanywa na serekali ya mafisiem hue hata wa manufaa kwa wananch ni madili na ufisad.

Linchi maskin eti mijitu inakimbilia DART daraja la kigambon cjui ninI. Wizi uvivu wa kufikir na misifa ya kijinga
 
Kila mradi unaofanywa na serekali ya mafisiem hue hata wa manufaa kwa wananch ni madili na ufisad.

Linchi maskin eti mijitu inakimbilia DART daraja la kigambon cjui ninI. Wizi uvivu wa kufikir na misifa ya kijinga


Na mbaya zaidi hili daraja limejengwa na fedha zetu za NSSF ambapo limepelekea shirika kuwa na matatizo makubwa sana ya kifedha imefikia mahali hata kulipa ya mishahra ya wafanyakazi ni kazi, na ndiyo NSSF wana matatizo ya kulipa mishahara, ni nani anaweza kuamini hili? Lkn ni ukweli ongea na insider watakwambia kwamba hali siyo nzuri shirikani lkn wanachukuwa biloni 200 kujenga daraja la kuhudumia chini ya asilimia 5 (5%) ya Wananchi, hizo akili au matope?
 
Sasa kama unafahamu kwamba Vipaumbele ni vingi je hilo Daraja lilifaa liwe hata Kipaumbele?
Kwa lipi hasa? Kwa ajili tu ya watu kwenda club na kushinda beach ndiyo tutumie bilioni 200?
tangu tupate uhuru tumeshatumia shilingi ngapi kwenye miradi mikubwa? madaraja makubwa duniani kama hilo la kigamboni yanajengwa kwa fedha kiasi gani?, ina maana hizo pesa zisingeweza kutumiwa katika shughuli nyinginezo? naweza kukubaliana nawe kwenye wingi wa fedha lakini sio kusema eti daraja halina umuhimu, haya majengo makubwa yanayojengwa na National Housing nchi nzima hayatumii fedha kidogo na sio kweli kwamba yote kwa wakati mmoja yatapata watu wenye uwezo wa kupangisha, huwezi kukwepa gharama za miradi kwa kigezo cha vipaumbele, kinachojengwa leo kinaweza kutoonekana muhimu leo lakini kuna wakati ambapo umuhimu wake utaonekana. Na sio lazima umuhimu wa daraja uonekane wakati mimi na wewe tupo bado hai. Waliojenga majiji makubwa kama New York, Paris na Moscow karibu asilimia 90 yao tayari wameshazikwa. Tusiweke ubinafsi kwa kuongelea vipaumbele kana kwamba maisha yanaisha baada ya siku tulizopewa na Mungu kumalizika.
 
tangu tupate uhuru tumeshatumia shilingi ngapi kwenye miradi mikubwa? madaraja makubwa duniani kama hilo la kigamboni yanajengwa kwa fedha kiasi gani?, ina maana hizo pesa zisingeweza kutumiwa katika shughuli nyinginezo? naweza kukubaliana nawe kwenye wingi wa fedha lakini sio kusema eti daraja halina umuhimu, haya majengo makubwa yanayojengwa na National Housing nchi nzima hayatumii fedha kidogo na sio kweli kwamba yote kwa wakati mmoja yatapata watu wenye uwezo wa kupangisha, huwezi kukwepa gharama za miradi kwa kigezo cha vipaumbele, kinachojengwa leo kinaweza kutoonekana muhimu leo lakini kuna wakati ambapo umuhimu wake utaonekana. Na sio lazima umuhimu wa daraja uonekane wakati mimi na wewe tupo bado hai. Waliojenga majiji makubwa kama New York, Paris na Moscow karibu asilimia 90 yao tayari wameshazikwa. Tusiweke ubinafsi kwa kuongelea vipaumbele kana kwamba maisha yanaisha baada ya siku tulizopewa na Mungu kumalizika.



Kwanza hakuna mahali niliposema kwamba hilo daraja halina mahitaji, najua kwamba linahitajika na watu wanaokwenda kipepepo wkend au kuangalia wanyama Dar zoo n.k ila hizo sababu ni ndogo sana ukilinganisha na mahitaji mengine ambayo hizi bilioni 200 zingeweza kufanya kama hizi hele zingeingizwa kwenye kupunguza msongamano ingetoa tofauti kubwa sana, sasa hivi tunavyoongea NSSF inashida ya fedha kwa sababu ya mradi kama huu, sasa kwa nini tufilishi shirika lenye kuweka akiba zetu za uzeeni kwa kuwekeza kwenye mradi ambao unafaidisha watu chini ya asilimia 5% ?

Na hapo ndipo Kipaumbele kinapokuwa na umuhimu, sababu kubwa ya kujengwa hilo daraja kama nilivyosema haina uhusiano wowote ule na manufaa ka Wananchi bali ni prestige project kwamba tuweze kupiga picha na kusema Dar tuna Daraja lkn siyo kumwezesha Mtz kiuchumi na hili litaonekana wazi daraja litakapofunguliwa utakuwa shahidi kama kweli vivuko vitapungukiwa na watu na ninaweza kukuhakikishia asilimia 90% ya wanaotumia vivuko wataendela kutumia hivi vivuko hata baada ya daraja kufunguliwa na watakao litumia niwachache ambao wanakwenda wk end kipepeo beach au kukagua mashamba yao, sasa dola 200 bilioni kutumika kufanya uwekazaji kama huu kwenye nchi ambayo ukifungua tu mlango umaskini umekuzunguka kila mahali na wali hata haujui uanzie wapi ni kutokuwa na uwezo wa kupanga vizuri!
 
kigamboni si ilishauzwa kwa wamarekani? Sasa watafikaje huko bila barabara
 
Back
Top Bottom