figganigga
JF-Expert Member
- Oct 17, 2010
- 25,492
- 54,895
Mbunge wa zamani wa Jimbo la Singida Mashariki (CHADEMA), Tundu Lissu ameuhutubia mkutano mkuu wa chama hicho unaoendelea katika ukumbi wa Mlimani City jijini Dar es Salaam akisema, mpango wa kukiua chama hicho iliyopangwa imeshindikana na zaidi imekiimarisha zaidi chama hicho.
Lissu amesema Madaktari wake wamemwambia amepona na yuko tayari kurudi Tanzania, kwa ajili ya kuungana na wanachama wenzake wa CHADEMA, na ameomba chama chake kimsaidie haraka iwezekanavyo aweze kurudi. “Madkatari wangu wamesema nimepona, nachechemea kidogo lakini nimepona na niko tayari kurudi nyumbani. “Nipo tayari kurudi nyumbani kuungana na makamanda wengine ili tutengeneze nchi. Naombeni tushirikiane ili niweze kurudi nyumbani haraka na salama.
Mbele ni kuzuri kuliko huko tulikotoka. "Niwatake wanachama wenzangu wa CHADEMA tufanye maandalizi ya kutosha, ili ngwe iliyobaki ambayo siyo ndefu itakuwa ni ngwe ya kurudisha nchi katika utu, demokrasia na haki binadamu. "Baada ya mateso yote tuliyopata, baada ya bonde la uvuli wa mauti, njia iliyobaki ni kuchukua nchi mwakani. Hakuna walichobakiza, wametufunga, wametujeruhi na kila mateso, leo tuna nguvu zaidi kuliko tulivyokuwa.
“Yote yaliyotokea mpaka leo ni utekelezaji wa azma ya kuua mfumo wa vyama vingi. Kwa ushahidi huu wa mkutano na mfumo wa uchaguzi katika chama mpaka siku ya leo, hicho walichokidhamiria hakijafanikiwa mpaka leo,” amesema Tundu Lissu kwa njia ya Video Call.
Lissu amesema Madaktari wake wamemwambia amepona na yuko tayari kurudi Tanzania, kwa ajili ya kuungana na wanachama wenzake wa CHADEMA, na ameomba chama chake kimsaidie haraka iwezekanavyo aweze kurudi. “Madkatari wangu wamesema nimepona, nachechemea kidogo lakini nimepona na niko tayari kurudi nyumbani. “Nipo tayari kurudi nyumbani kuungana na makamanda wengine ili tutengeneze nchi. Naombeni tushirikiane ili niweze kurudi nyumbani haraka na salama.
Mbele ni kuzuri kuliko huko tulikotoka. "Niwatake wanachama wenzangu wa CHADEMA tufanye maandalizi ya kutosha, ili ngwe iliyobaki ambayo siyo ndefu itakuwa ni ngwe ya kurudisha nchi katika utu, demokrasia na haki binadamu. "Baada ya mateso yote tuliyopata, baada ya bonde la uvuli wa mauti, njia iliyobaki ni kuchukua nchi mwakani. Hakuna walichobakiza, wametufunga, wametujeruhi na kila mateso, leo tuna nguvu zaidi kuliko tulivyokuwa.
“Yote yaliyotokea mpaka leo ni utekelezaji wa azma ya kuua mfumo wa vyama vingi. Kwa ushahidi huu wa mkutano na mfumo wa uchaguzi katika chama mpaka siku ya leo, hicho walichokidhamiria hakijafanikiwa mpaka leo,” amesema Tundu Lissu kwa njia ya Video Call.