Dar: Polisi waua watu watatu wanaodhaniwa kuwa Majambazi, wakamata silaha

Roving Journalist

JF Roving Journalist
Apr 18, 2017
2,810
11,977
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
POLISI YAZUIA TUKIO LA UJAMBAZI
KUKAMATWA SILAHA MBILI AINA YA SHORTGUN, BASTOLA PAMOJA NA KUUWAWA MAJAMBAZI WATATU (3)

Jeshi la Polisi kanda Maalum ya Dar es salaam mnamo tarehe 25/08/2019 majira ya tatu na nusu usiku huko maeneo ya Pugu, lilifanikiwa kukamata silaha mbili aina ya Shortgun na bastola.

Katika ufuatiliaji alikamatwa mtuhumiwa aliyefahamika kwa jina la OMARY ATHUMANI @ DANGA MIAKA (39), mkazi wa mkuranga amabaye pia alikuwa anatafutwa kwa kujihusisha na matukio mbalimbali ya unyang’anyi wa kutumia silaha, katika mahojiano ya kina mtuhumiwa alikiri kujihusisha na matukio mbalimba ya unyang’anyi wa kutumia silaha na kuwa amewahi kufungwa miaka 30 na alitoka kwa rufaa na kujiunga na kundi lingine la ujambazi.

Mtuhumiwa huyo pia alieleza kuwa kuna wenzake watatu ambao anashirikiana nao pia wamepanga wakavamie na kupora duka la M-pesa lililopo maeneo ya Pugu shuleni hivyo yuko tayari kuwapeleka Askari eneo la tukio, kikosi kazi wakiwa na mtuhumiwa waliweka mtego na ilipofika muda huo eneo la Pugu washirika wake walijitokeza toka kwenye kichaka wanakoficha silaha mara wakagundua kuwa wanafuatiliwa na askari maeneo hayo ghafla majambazi hao walianza kurusha risasi kuelekea kwa Askari na mtuhumiwa alianza kupiga kelele na kujaribu kuwakimbia askari.

Askari walijibu mapigo na walifanikiwa kuwajeruhi majambazi watatu OMARI ATHUMANI, FULLSABA NA BABU SHOBO sehemu mbalimbali za miili yao na mmoja aitwaye DOGO SIDE alifanikiwa kukimbia kusikojulikana, majeruhi wote walikimbizwa hospitali ya taifa Mhimbili kwa matibabu lakini baada ya Daktari kuwapima alithibitisha kuwa wameshafariki dunia.

Baada ya upekuzi majambazi hao walipatikana na silaha mbili No. YA- 1547 aina ya SHORTGUN iliyo katwa kitako na mtutu, Ikiwa na risasi tatu, ganda moja la risasi na BASTOLA moja iliyo futwa namba ikiwa na risasi mbili na maganda mawili(2) ya risasi.

Aidha silaha tajwa aina ya Shortgun ilibainika kuwa iliporwa tarehe 13.04/2019 saa nne na nusu usiku kesi ya unyang’anyi ilifunguliwa kituo cha Ukonga na silaha hiyo ilikuwa mali ya kampuni ya ulinzi iitwayo ALEMS SECURITY CO.LTD iliyopo njia panda Segerea Dsm na ilitumika kupora kiasi cha pesa Tsh 6,000,000/= huko MARKAZ Gongo la mboto kwa mfanyabiashara aitwaye JUSTINE CHAULA, pamoja na simu 5 za aina mbalimbali.

Awali mtuhumiwa alikiri kuwa yeye na wenzake wamewahi kushtakiwa kwa makosa ya mauaji na unyang’anyi wa kutumia silaha zaidi ya kesi 6 ambazo zilikuwa mahakamani kabla ya kutoka kwa rufaa mwaka 2017.

Tukio lingine mwezi wa 6, 2019 walipora maduka ya M-pesa, Tigo pesa maeneo ya mazizini Ukonga, mbezi juu wilaya ya ubungo na walipora Tsh 800,000/= kwa mfanyabiashara wa mchanga, maeneo ya Machimbo wilaya ya Mkuranga. Pia polisi wilaya ya mkuranga ilifanya upekuzi nyumbani kwa marehemu OMARY ATHUMAN@DANGA na kufanikiwa kukamata risasi 7 za silaha aina ya Shorgun na jalada la shauri hili linapelelezwa.

Kikosi kazi kinaendelea na msako mkali ili kuhakikisha jambazi aliyetoroka kwenye eneo la tukio anakamatwa haraka na kufikishwa mahakamani kujibu tuhuma zinazomkabili.

Wananchi wazidi kutoa taarifa za uhalifu na wahalifu ili kuliweka jiji letu la Dar es salaam katika hali ya amani na utulivu ili raia wema waendelee kufanya kazi za kuinua kipato chao na taifa kwa ujumla.

KUKAMATWA KWA JAMBAZI MMOJA, ALIYEKIMBIA KWENYE TUKIO LA UJAMBAZI, KUPATIKANA SILAHA MOJA, RISASI TATU NA VIFAA MBALIMBALI
Katika tukio la pili, Jeshi la Polisi kanda maalum Dar es salaam limefanikiwa kumkamata jambazi mmoja aitwaye ELIA MATAYO KITULI (55) mkazi wa Kivule, wilaya ya Ilala jijini DSM aliyekuwa anatafutwa, Baada ya kukimbia kwenye tukio la ujambazi lililotokea tarehe 04/07/2019 ambapo majambazi wawili waliuwawa na kupatikana silaha mbili aina ya bastola huko Kitunda machimbo ambapo nilitoa taarifa kwa vyombo vya habari.

Jambazi huyo alikamatwa akiwa na silaha moja aina ya Rifle yenye namba MK3-90893 ikiwa na risasi 3 ndani ya kasha(magazine) na vifaa mbalimbali vilivyoporwa maeneo mbalimbali kama ifuatavyo;

1. Ipad mbili aina ya Samsung na Apple
2. Smart phone nane(8) aina ya INFINX, Samsung, Nokia, Huawei, Techno na Iphone.

3. Saa moja ya mkononi aina ya Seiko 5 rangi ya dhahabu
4. Kisu kimoja
5. Digital camera moja aina ya Sony
6. Lap top moja aina ya Toshiba
7. Head phone moja na charger mbalimbali za simu

Mtuhumiwa aliendelea kuhojiwa kituo cha Polisi mara aliugua ghafla na kupelekwa hospitali ya taifa Muhimbili na baadaye alifariki dunia kwa maradhi yaliyokuwa yanamsumbua.

Baadhi ya wahanga waliofanyiwa matukio ya uporaji wamefanikiwa kutambua vifaa vyao ambapo simu 2 aina ya Iphone na Samsung moja zilitambuliwa.

LAZARO B. MAMBOSASA– SACP
KAMANDA WA POLISI KANDA MAALUM
DAR ES SALAM.
29/08/2019
 
Kwa sababu wakipelekwa gerezani, wanatoka kwa rufaa kurudi kuwasumbua wananchi na Polisi.
Upo sahihi lakini tuangalie na upande wa pili wa shillingi
Je ni kweli ni majambazi au ni kuumizana tu
 
Kwani una hakika wote ni majambazi?
Polisi yetu Hii ya kubambikizia watu kesi
Unajuaje hivyo wanavyosema wamewakuta navyo vimewekwa kujustify zoezi zima
kwa tz jambazi hua afungwi, akale ugali wa bure
 
Kwani una hakika wote ni majambazi?
Polisi yetu Hii ya kubambikizia watu kesi
Unajuaje hivyo wanavyosema wamewakuta navyo vimewekwa kujustify zoezi zima

Si utani hiyo hadithi aliyosimulia ziko nyingi sana za namna hiyo? Anawapeleka walikoficha silaha, mara wanatupiana lisasi, wanauawa. Kesi kwisha.
Mwingine nae kaugua akafa akihojiwa.
Hatari sana.
Majambazi muwe makini na muache, hatuendi mahakamani siku hizi.
 
Stori za majambazi
Eti akatupeleka porini
Wenzake wakaanza rusha risasi
Mtuhumiwa akaanza piga kelele na kuwakimbia polisi
Wakapelekwa Muhimbili


Wanaua watu afu stori zao kila siku ni hizi hizi.

Huyo Athuman aliuawa Polisi waliwajuaje hao wengine majina yao?
 
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
POLISI YAZUIA TUKIO LA UJAMBAZI
KUKAMATWA SILAHA MBILI AINA YA SHORTGUN, BASTOLA PAMOJA NA KUUWAWA MAJAMBAZI WATATU (3)

Jeshi la Polisi kanda Maalum ya Dar es salaam mnamo tarehe 25/08/2019 majira ya tatu na nusu usiku huko maeneo ya Pugu, lilifanikiwa kukamata silaha mbili aina ya Shortgun na bastola.

Katika ufuatiliaji alikamatwa mtuhumiwa aliyefahamika kwa jina la OMARY ATHUMANI @ DANGA MIAKA (39), mkazi wa mkuranga amabaye pia alikuwa anatafutwa kwa kujihusisha na matukio mbalimbali ya unyang’anyi wa kutumia silaha, katika mahojiano ya kina mtuhumiwa alikiri kujihusisha na matukio mbalimba ya unyang’anyi wa kutumia silaha na kuwa amewahi kufungwa miaka 30 na alitoka kwa rufaa na kujiunga na kundi lingine la ujambazi.

Mtuhumiwa huyo pia alieleza kuwa kuna wenzake watatu ambao anashirikiana nao pia wamepanga wakavamie na kupora duka la M-pesa lililopo maeneo ya Pugu shuleni hivyo yuko tayari kuwapeleka Askari eneo la tukio, kikosi kazi wakiwa na mtuhumiwa waliweka mtego na ilipofika muda huo eneo la Pugu washirika wake walijitokeza toka kwenye kichaka wanakoficha silaha mara wakagundua kuwa wanafuatiliwa na askari maeneo hayo ghafla majambazi hao walianza kurusha risasi kuelekea kwa Askari na mtuhumiwa alianza kupiga kelele na kujaribu kuwakimbia askari.

Askari walijibu mapigo na walifanikiwa kuwajeruhi majambazi watatu OMARI ATHUMANI, FULLSABA NA BABU SHOBO sehemu mbalimbali za miili yao na mmoja aitwaye DOGO SIDE alifanikiwa kukimbia kusikojulikana, majeruhi wote walikimbizwa hospitali ya taifa Mhimbili kwa matibabu lakini baada ya Daktari kuwapima alithibitisha kuwa wameshafariki dunia.

Baada ya upekuzi majambazi hao walipatikana na silaha mbili No. YA- 1547 aina ya SHORTGUN iliyo katwa kitako na mtutu, Ikiwa na risasi tatu, ganda moja la risasi na BASTOLA moja iliyo futwa namba ikiwa na risasi mbili na maganda mawili(2) ya risasi.

Aidha silaha tajwa aina ya Shortgun ilibainika kuwa iliporwa tarehe 13.04/2019 saa nne na nusu usiku kesi ya unyang’anyi ilifunguliwa kituo cha Ukonga na silaha hiyo ilikuwa mali ya kampuni ya ulinzi iitwayo ALEMS SECURITY CO.LTD iliyopo njia panda Segerea Dsm na ilitumika kupora kiasi cha pesa Tsh 6,000,000/= huko MARKAZ Gongo la mboto kwa mfanyabiashara aitwaye JUSTINE CHAULA, pamoja na simu 5 za aina mbalimbali.

Awali mtuhumiwa alikiri kuwa yeye na wenzake wamewahi kushtakiwa kwa makosa ya mauaji na unyang’anyi wa kutumia silaha zaidi ya kesi 6 ambazo zilikuwa mahakamani kabla ya kutoka kwa rufaa mwaka 2017.

Tukio lingine mwezi wa 6, 2019 walipora maduka ya M-pesa, Tigo pesa maeneo ya mazizini Ukonga, mbezi juu wilaya ya ubungo na walipora Tsh 800,000/= kwa mfanyabiashara wa mchanga, maeneo ya Machimbo wilaya ya Mkuranga. Pia polisi wilaya ya mkuranga ilifanya upekuzi nyumbani kwa marehemu OMARY ATHUMAN@DANGA na kufanikiwa kukamata risasi 7 za silaha aina ya Shorgun na jalada la shauri hili linapelelezwa.

Kikosi kazi kinaendelea na msako mkali ili kuhakikisha jambazi aliyetoroka kwenye eneo la tukio anakamatwa haraka na kufikishwa mahakamani kujibu tuhuma zinazomkabili.

Wananchi wazidi kutoa taarifa za uhalifu na wahalifu ili kuliweka jiji letu la Dar es salaam katika hali ya amani na utulivu ili raia wema waendelee kufanya kazi za kuinua kipato chao na taifa kwa ujumla.

KUKAMATWA KWA JAMBAZI MMOJA, ALIYEKIMBIA KWENYE TUKIO LA UJAMBAZI, KUPATIKANA SILAHA MOJA, RISASI TATU NA VIFAA MBALIMBALI
Katika tukio la pili, Jeshi la Polisi kanda maalum Dar es salaam limefanikiwa kumkamata jambazi mmoja aitwaye ELIA MATAYO KITULI (55) mkazi wa Kivule, wilaya ya Ilala jijini DSM aliyekuwa anatafutwa, Baada ya kukimbia kwenye tukio la ujambazi lililotokea tarehe 04/07/2019 ambapo majambazi wawili waliuwawa na kupatikana silaha mbili aina ya bastola huko Kitunda machimbo ambapo nilitoa taarifa kwa vyombo vya habari.

Jambazi huyo alikamatwa akiwa na silaha moja aina ya Rifle yenye namba MK3-90893 ikiwa na risasi 3 ndani ya kasha(magazine) na vifaa mbalimbali vilivyoporwa maeneo mbalimbali kama ifuatavyo;

1. Ipad mbili aina ya Samsung na Apple
2. Smart phone nane(8) aina ya INFINX, Samsung, Nokia, Huawei, Techno na Iphone.

3. Saa moja ya mkononi aina ya Seiko 5 rangi ya dhahabu
4. Kisu kimoja
5. Digital camera moja aina ya Sony
6. Lap top moja aina ya Toshiba
7. Head phone moja na charger mbalimbali za simu

Mtuhumiwa aliendelea kuhojiwa kituo cha Polisi mara aliugua ghafla na kupelekwa hospitali ya taifa Muhimbili na baadaye alifariki dunia kwa maradhi yaliyokuwa yanamsumbua.

Baadhi ya wahanga waliofanyiwa matukio ya uporaji wamefanikiwa kutambua vifaa vyao ambapo simu 2 aina ya Iphone na Samsung moja zilitambuliwa.

LAZARO B. MAMBOSASA– SACP
KAMANDA WA POLISI KANDA MAALUM
DAR ES SALAM.
29/08/2019
Askari walijibu mapigo na walifanikiwa kuwajeruhi majambazi watatu OMARI ATHUMANI, FULLSABA NA BABU SHOBO sehemu mbalimbali za miili yao na mmoja aitwaye DOGO SIDE alifanikiwa kukimbia kusikojulikana, majeruhi wote walikimbizwa hospitali ya taifa Mhimbili kwa matibabu lakini baada ya Daktari kuwapima alithibitisha kuwa wameshafariki dunia.
 
Kwa nini Polisi wanaua kila anayedhaniwa jambazi Kwa nini hawawakamati kuwapeleka mahakamani
Something is not right somewhere

Tena hadi majambazi wengine "wanaugua ghafla na kufariki" kwa maradhi yaliyokua yanawasumbua
 
Kama ni kweli majambazi kazi nzuri polisi hakuna kucheka na nyani,mwizi wa cm tu kitaa anauwawa wao nani waende mahakamani?
 
Back
Top Bottom