Sijajua kama ulikuwa na gari ama la, lakini iko hivi, hakikisha kama unaendesha gari uwe umefunga vioo vyote na umeweka lock za milango, wapo wanaojisahau kuweka lock za milango, epuka kushika simu gari inapokuwa imesimama, hii unajenga mazingira ya vishawishi kwa muhalifu kukushambulia, iwapo hauna gari epuka kutembea sehemu ya giza ama kuongozana na watu usiowafahamu na ukawa uko karibu yao, weka mazoea ya kumtumia dreva unayemfahamu akufate eneo lako la kazi kama usiku umeenda sana, hii ni kuanzia saa moja usiku na kuendelea. Maeneo hatarishi ni mengi sana kwa Dsm, usiamini kokote kwa kipindi hiki cha uchumi kuwapindia watu, hapo mbeleni uhalifu utazidi sana maana wahusika ambao ni polisi ni kama wameliweka pembeni swala la kuwadhibiti waporaji na zaidi nguvu zao wamezielekeza kudhibiti raia asiye hata na silaha.
Pole sana mkuu.