Dar: Majambazi yapora na kuua

Dar: Majambazi yapora na kuua

Ugumu wa maisha unawasababisha binadamu kuwa kama wanyama!! Hao watu inaonyesha wamemfuatilia tangu bank, ipo haja ya kuongeza umakini unapoenda kuchukua hela bank sio sawa kama utachukua hela openly(dirishani) ni vyema ukichukua kwa Siri wateja wengine wasione!! Hii habari imenigusa coz hata mie niliwahi kufuatiwa na watu nikiwa natoka M-city CRDB na mil 12 niliendesha mpk kituo cha polisi Mwenge then nikaomba escoat!!! R.I.P dada
 
It's very sad!! R.I.P
Ila mleta taarifa umejuaje kama zilizochukuliwa ni milioni kumi wakati waliozichukua wametokomea?
Aisee umejuaje? Hili swali liko poa sana, mtoa mada anatakiwa aisaidie police, kajuaje yule mama katoka bank, ana ten milion?
 
Majambazi yapora mama mmoja kiasi cha shilingi milioni kumi muda mchache uliopita na kutokomea kusikojulikana. Tukio hilo limetokea leo saa 11:16 jioni inavyosemekana mdada huyo alikua akitoka benki ya CRDB tawi la Uhuru ambapo majambazi yakiwa na pikipiki yalikua yakimfuatilia, alipotoka tu wakaligonga gari lake makusudi ndipo dada huyo
aliposimama ili angaalie nani kagonga gari yake ambapo jambazi mmoja alishuka na kumpiga risasi ya kifuani na kutokomea na kiasi hicho cha pesa.

Mpaka tunaingia mitamboni hakuna habari yoyote ya kukamatwa kwa wahalifu hao.

Kwa hisani ya audifacejackson blog

Du Huko kwetu Kimara Garage alfajiri ya kuamkia leo majambazi wamevamia na kuwakata vichwa walinzi wawili kweli inatia simanzi sana,kuna haja ya JWTZ kufanya kazi ya kulinda mali na raia wa nchi hii Jeshi la Polisi limeshindwa kazi
 
Na mdada aliuawa ? Mhh jamani source of info zingine tuwe makini waweza saidia polisi faster ukarudi huna meno na kucha !!!
 
Back
Top Bottom