Bantu Mhagama
Senior Member
- Feb 15, 2017
- 104
- 127
intellejensia ya polis embu mufanye mambo mengine ya maana hasa suala la mauaji Kibiti....Ukachelo wenu unaonekana kwenye mikutano ya wapinzani tu mambo mengine intellejinsia yenu hatuielewi.
mwenyewe hawezi kuishi bila kiki hata kama ni kunywa maji ya mvua yaliyotuama kwenye dimbwi!Hivi jamani haya mambo ya Bashite si yalishaisha? naona yanarudi kwa kasi...kulikoni tena?
Umeonaee maana maumivu ya Karusha live Dar mpya hayajaisha...Sirro anawatafutia nini Clouds? Si awaache? Wao walisema wanataka kuombwa msamaha hawataki kesi wala kumshitaki Bashite, yeye anawalizimisha kwa nini ? Kama Bashite Anaona hana kosa si basi wakae kimya
Kabisaaa,na clouds nao hawana msimamo watamsafisha tu.naona njia ya kumsafisha Bashite inaandaliwa
Matukio mangapi ya jinai yanayomalizika nje ya mamlaka ya Polisi..? Utamlazimisha victim akatoe taarifa polisi hata kama yeye ameamua kusamehe..? Halafu toka siku ya kwanza Clouds hawakuwa na nia ya kuendelea na hii kadhia.. Nashangaa tuu Sirro kuibuka nalo leo.. Kama hana kazi aende akasaidiane na Polisi wengine kibiti huko..Uvamizi ni tukio la jinai. Na jinai iko chini ya mamlaka ya Police. Hivyo Clouds wanatakiwa watoe ushirikiano. Kama ni kuombana radhi kwa nini hawakuyamaliza nyuma ya pazia?
Matusi yako wapi hapo?ibambasi huwezi kutoa maoni bila matusi
Hujakosea Mkuu.Anajikosha. Wanatafuta namna ya kulizima ili lisiendelee kusemwa kwenye media.
Kama hawakuwa na nia kwa nini walisambaza taarifa?Matukio mangapi ya jinai yanayomalizika nje ya mamlaka ya Polisi..? Utamlazimisha victim akatoe taarifa polisi hata kama yeye ameamua kusamehe..? Halafu toka siku ya kwanza Clouds hawakuwa na nia ya kuendelea na hii kadhia.. Nashangaa tuu Sirro kuibuka nalo leo.. Kama hana kazi aende akasaidiane na Polisi wengine kibiti huko..
ukimwambia akili juu chini ni tusi.Matusi yako wapi hapo?
Hahaha.... Mkuu mbona watakuchukia. Kweli wanamgambo wa kibiti hawashikiki.Hawa kiboko yao kibiti
Ndio hivyo tena. Ushazaliwa Bongo. Nchi ile ni bongolala.Wanapeleleza nn sasa......
Si watumie ile report ya nape inatosha mbona wanatifanya watanzania kama wajinga sana
Hiii ni dharau tena kubwa alafu eti mwanasheria atizame kama ata peleka kesi mahakamani au lah
Daaaah ina pain sana ila hakuna namna ndo nshazaliwa tz ntafanyaje ss
Lakini kutoa malalamiko polisi sio automatically ndio umefungua kesi. Phase 1. Wamewasilisha malalamiko Yao. Phase 2,wanatakiwa kutoa maelezo na vielelezo vya kujitosheleza kuhusu kuvamiwa. Unajua mtu kuonekana kwenye video anaingia na kutokea kwenye jengo sio necessary awe kavamia. Clouds wenyewe walisema jamaa Alikuwa anatia team kwao mara nyingi, sasa Kuna ushahidi gani kuwa clips zile ni uvamizi na sio tríp zake za kawaida hapo clouds ?Ingekuwa uvamizi huo umefanywa na kiongozi wa upinzani, angekuwa ashafungwa toka siku ile ile ya uvamizi bila hata kusikilizwa mahakamani. Sirro naye vyeti vyake vihakikiwe.
Kamanda wa Polisi Kanda Maalumu ya Dar Es Salaam, Simon Sirro amewataka uongozi wa Clouds Media Group kushirikiana na jeshi la polisi katika upelelezi wa tukio la uvamizi wa kituo chao cha matangazo.
Akiongea na waandishi wa habari leo Sirro amesema kesi yoyote inahitaji ushahidi na uvamizi wa Clouds bado upelelezi wake unaendelea ukikamilika utapelekwa kwa wakili wa Serikali ili aone kama anaipeleka kesi hiyo mahakamani au kutoipeleka.
"Ndugu zetu wa Clouds watoe ushirikiano kwa mpelelezi wa kesi yao, wao wanataarifa za kutusaidia kukamilika kwa upelelezi ila nasi tuweze kuipeleka katika hatua inayofuata. Na sio kwamba tukio limesahaurika bali upelezi wake unaendelea," amesema Sirro.
Chanzo: mwananchi