DAR: Kamanda Sirro awataka Clouds kutoa ushirikiano

DAR: Kamanda Sirro awataka Clouds kutoa ushirikiano

Pelekeni ushahidi wa kuvamiwa, ile clip haina any conclusive evidence ya uvamizi, ni kama clip ya joti na tanzazo la mtandao wa simu, hamna kitu!
Clouds kama WAMEVAMIWA watoe ushirikiano!

Poleni sana sana sana.Jamaa yako alikuwa anajua anakuwa recorded kwa kila kitendo na akajua akiwatisha wataifuta ile episode majanga akakutana na Muhaya ambaye hasikii lwa kuambiwa akaishia alipoishia,anachotakiwa kufanya si kumtukana Ruge ,bali kuomba radhi period.

Hatakati hata kwa jik
 
Kwani Clouds wao wametaka kumpeleka mtu mahakamani..? Nadhani kwao limeisha na wanachosisitiza wao ni wa Bashite kuomba radhi kwa tukio lile.. Sasa huyu Sirro hii ameitoa wapi..?
 
Upelelezi gani wanautaka wkt video zipo wazi kabisa
 
Anakaribia kustaafu? Naona anatafuta kiki kwa kipenzi cha bwana mkubwa ili apate udc.
 
Poleni sana sana sana.Jamaa yako alikuwa anajua anakuwa recorded kwa kila kitendo na akajua akiwatisha wataifuta ile episode majanga akakutana na Muhaya ambaye hasikii lwa kuambiwa akaishia alipoishia,anachotakiwa kufanya si kumtukana Ruge ,bali kuomba radhi period.

Hatakati hata kwa jik
Mwambie apeleke hiyo full clip ndo inayotakiwa ili Makonda ikiwezekana aende akaozee segerea, hiyo muhaya kaanza kumgeuka Makonda baada ya Makonda kuanzisha vita na mateja na wauza unga!
 
Ukistaajabu ya musa utayaona mengi kwa kwel.

Leo kwa masikio yangu nimemsikia 'Zero' akisema kwa nin Clouds hawatoi video ya CCTV cam ya nin kilitokea kule ndani, najiuliza tu kama kweli huo uchunguzi unafanyika 'kwa nia ya dhati', kwa nin wasiwatake Clouds watoe ile video ya CCTV kule ndan, nafikir itawasaidia sana kwenye uchunguzi wao, na clouds wakikataa wawaburuze mahakamani kama jinsi walivyofanya kwa Maxence Melo na wenzake ..
 
Kamanda wa Polisi Kanda Maalumu ya Dar Es Salaam, Simon Sirro amewataka uongozi wa Clouds Media Group kushirikiana na jeshi la polisi katika upelelezi wa tukio la uvamizi wa kituo chao cha matangazo.

Akiongea na waandishi wa habari leo Sirro amesema kesi yoyote inahitaji ushahidi na uvamizi wa Clouds bado upelelezi wake unaendelea ukikamilika utapelekwa kwa wakili wa Serikali ili aone kama anaipeleka kesi hiyo mahakamani au kutoipeleka.

"Ndugu zetu wa Clouds watoe ushirikiano kwa mpelelezi wa kesi yao, wao wanataarifa za kutusaidia kukamilika kwa upelelezi ila nasi tuweze kuipeleka katika hatua inayofuata. Na sio kwamba tukio limesahaurika bali upelezi wake unaendelea," amesema Sirro.

Chanzo: mwananchi
Sirro ni mteule wa rais na makonda ni mteule wa rais ambaye anasema rank yake sawa na PII EM,sasa Sirro ataweza kumgusa makonda?Na pia Bossi wa Siro ni Makonda kwenye ulinzi na Usalama DSM
 
mwanasheria yupi atakayempeleka bashite mahakamani? labda aje Fatou Bensouda kutoka ICC!
 
Sirro: "Clouds wanatakiwa kutoa ushirikiano"

Dar Es Salaam. Kamanda wa Polisi Kanda Maalumu ya Dar Es Salaam, Simon Sirro amewataka uongozi wa Clouds Media Group kushirikiana na jeshi la polisi katika upelelezi wa tukio la uvamizi wa kituo chao cha matangazo.

Akiongea na waandishi wa habari leo Sirro amesema kesi yoyote inahitaji ushahidi na uvamizi wa Clouds bado upelelezi wake unaendelea ukikamilika utapelekwa kwa wakili wa Serikali ili aone kama anaipeleka kesi hiyo mahakamani au kutoipeleka.

"Ndugu zetu wa Clouds watoe ushirikiano kwa mpelelezi wa kesi yao, wao wanataarifa za kutusaidia kukamilika kwa upelelezi ila nasi tuweze kuipeleka katika hatua inayofuata. Na sio kwamba tukio limesahaurika bali upelezi wake unaendelea," amesema Sirro

Kamanda Sirro , Je uko serious na kazi yako ???
 
Back
Top Bottom