DAR: Jeshi la Polisi Kanda Maalum kuwachukulia hatua kundi la kisanii la Orijino Komedi

komedi.jpg

Kosa lao kubwa ni kutumia mkanda wenye bendera ya taifa ambao itabidi waeleze wametoa wapi.

Halafu mmoja wao (kati) amejipa cheo cha usajini yaani V tatu! , na pia wana mikanda ya filimbi inayopita kwenye mifuko ya mashati.

Lakini kama wangevaa hizo nguo tu na kutafuta mkanda wa aina nyingine, isingekuwa tabu.

Hata kofia walizotumia si za kipolisi kabisa.

Ila ukiangalia sana hutaweza kutofautisha sare za hao Ze Comedy na zile za polisi ukiondoa viatu vyenye rangi tofauti.

Mimi niliwahi kupitia mafunzo ya JKT miaka ya mwanzo ya 90s.

Kuna siku nilikuwa nyumbani kwa rafiki yangu kwa mapumziko ya mwisho wa wiki, nikiwa nimevalia magwanda ya JKT, nikatoka kidogo na rafiki yangu ambae alikuwa akiishi maneno ya mitaa ya Magole Upanga ambao upo karibu kabisa na makao makuu ya JKT.

Lakini nilijisahau na kuchomoa koti langu la juu kwa kuwa nilitaka kuwa "relaxed", na mkanda nilitoa basi nikakatiza kwenye geti la jamaa, ambao bila mimi kufahamu walikuwa wakinitamani kwa sana ili wanitie adabu kwa utovu wa nidhamu na kwamba nilikuwa nalidhalilisha vazi rasmi la kijeshi.

Yaliyonikuta hapo ndipo nikagundua kuwa haya mavazi yana thamani sana kwa ama jeshi la JWTZ au polisi na yalindwa na sheria.

Hivyo nazungumza kutokana na uzoefu wangu na haya mambo ya hizi sheria za haya mavazi.
mkuu, umeichunguza hiyo mikanda yenye bendera ya taifa pamoja na hiyo ya filimbi umekuta ni ORIGINAL au FAKE? kwa hiyo mmeishawakamata au bado mnawahoji? labda tuanzie hapa ili unifafanulie vizuri.
 
Walifanya uhalifu?
Sasa huu ni Uonevu Wa hali ya juu. Walikuwa harusini wakiburudisha, then wakabadili wakavaa suti. Hata burudani za amani kabisa tena ukumbini zinaingiliwa hii ni too much jamani. Msiitie DOA harusi ya Masanja
 
View attachment 382631
Jeshi la Polisi Kanda Maalum kuwachukulia hatua kundi la kisanii la “ Original Comedy” kwa kuvaa mavazi yanayoshabihiana na sare za polisi.

Taarifa iliyotolewa na Msemaji wa Polisi, Advera Bulimba ameeleza kuwa wanatoa onyo kali kwa mtu ama kikundi chochote kuacha kutumia mavazi yanayofanana na sare zinazovaliwa na majeshi ya ulinzi na usalama hapa nchini na atakayebainika hawatasita kuchukua hatua kali za kisheria dhidi yake.

Hii hapa chini ni moja ya vichekesho walivyofanya wakiwa wamevaa nguo zinazodaiwa ni Sare ya Polisi.

Watoto wa magufli awo.. kesi imekwisha iyo
 
Wenzetu wana sheria inayoruhusu mavazi hayo kutumiwa katika kutengeneza filamu au kufanya michezo ya maigizo.

Kote Marekani na Ulaya zipo kampuni kabisa tayari kukodisha sare, silaha, magari, na kila aina ya kifaa kinachoshabihiana na majeshi au polisi na hata makomandoo katika kufanikisha utengenezaji filamu hizo.

Pia zipo studio maalum huko Hollywood na kwingine kwa makusudio hayo.

Lakini haya yote yanafanyika kwa kufuata sheria kali ambayo inaongoza matumizi ya vifaa hivi.

Tanzania bado hakuna kampuni za aina hiyo wala sheria inayoruhusu mambo hayo.

Ila ipo sheria inayopiga marufuku uvaaji au utumiaji wa sare au vifaa hivyo, that's it.

Ni mpaka tukifika walipo wenzetu ndipo (labda) tunaweza kufunguka kimtazamo, yaani kuona kwamba hayo mambo ni ya kawaida kabisa.

Kinachotakiwa kufanyika ni kuruhusu matumizi ya hayo mambo kwa kuweka "strict guidelines" na leseni kwa ajili hiyo.

Ila sidhani kama itawezekana kwa Tanzania.
Well said
 
Maujinga tu.Mbona wasanii marekani wanavaa nguo za jeshi, wanafanya sinema White house?
Jeshi letu limekosa kazi ya kufanya.Hawa ni wasanii na kazi yao ni kuigiza chochote katika hali ya uhalisia.Polisi wajikite katika kulinda raia.
Polisi wanatakiwa wawe karibu na raia wema na sio kuogopwa kama Mungu.
 
Ok, lakini mwisho wa siku wataachwa waendelee na maisha yao

Mkuu, ni kweli wanaweza achiwa ila ukweli ni kuwa wanapaswa kuchukuliwa hatua kali na hii itaonesha utendaji wa jeshi la polisi, kwa sababu hii ni sawa na yule anayezitumia kuibia watu mtaani anakuwa na makosa mawili la kuimiliki sare na kuiba

sasa KWA KOMEDI HAWA WAMATUMIA SARE ZA POLISI NI KOSA 1, LA PILI , KUZIVAA KATIKA SHEREHE YAANI KATIKA KUMBI ZA STAREHE AMBAPO HATA ASKARI NAAMINI HARUHUSIWI KUZIVAA MAHALI HAPO PA STAREHE KAMA WALIVYO FANYA HAWA JAMAA.

Ila mimi , nasubiri nione, UFANISI WA JESHI LA POLISI KATIKA HILI LA HAWA WANAKOMEDI WALIOVAA HIVI.
 
‪#‎MwananchiLeo‬

POLISI KUWACHUKULIA HATUA ORIGINAL COMEDY KWA KUTUMIA SARE ZAO

Jeshi la Polisi Kanda Maalum kuwachukulia hatua kundi la kisanii la “ Original Comedy” kwa kuvaa mavazi yanayoshabihiana na sare za polisi.


Taarifa iliyotolewa na Msemaji wa Polisi, Advera Bulimba ameeleza kuwa wanatoa onyo kali kwa mtu ama kikundi chochote kuacha kutumia mavazi yanayofanana na sare zinazovaliwa na majeshi ya ulinzi na usalama hapa nchini na atakayebainika hawatasita kuchukua hatua kali za kisheria dhidi yake.
Hivyo ni vitisho vya kawaida,ambavyo mtu anayefahamu kanuni na taratibu wala hawezi kujali kwa sababu hakuna hatua yoyote "ya maana" inayoweza kuchukuliwa kwa "comedians" hao.
Hakuna kati yao aliyevaa safe ya polisi pale! Kofia nyeusi, lakini hazina "croun" yaani bembo ya jeshi la polisi. Mikanda waliyovaa siyo ya jeshi la polisi,ingawa zina rangi ya bendera, lakini mikanda hiyo imegeuzwa "upsidedown" ambapo kwa nidham ya mavazi ya kijeshi haivaliwi hivyo.
Kunakitu kinaitwa "hakimiliki" pia na kununua na kuomba ama kupewa risiti. Nitaeleza:
Hao wachekeshaji hakuna kati yao aliyevaa sare ya jeshi la polisi. Hapo utaandaa mashitaka yepi? Kufanana? Je jeshi la polisi lina hakimiliki ya mavazi yote nchini yenye rangi ya khaki mpauko? Je ukienda madukani "kwa walipakodi" hakuna majora yenye vitambaa vyenye rangi hiyo vinavyouzwa kihalali?
Je hao wachekeshaji,sehemu walikoyapata mavazi hayo hata iwe kwenye mitumba hawakununua na kuomba risiti?
Nikwambie kama wamenunua nguo hizo kwasababu zinapatikana madukani na kupewa risiti, wallah kesi hiyo haiwezi kuchukua dk.5 mahakamani,kabla ya kumsikia hakimu akisema neno la mwisho "........naifuta kesi hii" na kufuatia sauti kuuubwa"Coooooooort".
 
Wawaone huruma maana hawa jamaa walikuwa ccm na waliwapigia kampeni magamba....

Ova
 
Yaan kusema ukweli huyu jamaa anaiharibu hii nchi..sio siri!!
Binafsi sasahv mimi siipendi hii nchi basi tu....natamani kuhama!!
 
ELIMU ELIMU ELIMU KWENYE JESHI LA POLISI WENGI LA 7
ukiambiwa uthibitishe kauli yako sijui kama utathibitishe angalia sana usije kujikuta mia tano ya bando imekutia kwenda jela hasara ni kwako na familia pamoja na wanaokutegemea
 
Back
Top Bottom