Dar inawapotezea watu muda

Sasa ndo useme Dar Kwa watu wa Aina yako ndo inawapotezea muda sio Kila mtu inampotezea muda.Kuna watu inawapotezea muda na kuna watu haiwapotezi muda.Isiwe general kuwa Kila mtu inampotezea muda.Sema baadhi ya watu
 
Mwanza nalo ni jiji kwani? Umeshajibiwa Kwa takwimu za NBS Mwanza wanaishi Kwa maisha ya dhiki hata Pato lake ni dogo ukilinganisha na Dar
Lakini mbona unakimbia swali langu we mzee wa Tandale ?, nionyeshe maeneo ya ovyo ya Mwanza , we si ulikuwa unajitia mjuzi ?
Dar nalo jiji kwani vinyesi kurandaranda juu ya barabara na uchafu ndo mnaona sifa eti ?
Hebu angalia hiyo kariakoo ilivyo ovyo kabisa mvua ikinyesha kidogo tu ni disaster , uchafu kwenda mbele
 
Hakika umesema ya kweli, nilikaa miaka 8 bila bila, kodi, usafiri, chakula, kuamka na kurudi mida mibovu, joto lisilo rafiki na mtu. Ila tangu ning'atuke nashukuru kwamba maisha haya ya sasa ningeishia kuyaona kwa wengine tu! Sitaki kusema nina nini na nini, ila amini kuacha maisha ya Dar na kuamua kuja mkoa, hakuna hata rafiki aliye kubaliana nami, sasa 'gap' halizibiki tena labda awe fisadi tu! Ukweli mchungu, ila watu ambao tuliwaacha mikoani ndo huja mara nyingi kununua magari huku sisi tuliokua wa 'mjini' tunawakwepa. Mwenye macho haambiwi tazama.
 
Ukiegemea kwenye hesabu za probability, uwezekano wa kutoboa ukiwa Dar ni mkubwa kuliko mkoani. Magari na majumba mazuri yako Dar. Mkoani mtu anayetembelea shangingi ni mkuu wa mkoa pekee, whats ur chance of getting one?
Hapa ni uongo . Inategemea mkoa gani . Mikoa kama arusha matajiri wanatembelea magar ya bei mbaya kuliko hata ya serikali na si moja. Yako mengi.

Labda hiko mikoa simiyu huko ndani ndani.

Chance ya kufanikiwa haipo dar tu bali iko sehemu yoyote utayoenda ishi. Mipango yako , nanidhamu ya muda vitwkufikisha mbali
 
Ina depend ...ila kuna majiji yana gharama juu za maisha kuliko dar
 
Sasa ndo useme Dar Kwa watu wa Aina yako ndo inawapotezea muda sio Kila mtu inampotezea muda.Kuna watu inawapotezea muda na kuna watu haiwapotezi muda.Isiwe general kuwa Kila mtu inampotezea muda.Sema baadhi ya watu
Mkuu kwan tunajadili au tunashindana ! Mi nime muunga mkono tu mtoa mada , ambaye kimantiki hoja yake imejikita kwenye majority ya watu wa dar , kuna wachache kama wewe ambao pengine Dar mnaimudu.
Maendeleo ya watu na vipato vyao, Mara nyingi yana structure ya pyramid ! yaan chini ni wengi , na juu ni wachache , unatakiwa utafute pyramid fupi ili uweze kuwa juu haraka ,
 
Washamba hatimaye wameumbuka nyumbani...wa Ocean Road bado tupo sana, maana hapa ndoio home
 
Ukiegemea kwenye hesabu za probability, uwezekano wa kutoboa ukiwa Dar ni mkubwa kuliko mkoani. Magari na majumba mazuri yako Dar. Mkoani mtu anayetembelea shangingi ni mkuu wa mkoa pekee, whats ur chance of getting one?
It's not true my dear, mikoa michache sana labda. Kwa sasa vijana wameamka, ndio maana wengi wa mjini wanaona aibu kurudi mkoa maana alikua na sifa za 'naishi Dar' ila akirudi mkoa kusalimia anashangaa kwa namna alivyo nyuma kiuchumia, kwa hiyo kurudi tena mtihani.
 
Kwa mujibu wa NBS wakazi wa Dar asilimia kubwa wana unafuu wa maisha kulinganisha na mikoa yote Tanzania. Hizi ni takwimu hizo nyingine ni porojo tu na ndio maana watu wanaongoza kukimbilia Dar na si kinyume chake.
 
Siyo kwamba Mwanza hakuna Sehemu za changanyikeni,naamini zipo.Tofauti ni population,sehemu yenye population kubwa haiwezi lingana na sehemu population ndogo.Ndiyo maana unalinganisha Tandale tu lkn hujaweza kwenda linganisha zile zenye ubora za Dar maana unajua kabisa kuwa Mwanza itakuwa nyuma.Igogo,Mabaytini,Nyanshana,Iseni,Nyakato Sokoni, ni kwa kisasa Kwa kadiri yako.Unapolinganisha Kwa ubaya linganisha na Kwa uzuri pia.Ni kama mimi niseme Kijijini kwetu hakuna sehemu ya Changanyikeni kama Tandale,sasa itakwepoje wakati kule ni kijijini? Huko Tandale unakokuona Uswahilini ndio sehemu expensive zijazo,
 
Maisha hayana formula moja mkuu.Kuna mwingine yupo Dar katoboa kuna mwingine yupo nje ya Dar katoboa Kila mtu na sehemu yake ya kutoboa.Dar kuna maskini wengi tu wa kutupwa mikoa mingine pia kuna maskini wengi tu.Kila mtu ana sehemu inayomfavor kuishi
 
True chance ya kufanikiwa haipo sehemu moja tu
 
Tuache kudanganyana,kila mtu ana sehemu yake ya kutoboa na hiyo sehemu haipo common Kwa Kila mtu.
 
Sitapingana na hilo, kikubwa ni kuangalia ni aina gani ya shughuli unataka kufanya, ni maisha ya aina gani unataka kuishi, kama ndivyo hiyo uliyopo ni sehemu sahihi kwako? Kama utaweza kuyatawala mazingira na kuwa huru bila shaka kambi popote.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…