Dar inawapotezea watu muda

Duh...kwahio huko mkoani wote mnaishi maisha kama peponi? Hebu tafuta ripori ya NBS ujionee.
Jamaa wanajifariji kweli wanahisi mkoani Kila mtu katoboa wakati sehemu kibao watu wanachangia maji/Dimbwi na Ng'ombe.
Ndiko ambako utakuta wananchi wake Kila siku wanaomba msaada serikali iwasaidie kujenga choo cha zahanati ya Kijiji.Wakitaka kupitisha harambee unakuta vikao wanakuja kufanyia Dar
 
Kwa mujibu wa NBS wakazi wa Dar asilimia kubwa wana unafuu wa maisha kulinganisha na mikoa yote Tanzania. Hizi ni takwimu hizo nyingine ni porojo tu na ndio maana watu wanaongoza kukimbilia Dar na si kinyume chake.
Na Kwa wale waliokuwa wanasikiliza vizuri walimu wao darasani kwenye topic ya migration moja ya sababu kubwa ya migration. Ni watu kutafuta unafuu wa maisha na huduma za binadamu Sasa tujiulize watu wanamigrate kwenda wapi sanasana,kama sio kuja Dar?
 
Hapa tunachanganya vitu viwili kwa wakati mmoja,,mtu anayetafuta maisha DAR,,wakati huo huo wazazi wake wanamijengo dar,,na mtu anayetoka mkoani,,kuja kutafuta,,,,huku wazazi wake wakiwa hawana asset yoyote dar,,hapo kuna tofauti kubwa ya maumivu yautafutaji,,,,,,chamsingi,,nikutokukata tamaaa,,maisha kokote
 
Sijasema wote, ila wengi wao. Cha msingi fanya unachopenda utafanikiwa, yatawale mazingira uliyopo.
Hiyo ndo point kuwa maisha ni popote ambapo wewe unaona unapamudu.Dar kuna matajiri Dar kuna maskini Dar kuna Raha Dar kuna shida zote.Dar pa rahisi Dar pagumu pia,kazi kichwani mwako.Hiyo mikoa ambayo maisha ni mepesi sehemu zote kuzuri tu na kufanikiwa nje nje sijui ni ipi
 
Ukijua kwann maisha ya huko ulipo yamekuwa rahisi utakuja na mrejesho wa kuishukuru Dar kwa kukupa elimu ya miaka mitatu
 
Kwenye kutafuta kuna hitaji kujitoa mhanga
 
Kwa mujibu wa NBS wakazi wa Dar asilimia kubwa wana unafuu wa maisha kulinganisha na mikoa yote Tanzania. Hizi ni takwimu hizo nyingine ni porojo tu na ndio maana watu wanaongoza kukimbilia Dar na si kinyume chake.
Hyo ripoti waifanye na mwaka huu!! Inaweza kuwa vice versa
 
Hyo ripoti waifanye na mwaka huu!! Inaweza kuwa vice versa
Kuna kipi kimefanyika kitakachobadili hali iliokuwa mwaka jana na leo? Mabadiliko huwa madogo sana.
 
Hahahaaa eti sehemu expensive zijazo , a hell on Earth !
 
Binafsi mi nimeondoka dar mwaka jana mwanzoni na sikuwa na mpango wa kuishi mkoani!! Nilikuwa nimeenda kupiga ishu flani then nigeuze , lkn kadri nilivyozidi kukaa nikashawishika kuwa kuna possibility ya kuishi mkoani na maisha yakawa mazuri tu! Now nipo mwanza na nishahamisha makazi ya kudumu na sina mpango wa kurudi dar tena!!!
 
Dar kwa fursa sawa kwa kuishi No. Naamini kungekua kuna usafiri affordable na realible lets say bullet train kutokea Dar to Arusha au usafiri wa ndege usingekua anasa kwamba hata mtu wa kipato cha kati angeweza kuafford watu wengi wasingeishi Dar.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…