connections
JF-Expert Member
- Apr 27, 2013
- 2,840
- 3,908
Nimepanda basi la DAR EXPRESS toka DAR kwenda ARUSHA kwanza kauli za wakatisha tiketi pale UBUNGO ni za ajabu hasa (Mr. Mamkwe) kuingia garini abiria tunatukanwa ovyo ovyo kisa kuuliza kwa nini Dereva anaenda mwendo kasi ulipititiliza (Dereva Mr. Robert), kufika hotelini kwao chakula kibovu/kiporo na bei ya juu kuuliza nimeambulia kuambiwa kama hutaki ACHA, chooni nako uchafu umejaa mpaka juuu. Hakika zama za DAR EXPRESS zimekwisha