Dar es Salaam tuitakayo, Jiji la pingili!

Dar es Salaam tuitakayo, Jiji la pingili!

Mshana Jr

Platinum Member
Joined
Aug 19, 2012
Posts
360,940
Reaction score
831,459
(Tusameheane kwa post za mfululizo)

Nimekutana na mabango makubwa ya kampuni ya matangazo ikiwa na mapicha makubwa kubwa ya viongozi wa kisiasa wakipanda miti na nyingine ya barabara iliyojaa mnazi ile ya mapambo

Nikajiuliza hii ndio Dar tunayoitaka kweli? Mnazi kwenye barabara chache za lami! Vipi miundombinu yote kwa ujumla?

Pale jangwani ndio kama kuingia kwenye moyo wa nchi au jiji vipi vile vibanda? Njia zote kuu za kuingia Dar zimesongwa na shughuli za biashara zilizo shaghala baghala, hakuna mpangilio kabisa mikaa chips mafundi washi mafundi magari machinga vitoroli nk nk

Kilichoonekana kwenye mabango ni upuuzi mwingine uliotengenezwa kwa gharama kubwa sana. Dar tuitakayo ni multibillion project sio hizi slogan za kukurupuka, mitaa kibao ya jiji barabara ziko hoi mitaro ya maji machafu iko hoi hivi vitu viwili tu kuviweka vizuri ni mamilioni ya dola na mpango madhubuti!!! Leo tunaonyeshwa picha za kutengeneza mtandaoni.

Vizuizi vya pingili ni fasheni mpya tuliaza kuona strabag lakini kwakuwa wenzetu wale walikuwa na mpango madhubuti, vya kwao havichukizi kivile
Sisi nasi tukaiga zilianza barabara ya Lumbuma kule watu wanakokatiza kusikohusika zikapigwa pingili za miti na kupakwa rangi na uzio wa Seng'enge! Ilikuwa haina namna ili kulinda bustani zetu katikati ya mji

Wenye kuona fursa wakachanganya na za kwao, kwenye maghala yao kuna tani za mabomba haziuziki, fasta ukatengenezwa mkakati pingili zikawa za mabomba ya chuma badala ya miti! What a nice deal! Zikapakwa na rangi ya Taifa sasa sijui zikichafuka nani ataziosha au zikioza na kuharibika?

Kilichonisikitisha sana ni pingili za barabara ya Sam Nujoma kutoka mwenge kwenda ubungo! Kwa kasi ya ajabu yakachimbwa mashimo na pingili zikafukiwa hata maeneo yasiyohitaji pingili, bwana mmoja akatangaza kuwa ukigonga pingili moja unalipa 5 , kesho yake kona ya mlimani city jamaa mmoja akazilaza kama kumi   

Kibaya zaidi bustani ya ile barabara ilikuwa imejazwa udongo uliotengeneza vifusi ila waweka pingili hawakulizingatia hilo pingili zikawekwa na rangi na minyororo juu! Siku chache baadae wakagundua kosa na kuleta excavator kuja kuondoa vifusi! Lilianza kidogo tu pale mwenge likachemsha kwasababu ya pingili

Upuuzi huu wa kukurupuka bila mipango umeleta gharama kubwa na umegeuka kichefuchefu, pingili nyingi zimegongwa mvua ya wiki iliyopita imezichafua rangi sasa sijui hii ndo Dar es salaam tuitakayo? Tusubiri mwakani sio mbali
 
1477247449006.jpg
1477247453726.jpg
 
Kiujumla hatuna tunachokiweza zaidi ya porojo na makelele. Mtafute kiongozi yoyote muulize kama Taifa kwa miaka 50 tumefanikiwa wapi ambapo tunaweza kujisifu bila kuwa nakigugumizi wala kupepesa macho.
 
Wakati mwingine huwa nawaza sipti jibu, ni sshule gani walisoma viongozi wetu, mbona sshule nilizosoma wanafunzi walikuwa na amawazo mazuri sana. Wanalolifanya ni jambo zuri lakin yapo ya msingi walitakiwa kuanza nayo
 
Kibaraka namba moja wa ccm nchi hii ni Mbowe, Tanzania inajua na Dunia inajua.

Kila ukifika uchaguzi anateua fisadi kutoka ccm awe mgombea wa chadema!!
 
Tuache kulalamika lalamika kama wanawake bhanaa.., haipendezi kwa kweli.., sure nawaambia. Hiki kimradi mnachokibeza kimependezesha sana mji na kimeonyesha mwanga kwa miaka ijayo. Kazi kulalamika tu..
Aisee! nawahurumia mama zetu kwa kuwa indicator ya mifano mibaya kila wakati
 
Duuuu, mbona mim naona kama zitakua mwarobaini wa kukatiza ovyo barabara lkn pia zitasaidia kulinda bustan zetuu?? Anyway sikuhiz kila jambo la serikali linaonekana baya! Hata Bombadier ziliitwa mapanga boi
Sijapingana na hili kabisa labda tu kwakuwa umenisoma kwa haraka...ni nacho maanisha ni kwamba ingependeza zaidi kama hili jambo lisingefanywa kwa kukurupuka na kuna maeneo haya hitaji kabisa hizo pingili. ...
Naamini umefika kimara mwisho kwenye stand ya Strabag na kile walichokifanya pale! Ishu ya kukatiza barabara pale imedhibitiwa, lakini angalia wamefanya penye uhitaji tuu na imependeza sio barabara yote
Mwanzoni mwa post nimezungumzia kuhusu Lumbuma na kupongeza na nikaja kuongelea kuhusu Sam Nujoma, na kile kilichofanyika pale (nikijaaliwa nitaweka picha kesho isionekane kama napayuka na kukosoa bila ithibati
kwa ufafanuzi zaidi ni kwamba kilichopaswa kufanyika pale Sam Nujoma kwanza ni kuondoa vile vifusi vilivyotengeneza matuta na vilima (kumbuka pia hii ni tenda alipewa mtu ya kusafisha barabara lakini kwa uzembe na kubania pesa michanga ikawa haizolewi bali inalundikwa kwenye bustani na pembezoni mwa barabara)
Baada ya kuondoa hivyo vifusi na kutengeneza level ile ya asili vizuri then mashimo yale ya kusimika pingili yangechimbwa na kingefuatia kusimika pingili sasa .... kwa mtazamo wa kawaida pingili nzuri za miti au za plastic ngumu zingekuwa nzuri zaidi kama ungefanyika utafiti wa kutosha kuliko pingili za vyuma! Je huu sio mradi wa mtu?
Pamoja na hayo yote kilichofanyika ni kwenda kinyume nyume kiasi kwamba sasa levelling imekuwa shida kufanyika kwa tingatinga, kuna maeneo ya mawasiliano hasa upande zinapojengwa hostel kule imebidi ile kazi ifanyike kwa mikono kwakuwa bustani ni nyembamba
Ungefuatwa utaratibu kama nilivyoainisha hapo hakika matokeo yangekuwa mazuri sana na kwa gharama ndogo
 
Duuuu, mbona mim naona kama zitakua mwarobaini wa kukatiza ovyo barabara lkn pia zitasaidia kulinda bustan zetuu?? Anyway sikuhiz kila jambo la serikali linaonekana baya! Hata Bombadier ziliitwa mapanga boi
Mkuu ukitaka kumpa nafasi mbongo ili ufanyie kazi mawazo yake utachanganyikiwa.
 
Back
Top Bottom