Robert Heriel Mtibeli
JF-Expert Member
- Mar 24, 2018
- 38,845
- 90,306
DAR ES SALAAM NI JIJI LA VILAZA.
Na, Robert Heriel.
Sijawahi kuona wanafunzi vilaza kama wa Mkoa wa Dar es salaam. Wanafunzi wa Dar es salaam ni vilaza hujapata kuona popote dunia hii. Ni vilaza ambao hawajawahi kutokea tangu kuumbwa kwa dunia. Wapende wasipende. Huo ndio ukweli. Ninyi ni Vilaza tena wa kutupa. Mnalitia taifa aibu kwa sifuri zenu.
Unajua maana ya mwanafunzi kilaza?
Ipo hivi; Kilaza ni mwanafunzi ambaye uwezo wake wa akili ni mdogo hata umuwekee mazingira wezeshi bado atabaki kuwa na uwezo mdogo.
Kwa maana hiyo na nyinginezo zinalifanya jiji la Dar es salaam kuwa jiji la Vilaza waliotukuka.
Haiwezekani jiji kubwa hapa nchini lenye miundombinu yenye unafuu bado lishindwe hata kuwa top ten ya mikoa. Mbaya zaidi ndilo linaloongoza kwa sifuri zilizotukuka. Huo ni ukilaza.
Wala hatuna muda wa kuongea maneno matamu katika hili. Yaani usome Dar es salaam bado upate sifuri wewe ni kiazi mbatata.
Dar es salaam karibu kila nyumba inaumeme. Nini kinafanya watoto wasisome mpaka wapate sifuri kama sio vichwa viazi. Iko hivi. Kama mtoto sio kiazi basi mlezi ndiye kiazi. Mtoto apate sifuri ilhali kuna umeme. Anapataje sifuri kwa mfano kama sio uzembe. Na uzembe ndio ukilaza wenyewe huo.
Watoto wanshindwa kuamka usiku wa manane kusoma? Haya hata wazazi wanashindwa kuwaamsha hao watoto kama wao wenyewe hawajitambui? Usijesema kuna kelele. Hiyo sio kweli. Mji wa Dar es salaam unaanza kupoa mida ya saa tatu usiku. Huo ni muda mzuri kwa mwanafunzi kujisomea. Akipeleka mpaka saa saba. Au alale kisha amke saa nane mpaka asubuhi kila siku kamwe hawezi kupata sifuri.
Jiji lina Tuition center kila kona. Ukigeuka huku mchikichini, huku mapambano, kule sijui nini huko. Yaani Tuition kila kona. Haya tuseme mzazi hana Pesa ya Tuition. Hivi mtoto kweli unashindwaje kuwa na marafiki wanaosoma tuition badala yake marafiki zako ni wacheza vigoma na mdundiko. Sijui Beach boy, sijui panya Road yaani utumbo utumbo tuu. Alafu unakuja kulitia aibu taifa.
Hivi unapataje sifuri kwenye jiji ambalo kila nyumba inammiliki wa Smartphone kama sio Laptop kabisa. Hivi mnashindwaje kudownload notes na material mbalimbali ya kujisomea. Matokeo yake mnatumia simu kudownlooad Video za ponograph, kuchat Whatsapp, instagram, sijui imo, na Telegram.
Yaani unaishi Dar alafu unapata sifuri wewe kama sio kichaa ni nani. Hakuna mwanafunzi mwenye akili timamu ambaye atasoma Dar apate sifuri. hata hiyo division four haiwezekani.
Haiwezekani jiji lenye chuo cha taifa, chuo kikuu cha Dar es salaam - UDSM , vyuo vingine vingi tuu kama CBE, IFM, NIT, DIT, Ardhi, Muhimbili n.k alafu bado mtu anapata zero huo si upunguani.Sisi wengine wamikoani vyuo vikuu tumeviona tulivyomaliza kidato cha sita. Tukaja mjini tukanyuka misonge tukasepa. Ninyi mmebaki kushangaana hapo kama vichaa.
Ujinga ni pamoja na kutokujua matumizi ya rasilimali. Yaani jiji lenu lina vyuo kama vyote, mnashindwa kwenda kujifunza hata kwa kaka zenu wa chuo. Mnatia aibu kwa kweli.
Jiji la Dar es Salaam ndio jiji pekee lenye vitabu, vitini, na madesa kuliko mkoa wowote hapa nchini. Lakini shangaa ndilo linaloongoza kwa sifuri nyingi ambazo ni zaidi ya mara mbili kwa mikoa ya Kilimanjaro, Arusha na Iringa.
Nina uhakika jiji la Dar es salaam kama lisingekuwa na miundombinu wezeshi kama hiyo hakuna mwanafunzi ambaye angepata hata divisio four. Wote wangepata sifuri kwa sababu ni vilaza.
Jiji la Dar es Salaam hakuna changamoto ya usafiri. Kwa vile wamezoea mambo ya legelege utasikia kugombania daladala ni changamoto. Wewe ni kichaa kama utafikiri hivyo. Nenda mkoani uone wenzako wakitembea kilomita za kutosha zaidi ya masaa mawili na bado wakifika wachapwe bakora kwa kuchelewa. Wewe unatembea dakika mbili upo kwenye daladala huyo mpaka shule. Tena kwenye Daladala mnapiaga kelele wazazi wenu kwa sababu nao ni wendawazimu kama nyie. Yaani matoto yanapanda gari yanaanza kutukana, sijui hadithi ya msanii gani kafanya nini. Mara matusi kibao. Hapo kuna wazazi nao wanasikiliza kwa sababu nao ni walewale. Badala wawakanye ikiwezekana wawachape bakora za uhakika. Looh! Ndio mambo ya vilaza hayo.
Mkoani huwezi sikia ujinga ujinga kama huo. Nenda Misungwi huko, nenda muleba, nenda Rombo, Nenda Bukoba, Nenda Mbeya kama utasikia upuuzi huo.
Jiji la Dar es Salaam hakuna kazi ngumu kwa wanafunzi bado toto lipate sifuri kama sio ukilaza huo ni nini. Mkoani watu wanatoka shule wanasubiriwa na majani ya mbuzi, ng'ombe, kuni, kuchunga mifugo na kulima. Mtoto akirudi nyumbani akichelewa anakula mbata/bakora za uhakika na mzigo unamsubiria shambani. Lakini mwisho wa siku matokeo ya kidato cha nne anasimamisha msonge alafu wewe unayerudi nyumbani saa nane mchana unakalia kucheza PS, au unaenda kwenye mabanda umiza ya kina Acheche na Kimoda kuangalia Muvi unapata sifuri kwa ukilaza wako. Wewe ni kilaza na atakayekutetea ni kilaza bila kujali nafasi yake.
Huwezi ukafeli sehemu yenye shule zilizokaribu karibu.Jamani unashindwa kupata marafiki wa kitaaluma. Wenzako mkoani unakuta wilaya kata nzima kama sio wilaya shule ipo moja na bado anakupiga kipigo cha mbwa koko. Wewe bado uwe mzima kichwani.
Huwezi ukafeli ilhali kuna vipindi vya bungo kids sijui Skonga kwenye Luninga. Hivi unajua huko mikoani wenzako hivyo vipindi hawavijui kabisa kutokana na kutokuwepo na nyumba za umeme. Mfuate yule kijana wa Simiyu aliyechapa one ya Saba uone kama anajua hivyo vipindi. Usishangae kwao hakuna hata umeme. Alafu wewe unashindwa na mluga luga asiyeijua hata smartphone bado ujione kichwani zimo.
Watoto wa Dar es Salaam wanajiona wajanja lakini hakuna ujanja waliokuwa nao zaidi ya ujinga ujinga tuu. Wewe ukimuona kijana wa Dsm anaongea sana ujue kichwani hamna kitu. Usishangae kwa nini jiji hilo ni chafu kupita maelezo. Jibu ni kwa sababu ya ukilaza.
Wewee fikiria mtu anazibua chemba wakati wa mvua ikinyesha alafu yale mavi yanazagaa mtaani. Kama huo sio ukichaa ni nini.
Embu angalia mikoa inayofanya vizuri hapa nchini uone kama utaona hayo mambo ya hovyo. Embu nenda kule Kilimanjaro, Arusha, Iringa, Kagera, Mbeya na Simiyu uone kama utakuta mambo hayo. Ujinga unaendana na uchafu. Ndio maana vichaa huwa ni wachafu na wanaishi kwenye majalala. Ndio sifa hiyo.
Wewe mtu mzima unapangiwa ratiba ya usafi bado ujione unaakili kweli. Kazi kusumbua viongozi.
Vitoto vya Dar es salaam ni moja ya vitoto vilivyo changanyikiwa. Yaani kitoto kidogo lakini mambo yake mazito. Unakuta kijana wa kiume katoboa pua na anasoma. Mara kanyoa kiduku, mara kabana suruali na matako kama shoga na bado kanasoma. Alafu Baba yupo, Mama yupo, Bibi yupo, Shangazi yupo, na anapewa ugali pumbavu kabisa. Alafu mtu aone nawatukana watu wa Dsm. Ninyi ni vilaza.
Ati mnasingizia maisha magumu huo ni uongo. Mngeishi huku mkoani kwa watabe. Huku maisha magumu lakini watu hawajiharibu kwa upuuzi.
Wanafunzi wa Dsm wanalala na wazungu lakini kingereza weupe yaani kapa. Mkoani watu wanalala na ng'ombe, kuku. mbuzi na kondoo chumba kimoja na bado kijana anamwaga ung'eng'e kama mzungu wa London.
Nakumbuka miaka nikiwa nasoma sekondari nilikutana na kijana maneno mengi wa Dsm. Yaani kijana anaongea yule sijapata kuona. Nikamuuliza swali dogo tuu la Biology kwamba aelezee Mechanism of Hearing. Dogo chali. Nikaona nimmalize kabisa, (physics) nikamwambia aelezee Paschal's Principle dogo jasho linamtoka. Nikasema huyu ili akiniona anisalimie kabisa nikamwambia (history) aelezee WWI. Hapa nilimuuliza swali la history ili nimpumzishe lakini kumbe hata hiyo WWI haijui. Nilishangaa akiongea habari za mieleka. Mama yangu! Nikamtemea mate usoni nikamwambia tokaa hapa! Kwa kweli aliniudhi mno. Japo tulishikana mashati lakini hatakuja kunisahau maana alibadilika na tulikutana Udsm. Alinambia dharau zangu zilimsaidia. Mate yangu yaligeuza upuuzi wake kuwa akili.
Ninachotaka kusema ni kuwa, Jiji la Dar es salaam mnatia aibu. Mbadilike. Ndio maana mnaitwa wanaume wa Dar. Yaani watu legelege.
Haiwezekani muwe na kila kitu bado mnafeli. Kama sio ukilaza huo ni nini.
Mwisho; Najua wapo wanaojitahidi hapa Dsm lakini mnamezwa na wanaoangua mayai viza. Wanawaabisha hao watu.
SIshangai kwenye media nikiona mambo ya hovyo, najua ni matokeo ya vilaza. Mtu anashabikia udaku, shilawadu, na upuuzi mwingine kama huo. Na wenye media nao kwa vile wengi wao ni vilaza wanaruhusu vipindi kuruka hewani. Kwa kweli tunahitaji mabadiliko makubwa katika jiji letu hili.
Ukiishi Dar miaka mitano mfululuzi lazima akili yako iyumbe. Hii ni kutokana na mvutano utakaoupata kutoka kwa vilaza.
Wana- Dar es salaam tubadilike kwa maana mimi mwenyewe ni mkazi wa Dsm.
Ikumbukwe kuwa; nimeitumia Dar kama kielelezo cha mikoa yenye vilaza wa kutupa. Mikoa mingine ambayo sijaitaja ambayo inamiundombinu wezeshi lakini bado inafelisha, huu ujumbe pia unawahusu.
Robert Heriel
Taiko wa Fasihi
0693322300
Na, Robert Heriel.
Sijawahi kuona wanafunzi vilaza kama wa Mkoa wa Dar es salaam. Wanafunzi wa Dar es salaam ni vilaza hujapata kuona popote dunia hii. Ni vilaza ambao hawajawahi kutokea tangu kuumbwa kwa dunia. Wapende wasipende. Huo ndio ukweli. Ninyi ni Vilaza tena wa kutupa. Mnalitia taifa aibu kwa sifuri zenu.
Unajua maana ya mwanafunzi kilaza?
Ipo hivi; Kilaza ni mwanafunzi ambaye uwezo wake wa akili ni mdogo hata umuwekee mazingira wezeshi bado atabaki kuwa na uwezo mdogo.
Kwa maana hiyo na nyinginezo zinalifanya jiji la Dar es salaam kuwa jiji la Vilaza waliotukuka.
Haiwezekani jiji kubwa hapa nchini lenye miundombinu yenye unafuu bado lishindwe hata kuwa top ten ya mikoa. Mbaya zaidi ndilo linaloongoza kwa sifuri zilizotukuka. Huo ni ukilaza.
Wala hatuna muda wa kuongea maneno matamu katika hili. Yaani usome Dar es salaam bado upate sifuri wewe ni kiazi mbatata.
Dar es salaam karibu kila nyumba inaumeme. Nini kinafanya watoto wasisome mpaka wapate sifuri kama sio vichwa viazi. Iko hivi. Kama mtoto sio kiazi basi mlezi ndiye kiazi. Mtoto apate sifuri ilhali kuna umeme. Anapataje sifuri kwa mfano kama sio uzembe. Na uzembe ndio ukilaza wenyewe huo.
Watoto wanshindwa kuamka usiku wa manane kusoma? Haya hata wazazi wanashindwa kuwaamsha hao watoto kama wao wenyewe hawajitambui? Usijesema kuna kelele. Hiyo sio kweli. Mji wa Dar es salaam unaanza kupoa mida ya saa tatu usiku. Huo ni muda mzuri kwa mwanafunzi kujisomea. Akipeleka mpaka saa saba. Au alale kisha amke saa nane mpaka asubuhi kila siku kamwe hawezi kupata sifuri.
Jiji lina Tuition center kila kona. Ukigeuka huku mchikichini, huku mapambano, kule sijui nini huko. Yaani Tuition kila kona. Haya tuseme mzazi hana Pesa ya Tuition. Hivi mtoto kweli unashindwaje kuwa na marafiki wanaosoma tuition badala yake marafiki zako ni wacheza vigoma na mdundiko. Sijui Beach boy, sijui panya Road yaani utumbo utumbo tuu. Alafu unakuja kulitia aibu taifa.
Hivi unapataje sifuri kwenye jiji ambalo kila nyumba inammiliki wa Smartphone kama sio Laptop kabisa. Hivi mnashindwaje kudownload notes na material mbalimbali ya kujisomea. Matokeo yake mnatumia simu kudownlooad Video za ponograph, kuchat Whatsapp, instagram, sijui imo, na Telegram.
Yaani unaishi Dar alafu unapata sifuri wewe kama sio kichaa ni nani. Hakuna mwanafunzi mwenye akili timamu ambaye atasoma Dar apate sifuri. hata hiyo division four haiwezekani.
Haiwezekani jiji lenye chuo cha taifa, chuo kikuu cha Dar es salaam - UDSM , vyuo vingine vingi tuu kama CBE, IFM, NIT, DIT, Ardhi, Muhimbili n.k alafu bado mtu anapata zero huo si upunguani.Sisi wengine wamikoani vyuo vikuu tumeviona tulivyomaliza kidato cha sita. Tukaja mjini tukanyuka misonge tukasepa. Ninyi mmebaki kushangaana hapo kama vichaa.
Ujinga ni pamoja na kutokujua matumizi ya rasilimali. Yaani jiji lenu lina vyuo kama vyote, mnashindwa kwenda kujifunza hata kwa kaka zenu wa chuo. Mnatia aibu kwa kweli.
Jiji la Dar es Salaam ndio jiji pekee lenye vitabu, vitini, na madesa kuliko mkoa wowote hapa nchini. Lakini shangaa ndilo linaloongoza kwa sifuri nyingi ambazo ni zaidi ya mara mbili kwa mikoa ya Kilimanjaro, Arusha na Iringa.
Nina uhakika jiji la Dar es salaam kama lisingekuwa na miundombinu wezeshi kama hiyo hakuna mwanafunzi ambaye angepata hata divisio four. Wote wangepata sifuri kwa sababu ni vilaza.
Jiji la Dar es Salaam hakuna changamoto ya usafiri. Kwa vile wamezoea mambo ya legelege utasikia kugombania daladala ni changamoto. Wewe ni kichaa kama utafikiri hivyo. Nenda mkoani uone wenzako wakitembea kilomita za kutosha zaidi ya masaa mawili na bado wakifika wachapwe bakora kwa kuchelewa. Wewe unatembea dakika mbili upo kwenye daladala huyo mpaka shule. Tena kwenye Daladala mnapiaga kelele wazazi wenu kwa sababu nao ni wendawazimu kama nyie. Yaani matoto yanapanda gari yanaanza kutukana, sijui hadithi ya msanii gani kafanya nini. Mara matusi kibao. Hapo kuna wazazi nao wanasikiliza kwa sababu nao ni walewale. Badala wawakanye ikiwezekana wawachape bakora za uhakika. Looh! Ndio mambo ya vilaza hayo.
Mkoani huwezi sikia ujinga ujinga kama huo. Nenda Misungwi huko, nenda muleba, nenda Rombo, Nenda Bukoba, Nenda Mbeya kama utasikia upuuzi huo.
Jiji la Dar es Salaam hakuna kazi ngumu kwa wanafunzi bado toto lipate sifuri kama sio ukilaza huo ni nini. Mkoani watu wanatoka shule wanasubiriwa na majani ya mbuzi, ng'ombe, kuni, kuchunga mifugo na kulima. Mtoto akirudi nyumbani akichelewa anakula mbata/bakora za uhakika na mzigo unamsubiria shambani. Lakini mwisho wa siku matokeo ya kidato cha nne anasimamisha msonge alafu wewe unayerudi nyumbani saa nane mchana unakalia kucheza PS, au unaenda kwenye mabanda umiza ya kina Acheche na Kimoda kuangalia Muvi unapata sifuri kwa ukilaza wako. Wewe ni kilaza na atakayekutetea ni kilaza bila kujali nafasi yake.
Huwezi ukafeli sehemu yenye shule zilizokaribu karibu.Jamani unashindwa kupata marafiki wa kitaaluma. Wenzako mkoani unakuta wilaya kata nzima kama sio wilaya shule ipo moja na bado anakupiga kipigo cha mbwa koko. Wewe bado uwe mzima kichwani.
Huwezi ukafeli ilhali kuna vipindi vya bungo kids sijui Skonga kwenye Luninga. Hivi unajua huko mikoani wenzako hivyo vipindi hawavijui kabisa kutokana na kutokuwepo na nyumba za umeme. Mfuate yule kijana wa Simiyu aliyechapa one ya Saba uone kama anajua hivyo vipindi. Usishangae kwao hakuna hata umeme. Alafu wewe unashindwa na mluga luga asiyeijua hata smartphone bado ujione kichwani zimo.
Watoto wa Dar es Salaam wanajiona wajanja lakini hakuna ujanja waliokuwa nao zaidi ya ujinga ujinga tuu. Wewe ukimuona kijana wa Dsm anaongea sana ujue kichwani hamna kitu. Usishangae kwa nini jiji hilo ni chafu kupita maelezo. Jibu ni kwa sababu ya ukilaza.
Wewee fikiria mtu anazibua chemba wakati wa mvua ikinyesha alafu yale mavi yanazagaa mtaani. Kama huo sio ukichaa ni nini.
Embu angalia mikoa inayofanya vizuri hapa nchini uone kama utaona hayo mambo ya hovyo. Embu nenda kule Kilimanjaro, Arusha, Iringa, Kagera, Mbeya na Simiyu uone kama utakuta mambo hayo. Ujinga unaendana na uchafu. Ndio maana vichaa huwa ni wachafu na wanaishi kwenye majalala. Ndio sifa hiyo.
Wewe mtu mzima unapangiwa ratiba ya usafi bado ujione unaakili kweli. Kazi kusumbua viongozi.
Vitoto vya Dar es salaam ni moja ya vitoto vilivyo changanyikiwa. Yaani kitoto kidogo lakini mambo yake mazito. Unakuta kijana wa kiume katoboa pua na anasoma. Mara kanyoa kiduku, mara kabana suruali na matako kama shoga na bado kanasoma. Alafu Baba yupo, Mama yupo, Bibi yupo, Shangazi yupo, na anapewa ugali pumbavu kabisa. Alafu mtu aone nawatukana watu wa Dsm. Ninyi ni vilaza.
Ati mnasingizia maisha magumu huo ni uongo. Mngeishi huku mkoani kwa watabe. Huku maisha magumu lakini watu hawajiharibu kwa upuuzi.
Wanafunzi wa Dsm wanalala na wazungu lakini kingereza weupe yaani kapa. Mkoani watu wanalala na ng'ombe, kuku. mbuzi na kondoo chumba kimoja na bado kijana anamwaga ung'eng'e kama mzungu wa London.
Nakumbuka miaka nikiwa nasoma sekondari nilikutana na kijana maneno mengi wa Dsm. Yaani kijana anaongea yule sijapata kuona. Nikamuuliza swali dogo tuu la Biology kwamba aelezee Mechanism of Hearing. Dogo chali. Nikaona nimmalize kabisa, (physics) nikamwambia aelezee Paschal's Principle dogo jasho linamtoka. Nikasema huyu ili akiniona anisalimie kabisa nikamwambia (history) aelezee WWI. Hapa nilimuuliza swali la history ili nimpumzishe lakini kumbe hata hiyo WWI haijui. Nilishangaa akiongea habari za mieleka. Mama yangu! Nikamtemea mate usoni nikamwambia tokaa hapa! Kwa kweli aliniudhi mno. Japo tulishikana mashati lakini hatakuja kunisahau maana alibadilika na tulikutana Udsm. Alinambia dharau zangu zilimsaidia. Mate yangu yaligeuza upuuzi wake kuwa akili.
Ninachotaka kusema ni kuwa, Jiji la Dar es salaam mnatia aibu. Mbadilike. Ndio maana mnaitwa wanaume wa Dar. Yaani watu legelege.
Haiwezekani muwe na kila kitu bado mnafeli. Kama sio ukilaza huo ni nini.
Mwisho; Najua wapo wanaojitahidi hapa Dsm lakini mnamezwa na wanaoangua mayai viza. Wanawaabisha hao watu.
SIshangai kwenye media nikiona mambo ya hovyo, najua ni matokeo ya vilaza. Mtu anashabikia udaku, shilawadu, na upuuzi mwingine kama huo. Na wenye media nao kwa vile wengi wao ni vilaza wanaruhusu vipindi kuruka hewani. Kwa kweli tunahitaji mabadiliko makubwa katika jiji letu hili.
Ukiishi Dar miaka mitano mfululuzi lazima akili yako iyumbe. Hii ni kutokana na mvutano utakaoupata kutoka kwa vilaza.
Wana- Dar es salaam tubadilike kwa maana mimi mwenyewe ni mkazi wa Dsm.
Ikumbukwe kuwa; nimeitumia Dar kama kielelezo cha mikoa yenye vilaza wa kutupa. Mikoa mingine ambayo sijaitaja ambayo inamiundombinu wezeshi lakini bado inafelisha, huu ujumbe pia unawahusu.
Robert Heriel
Taiko wa Fasihi
0693322300