Daliliz za mchepuko😂

Newbies

JF-Expert Member
Jul 13, 2018
1,477
2,148
KUPENDA KUTEMBEA NA MIPIRA YA KINGA

Ukiona mpenzi wako ana tabia ya kubeba kondomu kwenye pochi yake au mfukoni kwa kisingizio kuwa anajali, elewa kwamba yuko katika mahusiano na mtu mwingine.

UTATANISHI KATIKA MATUMIZI YA SIMU

Ukiona simu zinamiminika mpaka usiku wa manane naye anapokea kwa siri. Yamkini pia alikuwa yuko huru hata simu yake inapolia waweza ukaichukua na kumpatia lakini ghafla anakuwa na hofu kubwa na kuificha simu yake, au anakwenda na simu hadi bafuni isije ikasikika juwa kuna jambo.

Wengine wanaondoa milio katika simu zao wakati haikuwa kawaida yao, kuweka nenosiri (password) ngumu hadi mwenyewe anashindwa kuikumbuka, wako ambao simu zao zikipigwa hawawezi kupokea na kuongea kwa uhuru kama kawaida, ataondoka na kujitenga pembeni akijifanya anaongea kiuaminifu kabisa.

HARUFU MPYA KWAKO

Kwa kuwa wapendanao huwa wamezoeana, mara nyingi hata aina ya manukato mmoja anayotumia yanakuwa yanajulikana kwa mwenzake, sasa fikiri unamkuta mpenzi wako ana harufu ya tofauti kabisa na uliyoizoea, umeisikia harufu hiyo akiwa amerudi toka kazini wakati asubuhi alipoondoka alikuwa na harufu ile uliyoizoea, elewa kwamba kuna jambo!

MABADILIKO FARAGHANI

Jambo hili linaweza kujidhihirisha katika picha mbili tofauti. Kwa kawaida wapenzi huwa na mazoea fulani katika tendo la ndoa, kwa muda waliokaa pamoja kila mmoja humfahamu mwenzake kwa kiasi fulani. Inawezekana likawa jambo la kushangaza pale ambapo ghafla unamuona mpenzi wako anapoteza kabisa hamu ya tendo la ndoa, au hata mnapokuwa katika tendo hilo humuoni akifurahia bali anakuwa kama anayelazimishwa au kutohamasishwa na chochote, hapo elewa kwamba huyo ana mchepuko.

KUJIPENDA KUPITA KIASI

Yawezekana mpenzi wako alikuwa amezoea kuvaa kawaida, hapa simaanishi kutopendeza na wewe ulikuwa umemzoea katika hali fulani ya mavazi au mitindo mara ghafla anabadilika na kuwa mtanashati zaidi ana badilisha mavazi, anapenda mavazi ya gharama, labda alikuwa hatumii manukato lakini ghafla anaanza kupenda manukato, anajijali zaidi ya kawaida yake kiasi ambacho hukumzoea na kutoka mara kwa mara. Katika hali hii jaribu kuwa macho zaidi kufahamu nini kilicho sababisha mabadiliko hayo.

KUCHELEWA KURUDI KAZINI

Sio kwamba kila mtu anapochelewa kurudi kazini basi anakuwa sio mwaminifu, lakini zaidi ya asilimia 75 (kutoka kwenye tafiti) ya ambao wamekuwa na mahusiano nje wamekuwa wakitoa visingizio vinavyohusiana na kazi, vikao, mikutano na safari za kikazi, yamkini wewe ni shahidi wa hili.

Soma zaidi Ukiona Dalili Hizi, Mwenzako Anamchepuko
 
KUCHELEWA KURUDI KAZINI
hii haiwezi ikawa sababu.mwanamke nae akikuzoea muda wako wa kurudi toka
kazini anaanza kuleta mambo ya kiwaki
mimi kama mwanaume,mwanamke hapaswi kujua ratiba yangu ya kurudi toka kazini
 
KUCHELEWA KURUDI KAZINI
hii haiwezi ikawa sababu.mwanamke nae akikuzoea muda wako wa kurudi toka
kazini anaanza kuleta mambo ya kiwaki
mimi kama mwanaume,mwanamke hapaswi kujua ratiba yangu ya kurudi toka kazini
Sawa
 
Back
Top Bottom