Dalili mbaya za kushindwa kwa ukawa/chadema

Dalili mbaya za kushindwa kwa ukawa/chadema

Mugisher

JF-Expert Member
Joined
Jul 11, 2015
Posts
411
Reaction score
360
Wakuu-

Nadhani niseme hili kwa ukweli kabisa na bila kuungaunga maneno.

CHADEMA/CDM hawajipanga kabisa kwa ajili ya uchaguzi huu. Nadhani bado wako kwenye ile ‘excitement’ au furaha ya Lowasa na imani kuwa watashinda uchaguzi wakiwa naye. Mwenendo wao unatia shaka kama kweli hiki ni chama kinachotaka kwenda ikulu. Hii ni wiki sasa inapita na CDM hawajaanza kampeni. Haiwezekana eti unapanga kampeni zako zianze wiki moja baada ya filimbi kulia. Kwangu mimi hii nikukosa mbinu. Ukipita mitaani ‘hamna poster’ hata moja ya mgombea Urais wa CDM au wabunge na hata madiwani wao. Hii ni dalili mbaya na inaonyesha kushindwa na kutokuwa na mipango. Kuhusu kiwanja cha Jangwani kuzuiwa, chama makini lazima kiwe na PLAN B na sio kungangania sehemu moja. Kwanini wasiende kuzindua campaign sehemu nyingine? CDM wanakubalika Mbeya Mjini, Moshi Mjini, Arusha Mjini- kwanini wasiende huko? Sasa Imani yenu kuwa CCM imechokwa kila sehemu mbona haiwapi ‘confidence’ yakuenda sehemu zingine? Nchi yetu ni kubwa sana, huwezi kupiga siasa Dar halafu ukadhani umeshinda uchaguzi. Jamani kati ya watu milioni 24 waliojiandikisha DAR ni watu 2.8 milioni tu. Elekezeni akili zenu kwenye HESABU HIZI si kuwa na maneno, maneno ambayo hayana tija.

Kupambana na CCM kunahitaji mbinu na maarifaa sio maneno matupu. Angalia CCM walivyokuwa organised. Myonge mnyongeni lakini haki yake mpeni. Hili halina ubishi. Angalia ‘nyomi’ ya Magufuli kila sehemu anayoenda. Hii yote inaonyesha hawa watu wamejipanga. Hata mkibisha CCM bado inapendwa. Kama ‘inachukiwa’ ni sehemu za mjini tu, ambazo kihesabu zinaweza zisiwe na maana sana kulinganishwa na huko kwingine.

Haiwezekani campaign za chama ziwe zinamzunguka mtu mmoja. Chama ni taasisi na si mtu. Na hilo ndilo naliona kwa CDM. Yaani kila kitu ni Lowasa. Viongozi wao wanatakiwa wawajibike. Bado sijaona nia hasa ya kuingia ikulu zaidi ya makelele ya mabadiliko ambayo hayana vitendo vya kusambaza hilo kwa wananchi. Makelele pekee hayawezi kushinda uchaguzi. Acheni kuchanganyikiwa na anzeni mipango sasa ili tuwe na opposition yenye nguvu bungeni. CHADEMA KUWENI NA PLAN B KILA WAKATI.
 
Una haraka ya nini wewe? acha upumbavu....Chadema/Ukawa itashinda Asubuhi sana huu uchaguzi...
 
Hata hapa nilipo sijaona bendera,poster ama tangazo lolote la chama chochote.

Naona mwenzetu upo ktk kile kitengo cha lumumba.
 
Usiwe na hofu . Unakumbuka Magufuri alivyoanza kuchukua form walipiga kelele sana ilA UKAWA taiz moja tu maandamano yote yakazuiwa. Sasa. Nakwambia kampeni moja tu ya ukawa utasikia ccm imefunga kampeni zoote.
 
Mugisha unachokisema kwa watu waelewa wangechukua Ushauri wak maana swala la uzinduzi wa kampeni ni sawa na Kutangaza nia ,kila mmoja anaandaa mazingira yake,tatizo la CDM ni wivu unawasumbua na upunguvu wa HR.Maana HR yao wengi wao wanapigana kurudi Bungeni na wako mashakani kabisa.Mbowe Mwenyewe anatakiwa arudi Hai kujaribu bahati yake.CDM mnakera acheni kulalamika kuwenu wabunifu,tatizo badala ya kuwa wabunifu mnakuwa wasanii na kupoteza muda kupambana na Dola wakati hamna dola.Chukueni ushauri huu utawasaidie.
 
hahahahhahaah...Usipanic....CCM watapotezwa asubuhi

Kwani baada ya Magufui kuteuliwa Dodoma ilikuwaje?
 
Sasa hivi tukiingia kwenye uchaguzi, pamoja na kampeni nyingi za CCM ila Ukawa itashinda.
 
Hata UZI wako ni kampeni tosha kwa UKAWA. Hatuhitaji kutumia nguvu nyingi kwa sbb UKAWA ni trademark tosha, si unaona ht wewe kila wkt unafikiria UKAWA? Siku 5 tu zinatosha ht tukianza October trh 19.
 
Mugisha unachokisema kwa watu waelewa wangechukua Ushauri wak maana swala la uzinduzi wa kampeni ni sawa na Kutangaza nia ,kila mmoja anaandaa mazingira yake,tatizo la CDM ni wivu unawasumbua na upunguvu wa HR.Maana HR yao wengi wao wanapigana kurudi Bungeni na wako mashakani kabisa.Mbowe Mwenyewe anatakiwa arudi Hai kujaribu bahati yake.CDM mnakera acheni kulalamika kuwenu wabunifu,tatizo badala ya kuwa wabunifu mnakuwa wasanii na kupoteza muda kupambana na Dola wakati hamna dola.Chukueni ushauri huu utawasaidie.

Eti umesema chadema wana wivu? hahahaha eti chadema sio wabunifu? au ulimaanisha CCM? we utakua mgonjwa wa akili
 
Hata hapa nilipo sijaona bendera,poster ama tangazo lolote la chama chochote.

Naona mwenzetu upo ktk kile kitengo cha lumumba.

Kaka cha msingi uliza. Labda upo Monduli. Lakini nilipo mimi kuna posters za CCM kila sehemu.
 
Sasa kama Mimi kura yangu iko kwa Lowassa hata nisipomwona hadi siku ya uchaguzi. Nimechoshwa na blabla. Wote huku mbezi ni ukawa mwambieni kova kuna kituo maalumu tumejichanga tukaanxisha kwa ajili ya kufwatilia mikutano yote ya ukawa. Kuna tatizo?
 
Unaposema ccm bado inapendwa vijijini na kuchukiwa mjini unamaanisha nini? Watu wa vijijini ni wajinga sana au! Endelea kujipa moyo na ccm yako.
Hata hapa nilipo sijaona bendera,poster ama tangazo lolote la chama chochote.

Naona mwenzetu upo ktk kile kitengo cha lumumba.
 
Hata UZI wako ni kampeni tosha kwa UKAWA. Hatuhitaji kutumia nguvu nyingi kwa sbb UKAWA ni trademark tosha, si unaona ht wewe kila wkt unafikiria UKAWA? Siku 5 tu zinatosha ht tukianza October trh 19.

Kaka mimi nasema haya kwa wema, wewe unaleta utani na kejeli.
 
Kampeni za kiccm hatufanyi tutafanya kampeni za kisayansi zaidi posters bila kuwafikia watu ni kazi bure
 
Mugisher

Kumbe ndio ilikua nia yenu kuzuia uwanja wa Taifa! Tulishawasoma kitambo, Kama wewe sio Lumumba Jocker kwanini usijiulize utaanzaje kampeni kabla ya uzinduzi? Katikati ya wiki haiwezekani,jumapili uwanja wa Taifa umetiwa mfukoni,Ukitaka uwapangie wewe UKAWA siku yao uzinduzi?
Team za kazi zimeshaingia mkuu mambo ni Jangwani kama ilivyopangwa kwa mujibu wa tume tar 29/8/2015 karibu sana.
 
Last edited by a moderator:
#Kawembe huwa hufikirii halafu pia hutumii busara katika kutatua matatizo. Nchi hii usipokuwa makini ni sawa na mtoto asiyena uwezo wa kumhama mama yake mkatili. MANENO MATAMU YA MAGUFULI HAYABADILI MFUMO WA CCM. MAGUFULI HANA UZOEFU NA CHAMA SO ATAENDELEA KUBURUTWA NA SYSTEM YA CHAMA
 
Mugisher

OK. unaweza kuwa na point Fulani, sasa sielewi kama unayo macho na masikio juu ya rough za ccm dola kutumia dola zake kuzuia kila aina ya jitihada za UKAWA kufungua kampeni na kuziendeha.
 
Last edited by a moderator:
Acheni kukariri nyie! Ukawa wanafanya kampeni zenye akili na massive effects. Tatizo mnafikiria kwa mazoea na kukariri tu, I hate tabia hii!
 
Back
Top Bottom