Mtambuzi
Platinum Member
- Oct 29, 2008
- 8,810
- 15,398
Kuna baadhi ya wanaume huziona dalili za mwanamke kumtaka kimapenzi kwa namna ambayo siyo kabisa. Na ndio maana mara nyingi mwanamke anapomchangamkia mwanaume na kuwa naye karibu kimazungumzo katika hali ya kawaida, lakini mwenzake akaona kuwa hiyo ni dalili ya kupendwa na mwanamke huyo.
Na hiyo huwapa wakati mgumu sana pale wanapogundua kuwa mwanamke husika hakuwa na fikra za kuwa na uhusianao nao kimapenzi kama walivyodhani. Na hapo ndipo fedha na nguvu itatumika ili kuhakikisha anampata mwanamke huyo na wakati mwingine hata vitisho pale njia hizo mbili zinaposhindwa.
Yaani anaweza kuamini kabisa kuwa mwanamke fulani amempenda kimapenzi, wakati sio kweli. na anapomtongoza mwanamke huyo na kukataliwa, hapo ndipo mbinu chafu zinapoanza kutumika kwa kuwa wanaume hawakubali kushindwa na hasa katika jambo hilo.Kwa kawaida wanawake na wanaume, wanayo mikabala tofauti katika kuonesha dalili za kupenda.
Wakati kwa mwanaume kuchekewa, kuchangamkiwa na na kutaniwa na mwanamke, kuna maana ya mwanamke huyo kumpenda mwanaume husika. Lakini kwa manamke, kufanya chochote kati ya hayo au kufanya yote hakuna maana ya kumpenda mwanaume husika.
Na hapo ndipo wanawake wanapotakiwa kuwa waangalifu pale wanapofanya masihara na baadhi ya wanaume maana wanaweza kutafsiri vibaya, ule utani na ukaribu wenu kwao.
Kila mwanamke anayo dalili ya kuonesha kuvutiwa na mwanaume lakini sio dalili za wazi kiasi hicho. Waswahili wanasema, 'ada ya mja hunena, muungwana ni vitendo.' kwa kawaida wanawake huonesha vitendo kuliko maneno....